Makonda, Lukuvi pamoja na Kabudi waelekea ziarani Ngorongoro

Uzalendo wa Kitanzania

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2020
Posts
3,585
Reaction score
8,106
Wadau hamjamboni nyote?

Hatimaye Mawaziri Vigogo ya Serikali ya Rais Samia ambao ni Profesa Kabudi, William Lukuvi na Kamishna wa mafunzo Jeshi la polisi Awadhi wakutana na Paul Makonda na kufanya kikao kizito na Kamati ya Usalama ya Mkoa Arusha.
Your browser is not able to display this video.



Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi (kushoto), Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu William Lukuvi (kulia) pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Paul Makonda wakiwa katika picha ya pamoja walipowasili kwenye ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Karatu ambapo wakiwa wilayani humo leo Agosti 23, 2024 watafanya shughuli mbalimbali.

Soma Pia:
Viongozi hao ambao wameongozana na Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi nchini Awadhi Juma Haji, tayari wamekutana na Kamati ya Usalama ya mkoa wa Arusha. Viongozi hao wanatarajiwa kwenda Ngorongoro kuzungumza na wananchi wa Tarafa ya Ngorongoro.

 
Ndugu zangu Watanzania,

Hiyo ndio habari kuu inayoendelea kusambaa Nchini kwote na nje ya mipaka ya Tanzania .Ambapo Mwamba Mwenyewe na kijana jasiri kusini mwa jangwa la Sahara Mheshimiwa Paul Christian Makonda ataongoza msafara mzito wa mawaziri wazito na wasomi kwelikweli kuitembelea na kuzungumza na wananchi wa Ngorongoro.

Ambapo katika msafara huo yupo waziri wa katiba na sheria Mheshimiwa Profesa Palamagamba Kabudi. Huyu ni waziri na mhadhiri mstaafu wa chuo kikuu cha Dar es salaam kitivo cha sheri.ambaye amewahi kuweka rekodi ya Mwanafunzi bora kabisaa katika Historia ya Taifa letu na huo kikuu cha UDSM .

kwa kupata alama za juu sana katika sheria .narudi kusisitiza kuwa alama za juu katika sheria.maana ukienda katika uchumi yupo Mwamba Mwingine Profesa Ibrahim haluna Lipumba..

Lakini pia katika ziara hiyo yupo pia Waziri Mwingine wa muda mrefu sana na katika awamu tofauti tofauti na aliyekuwa mshauri wa Mheshimiwa Rais wetu mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan Mheshimiwa William Lukuvi.

Kwa hakika naamini kwa safu hiyo ya magwiji hawa basi wananchi wa Ngorongoro watapigwa Simo zuri mpaka wabakie wanabubujikwa machozi ya furaha bila kukatika utafikiri wamepakwa pilipili machoni.

Kikubwa endelea kubwa hapa hapa jukwaani na kuendelea kuwa karibu yangu ili kuendelea kupata habari motomoto kutoka huko Ngorongoro mkoani Arusha. Tarajieni hotuba nzito nzito kutoka kwa miamba na majabali haya zitakazo teka Nchi



Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
 
[emoji7]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
[emoji7][emoji7]

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Kuna jipya wanakuja nalo?
 
Kumbe naye kavaa samia kifuani. Njaa hizi kama vile hawatakufa
 
Lile sambwanda la Bashite limepungua sana kumbe kweli alikuwa mgonjwa
 
Lile sambwanda la Bashite limepungua sana kumbe kweli alikuwa mgonjwa
 
Hiyo imekaa safi
 
CCM wakukumbuke Lucas,unajitoa sana Mkuu!
Mwanzo nilikuwa nakuona chawa tu,ila consistency yako imenifanya niamini kuwa hii kwako ni DEDICATION.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…