Makonda kuapa kesho kuwa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, ataondoka na msafara wa gari moja, tofauti na awali magari sabini

Ndugu zangu Watanzania,

Watanzania mitaani wanasubiri kwa hamu kubwa na shauku kubwa sana kumuona Mheshimiwa Mwamba Mwenyewe Paul Christian Makonda akila kiapo cha ukuu wa Mkoa wa Arusha,mbele ya Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka, jasiri muongoza njia na shujaa wa Afrika.

Nimepita maeneo mbalimbali nimeona namna Mwamba Makonda alivyogumzo na kuteka mijadala mbalimbali ya kisiasa mitaani na vijiweni,kubwa zaidi ni namna na juu ya urejeo wa Mwamba huyo serikalini utakavyoleta taswira mpya ya kiutendaji na matokeo chanya kwa wananchi wa Arusha na kanda ya kaskazini,hasa kwa kuzingatia kuwa Arusha ni kitovu cha biashara na utalii kanda hiyo.

Kwa hakika Makonda ni Mwamba kwelikweli anayeishi katika mioyo ya watanzania na kukubalika sana kwa watu. Leo atakapoapishwa mtaona namna mitandao ya kijamii na vyombo mbalimbali vya habari vitakavyotekwa na kutawaliwa na Makonda.Mtaona namna atakavyoisimamisha nchi siku atakapotua Arusha,mtaona namna atakavyo pamba kurasa za magazeti na mitandao ya kijamii na Tv zote siku atakapofungua kinywa chake kuzungumza kama mkuu wa Mkoa wa Arusha akiwa katika ardhi ya Arusha. kwa hakika jiji litalipuka kwa shangwe ,nderemo na vifijo utafikiri Nchi imetoka kupata uhuru wake..

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
 
Hata kama weekend angekuwa anaenda Marekani kupumzika(Japo huko alishapigwa ban kwa tuhuma za mauaji) swala la Bashite kuwa kiongozi muovu liko pale pale. Ila kama wewe ni chawa wake hakuna shida mkuu
Alimteua hajui hilo?

Au na yeye ni chawa wa Makonda?
 
Ulaji?
 
Yaani baada ya kumdhalilisha kiasi hicho ndiyo mnaanza kumpamba?? Maskini Makonda wa watu, pole yake!!


Ataficha wapi uso wake Makonda pale anapoona aliyokuwa anawafokea wanakula viapo vya kuwa mabosi zake??

Hakika Makonda angelikuiwa na uwezo angekataa udhalilishaji kwa kugomea uteuzi huu na kuhamia Burundi.
 
Hii ni ishara kuwa ccm haina sera Bali matukio. Badala ya kukisifia chama kwa sera zake, unasifia muhalifu aliye ndani ya chama!
 
Kwa sifa hizo asingeshushwa kutoka kule juu hadi huku chini atakapokemewa na Mwenezi Taifa atakapofanya ziara zake!
 
Unahangaika sana hebu taga tujue moja....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…