52.
ARI lake la kuiba lingeweza kumpeleka popote. Usiku kwake ulikuwa bado mchanga sana na alikuwa na mengi ya kufanya. Sasa angependa kufanya safari ya kumtafuta Nuru na kumtoa katika mikono ya binadamu hao wenye kiu kali ya damu. Lakini alisita kulifanya. Hakuwa na shaka zaidi mateso na majeraha ya hapa na pale Nuru yuko hai na salama. Vinginevyo angekwishapokea furushi la kichwa chake badala ya kidole. Zaidi ya hayo, Joram alikuwa na hakika kuwa maadamu majambazi hayo yalikuwa na Nuru katika himaya yao, yalikuwa na hakika kuwa Joram asingethubutu kwenda kinyume cha maagizo yao. Hivyo, alijiona kuwa alikuwa katika nafasi nzuri ya kwenda atokako na kufanya atakalo katika upelelezi wake. Lakini angekwenda wapi zaidi? Alijiuliza kwa masikitiko. Kama kumwona kwake Waziri kulimwongezea chochote katika uchunguzi wake, basi nyongeza hiyo haikuwa zaidi ya kitu kama kumimina sukari katika bakuli la mboga kwani alichanganyikiwa zaidi. Kwanza, alimwona kwa urahisi zaidi ya alivyotegemea; jambo ambalo, licha ya kushangaza lilimchukiza. Alitegemea kumwona kwa taabu, kama anayeonana na kifo; huku risasi zikimkosakosa. Si kwa ajili ya Waziri Mkuu huyu ambako kulifanya msichana wa watu Betty, auawe kinyama? Si kumwona Waziri huyuhuyu ambako kumeyahatarisha maisha ya dereva asiye hatia. Si
kwa ajili yake huyuhuyu ambako sasa hivi kunamfanya Nuru awe mikononi mwa mauti, tayari kufa wakati wowote? Sio Waziri huyu?...siye?
Na kama ndiye basi imekuwa rahisi kumwona! vipi kuonana naye imekuwa kama kumwona mtu yeyote wa kawaida, si mtu ambaye mauaji ya kutisha yanatokea kwa ajili yake? Na vipi maongezi yake yamekuwa ya kawaida kiasi hicho, sauti yake ikiwa haina dalili yoyote ya hofu wala hatia kwa yote aliyosimuliwa? Zaidi, vipi Waziri huyo aonyeshe kushangaa kwa maelezo ya Joram. Au ni mwigizaji mwingine mzuri?
Kisha, Joram alikumbuka kitu kingine alichokipata katika macho na sauti ya Shubiri. Naam, kulikuwa na kitu zaidi ya mshangao, kitu kama huruma. Shubiri alikuwa kama anayemhurumia Joram zaidi ya anavyojihurumia mwenyewe. Kwa nini? Au angesema mengi iwapo kisingetokea kile kifo cha uzee cha mwalimu Puta?
Maswali yaliongezeka kila dakika, majibu yakiwa ndoto iliyokuwa mbali mno na kichwa chake. Kitu pekee alichokuwa na jibu lake ni kwamba mkasa huo ulimvutia katika kiza kizito zaidi, kinachotisha na kutatanisha.
Laiti ingekuwa hadithi tu, au ndoto, aamke kesho na kujikuta yuko Tanzania, katika chumba chake kilekile chenye kunguni na mbu. Lakini haikuwa ndoto. Alikuwa macho na akishuhudia au kujihusisha na vifo vya kikatili. Watu walikuwa wakiteketea. Nchi ilikuwa mashakani. Nuru alikuwa mikononi mwa mauti. Kisa na mkasa?
Wakati msongamano huo wa mawazo ukikisumbua kichwa chake, Joram alikuwa amekiacha kijiji kitambo na kuingia mjini. Tena, tamaa ilimshika ikimshawishi ageuze gari na kuelekea huko ambako aliamini angeweza kumkuta Nuru, amtoe mikononi mwa wauaji hao kwa gharama yoyote. Lakini roho nyingine ilimshikashika ikimtaka aiharishe safari hiyo na kusubiri wakati unaostahili. Hivyo, akalielekeza gari hotelini kwake. Akaliacha mtaa wa pili na kwenda hotelini kwa miguu.
Mapokezi alipewa karatasi yenye maagizo yaleyale; piga namba ileile mara ufikapo pamoja na kifurushi kingine kidogo. Ndani ya lifti alifungua kifurushi hicho. Mlikuwa na kidole kingine. Hakujishughulisha kukitazama kwa makini. Badala yake aliingia nacho hadi chumbani mwake ambamo alikitupia
mezani na kuwasha taa. Alipoyatupa macho yake kitandani hakuweza kuamini.
