Maktaba yapokea Vitabu Kutoka Songea, Ujerumani na Marekani

Maktaba yapokea Vitabu Kutoka Songea, Ujerumani na Marekani

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Nawashukuru ndugu zangu kupita kiasi.

Kila siku wananikumbuka na kuniletea vitabu ama wavitume au kuja wenyewe maktaba kwa miguu yao.

Abdulaziz Ali Khamis yeye anatoka Mombasa.
Mara kwa mara huja nitembelea Maktaba.

Safari hii alikuja Tanzania akafika hadi Songea kutembelea Makumbusho ya Vita Vya Maji Maji.

Hapo kuna duka la vitabu basi akaninunulia kizigo cha vitabu kaniletea.

Kitabu kilichogusa moyo wangu ni hicho nilichoshika kitabu cha Nduna Abdulrauf Songea Mbano kiongozi wa Wangoni.

Wanahistoria hupenda kumwita Songea Mbano wakaliacha jina la Abdulrauf.

Mimi hupenda kumwita kwa majina yake kamili: Nduna Abdulrauf Songea Mbano.

Alinyongwa na Wajerumani na kukata kichwa chake wakakipeleka Ujerumani.

Ndugu yangu Mohammed Abdulrahman, somo yangu na mwanaKariakoo mwenzangu nguli wa utangazaji sihitaji kumweleza sana.

Mohammed kapinda mgongo kaandika kitabu cha maisha yake.
Majuzi kanituliza.

Kanambia nitulie nikimalize kitabu kwani maswali ninayomvurumishia mbona yote majibu yamo kitabuni?

Nina wahka.
Nashindwa kutulia.

Mohammed ni kamusi kubwa ya historia ya kudai uhuru wa Ngazija.

Nilijua hili miaka michache iliyopita nilipoandika taazia ya rafiki yangu Salim Himidi aliyefariki Paris.

Aliniletea picha na maelezo mengi.

Katika kitabu hiki nina deni kubwa lazima In Shaa Allah nililipe.

Kitabu kinanidai pitio.

Bi. Zawadi Sakapala wa Mtoni Kijichi na Washington DC leo kaniletea mabuku makubwa matatu.

Naamini kabisa kwenye ndege mzigo huu wenye uzito wa nusu mfuko wa sementi umemgharimu.

Yote historia ya Marekani ya kale na leo. Namshukuru sana kupita kiasi.

Buku moja kaandika Peter Jennings nguli katika utangazaji Marekani, alikuwa Anchor wa ABC News.

Sasa ni marehemu.
Sapakala ni katika koo kubwa za Dar-es-Salaam ingawa hawavumi.

Lakini ukifika Mtoni Kijichi utawajua.

Wamejenga kituo kikubwa cha elimu kwa watoto wa Mtoni.

Huu ni mfano mkubwa wa kuigwa na wote ambao Allah kawaneemesha.

Ukoo wa Sakapala wamevunja nyumba moja ya baba yao kujenga kituo hicho na kila mwaka anakuja na timu ya wanaelimu kutoka Marekani kuja kujifunza historia na utamaduni wa Watanzania waishio Mtoni.

Hakika ndugu zangu wote hawa watatu wamenifurahisha nami namuomba Allah awafurahishe kama walivyonifurahisha mimi.

1730132465785.jpeg

1730132506083.jpeg
1730132539398.jpeg

1730132567770.jpeg

 
MAKTABA IMEPOKEA VITABU KUTOKA MAKUMBUSHO YA MAJIMAJI SONGEA, UJERUMANI KUTOKA KWA MTANGAZAJI NGULI MSTAAFU NA KUTOKA MAREKANI

Nawashukuru ndugu zangu kupita kiasi.

Kila siku wananikumbuka na kuniletea vitabu ama wavitume au kuja wenyewe maktaba kwa miguu yao.

Abdulaziz Ali Khamis yeye anatoka Mombasa.
Mara kwa mara huja nitembelea Maktaba.

Safari hii alikuja Tanzania akafika hadi Songea kutembelea Makumbusho ya Vita Vya Maji Maji.

Hapo kuna duka la vitabu basi akaninunulia kizigo cha vitabu kaniletea.

Kitabu kilichogusa moyo wangu ni hicho nilichoshika kitabu cha Nduna Abdulrauf Songea Mbano kiongozi wa Wangoni.

Wanahistoria hupenda kumwita Songea Mbano wakaliacha jina la Abdulrauf.

Mimi hupenda kumwita kwa majina yake kamili: Nduna Abdulrauf Songea Mbano.

Alinyongwa na Wajerumani na kukata kichwa chake wakakipeleka Ujerumani.

Ndugu yangu Mohammed Abdulrahman, somo yangu na mwanaKariakoo mwenzangu nguli wa utangazaji sihitaji kumweleza sana.

Mohammed kapinda mgongo kaandika kitabu cha maisha yake.
Majuzi kanituliza.

Kanambia nitulie nikimalize kitabu kwani maswali ninayomvurumishia mbona yote majibu yamo kitabuni?

Nina wahka.
Nashindwa kutulia.

Mohammed ni kamusi kubwa ya historia ya kudai uhuru wa Ngazija.

Nilijua hili miaka michache iliyopita nilipoandika taazia ya rafiki yangu Salim Himidi aliyefariki Paris.

Aliniletea picha na maelezo mengi.
Katika kitabu hiki nina deni kubwa lazima In Shaa Allah nililipe.

Kitabu kinanidai pitio.

Bi. Zawadi Sakapala wa Mtoni Kijichi na Washington DC leo kaniletea mabuku makubwa matatu.

Naamini kabisa kwenye ndege mzigo huu wenye uzito wa nusu mfuko wa sementi umemgharimu.

