Makosa makubwa ya Muswada wa TISS

Makosa makubwa ya Muswada wa TISS

Vitu vingine ni kuelimishana tuu, sio kila kukamata na kupekua ni kwa ajili ya kutafuta ushahidi, yaani evidence, kazi ya hawa jamaa ni kutafuta tuu info, wakiishapata ushahidi, wanawaita wahusika kuendelea na mazagazaga yao!. Kila siku hawa jamaa, wanawadakua watu na wanadukua simu zetu, wanafungua barua zetu na vifurushi, wana intercept emails zetu, wanajivinjari kwenye banks accounts zetu na miamala yeti lakini, ukiondoa wale ma PW. X, Y na Z kwenye kesi ya uhaini ya 1982, uliishawahi kusikia wakisimama mahakama yoyote kutoa ushahidi wowote popote?.
Usiwe na wasiwasi kabisa na vipengele hivyo vina lengo zuri na jema la kuimarisha ulinzi na usalama.
P

Wako kisiasa zaidi, na kazi yao kubwa ni kuhakikisha ule msemo maarufu wa Makada wa CCM kuwa CCM itatawala milele. Ukishaona usalama wa taifa wanapatikana kwa kujuana basi ujue hapo hakuna usalama wa taifa, bali usalama wa viongozi.

Walichokifanya uchaguzi wa SM 2019 na uchaguzi mkuu 2020, ule ulikuwa ni ushahidi kuwa usalama wa taifa wako kwa ajili ya maslahi ya CCM. Hivi sasa wanapewa nguvu hiyo kisheria, na hawataruhusiwa kushitakiwa! Machafuko ama serikali kupinduliwa, ndio yataondoa hizi sheria zenye nia ovu ndani ya nchi hii.
 
Kama huwa wanafanya yote haya unayosema...vipi kuhusu wizi uliowekwa wazi kwenye ripoti ya CAG walikuwa wapi?
Usiwe na haraka!, ripoti ya CAG ni ripoti ya ukaguzi, hivyo matumizi yoyote ya fedha za umma ambazo hazikufuata taratibu, CAG anaripoti, hivyo sio lazima iwe ni wizi!. Subiria Bunge la November.
P
 
MAKOSA MAKUBWA YA MSWADA WA TISS

Sehemu ya 1.

Moja ya makosa ya mswada wa sheria ya Usalama wa Taifa, kipengele cha 5 cha mswada huo kinampa mamlaka Afisa usalama kukamata na kupekua viongozi, hapa Kifungu hicho kina kinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayosema kila mtu sawa mbele ya sheria, Kifungu kinaweka tabaka kwamba viongozi wa kitaifa hawatawajibika mbele ya sheria ya makosa ya jinai inayosimamiwa na jeshi la polisi, Viongozi wote watakuwa na sheria yao na chombo chao cha kuwakamata, kuwapekua na pengine wanaweza kuwa na mahakama zao.

Duniani kote Afisa usalama hafanyi kazi ambazo ni za wazi. Ukishamruhusu akamate na kupekuwa ni automatically umeamrisha afisa usalama huyo afike mbele ya mahakama kutoa ushahidi wa mtuhumiwa kama mkamataji na mpekuzi. Kazi hii iliwekwa kwa Idara ya upelelezi pekee na sio TISS.

Ajabu katika mswada huohuo, unajipinga katika kifungu cha 16 ambapo umeweka katazo la Afisa usalama kutotajwa wala kutojulikana popote yeye binafsi na kazi zake. Unajiuliza hivi hawa walipoweka kifungu cha Afisa usalama kukamata na kufanya upekuzi walijua hata onekana na kujulikana? Wanafahamu taratibu za ukamataji na upekuzi huanzia kwa Mwenyekiti/mjumbe wa mtaa/kitongoji na kisha mashahidi wa mtuhumiwa ndipo mtu apekuliwe? Je hapo afisa huyo atakuwa kafichwa utambulisho wake, sura yake au?

Mswada huu ni wa hovyo na haufai kabisa kupitishwa kuwa Sheria. Ukipitishwa kama ulivyo ni automatically hatutakuwa na Usalama wa Taifa, bali tutakuwa na Jeshi jipya lililochukua nafasi ya Idara ya Polisi ya upelelezi tu.

