Bob Manson
JF-Expert Member
- May 16, 2021
- 4,158
- 7,787
Imekuwa kawaida kwa Makonda wa mabasi ya safari za mbali kukaa au kusimama pembezoni mwa kioo cha mbele, wana nin'giniza sura zao bila kuzingatia usalama wao.
Dereva pamoja na abiria ni lazima wafunge mikanda, je Makonda nao wanachukua tahadhari gani katika kuzingatia usalama wao wakati wa safari?
Gari ikielekea kugonga obviously dereva anaitoa upande wake na kuelekeza upande wa kushoto ambapo Makonda husimama, ajali ndogo ya kugonga inaweza kuondoka na maisha ya konda pekee.
Jana basi la Mallesas limegonga lori kwa nyuma, binti mrembo ambaye alikuwa ni konda akapoteza maisha papo hapo.
Apumzike kwa amani na Makonda wengine wachukue tahadhari kama sio kubadili utaratibu wa kukaa karibu na kioo cha gari.
Dereva pamoja na abiria ni lazima wafunge mikanda, je Makonda nao wanachukua tahadhari gani katika kuzingatia usalama wao wakati wa safari?
Gari ikielekea kugonga obviously dereva anaitoa upande wake na kuelekeza upande wa kushoto ambapo Makonda husimama, ajali ndogo ya kugonga inaweza kuondoka na maisha ya konda pekee.
Jana basi la Mallesas limegonga lori kwa nyuma, binti mrembo ambaye alikuwa ni konda akapoteza maisha papo hapo.
Apumzike kwa amani na Makonda wengine wachukue tahadhari kama sio kubadili utaratibu wa kukaa karibu na kioo cha gari.