Naunga mkono hojaPopote nikona maneno hayo kwenye red najua msemaji ni tikiti maji kichwani, ukiwa na kitu kichwani utakuwa mpuuzi kuamini mtu au kiongozi kushauriwa vibaya na watu wa chini yake. Ukiona unashauriwa vibaya na huyo wa chini yako tafsiri yake you are not competent enough na bora umuachie huyo mshauri kiti chako. Tukubali kusema kiongozi fulani kakosea, awe nani au kiongozi mwenye ndevu hadi kwenye magoti akikosea tuseme kakosea ama kwa kutokujua au kwa kupuuzia siyo kusingizia washauri.
Mungu anakuona ujueKuna madarasa na ofisi nyingi za walimu Dar zinajengwa kwa juhudi binafsi za Makonda
JKT wamejitolea kujenga bure hizo ofisi .
Ngoja ziishe kujengwa alafu walimu wataenda kukaa chini humo
Sent using Jamii Forums mobile app
SAKATA LA MAKONTEÑA YA MAKONDA KUPIGWA MNADA LITIZAMWE UPYA
Na: Mtetezi wa Wanyonge.
Nimemsikia Waziri Mipango akisema kuwa Lazima Makontena hayo Yalipiwe Kodi ama yapigwe Mnada ili serikali ipate Kodi yake...
My Take
Tukumbuke kuwa Makontena hayo ya Vifaa ni Watanzania wenzetu wamejitolea na ndiyo maana hakuna kiwanda kilichopewa tenda hiyo na huo ni msaada kama alivyopata misaada ya Miguu Bandia, Ujenzi wa Hospital, Viwanja vya Mpira, magari ya Police , Pikipiki, Computer [emoji335] na vingine vingi alivyowai kufanya.
Makonda aliomba Samani si kwa faida yake bali kwa faida ya Watanzania na Kuipunguzia Serikali mzigo wa Manunuzi ya Vifaa hivyo.
Leo Kigezo Kimekuwa SHERIA! Sawa lakini Sheria zinatungwa, kusomwa na kutafsiriwa na wanadamu na bado huacha mwanya wa busara kutumika na kila kesi huamliwa kulingana na mazingira na ushahidi wake. (Ndio maana kuna Dissenting decision/Opinion and or Consential/Concurring Opinion)
Na Ikumbukwe Kuwa Sheria ya kodi inaruhusu busara kutumika pale inapoonesha kuwa vitu au mali zitatumika kwa manufaa ya jamii ya wanyonge na sio mtu binafsi.
Ikiwa Makanisa, NGOs nk. Kila kukicha yanapewa misamaha ya kodi kwa idhini ya MaRC na MaDC kulikoni hasa haya Makontena ya Viti vya Walimu? Computer za Shule? Meza na nk...?
Nikweli Yalitumwa kwa Jina la Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Lakini kampeni yake Iko wazi tangu awali na si ya kificho, Walioyatoa walitamka wazi ni ya nini na hayana faida kwa Makonda bali kwa Taifa na Watu wake hasa Wanyonge walio wengi.
Sasa Msuguwano Huu unatoka wapi?
Hiyo Kodi Ni Bei gani?
Kodi inadaiwa hapo inathamani Kubwa kuliko Samani ya hivyo Vifaa?
Hiyo Kodi Inaweza kununua vifaa vyote hivyo?
Haya Vikipigwa Mnada Serikali itapata Bei Gani? Hiyo Bei Inaweza kununua Samani zote hizo?
Tusing'ang'ane na Sheria inayotupotezea kingi zaidi kwa Kukomalia Kodi nakupoteza Mali Kubwa zaidi ya Kodi, Hekima na Busara zinaweza Tatua hili kwa Kukaa nakujadili Faida na Hasara za Kodi, Faida na Hasara zakuendelea kuwa na Vifaa hivyo, Faida na Hasara za Vifaa hivyo Kuingia kwenye Majengo yanayongoja Vifaa na Wanyonge kuvitumia.