Dunia inapambana kufanya mageuzi Mashiriks ya Ujasusi yawe na mrengo wa kuhami uchumi, Lakini Serikali ya CCM imeleta mswada unaoirudisha TISS nyuma kuwa genge la kisiasa kulinda madaraka rasmi kutoka awali kuwa TISS ilifanya shughuli za kisiasa/kichama kinyemera, Sasa Rais Samia anairasmisha kuwa kikundi cha kulinda na kutetea madaraka ya kisiasa. Very sad!

Napendekeza kifungu hiki cha 5A kirekebishwe, TISS isihusike na ukamataji wala Upekuzi wa mtu yoyote katika nchi, isipokuwa ipewe idhini ya "kudhibiti" kwa mtindo wa elimination ama equity/excute katika eneo muhimu tu. Ukamataji na upekuzi ubakie kwa Idara ya upelelezi ambayo ndio itahusika na mambo ya Mahakamani pia. Kifungu cha 16 kirekebishwe, kimeweka mkazo sana katika kuficha utambulisho, dunia ya Teknolojia ni vigumu sana kwa maafisa kuficha utambulisho wake, badala yake kazi/Oparesheni ndio ziwekwe kwenye sheria ya kuzuia utambuzi wake.

Leo naomba niongelee juu ya contradiction ya vifungu hivi viwili cha 5A na 16 vya mswada huu, kati ya vifungu 27 vya marekebisho ya sheria ya Usalama wa taifa.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2641730View attachment 2641731View attachment 2641733
Si lazima kila afisa wa TISS asijulikane, wanaweza kuwa na idara iliyo wazi kwa makosa maalum na maafisa wakafika mahakamani kutoa ushahidi.

Hata nchi zilizoendelea kuna issue za kipolisi, zingine FBI na pia CIA! Sheria ni nzuri ila inataka kuangaliwa kwa kina kuepusha kuingiliana majukumu.
 
Vitu vingine ni kuelimishana tuu, sio kila kukamata na kupekua ni kwa ajili ya kutafuta ushahidi, yaani evidence, kazi ya hawa jamaa ni kutafuta tuu info, wakiishapata ushahidi, wanawaita wahusika kuendelea na mazagazaga yao!. Kila siku hawa jamaa, wanawadakua watu na wanadukua simu zetu, wanafungua barua zetu na vifurushi, wana intercept emails zetu, wanajivinjari kwenye banks accounts zetu na miamala yeti lakini, ukiondoa wale ma PW. X, Y na Z kwenye kesi ya uhaini ya 1982, uliishawahi kusikia wakisimama mahakama yoyote kutoa ushahidi wowote popote?.
Usiwe na wasiwasi kabisa na vipengele hivyo vina lengo zuri na jema la kuimarisha ulinzi na usalama.
P
Kuna tofauti kubwa. Kunusa kwa siri ni tofauti sana na kuwa na mamlaka kisheria ya kumkamata na kumpekua mtu.

Kwa mfano huyo afisa usalama ambaye sheria inataka utambulisho wake uwe siri akija kukukamata atajitambulisha?? Au atakuvamia tu kama jambazi na kukuteka?

Nini kitawazuia watu wenye nia ovu kujifanya ni ma 'afisa usalama' kisha wakawa wanateka na kuibia watu?

Utaratibu wa ukamataji watuhumiwa umewekwa sio tu kwa lengo la kulinda haki za mtuhumiwa, bali pia kuwalinda askari waonafanya ile kazi. Likija kundi la watu ambao hawajulikani kutaka kukuteka kama unao uwezo wa kujilinda unayo haki ya kuwamaliza kabisa kama alivyofanya Zakari. Lakini siku ile laiti wangeenda polisi wenye uniform bwana Zakaria asingethubutu kuwapiga risasi.
 
Kama wanaona jeshi la polisi halina ufanisi kwenye upelelezi na wanatamani kuwa na taasisi kama FBI basi ni afadhali waanzishe taasisi mpya ya kufanya kazi hizo pamoja na kulinda viongozi.
Ishu ni Ufanisi au kuuza taarifa wakati wa arrest au mwenendo wa uchunguzi?
 
