Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Makonda: Atakayenunua makontena yangu atalaaniwa yeye na kizazi chake! Atoa onyo kwa atakayethubutu kununua

Ni kitu cha kushangaza kuona uwepo wa taarifa ya familia moja yaani watoto wa baba mmoja kugombana hadharani kwa vitu vidogo ambavyo vinaweza kumalizwa aidha na wakubwa zao kiumri au wazazi wao, hapa namaanisha baba au mama ndani ya familia.

Ugomvi unao dharirisha familia, ugomvi unao ruhusu majirani kuwasema vibaya,
unaonesha hakuna mawasiliano mazuri ndani ya familia moja.

Kwanini haya yanatokea, ni uoga, kumuogopa baba yao au ni misimamo tu.

Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Makonda aliomba msaada kutoka Kwa watanzania wanaoishi marekani thamani pamoja na vifaa vya mashuleni, vifaa hivyo vimekuja lakini vimekwama bandarini Kwa sababu ya kodi, waziri wa fedha pamoja na mamlaka ya mapato wanao shughurika na kodi wametoa Kauli yao kwamba vifaa hivyo vimekuja lazima vilipiwe kodi na Kama sivyo vitapigwa Mnada Kama sheria inavyotaka.

TATIZO NINI?
vifaa hivyo ingawa ni vifaa kwa ajili ya mashuleni, lakini havikuja kwa Jina la wizara husika, ila vifaa hivyo vimekuja kwa jina la Paul Makonda, hii inamaana kwamba ni vifaa vyake yeye mwenyewe anataka atoe msaada yeye mwenyewe au labda kwa niaba ya hao rafiki zake wa ughaibuni, sasa kwa utaratibu wa sheria za kodi kuna vitu ambavyo vinamsamaha lakini Mkuu wa Mkoa hana msamaha wa kodi kwa vitu vyake anavyoagiza au kupewa toka nje ya nchi labda kwa maelekezo toka kwa mwenye madaraka makubwa kuliko yoyote ndani ya nchi.

KIPI KIFANYIKE!
Mkuu wa Mkoa aidha alipe kodi, au vile vifaa vikiwa palepale bandarini aandike barua kwa waziri wa fedha kupitia mamlaka ya mapato, akivitoa vitu hivyo kwa wizara husika, wizara ya elimu, akielezea ujio wa hivyo vitu hapa nchini kwa lengo la kutokomeza mazingira magumu mashuleni, sasa wizara husika ndiyo itashughurika na kodi kama kuomba isamehewe au kulipa, kwasababu bajeti ya kununua thamani mbalimbali mashuleni naamini ilikuwepo kama kuna huu unafuu wanaweza kulipa kodi.

HAIWEZEKANI.......!!!!!!!
haiwezekani husamehewe kodi kwa vitu ulivonunua au kupewa iwe unataka kutoa msaada au kugawa bure kama sheria haijatoa maelekezo tofauti haiwezekani ata umwambie prezo hiyo sahau, sio kwa jina lako, waziri na mamlaka ya mapato wako sahihi.

SWALI LA KUJIULIZA....?
hivi kweli mmeshindwa kuwasiliana kiofisi na kuyamaliza kiofisi hadi mnaongea kwenye madhabaho ya kanisa, kwenye mitandao ya kijamii?

Mmeshindwa kulifanya hili jambo kuwa ni la ndani kwa kupeana maelekezo kupitia vi- memo?




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alipe makonda mimi siwezi beba box kwenye mazingira magumu kwenye barafu, ubaguzi Alafu nikachangia upuuzi

Exactly, kwanza kapakazia diaspora ndo wamempa msaada, wee box ubebe hadi lifike kodi ya bilioni 21 kwa hela zipi nyingi hivyo walizonazo hao diaspora[emoji15]
 
Kaandika majina ili yajulikane ni juhudi zake sasa wewe unaleta hadithi ya kuyageuza yawe ya wizara ya elima sasa huoni unaenda against na mpango wake wa kujitengenezea publicity kwenye jamii ili ateuliwe kuwa waziri wa mambo ya ndani then agombee urais

Sent using Jamii Forums mobile app
dhamira ya nje inaonyesha msaada lakini ya ndani inaonyesha fursa na kujijenga katika utukufu bila mimi.... hakuna anayeweza.
afate tu taratibu na kiukweli hivyo viti havifai sana kwa waalimu wetu labda kama wanapewa wafungulie stationary
 
Wapige mnada fasta, kwanza hizo fanicha nimezipenda lazima na mimi niondoke na viti hapo na ili kupunguza makali ya laana yake vingine nitatoa sadaka kanisani
 
Kwanza kwa mlio walimu mtanielewa ninaposema waziri kakurupuka wala hazijui changamoto za elimu
ukisikiliza kwa umakini kwenye hotuba yake ya juzi utagundua kabisa aelewi anachokiongea...