RC Makonda Ameomba Misaada Majengo yamejengwa yanahitaji Samani, Serikali Imesaidiwa na Wazalendo wa Taifa hili waishio ughaibuni kwanini Tuwafanye wajione hawana Thamani kwa Kujitoa kwao kusaidia Nchi yao?
Mh Waziri Mipango na Wasaidizi wako na Watu wa TRA mlitizame Upya Jambo hili.
Mlio Karibu na Mh Rais Fikisheni Kilio cha Wanyonge wakatumie Vifaa hivi.
Iko Misamaha Mingi sana ya Kodi Kupitia Vifaa hivyo kuwa Vinaenda kuhudumia Jamii basi Dhamila Kuu ikatimie kwa Vifaa hivyo Kusamehewa Kodi na Vikatumike Mashuleni.
Mnyonge Mnyongeni haki yake Mpeni!
Hapa Hatumkomoi Makonda ila Tunataka Kuwakomoa Walimu na Watoto wa Shule wenye uhitaji wa Vifaa hivyo.
Sakata la Makontena Liangaliwe upya kwa Maslahi Mapana ya Taifa Hili na Wanyonge wenye Uhitaji wa Vifaa hivyo.
Waziri Mipango Fanya Mipango Vifaa viwafikie Wanyonge bila Kodi, Manake hata Mkisema Kodi ilipwe analipa nani?
Makonda aloomba kwa Niaba ya serikali?
Au Tuwaombe Pesa Walotupa Msaada tena wao Ndo walipe Kodi tena?
Kwani Tunataka Kumfurahisha nani katika hili? Au Kumkomoa Nani katika Hili?
Wanaoteseka ni Walimu na Watoto wa shule, Misuli tunayotunishiana Viongozi Haitusaidii sisi watanzania kwa ujumla.
Kodi na Mnada kwa Vifaa hivyo Vyote vinatuumiza kwani Vinapelekea Kupoteza Vifaa vyenye uhitaji kwa wanyonge.
Kodi tunazikusanya ili Tununue Vifaa vya Shule, Leo Hii Vifaa Vimekuja Buree na Vingi vyenye ubora zaidi sisi hatuvitaki kisa Kodi.
Inasikitisha sana hii Hali....
Tunaomba Viongozi walitizame upya jambo huli.
Makontena haya Faida kwa Mkonda zaidi ya Faida kwa Wanyonge na Serikaki yao ambao wanahitajika Kuhenyeka kwa Mika kadhaa huku wakilipa kodi ndo waweze kununua Vi
Acha ujinga wew na msitumie nguvu nyingi sana kumtetea huyo shetani wenu ,lipeni ushuru kama vip tunayapiga mnada tu shenzi nyie!
Tatizo ukuu wa Mkoa kigezo kikubwa ni kujua kusoma na kuandika tu.Hii aibu kabisa na Mh. Rais chukua hatua sasa..
Mkoa wa Mkoa anatia aibu, iweje anashindwa kuongea na mamlaka husika ya kodi TRA hadi kufikia aibu hii? Ina maana kama ni vifaa kweli vya shule alishindwa nn kuongea na Waziri wake wa TAMISEMI ili aongee na Waziri wa Fedha ili vikaguliwe na vipatiwe exemption kwa asilimia fulani alafu kama ni vifaa vya shule basi viruhusiwe... Mm nahisi kuna ujanja fulani labda Mkuu wa Mkoa anataka kuufanya.. Kodi ni lazima ilipwe na jina ni lake ktk makontena, so TRA wako sahihi kudai kodi, Mh. Rais anaweza chukia akamwondoa RC Makonda kwa kosa hili hili la kodi... Ooohh shauri yake...
uzuri wake Mpango ameapa kuzaaa na mtu na yuko tayari kufukuzwa kazibahasha za khaki kazini
Acha ubwege. Aliyekudanganya kuwa Dkt Mpango ni mwana-Chadema hakupendiChadema wana wivu sana na Makonda lakini mkae mkijua amewaacha mbali sana na saco cos yenu
Sent using Jamii Forums mobile app
Waganga njaa wametumwa na Bashite.Mbona watetezi ni wengi sana kwenye hili swala?