Juu ya kitanda hicho alilala mwanamke. Shuka laini alizojifunika hazikufaulu kufanya siri kuwa mwanamke huyo alikuwa kama alivyozaliwa. Mwili wake ulipendeza na kuvutia sana katika shuka hizo.
Hakuwa Nuru. Hilo Joram alikuwa na hakika nalo. Mwanamke huyu ni nani basi na aliingiaje katika chumba hiki ambacho kilikuwa kimefungwa? Na hasa anataka nini? Joram alimtazama kwa muda. Akasogea na kujiketisha juu ya kitanda taratibu. Kwa utulivu huohuo aliivuta shuka toka usoni mwa mgeni huyo na kumtazama. Alikuwa mwanamke wa makamo. Lakini uzuri ulikuwa wazi katika sura hiyo japo macho yalifumbwa. Nywele ndefu laini, nyusi nyingi nyeusi, pua pana iliyonyooka na kinywa kidogo cha kuvutia vilikuwa dalili tosha ya uzuri wa umbile la mwanamke huyo aliyelala kwa utulivu kama yuko kwake.
Joram alikuwa na hakika kuwa mtu huyo yuko macho. Alikuwa na hakika pia kuwa kuna jambo zaidi ya jambo ambalo lilimleta. Hakuonekana kuwa na haraka. Hivyo, Joram aliamua kumpa muda wote anaoutaka kwa kutomwamsha. Badala yake aliinuka taratibu kukiendea kitanda cha pili ili alale.
“Usinikimbie Joram,” sauti ya kike ikanong’ona ghafla.
Joram akageuka kumtazama.
Msemaji alikuwa akitabasamu alipoongeza, “Au naonekana mzee sana kwako?”
***
“Naonekana mzee?” aliuliza tena. Sasa alikuwa amekiacha kitanda chake na kusimama kama alivyozaliwa, akiyaruhusu macho ya Joram kutalii juu ya umbo lake. Alikuwa katika kila hali ya kujiamini, kwamba Joram asingekosa kuridhika na anachokiona. Na alikuwa na kila haki ya kujiamini kwani umri ulikuwa haujadokoa chochote cha haja katika umbo lake. Zaidi ya idadi ya miaka, bado alikuwa msichana. Matiti yake mekundu, laini yanayomeremeta yalikita kifuani kama yanayoshindana na wakati. Kiuno chake chembamba kilichokatika kama kinavyostahili kilikuwa daraja zuri lililounga umbo hilo na mapaja laini ambayo yalimeremeta kwa wekundu. Uzuri huo ulikamilishwa na sura nzuri ya kupendeza, yenye macho ya
kuvutia na kinywa cha kusisimua, kinywa kilichobeba tabasamu ambalo lilipendeza zadi kwa jinsi lilivyokuwa mchanganyiko wa haya, kushawishi na kubembeleza pamoja. Hata sauti yake sasa ilikuwa yenye haiba aliponong’ona, “Kama nimekuudhi…”
Joram hakuyasikia yote. Rohoni alikuwa akitaabika kwa kutiana mieleka na shetani wake ambaye alimtaka ainue mkono na kuugusa mwili huo ambao ulikuwa umejitunuku kwake. Alimtazama mama huyo kwa makini zaidi kwa nia ya kumtia aibu avae, aondoke zake. Lakini haikuwa hivyo. Kinyume chake, Joram alijikuta akizidiwa na tamaa kiasi cha kujikuta akijihurumia zaidi ya alivyokuwa akimhurumia mwanamama huyo. Kisha, Joram alikumbuka jambo. Alikumbuka kuwa alipata kumwona huko mbeleni mama huyo mzuri. Wapi vile? Wapi?
Asingeweza kukumbuka kikamilifu. Akili yake ilikuwa haifanyi kazi kikamilifu. Baadhi ya shurubu zilikuwa zikichezacheza huku nyingine zikikaza kuliko inavyostahili. Hata hakuiamini sauti yake alipouliza, “Kama nimepata kukuona mahala!”
Tabasamu la mama huyo lilipata nguvu zaidi. “Ndiyo,” alijibu akizidi kumsogelea Joram na kuketi kando yake. “Lakini, ya nini?” Aliuliza akiuchukua mkono wa Joram na kuanza kuchezea vidole. “Tuna usiku mrefu sana mbele yetu,” aliongeza taratibu. “Hadi kesho tutakuwa tumefahamiana vya kutosha.” Alikuwa havichezei tena ila kunyonya vidole vya Joram. “Uwe mwanangu mzuri,” sauti yake iliendelea kunong’ona kama kinanda.
Na sasa alikuwa amelishika titi lake na kumnyonyesha Joram. Lilikuwa zito, lililojaa, lenye uhai na joto, titi zuri, la mwanamke mzuri. Joram ni mwanaume shujaa. Lakini ni mwanaume kwanza, shujaa baadaye. Alikuwa na kila chembe ya udhaifu wa kiume. Yawezekana hali hiyo ilisababishwa na kutokuwepo mpenzi wake Nuru? Kwani muda si mrefu alijikuta akishuhudia mavazi yake yakitolewa moja baada ya jingine… alitaabika mikono hiyo laini ilipoanza kuteleza juu ya mwili wake katika kila kichochoro ambacho kilihifadhi faraja iliyoburudisha mwili na kuifariji roho… aliteseka zaidi mikono hiyo ilipoacha kazi hiyo na kinywa kuichukua, kililamba hapa, kunyonya pale na kuonja huku. Kisha…
“Wewe… wewe nani?...” Joram aliuliza kidhaifu. “Baadaye…”
“…Ndiyo… Baadaye.” alijibu akiushuhudia mkono wake mmoja, bila hiari yake, ukiuacha mwili wake na kusafiri hadi katika mwili wa mwanamke huyo, ukitomasa hapa na kupapasa pale. Mkono wa pili ulimtoroka na kusaidia kazi hiyo. Ni hapo lilipotokea jambo ambalo Joram hakulitegemea. Mwanamke huyo aliacha ghafla kufanya alichokuwa akifanya mwilini mwake na kutulia mara tu mguso wa Joram ulipomkolea. Kisha, ghafla mwili huo uliokuwa mtulivu ulianza kutetemeka kwa nguvu, huku akiangua kilio chembamba kwa sauti laini, machozi mengi yakimmiminika.
Kwanza, Joram hakuelewa. Alisita chochote alichokuwa akiutendea mwili wa mwanamke huyo na kumkazia macho ya mshangao. ‘Anakufa?’ alijiuliza. Kisha alielewa. Pamoja na orodha yake ndefu ya wanawake mbalimbali, wenye tabia mbalimbali kitandani huyu alikuwa mwanamke wake wa kwanza ambaye mahaba yangeweza kumwua. Alikuwa na njaa au kiu kubwa ya mahaba, kama mtu ambaye ameokotwa katikati ya jangwa baada ya siku nyingi ya ukosefu wa maji na chakula. Hayo Joram aliyafahamu baada ya kuisikia sauti yake dhaifu ikinong’ona, “Endelea…” mara alipoduwaa.
Aliendelea. Na ilikuwa safari ya kihistoria. Paa lingeweza kufunuka kwa kelele. Kitanda kingeweza kugeuka bahari kwa machozi… lakini aliendelea. Ni baada ya muda mrefu sana, ndipo waliachana lakini bado walikuwa wamekumbatiana.
Joram aliuiba mkono wake mmoja na kuutumia kuvuta kijimeza chenye sigara zake. Akauiba mkono wa pili na kujiwashia sigara moja. Alivuta huku akifikiri. Fikara zake zilikuwa nyingi, za kutatanisha na zilimhusu mwanamke huyo aliyelala ubavuni mwake. Hakuhitaji tena kumwuliza kuwa ni nani. Saa chache walizosumbuana kitandani zilifanya agundue kuwa huyo ni mke wa Abdul Shangwe, Rais wa nchi. Kitandani na mke wa Rais wa nchi! Hilo lilimtisha Joram, lakini halikumsumbua sana. Alijua kuwa mwanamke huyo alikuwa na yake, angeyajua kitambo si kirefu. Ambalo lilimsumbua Joram ni jinsi mwanamke huyo, pindi wakifanya mapenzi alivyosahau kuwa yuko na Joram Kiango, badala yake bila ya kujifahamu alilia “…Shubiri ….Shubiri…” sauti hii haikuwa ya hila. Ilitamkwa kimapenzi kabisa, toka katikati ya fungate la moyo wa mwanamke anayempenda. Ni hilo lililomtatanisha Joram. Alikuwa na kila hakika kuwa Shubiri
anayetajwa si mwingine zaidi ya Shubiri Makinda, Waziri Mkuu. Kwamba kuna mapenzi mazito kiasi hiki, baina ya mwanamke huyu na Shubiri, hilo Joram hakulitegemea. Pamoja na upelelezi wake mgumu, pamoja na vifo vya watu wengi, pamoja na marehemu mmoja kufa baada tu ya kutoa siri ya mapenzi haya bado Joram alikuwa na mashakamashaka juu ya ukweli wa suala hilo, mashaka ambayo yalianza kukamilika usiku huu baada ya kuonana na Shubiri ana kwa ana na kumwona alivyoyapuuza maswali yake yote. Ni hapo Joram alipoanza kushuku kuwa kuna jambo jingine zaidi ya mapenzi na tamaa ya vyeo katika mkasa huu. Lakini sasa mashaka hayo yalielekea kusambaratika tena na kumwacha palepale alipokuwa, katika lindi la bahari ya kutatanisha, yenye kiza na mashaka kwani mapenzi yalikuwa wazi katika macho na sauti ya mwanamke huyu. Mapenzi halisi. Au anaigiza? Aweza kuwa mwigizaji mzuri kiasi hicho? Naye Joram amekuwa kipofu na kiziwi kiasi gani hata ashindwe kuona nuru ya mapenzi halisi katika macho na tetemo la huba katika sauti ya mwanamke huyu? La. Lazima liko
jambo zaidi ya jambo.
