Malezi: Mambo 20 ambayo hutakiwi kumwambia mtoto wako

Malezi: Mambo 20 ambayo hutakiwi kumwambia mtoto wako

Kati ya Joyce Mkuya na Konyagi ni nani alimwangusha mh Mbowe?
 
Tumeambiwa sana ujinga na bado tumetoka fureshiii tu, endeleeni kuiga kwenye tamthilia.
 
  • Thanks
Reactions: BRB
Namba 5 napinga.

Hiyo unaweza kumuharibu mtoto au akawa anaharibika bila wewe kujua au kwa kujua kisha ukamuacha.
 
Hapo point kubwa ni kutomtusi mtoto tu. Hayo mengine yanafuatana na mazingira.

Mf. Kuna tatizo gani kumwambia mtoto "niache nipumzike?" Au katoto kamevaa sketi unakaambia "wavulana hawafanyi/hawavai hivyo?'
 
Naona sasa humu ndani mmeanza kuvuka mipaka hadi mnatufundisha jinsi ya kulea eehhhh....
 
Namba moja mpaka ishirini asiambiwe lolote,litakuwa toy lisilukuwa na betri na siyo mtoto.
 
Hiyo namba 5 hiyo utawapoteza watu.

Huo utaratibu wa kuwalea watoto open minded kwamba wakikua watakuja kuchagua wanataka kuwa nani utajikuta umekuza wa kina delicious.
 
Mimi baba yangu alikua bandidu balaa.

Nakumbuka nilikua msingi kila nikimletea report home niko wa kwanza darasani baasi akawa ananifokea balaa. Ananiambia sio unafikiri kuwa wa kwanza ni issue hakuna atakae kusifia hapa unatakiwa ukaze buti uendelee kuwa hapo maana hiyo ni kazi kubwa. Baasi mpaka nilikua nalia yaani nasema huyu mzee vipi badala afurahi ananigombeza.

Sema baadae ananinunulia soda na kuku baasi maneno yake yoote ya shombo natupa kule naji noma vitu vizuri.

Mpaka sasa hivi ana principle yake moja kwamba mtoto wa kiswahili usimuonyeshe jino. Yaani usimchekee. Dah hili kwa kweli alilitekeleza maisha yetu karibia yote ya utoto. Yaani baba atacheka na wenzake tukiingia tu sisi anaweka wa mbuzi. Kakunja uso. hahahahaha.

Hizi principle zake bhana kijeshi sana na nimeshindwa kabisa kuzi implement kwa mwanangu. Ujeshi mwingi sana aisee, Japo mwanangu akifanya kosa kichapo cha mbwa koko kinamuhusu then baada ya hapo tunacheza kama watoto vile.
Sifa kubwa ya mtoto kutokuwa na dukuduku moyoni,mtoto abebi mambo moyoni na pia sifa nyngne ya watoto hawabaguani hata ukisema usicheze na yule hatokuelewa tuishi kwa upendo na kuwajali watoto
 
Hiyo namba 15, wazazi wengi hawajui kuwa watoto hawabaguani hata siku moja sifa kuu ya watoto kupendana hata ukipandikiza chuki utafeli ww
 
Najaribu kuwaza nisingeadhibiwa na wazazi wangu pale ninapokosea sijui ningekuwa kwenye mazingira gani.nahisi ningekosa adabu kwa kiwango kikubwa mno.

Watoto wangu watakapofanya makosa,adhabu lazima iwepo 💯.nitakuwa Rafik yao sana lakini wakileta uzembe watachezea mikwaju.

Hiyo ya kusema ngoja baba yako aje!😅😅nahisi haitokuja kutoka kinywani kwangu hata siku moja(nafikiri ni kwa sababu na mimi sikuwahi kuisikia ikitoka kinywani mwa mama yangu).

Mtoto ukimlegezea sana anakuja kukuaibisha aiseh.mlee vizuri,mpatie anachostahili kwa wakati husika.
 
Back
Top Bottom