Anaongelea maswala ya elimu bure kitu ambacho ni nje kabisa ya mada ya makontena

swala hapa ni vifaa kwa ajiri ya kusaidia elimu ya dsm ambayo ina changamoto nyingi ikiwa na mrundikano wa wanafunzi na mambo kibao

Makonda inawezekana kuna sehemu alikosea katika mchakato huo lakini serikali walitakiwa kuwa wajanja wangeruhusu kwanza vitu viingie ndio waanze kuvimonitor wapate ushahidi wa kutosha ndio waje kumtuhumu.

matokeo yake wananchi nao wameyabeba na kusahau watoto wao ndio wanakaa chini milele
mimi niko na ushahidi kabisa nilienda shule moja na taasisi fulani kutoa msaada wa computer lakini unakuta walimu stafu viti tu vya kukalia haviwatoshi hii ni aibu kama mwalimu hana kiti stafu mwanafunzi je darasani itakuwaje?

tukiweka siasa pembeni Makonda yupo sahihi kabisa na ana nia njema ingawa anaweza kuwa kafanya makosa kutumia jina lake kwa ushauri mbovu wa watendaji waliopo chini yake lakini naamini tatizo letu la elimu ni kubwa mno kuliko jina la makonda kuwa kwenye makontenana hili swala tunalibabe kishabiki sana kama kawaida yetu...

kwamba mimi ni chadema Gambo akifiwa na mzazi wake nashangilia, mimi ni ccm Sugu akipata msiba nashangilia upuuzi mtupu.

Hivi waziri anavipiga mnada vitu vya shule za dsm watu tunashangilia leo halafu kesho jangwani secondary inakuwa ya mwisho tunaanza kumponda makonda ...

Hivi vitu vikinunuliwa na wafanya biashara sisi wananchi wa kawaida tutafaidika vipi direct kama ambavyo tungeviona kwenye shule zetu? namimi naongeza na alaaniwe kabisa atakae vinunua.

"Form four wanakaribia pia kuanza mtihani msisahau kuleta mrejesho hapa wa shule za umma"
 
Mkiendekezi hii tabia, ipo siku mtu ataingiza mizigo yake kwa style hii ambayo kwanza hakuna mwenye uhakika kama vifaa hivyo vyote kweli vinawafia walengwa au ni janja tu.

Na kwa jinsi jambo hili linavyokwenda mpaka sasa, ni dhahiri unahitajika uchunguzi wajulikane ni kina nani walituma vifaa hivyo na shule gani hasa zilizolengwa kupewa hiyo misaada.

Hili jambo lina ukakasi unaohitaji uchunguzi maana huenda si kila kifaa kitaenda kutolewa kama msaada.

Na nikwambie tu, vifaa hivyo vingekuwa vimeingizwa na mtu kutoka upinzani, vingeshapigwa mnada siku nyingi tena huyo Makonda angeweza hata kuingilia viuzwe haraka japo kisheria hahusiki.

Tena namshauri waziri Mpango awe makini na kama kuna mtu atamshinikiza atoe msamaha,basi ahakikishe mtu huyo anatoa agizo kwa njia ya maandishi vinginevyo ajiuzulu kwani ipo siku anaweza kuja kujikuta anawajibika kwa matumizi mabaya ya madaraka na kuikosesha serikali mapato.

Wanasiasa sio watu, hawachelewi kukugeuka.

Tukumbuke sheria tunatunga wenyewe na kuzipitisha kwa mbwembwe.

Swali: Iweje leo tuzione chungu?

Tunavuna tulichopanda.
 
Kwanza kwa mlio walimu mtanielewa ninaposema waziri kakurupuka wala hazijui changamoto za elimu
ukisikiliza kwa umakini kwenye hotuba yake ya juzi utagundua kabisa aelewi anachokiongea...

Anaongelea maswala ya elimu bure kitu ambacho ni nje kabisa ya mada ya makontena

swala hapa ni vifaa kwa ajiri ya kusaidia elimu ya dsm ambayo ina changamoto nyingi ikiwa na mrundikano wa wanafunzi na mambo kibao

Makonda inawezekana kuna sehemu alikosea katika mchakato huo lakini serikali walitakiwa kuwa wajanja wangeruhusu kwanza vitu viingie ndio waanze kuvimonitor wapate ushahidi wa kutosha ndio waje kumtuhumu.

matokeo yake wananchi nao wameyabeba na kusahau watoto wao ndio wanakaa chini milele
mimi niko na ushahidi kabisa nilienda shule moja na taasisi fulani kutoa msaada wa computer lakini unakuta walimu stafu viti tu vya kukalia haviwatoshi hii ni aibu kama mwalimu hana kiti stafu mwanafunzi je darasani itakuwaje?

tukiweka siasa pembeni Makonda yupo sahihi kabisa na ana nia njema ingawa anaweza kuwa kafanya makosa kutumia jina lake kwa ushauri mbovu wa watendaji waliopo chini yake lakini naamini tatizo letu la elimu ni kubwa mno kuliko jina la makonda kuwa kwenye makontenana hili swala tunalibabe kishabiki sana kama kawaida yetu...

kwamba mimi ni chadema Gambo akifiwa na mzazi wake nashangilia, mimi ni ccm Sugu akipata msiba nashangilia upuuzi mtupu.

Hivi waziri anavipiga mnada vitu vya shule za dsm watu tunashangilia leo halafu kesho jangwani secondary inakuwa ya mwisho tunaanza kumponda makonda ...

Hivi vitu vikinunuliwa na wafanya biashara sisi wananchi wa kawaida tutafaidika vipi direct kama ambavyo tungeviona kwenye shule zetu? namimi naongeza na alaaniwe kabisa atakae vinunua.

"Form four wanakaribia pia kuanza mtihani msisahau kuleta mrejesho hapa wa shule za umma"
Yani hapa ndo Wana ccm wameshindwa wawe wapi either kwa RC or Waziri.
Mana unaweza ukawa kwa Wazira yakamkuta ya Nape wakashindwa kula matapishi yao, wakawa kwa RC ukasikia amepangiwa majukumu mengine? Niwashauri tu Wana ccm mlivyokua ni wafuata upepo kuweni tu katikati uku mkisubri Baba yenu ataamua nini, ili atakako favor ndo muende uko.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom