Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Makosa ndani ya Makala ya Mama Maria Nyerere Kutimiza Miaka 93

Historia yako yote imeegemea kwa Sykes na uislamu kana kwamba hii nchi ilikuwa ya kiislamu. Maandiko yako karibu yote sijaona ukitaja jitihada zilizofanywa na mtu mwenye jina la kikristo. Hao wazungu waliokuita ukafanye mhadhara vyuoni kwao hawawezi kujua mambo yote yanayohusu nchi yetu. Hata mimi nikitaka kuandika kitabu kwa kusikiliza stori za babu zangu ninaweza. Kuna mzee wangu anaishi Ilala alikuwepo siku ya sherehe za uhuru 1961 na huwa ana mambo mengi sana ya kusimulia. USILAZIMISHE SIMULIZI ZA WAZEE WAKO NDO ZIKAWA MSIMAMO WA NCHI.
Andika kitabu tujifunze na tuone historia ya uhuru wa Tanganyika.
Naamini huwezi na hutaweza. Wameshindwa wenzio wengi walioahidi kufanya hivyo.

Wenzio waliokuwa wanampinga Mzee Mohamed Said na wameshindwa hoja,
huu uzi wanaupitia kimyakimya. Wenzio walipinga kwa hoja nzito lakini
mwisho walikimbia.

Kusimamia batili ni kazi ngumu sana.
 
Historia yako yote imeegemea kwa Sykes na uislamu kana kwamba hii nchi ilikuwa ya kiislamu. Maandiko yako karibu yote sijaona ukitaja jitihada zilizofanywa na mtu mwenye jina la kikristo. Hao wazungu waliokuita ukafanye mhadhara vyuoni kwao hawawezi kujua mambo yote yanayohusu nchi yetu. Hata mimi nikitaka kuandika kitabu kwa kusikiliza stori za babu zangu ninaweza. Kuna mzee wangu anaishi Ilala alikuwepo siku ya sherehe za uhuru 1961 na huwa ana mambo mengi sana ya kusimulia. USILAZIMISHE SIMULIZI ZA WAZEE WAKO NDO ZIKAWA MSIMAMO WA NCHI.
Mama...
Nimeegemea kwa Sykes kwa sababu ndiyo walioasisi African Association 1929 kisha Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika 1933.

Naegemea kwao kwa kuwa ukimtoa Martin Kayamba ndiyo pekee walioandika historia ya nyakati zile kueleza mambo yalikuwaje.

Naegemea kwa Sykes kwa kuwa huwezi kuandika historia ya AA, TAA na TANU bila kusoma nyaraka zao.

Naegemea kwa Sykes kwa kuwa huwezi kumweleza Julius Nyerere katika harakati za TANU kama hujapita kwao.

Katika waasisi 17 walioasisi TANU wawili ni watoto wa Kleist Sykes muasisi wa AA.

Baba muasisi wa AA watoto waasisi wa TANU.

Ikiwa Uislam unakupa shida hilo litakuwa tatizo kubwa kwako kwa sababu Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika viongozi wake ni walewale waliokuwa wakiongoza AA - Kleist Sykes na Mzee bin Sudi na katika TANU wakawepo Ali Mwinyi Tambwe na Iddi Faiz Mafungo.

Mimi sina nguvu ya kulazimisha chochote.

Waliosoma kitabu changu ndiyo waliokifanya kitabu hiki kiwe juu na kutolewa matoleo manne.
 
Andika kitabu tujifunze na tuone historia ya uhuru wa Tanganyika.
Naamini huwezi na hutaweza. Wameshindwa wenzio wengi walioahidi kufanya hivyo.

Wenzio waliokuwa wanampinga Mzee Mohamed Said na wameshindwa hoja,
huu uzi wanaupitia kimyakimya. Wenzio walipinga kwa hoja nzito lakini
mwisho walikimbia.

Kusimamia batili ni kazi ngumu sana.
Hatuwezi wote tukawa waandishi ila haitunyimi nafasi ya kukosoa mtu anapotaka kupotosha umma.
 
Hatuwezi wote tukawa waandishi ila haitunyimi nafasi ya kukosoa mtu anapotaka kupotosha umma.
Mama...
Lakini unakosoa nini?
Kuwa mimi babu yangu Salum Abdallah yote aliyofanya katika kuongoza migomo mitatu (General Strike) 1947, 1949 na 1960 si kweli ni uongo; kuwa ni muasisi wa TANU si kweli, alikuwa kiongozi wa TRAU 1955 si kweli unakosoa nini?

Kuwa African Association ilianzishwa na babu zangu si kweli.
Kuwa baba na babu zangu waliakuwamo katika TAA na TANU si kweli.

Kuwa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika ilikuwa ndani ya AA si kweli, kuwa Abdul Sykes kadi yake no 3 si kweli kuwa kuwa kuwa...

Nini khasa hautaki kukisikia au ni cha uongo.

Kuwa Sheikh Hassan bin Ameir Mufti wa Tanganyika akizungumza na Abdul na Dossa na Nyerere ndani ya madrasa yake Mtaa wa Mvita ni uongo, kuwa alikuwa anauza kadi za TANU ndani ya misikiti si kweli.

Kuwa historia hii haikuwapo hadi Mohamed Said alipoiandika.
Nini khasa kinakutaabisha?

Kuwa unataka tuifute historia hii tubakie na ile ya zamani.
Nini khasa.
 
Nkanini,
Naamini kabisa mwandishi hakuwa na nia ya kupotosha historia yeye kaandika kama alivyopokea historia hiyo kutoka vyanzo.

Tofauti iliyopo kutoka vyanzo hivyo na historia niliyoandika mimi baada ya kuona makosa ya historia iliyokuwako ni kuwa mimi nimeiandika historia upya kutokana na kwanza Nyaraka za Sykes.

Hawa ndiyo waliokuwa na yote kuanzia mwanzo African Association ilipoundwa na baba yao 1929.

Watoto na wao wakawa ndani ya uongozi wa siasa za Tanganyika kuanzia 1947 baada ya WW II.

Na hawa watoto ndiyo wakaja kumpokea Julius Nyerere 1952 na wakawa nae Mwalimu akiwa Pugu anasomesha kisha wakaishi nae nyumbani kwao 1955 alipoacha kazi na kuwa mtumishi wa TANU.

Ilipoandikwa historia ya TANU na Chuo Kikuu Cha CCM Kivukoni akina Sykes hawakuhojiwa.

Huu ndiyo ukawa mwanzo wa kuwa na historia iliyokuwa haina ukweli.

Ally Sykes akanipa nyaraka alizokuwanazo kuhusu historia hii nami nikaandika kitabu ambacho wengi sasa mnakifahamu.
Imeina story imewaacha waislamu ndiyo maana ukaandika. Mzee huwezi kuwadangaya watu wote, Kwa miaka yote umekuwa unapromote waislamu ndiyo wenye Mchango pekee wa nchi hii! Lakini hakuna mtu aliyedhaminu historia hiyo maana hajabalance. Jipange upya
 
Hatuwezi wote tukawa waandishi ila haitunyimi nafasi ya kukosoa mtu anapotaka kupotosha umma.
Huna unachokosoa umejaa chuki tu.
Leteni ukweli hamna.

Kazi kulalamika tu. Anaandika waislamu tu, mlitaka aandike wasio kwenye historia ili abalance.

Historia ya uhuru hamuijui, mmelishwa matango pori kwa miaka mingi, eti mtu mmoja tu ndiye mpigania uhuru. Hakuna kitu kama hicho.

Wanatajwa wengine walioshiriki harakati za uhuru mnakasirika.

Tunashukuru sasa kizazi kimejua kuna wengine walioshiriki harakati za uhuru na si mtu mmoja.