Akanyoosha mkono na kupapasa titi lililoshiba, ambalo lilikuwa wazi likimtazama kama linalomdhihaki. Mtoto wa kike aliamka. Akafumbua macho na kuachia miayo mirefu. Kisha, alimtazama Joram. Tabasamu likaumeza ghafla moyo wake, tabasamu refu, pana, ambalo lilisema yote ambayo mwili wake ulipenda kusema. Yote, ingawa yalijumuishwa katika neno moja tu “Ahsante.” Naam, kuridhika kulikuwa wazi katika macho yake, kutosheka kukiwa dhahiri katika sauti yake alipoongeza kwa mnong’ono, “Sikujua, kumbe nimekuwa nikiusumbua bure mwili wangu katika kitanda cha mwanaume ambaye hajui thamani ya mwili wa mwanamke. Nusu ya maisha yangu imepotea bure kabisa. Damu ya ujana wangu imekauka bila thamani. Kama ningejua!”
Joram alimtazama. Macho yake maangavu, japo hayakudhihirisha hasira wala furaha, yalimfanya mama huyu akose raha na kunong’ona kitu kama “Samahani” ingawa Joram hakumsikia vizuri.
“Ulifikiri unafanya nini kujipenyeza chumbani humu kwa siri na kunisubiri uchi kitandani?” aliuliza. Mwanamke huyo alipochelewa kujibu Joram aliongeza, “Na unadhani ni heshima
kwa mke wa Rais wa nchi kubwa kama hii kujiuza kwa bei rahisi kiasi hicho?” mama huyo alipofunua mdomo wake kujibu Joram alimkatiza tena. “Usijisumbue kunidanganya. Naifahamu tabia ya wanawake wa aina yako. Umalaya na uongo ni mchezo wenu wa kawaida.”
Haja yake ilikuwa kumtia hasira na aibu. Kumpokonya ushujaa ambao alikuwa nao kwani Joram alikuwa na kila hakika kuwa tamaa ya mwili lisingekuwa jambo pekee lililomleta chumbani humo. Alikuwa mjumbe. Mjumbe wa nani? Ni hilo alilotaka kulifahamu. Ni hilo lililomfanya amruhusu mwanamke huyo kumchezea kimwili, ili apate siri. Hawakusema kuwa kitanda hakina siri?
“Nadhani huna haki ya kuniita malaya mapema kiasi hicho,” mwanamke alisema. “Kuwa mke wa Rais hakunifanyi kuwa mwanamke, mwenye kila udhaifu wa kike.” Alisita kwa muda. Halafu akaendelea, “Ningeomba uelewe kuwa niko hapa kwa ajili ya kuiokoa roho yako. Sikuwa na njia nyingine zaidi ya kujifanya mwanamke malaya na kumhonga mhudumu mmoja ili aniruhusu kukusubiri chumbani humu.”
“Mume wako…”
“Hana habari. Yuko nje ya nchi. Hukusoma gazeti la jana? Ameenda Ethiopia kuudhuria mkutano wa viongozi wa nchi huru. Nadhani atarudi leo.”
“Walinzi wako…”
“Kwao, sasa hivi niko nyumbani, chumbani kwangu; nikimsubiri mume wangu. Hakuna anayejua kuwa nilitumia mlango wa siri hadi nje ambako nilikodi gari iliyonileta hapa.”
“Na ni kipi kilichokuleta?” “Kuyaokoa maisha yako…” “Ongea kwa tuo, tafadhali.”
Mwanamke alimtazama Joram kwa utulivu. Kisha akatabasamu. “Kijana mzuri,” alisema. “Kwanza umejuaje kuwa mimi ni mke wa Rais?” aliuliza.
“Kwa jinsi unavyotapatapa kitandani kama samaki anayekaangwa hai,” Joram aliamua kumtusi tena. “Hakuna ambaye angeshindwa kufahamu.”
Kwa mshangao wake Joram hilo pia halikumkera mwanamke huyo. Ndio kwanza alicheka na na kusema, “Hujui. Usiku wa leo umekuwa wa aina yake katika maisha yangu. Sikutegemea…”