Makonda: Wanaume wafanyakazi wakatwe asilimia 40 ya mishahara yao wapewe wake zao

Muwe vichaa kisa jambo dogo hilo!! Kwani mnawezaje kuhudumia michepuko, bar nk na bado mkafanya hayo mengine uliyoorodhesha? Mbona mnakuza mambo ilihali hili linawezekana kabisa.
 
Kuna jamaa mmoja anauliza ina maana na yanga nayo ikatwe 40% iende kwa simba?au mpaka mwezi ujao
 
Hiyo 40% no kwenye salary hizi hizi za laki tatu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sheria yetu ya ndoa ni ya mwaka 1972 na sio ya India .


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Tena 40 ni ndogo sana inabidi iwe 60 kabisa.

Mpewe hela ya nini na wakati mnasema haki sawa?

Kwanini msi-fight na nyie muwe na mshahara wenu?

Hata angesema 2 bado agizo hilo lisinge tekelezwa
 
Wife amefoka Sana juu ya hii habari anahoji RC wa Dar ni nani hata aingilie mshahara wa Mr wake?
 
Ni kweli kuna baadhi ya vijidume kwale lakini mtwambie ninyi kina mama mnaomiliki uchumi kwenye familia zenu pesa zenu ninanufaishaje familia? Mbona mnaviteka vijana vidogo mnavionga na kuviambukia magonjwa gono? Kama ni sheria ikate pote maana fedha tunatafuta wote.
Upo sahihi mkuu wa mkoa wanaume pesa zao zinaishia kwa mchepuko na bar nakuwasahau wake na watoto wanateseka majumbani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Vipi kama mie namna mke wangu 60% before sheria? Hii Dhana ya wanawake kuteswa haipo kwenye kila ndoa! Ni mawazo Finyu sana hayo!
 
Kwani sheria ikipita inalenga Dar au nchi nzima. Sheria iandaliwe ila ikate pote hata wanawake wanaofanya kazi wakatwe wapewe wanaume %40 ili twende sawa. Vinginevyo wanawake waolewaji watahesabiwa na kabla ya ndoa itabidi mle mkataba wa kukataa sheria hiyo.
Sijui wanaume wa Dar mmemkosea nini bashite[emoji16][emoji16]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…