Yote historia ya Marekani ya kale na leo.
Namshukuru sana kupita kiasi.

Buku moja kaandika Peter Jennings nguli katika utangazaji Marekani, alikuwa Anchor wa ABC News.

Sasa ni marehemu.
Sapakala ni katika koo kubwa za Dar-es-Salaam ingawa hawavumi.

Lakini ukifika Mtoni Kijichi utawajua.
Wamejenga kituo kikubwa cha elimu kwa watoto wa Mtoni.

Huu ni mfano mkubwa wa kuigwa na wote ambao Allah kawaneemesha.

Ukoo wa Sakapala wamevunja nyumba moja ya baba yao kujenga kituo hicho na kila mwaka anakuja na timu ya wanaelimu kutoka Marekani kuja kujifunza historia na utamaduni wa Watanzania waishio Mtoni.

Hakika ndugu zangu wote hawa watatu wamenifurahisha nami namuomba Allah awafurahishe kama walivyonifurahisha mimi.

View attachment 3137478
Ikowapi hii maktaba walau nikitembelea bandari salama nifike
 
Sijui kama mwandishi Mohamed Said angekuwa kinyume chake anaandika historia ambayo ingewahusu wakristo au wasio waislamu kama mngekuwa na hizi kauli zenu mnazo zisema sasa

HIvi baadhi yenu humu huwa mnasoma historia au mnasoma huyu aliyeandikwa ni dini gani?

Mtakuwa watumwa wa fikra mbovu mpaka lini?
 
Mzee wangu Mohammed nikupongeze naona umri wako umesogea kiasi,unaweza kutushirikisha una miaka mingapi kwa sasa japo kufahamu tu?
 
Saint...
Nina miaka 72.
Mungu aendelee kukulinda mzee wangu.

Upo kwenye umri wa bonus nakuombea ujaaliwe kurithisha ufahamu wako kwa walio nyuma yako pia ukiwafundisha kuepuka biases za aina yoyote maana ardhi tunayoishi ni yetu sote ubaguzi au ujuaji wowote hautatufikisha mahali(hii statement unaweza usiielewe vizuri lakini usiichukulie kwa ubaya)
 
Mungu aendelee kukulinda mzee wangu.

Upo kwenye umri wa bonus nakuombea ujaaliwe kurithisha ufahamu wako kwa walio nyuma yako pia ukiwafundisha kuepuka biases za aina yoyote maana ardhi tunayoishi ni yetu sote ubaguzi au ujuaji wowote hautatufikisha mahali(hii statement unaweza usiielewe vizuri lakini usiichukulie kwa ubaya)
Saint...
Nakuelewa vizuri sana kuhusu ubaguzi.

Huo ubaguzi nimeishinao maishani kote.

Kuhusu kufundisha utu.

Nimeandika kitabu kizima kueleza historia ya wazee wangu walivyopigania uhuru wa Tanganyika wakiwa mstari wa mbele na wema walioonyesha kwa wageni kutoka nje ya Dar es Salaam waliojiunga na harakati za uhuru.

Ama kuhusu ujuaji au kinyume chake ningeoenda kukufahamisha kuwa hapa JF nimechaguliwa Mwandishi Bora miaka miwili mfululizo.
 
Ungetumia lugha ya kawaida ingependeza sana.
Hata mimi nakubali kabisà kwamba leñgo la uzi huu ni muendelezo wa udini wa Mohammed Said.
Absolutely hapo akikaa siku kadha atakuja na mada ya mkwawa kuitwa abdallah hapohapo akilalama kwanini jina hilo halitajwi..

Mara alifundishwa kiarabu na abushiri wa pangani...
Atakaa siku mbili ataleta stori ya abushiri kwamba hakuwa muuza watumwa kwa kuwa tu alikuwa muislamu.
 
Absolutely hapo akikaa siku kadha atakuja na mada ya mkwawa kuitwa abdallah hapohapo akilalama kwanini jina hilo halitajwi..

Mara alifundishwa kiarabu na abushiri wa pangani...
Atakaa siku mbili ataleta stori ya abushiri kwamba hakuwa muuza watumwa kwa kuwa tu alikuwa muislamu.
Inside...
Kwani hairuhusiwi kuandika hayo hapo?

Tujaalie mada hizi wewe huzipendi.
Tatizo liko wapi?

Unachotakiwa kufanya ni kuacha kuzisoma.

Wako wanaopenda kusoma kalamu yangu.

Kunibughudhu mimi kwa kuandika nikipendacho huo si uungwana.
 
Na hiko kitu cha songea kutojumuishwa kwa jina lake la uislamu huwa linamkera sana mzee MS mara anyingi amepata kulalama.
🤣
Inside...
Hapana sikereki.
Wala silalami.

Ningekuwa mtu wa kulalama.
Nisingesomwa.

Wewe ndiye unalalama.
 
Inside...
Kwani hairuhusiwi kuandika hayo hapo?

Tujaalie mada hizi wewe huzipendi.
Tatizo liko wapi?

Unachotakiwa kufanya ni kuacha kuzisoma.

Wako wanaopenda kusoma kalamu yangu.

Kunibughudhu mimi kwa kuandika nikipendacho huo si uungwana.
Nisamehe kwakukwanza..
Shida sio kuandika nikutanguliza uislamu kwenye historia zako.
 
Lengo la uzii kuonyesha kuwa mbano songea alikuwa mvaa kobazi
Hao ndio wapigania uhuru, una enjoy Leo uhuru wa kuandika JF kuwakejeli sababu walisimama imara na kumwaga damu yao Ili mwafrika awe huru na aheshimike.
Walio batizwa wao walizibwa macho na walikua na mkoloni
 
Back
Top Bottom