Malezi...Step Parenting.


...hapo sasa, halafu eti baba mzazi anamkurupua ex-wife wake kwanini mtoto kaenda outing na 'uncle' wake!
Mke/mtoto ana kosa gani kuendelea na maisha yao?
 

Nimependa saana hayo maelezo hapo juu Mbu... for yanakubaliana na haya nilogusia mwanzoni kwenye post yangu ya kwanza.... Observe....





Hilo nakubaliana nawe kabisa na it is the most logical way of handling it... However Mbu wazazi nao hupishana, wewe mpaka ukaongea hivo it means you are a very responsible parent (or will be) na una ile ya misingi ya kua a child is better brought up by the biological parents... which is true and very good perspective.. Lakini bahati mbaya wazazi wengine mki achana kaachana na watoto pia, anaenda huko na kuanza a new family au hata kutelekeza - this i have learned at first hand.... Hivo basi kama you are a good parent siio mbaya ukawa a parent hata kwa huyo step kid ambae mara nyingi huitaji presense ya baba (ambae yuko mbali na hana habari) - hivo in one way or another filling the gap....
 
Reactions: Mbu


Mbu mh kuna scenerio nyingine ni ngumu kidogo kwa Current spouse kuingilia bana........Mfano mie najua Ex-wangu hatoi matunzo lakini kila kukicha aja na visharti vya kumpeleka mtoto shule zenye majina na accounts ambazo mwisho wa siku jukumu lote linaangukia kwangu, afu we uje useme ni haki ya mtoto au ya Ex kwa kuwa analazimik kuingia katika maisha yangu by default......hapana
 

...hapo sasa, halafu eti baba mzazi anamkurupua ex-wife wake kwanini mtoto kaenda outing na 'uncle' wake!
Mke/mtoto ana kosa gani kuendelea na maisha yao?


Mzazi ambae yupo genuine hawezi chukia mtoto wake akienda na uncle wake (hasa kama imehalalishwa) for ataelewa kua mtoto needs some balance na breathing space ya hio divorce amepitia, na pia kua mtoto hatakiwi kabisa ku smell any hint of hate between the parents and step parent... Yaani wivu tu ndo yaweza fanya hayo ulosema yatokee...
 
Reactions: Mbu

...lol...mwaj1 sio hivyo darling, pheewwww,...hebu kunywa glass ya maji baridi kwanza, leo hawakuzima umeme dahhh...
Nazungumzia kushirikishwa kwenye maamuzi bana. Maana hata hiyo ya kuhimiza mtoto apelekwe IST ilhali mie naona anamnyanyasa mamsapu, si itabidi nimwite tukae kitako tuongee kiume?

Haiwezekani sie bajeti yetu ni ya Bunge Primary, halafu yeye aje na mikwara eti mtoto asiposoma IST apelekwe Academy! ala? Kama atamsomesha haya, lakini sio kutoa amri kisha zigo la ada na malezi anawatupia wengine. Bila kumshirikisha unampa mwanya wa kuja na zile za 'Oooh,...kama hamuwezi kumsomesha kwanini msingeniambia niwasaidie ada!'...
I hope umenielewa.
 


Akhsante....
 
Reactions: Mbu

...kuhalalishwa vipi tena naye keshamuacha mke bana?...'asokuwapo na lake halipo!'
yaani mimi leo wanangu waende Outing na Boyfriend/fiancee wa mama yao basi nihamaki? Busara gani hiyo...lol!

Akhsante....

dahhh,...akhsante ya nini sasa na wewe..lol...yani umeona maneno ya Mwj1 kamili 100%?
Topik ya Msukule mshaisahau nyie,...hawa Ex-Spouses wanakausumbufu sana kwenye masuala ya mtoto/watoto
inabidi kwenda nao hivyo hivyo...'unauma huku unapuliza!'
 
...kuhalalishwa vipi tena naye keshamuacha mke bana?...'asokuwapo na lake halipo!'
yaani mimi leo wanangu waende Outing na Boyfriend/fiancee wa mama yao basi nihamaki? Busara gani hiyo...lol!


Mbu hicho kitu cha kuangalia saana sema tu wazazi wengi hupuuzia...
Haipendezi kabisa kuonesha wanao your boyfriend/lover kama you are
not yet sure about the relationship... believe me you.... mpaka pale you
know you have a future then the kids can be involved - for waweza ishia
kua in a few years ume wa introduce to more than four of your lovers...
Not healthy for the child(ren), na hata ile heshima kwa watoto plus morals...