Watumishi tunakatwa Kodi kila uchao.
Kinachoshindikana nini yeye kulipa kodi?
Acheni 'sound' acha MTU alipe kodi.
Vimishahara vya kuunga tu huku serikalini kodi yake mpaka unasema ebwana ndio.
Huyu anatafuta janja janja ya kutolipa.
Mpango komaa atoe mzigo wetu
Tujifunze ustaarabu, tulipa kodi. MTU wa kodi kodi!!!
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] Kweli ukiwa ccm akili lazima iwe ndogo, Ni lini Mpango akawa chadema?Chadema wana wivu sana na Makonda lakini mkae mkijua amewaacha mbali sana na saco cos yenu
Sent using Jamii Forums mobile app
Mie nnaona Waziri Mipango katumia staha tu hajataka kumwaibisha Makonda... Ya laiti samani zote kwenye hizo containers zingekuwa kweli za shule nnahisi hizi kelele za kwamba anatakiwa kulipa kodi tusingezisikia kabisaMaswali mawili unayopaswa kujiuliza. SWALI NO 1 inakuingia akilini kuwa diaspora waishio marekani wakakuchangia vifaa vya elimu kontena ishirini? SWALI NO 2 unao uhakika kuwa kwenye hayo makontena ishirini kuna hizo samani za shule peke yake? NOTE, TRA na waziri hawajakurupuka
Sent using Jamii Forums mobile app
Mnatujazia tu upuuzi wenu. Huyo Bashite na Dkt Mpango si wote ni CCM? Sasa Jamii Forums imekuwa NEC au Kamati Kuu ya CCM? Kwendeni huko!SAKATA LA MAKONTEÑA YA MAKONDA KUPIGWA MNADA LITIZAMWE UPYA
Na: Mtetezi wa Wanyonge.
Nimemsikia Waziri Mipango akisema kuwa Lazima Makontena hayo Yalipiwe Kodi ama yapigwe Mnada ili serikali ipate Kodi yake...
My Take
Tukumbuke kuwa Makontena hayo ya Vifaa ni Watanzania wenzetu wamejitolea na ndiyo maana hakuna kiwanda kilichopewa tenda hiyo na huo ni msaada kama alivyopata misaada ya Miguu Bandia, Ujenzi wa Hospital, Viwanja vya Mpira, magari ya Police , Pikipiki, Computer [emoji335] na vingine vingi alivyowai kufanya.
Makonda aliomba Samani si kwa faida yake bali kwa faida ya Watanzania na Kuipunguzia Serikali mzigo wa Manunuzi ya Vifaa hivyo.
Leo Kigezo Kimekuwa SHERIA! Sawa lakini Sheria zinatungwa, kusomwa na kutafsiriwa na wanadamu na bado huacha mwanya wa busara kutumika na kila kesi huamliwa kulingana na mazingira na ushahidi wake. (Ndio maana kuna Dissenting decision/Opinion and or Consential/Concurring Opinion)
Na Ikumbukwe Kuwa Sheria ya kodi inaruhusu busara kutumika pale inapoonesha kuwa vitu au mali zitatumika kwa manufaa ya jamii ya wanyonge na sio mtu binafsi.
Ikiwa Makanisa, NGOs nk. Kila kukicha yanapewa misamaha ya kodi kwa idhini ya MaRC na MaDC kulikoni hasa haya Makontena ya Viti vya Walimu? Computer za Shule? Meza na nk...?
Nikweli Yalitumwa kwa Jina la Paul Makonda Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Lakini kampeni yake Iko wazi tangu awali na si ya kificho, Walioyatoa walitamka wazi ni ya nini na hayana faida kwa Makonda bali kwa Taifa na Watu wake hasa Wanyonge walio wengi.