MAKOSA MAKUBWA YA MSWADA WA TISS

Sehemu ya 1.

Moja ya makosa ya mswada wa sheria ya Usalama wa Taifa, kipengele cha 5 cha mswada huo kinampa mamlaka Afisa usalama kukamata na kupekua viongozi, hapa Kifungu hicho kina kinakinzana na Katiba ya Jamhuri ya Muungano inayosema kila mtu sawa mbele ya sheria, Kifungu kinaweka tabaka kwamba viongozi wa kitaifa hawatawajibika mbele ya sheria ya makosa ya jinai inayosimamiwa na jeshi la polisi, Viongozi wote watakuwa na sheria yao na chombo chao cha kuwakamata, kuwapekua na pengine wanaweza kuwa na mahakama zao.

Duniani kote Afisa usalama hafanyi kazi ambazo ni za wazi. Ukishamruhusu akamate na kupekuwa ni automatically umeamrisha afisa usalama huyo afike mbele ya mahakama kutoa ushahidi wa mtuhumiwa kama mkamataji na mpekuzi. Kazi hii iliwekwa kwa Idara ya upelelezi pekee na sio TISS.

Ajabu katika mswada huohuo, unajipinga katika kifungu cha 16 ambapo umeweka katazo la Afisa usalama kutotajwa wala kutojulikana popote yeye binafsi na kazi zake. Unajiuliza hivi hawa walipoweka kifungu cha Afisa usalama kukamata na kufanya upekuzi walijua hata onekana na kujulikana? Wanafahamu taratibu za ukamataji na upekuzi huanzia kwa Mwenyekiti/mjumbe wa mtaa/kitongoji na kisha mashahidi wa mtuhumiwa ndipo mtu apekuliwe? Je hapo afisa huyo atakuwa kafichwa utambulisho wake, sura yake au?

Mswada huu ni wa hovyo na haufai kabisa kupitishwa kuwa Sheria. Ukipitishwa kama ulivyo ni automatically hatutakuwa na Usalama wa Taifa, bali tutakuwa na Jeshi jipya lililochukua nafasi ya Idara ya Polisi ya upelelezi tu.

Dunia inapambana kufanya mageuzi Mashiriks ya Ujasusi yawe na mrengo wa kuhami uchumi, Lakini Serikali ya CCM imeleta mswada unaoirudisha TISS nyuma kuwa genge la kisiasa kulinda madaraka rasmi kutoka awali kuwa TISS ilifanya shughuli za kisiasa/kichama kinyemera, Sasa Rais Samia anairasmisha kuwa kikundi cha kulinda na kutetea madaraka ya kisiasa. Very sad!

Napendekeza kifungu hiki cha 5A kirekebishwe, TISS isihusike na ukamataji wala Upekuzi wa mtu yoyote katika nchi, isipokuwa ipewe idhini ya "kudhibiti" kwa mtindo wa elimination ama equity/excute katika eneo muhimu tu. Ukamataji na upekuzi ubakie kwa Idara ya upelelezi ambayo ndio itahusika na mambo ya Mahakamani pia. Kifungu cha 16 kirekebishwe, kimeweka mkazo sana katika kuficha utambulisho, dunia ya Teknolojia ni vigumu sana kwa maafisa kuficha utambulisho wake, badala yake kazi/Oparesheni ndio ziwekwe kwenye sheria ya kuzuia utambuzi wake.

Leo naomba niongelee juu ya contradiction ya vifungu hivi viwili cha 5A na 16 vya mswada huu, kati ya vifungu 27 vya marekebisho ya sheria ya Usalama wa taifa.

Na Yericko Nyerere
View attachment 2641730View attachment 2641731View attachment 2641733
Mkuu endelea kuwafunda ili wabadilike.
 
Naona unaamini kuwa watanzania wataendelea kuwa mazombie wa kudumu.
Tuna watu wa aina mbili, the wishful thinkers na the realists. Wishful thinkers ni wale wanao wish tuu!, hata the impossible, they'd wish. The realist ni wale wanadeal na the reality only. Mimi ni realist, hatuna Watanzania wa kuleta machafuko, wala Watanzania wa kupindua nchi!.
Keep on wishing!.
P
 
Back
Top Bottom