I never forget rich insightful threads... na ile Msukule is one of my favourites....
Maneno ya MJ1 haitakiwi hata nitie neno.... for alosema ni kweli, na hilo mimi
ni direct mfano for ndio ilivyo na ex....
 
Reactions: Mbu

...busara sana hizi. Ahsante sana.
 
solution usioe mtu aliyezaa tayari.

inawezekana una hoja ya msingi sana, ila tu hujaielezea kwa kirefu.
Kwanini umesema hivyo mkuu?

Wengine tayari tuna mtoto, ukinambia nisioe kwakuwa Fiancee wangu naye ana mtoto inakuwaje mambo haya?
 
...kwenye hoja ya msingi niligusia mila na tamaduni zinavyoweza leta athari pia kwenye jambo hili.
Hapa sitazungumzia ukabila, mfano binti wa kizaramo kalelewa na baba wa kambo huko Usukumani
kiasi cha binti kwa kiwango kikubwa kachukua mila na tamaduni za huko.

Linapokuja suala la binti anataka kuchumbiwa, JE? zile taratibu zetu za kupeleka posa sijui ndio kifunga uchumba,
mahari nakadhalika, Je?....hapa napo pakoje? Watafutwe ili washirikishwe ndugu na jamaa wa mke, au haya mambo yeshapitwa na wakati? Sidhani kama ni jambo la ajabu kuona siku ya harusi hata mama mlezi anapewa tuza zake kwa kumlea vyema mtoto japo mzazi wake yupo!
 
Akhsante....

Umeona AshaDii! Kuna vitu vingine bana mtu wa nje hawezivielewa kivile kwa kuwa si yeye alokivaa kiatu kile...kunamaudhi mengine hukufanya mpaka sometimes u'mnunie' hata spouse wako kisa unaona anamtetea Ex lol!!

Kuna mdada mmoja yeye ameolewa akiwa na watoto wawili wa Ex- ni baada ya kuteswa na kupigika ipasavyo na Ex akamhakikishia kabisa kuwa hakuna atakae'mpenda'........akapendwa yeye na wanae.......Ex kagoma kutoa matunzo anadai akitaka awalipie wanae ada basi agaiwe na mbuchuchu kwanza!!............Mdada current spouse yuko njema na hana shida kabisa juu ya watoto hawa na watoto wanampenda kuliko! but sometimes mtu unajisikia tu vibaya maana unaona kama unamtwisha mzee wa watu mzigo uso na lazima.


Asa huyu Ex- kama si ubahau nn...... mbwai!! ah
 

Hapa Mbu kusema ukweli mie nitakuwa mshamba tu ila ninavyoelewa mie haijalishi mmeachanaje linapofikia swala kama hili ni vema kushirikishwa mzazi halisi i.e. biological parent.......tena kwa mie kaka ndo step nitajiweka kando kabisaaa nikisubiri tu nipewe kibwebwe cha kuandaa shughuli but maamuzi ya kila itakavyokuwa yafanywe na wazai wake halisi......nitaingilia tu pale nitakapoombwa kufanya hivyo otherwise mie nitabakia mtekelezaji

Na siku ya sherehe, Ukumbini nitaomba niwe naserve 'High Table' huku Mr na Ex wake wawe wamekaa pale pa wazazi........Unless niitwe kutambulishwa LOL.
 

lol....hhahhahhaha....asalaaale, Mwj1 nimekuelewa mahbouba,...lol...
eti whaaaat? agawiwe nanihii ndio atoe ada ya wanawe? huyo kadata|!

Well, kwa issue hii sasa akili inaniingia nifuate muongozo wa Spouse jinsi anavyo deal na Ex-wake,
maana kujitia 'kichwa cha nyumba' hapa naweza jikuta naharibu kuliko kurekebisha nyufa,
Lohhh,...nakushukuru Mwj1 kwa darasa hili...
 

...Enheee, hapa ndio napataka.

Iweje wewe mama mzazi uliyemlea binti mfano ana 2-3 years, ukahangaika nae kwa uzima na ugonjwa, mpaka binti kavunja ungo, kamaliza madarasa na leo anaolewa halafu eti shughuli ya kuozesha isiwe yako? Huyo mama/baba mzazi aliyemtelekeza/kunyang'anywa mtoto ananafasi gani kwenye shughuli hiyo kama sio 'mgeni mwalikwa' tu kwasababu za ki itifaki? Nishayashuhudia haya, msinibishie.