Sasa Msuguwano Huu unatoka wapi?
Hiyo Kodi Ni Bei gani?
Kodi inadaiwa hapo inathamani Kubwa kuliko Samani ya hivyo Vifaa?
Hiyo Kodi Inaweza kununua vifaa vyote hivyo?
Haya Vikipigwa Mnada Serikali itapata Bei Gani? Hiyo Bei Inaweza kununua Samani zote hizo?
Tusing'ang'ane na Sheria inayotupotezea kingi zaidi kwa Kukomalia Kodi nakupoteza Mali Kubwa zaidi ya Kodi, Hekima na Busara zinaweza Tatua hili kwa Kukaa nakujadili Faida na Hasara za Kodi, Faida na Hasara zakuendelea kuwa na Vifaa hivyo, Faida na Hasara za Vifaa hivyo Kuingia kwenye Majengo yanayongoja Vifaa na Wanyonge kuvitumia.
RC Makonda Ameomba Misaada Majengo yamejengwa yanahitaji Samani, Serikali Imesaidiwa na Wazalendo wa Taifa hili waishio ughaibuni kwanini Tuwafanye wajione hawana Thamani kwa Kujitoa kwao kusaidia Nchi yao?
Mh Waziri Mipango na Wasaidizi wako na Watu wa TRA mlitizame Upya Jambo hili.
Mlio Karibu na Mh Rais Fikisheni Kilio cha Wanyonge wakatumie Vifaa hivi.
Iko Misamaha Mingi sana ya Kodi Kupitia Vifaa hivyo kuwa Vinaenda kuhudumia Jamii basi Dhamila Kuu ikatimie kwa Vifaa hivyo Kusamehewa Kodi na Vikatumike Mashuleni.
Mnyonge Mnyongeni haki yake Mpeni!
Hapa Hatumkomoi Makonda ila Tunataka Kuwakomoa Walimu na Watoto wa Shule wenye uhitaji wa Vifaa hivyo.
Sakata la Makontena Liangaliwe upya kwa Maslahi Mapana ya Taifa Hili na Wanyonge wenye Uhitaji wa Vifaa hivyo.
Waziri Mipango Fanya Mipango Vifaa viwafikie Wanyonge bila Kodi, Manake hata Mkisema Kodi ilipwe analipa nani?
Makonda aloomba kwa Niaba ya serikali?
Au Tuwaombe Pesa Walotupa Msaada tena wao Ndo walipe Kodi tena?
Kwani Tunataka Kumfurahisha nani katika hili? Au Kumkomoa Nani katika Hili?
Wanaoteseka ni Walimu na Watoto wa shule, Misuli tunayotunishiana Viongozi Haitusaidii sisi watanzania kwa ujumla.
Kodi na Mnada kwa Vifaa hivyo Vyote vinatuumiza kwani Vinapelekea Kupoteza Vifaa vyenye uhitaji kwa wanyonge.
Kodi tunazikusanya ili Tununue Vifaa vya Shule, Leo Hii Vifaa Vimekuja Buree na Vingi vyenye ubora zaidi sisi hatuvitaki kisa Kodi.
Inasikitisha sana hii Hali....
Tunaomba Viongozi walitizame upya jambo huli.
Makontena haya Faida kwa Mkonda zaidi ya Faida kwa Wanyonge na Serikaki yao ambao wanahitajika Kuhenyeka kwa Mika kadhaa huku wakilipa kodi ndo waweze kununua Vifaa vyote hivyo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Mwanzoni alikua anajijua yeye ni "Daudi Albert Bashite" baada ya sekeseke la vyeti na Makontena yana jina la "Makonda" kwa vyovyote yasingeweza kuwa ya kwake, lakini sasa amerudi kwenye umakonda wake😀Kwani huyu mheshimiwa awali si aliyakana!?
Walipe tuuwewe pumbavu kabisa ,acheni ujinga wenu wa kutafuta public sympathy lipeni ushuru wa hayo makontena basi!