Na kumbe watu walianza harakati kabla hajaja mjini.
 
Imeina story imewaacha waislamu ndiyo maana ukaandika. Mzee huwezi kuwadangaya watu wote, Kwa miaka yote umekuwa unapromote waislamu ndiyo wenye Mchango pekee wa nchi hii! Lakini hakuna mtu aliyedhaminu historia hiyo maana hajabalance. Jipange upya
Jesus,
Wakujipanga ni wewe.
Mimi nimeiandika historia ya TANU kama ilivyotakiwa.

Wewe sasa andika historia yako yenye balance.
 
Huna unachokosoa umejaa chuki tu.
Leteni ukweli hamna.

Kazi kulalamika tu. Anaandika waislamu tu, mlitaka aandike wasio kwenye historia ili abalance.

Historia ya uhuru hamuijui, mmelishwa matango pori kwa miaka mingi, eti mtu mmoja tu ndiye mpigania uhuru. Hakuna kitu kama hicho.

Wanatajwa wengine walioshiriki harakati za uhuru mnakasirika.

Tunashukuru sasa kizazi kimejua kuna wengine walioshiriki harakati za uhuru na si mtu mmoja.

Na kumbe watu walianza harakati kabla hajaja mjini.
Acha kutetea upuuzi. Au unalipwa na huyo mzee?
 
Anachofanya Mohamed Said kulazimisha "wazee wake" kuwa daraja moja sawa na Nyerere ni propoganda mbovu sana.
Historia yako yote imeegemea kwa Sykes na uislamu kana kwamba hii nchi ilikuwa ya kiislamu. Maandiko yako karibu yote sijaona ukitaja jitihada zilizofanywa na mtu mwenye jina la kikristo. Hao wazungu waliokuita ukafanye mhadhara vyuoni kwao hawawezi kujua mambo yote yanayohusu nchi yetu. Hata mimi nikitaka kuandika kitabu kwa kusikiliza stori za babu zangu ninaweza. Kuna mzee wangu anaishi Ilala alikuwepo siku ya sherehe za uhuru 1961 na huwa ana mambo mengi sana ya kusimulia. USILAZIMISHE SIMULIZI ZA WAZEE WAKO NDO ZIKAWA MSIMAMO WA NCHI.
 
Anachofanya Mohamed Said kulazimisha "wazee wake" kuwa daraja moja sawa na Nyerere ni propoganda mbovu sana.
Yoda,
Ningejaribu kutia uongo katika historia ya Mwalimu Nyerere leo nisingefika katika kiwango hiki cha kuaminika kuwa naijua vyema historia yake.

Abdul Sykes na Hamza Mwapachu ndiyo watu wa karibu sana na Mwalimu ns siwezi kusema walikuwa sawa na yeye.

Nitasemaje hivyo ilhali wao waliujua uwezo wake na wakampa uongozi wa TAA mwaka 1953?

Wewe kuwa mkweli na nionyeshe wapi haya yameelezwa au wapi Nyerere kawaadhimisha wazalendo hawa wawili katika maisha yake?

Nimeshirikishwa katika miradi mitatu ya kuandika historia ya Mwalimu: Kitabu cha Jim Bailey wa Afrika Kusini, Nyerere Biography ya Shivji na wenzake na mradi wa historia ya Magufuli.

Ushindi wangu katika kuijua historia ya Nyerere uko wazi.

Vitabu viwili vya historia ya TANU vilivyowafuta watu kama Hamza Mwapachu na Abdul Sykes kitabu cha CCM Kivukoni na kitabu cha Abubakar Olotu vyote vimekufa.

Kitabu changu cha maisha ya Abdul Sykes miaka 25 leo kila uchao kipo midomoni mwetu tunakijadili.

Si hayo tu nimekizungumza kitabu changu katika vyuo vingi hadharani na pia katika faragha na wasomi mabingwa wa historia ya Afrika.
 
Back
Top Bottom