Kwa upande wa kijana wa kiume ni hivyo hivyo, mama mlezi kwenye scenario ya hapo juu inaingiliana vile vile.
Hapana, naamini mama na baba mlezi wana nafasi kubwa kwenye kuamua shughuli nzito kama hiyo, hata panapotokea msiba.
Haya mambo kiukweli si ya kupuuzwa, maana kila siku ya mwenyezi mungu kuna jipya linalozuka kugombea uhalali wa mtoto.
Kuna watu walifikia hata kugombea maiti!
 

HApana Mbu sio ufuate tu ni kujadiliana...ukisoma post yangu ya kwanza kabisa kwenye mada hii nimeainisha ni wewe ukae na spouse wako, akupe picha halisi ya yeye na Ex- akupe 'mawazo' yake ambayo yanaweza kabisa yakawa yana mapungufu nawe ukamsaidia kuyanyoosha. Akikupa anachofikiria nawe unakiangalia kwa jicho la tatu kisha unampa faida na hasara ya maamuzi yake.....na hata akitoa msimamo wake wewe utamwuliza sababu........tukichukulia mfano huo wa hapo juu, suppose ndo Spouse wake angekuwa si mwelewa, aseme sitoi ada kwa kuwa Ex- wako ana hela 'chafu' nenda kachukue ada kule.........si angemforce huyo mdada akachakachuliwe naniliu!! lol God forbid!

So dia ni kukaa chini na kustrategize! Mfano the way huyo mdada anavyolihandle swala zima la visitation right ya huyo Ex- wake...ikifika siku ya siku ni Spouse ndiye anayewapeleka watoto kwa Ex mpaka getini, anapiga honi, anasalimia anaacha watoto baada ya kuhakikishiwa whether atawarudisha u aje awachukue! na ni mke ndo aliiomba hiyo (Ofkoz inategemea maana MaEx wengine vichaa mwe.....nsingependa kumuexpose Spouse wangu kwenye risks za kijinga!
 
Reactions: Mbu

.........Hapo sasa Mbu mzazi ni mzazi, mie nilishuhudia dadangu alipoolewa, mamake alikuwa Mgeni rasmi haswaaa tena mgeni rasmi asiyecheka wala kutabasamu!! nilimwelewa kwani nafsi ilikuwa inamsuta maana yeye alimkimbia (wakimia maana walikuwa watatu) akenda kwa mwenye pesa (ndivyo tulivyoambiwaga). But kuna ile ya mmama amenyang'anywa watoto wakingali wachanga...huyo ukisema umzuie kushiriki kwenye shughuli ya mtoto wake utakuwa unamuonea kupita kiasi! Maana sometimes bana inabidi mtu uchunguze authenticity ya 'stori' ulopewa.

Kuna mkaka mmoja alilelewa na Baba wa Kambo!! iakaambiwa kuwa Babake alikwendaoa mzungu akamtelekeza mama mtu huko Unyakyusani. Wakati wa arusi kijana kakomaa anamtaka babake aje arusini, watu wakamwambia ni haki yake, wakaafiki.........ikaanza saka baba yangu, saka baba yangu, Mbeya hayupo, Dar hayupo.........akaenda Arusha akampata!, kumbe ni Babake Mkubwa!! Yaani Mama alizaa na shemeji mkubwa na ndo ikawa chanzo cha talaka!
 
Harusi, misiba ni vitu vya siku moja na si malipo ya kulea. Kwa hiyo na mimi nakubali kuwa biological parent ndiye anayepaswa kuwa muhusika mkuu kwenye issue hata kama hakuchangia hata senti tano kwenye kukuza mtoto. Mimi mfano ikitokea nikaachika afu hubby akaniacha nikae na wanangu hata kama nia yake ilikuwa kukomoa, kwangu hilo ni zawadi kubwa sana kwa hiyo mzazi mmoja kupewa jukumu la kulea watoto kama hilo jukumu liko ndani ya uwezo wake ni kushukuru kwa kweli. Ku separate na watoto kunauma (kwa mtu mwenye akili timamu) waache walau wapate faraja ya kuwa wazazi kwenye harusi/misiba.


Na kingine kama binti au kaka anaolewa afu upande wa ukweni wajue kuwa mzazi halisi yupo kawekwa kando; mtafanya wakwe waogope familia yenu. Inatoa picha ya ubabe fulani hivi ambayo watu wengine wanafikia hata kusema kuwa hata huyu tulochukua atakuwa hivi hivi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…