Mbu
JF-Expert Member
- Jan 11, 2007
- 12,752
- 7,861
- Thread starter
- #81
Hapo mimi ndio hushangaa hawa wanaume... kakuacha wewe anaacha na wanae... cha ajabu anaenda oa mwanamke mwingine mwenye watoto na kuanza kulea watoto sio wake (which is not bad kama he is doing the same to his kids..); wapi na wapi tusha talakiana anataka kuja maliza gunge zake kwako ndo atimize majukumu ya wanawe?? Khaaa!! Hata kama una hamu vipi yayeyuka....
...mara nyingi wanaume kama hao hudhani eti kwa kufanya hivyo anamkomoa Ex wife wake. Ujinga mtupu!
I wish Tulizo angekuja kwenye huu ulimwengu tuliopo kabla ya kuongea hilo.
Watu wnapotengana sidhani kama kuna anayewaza mustakabali wa wale watoto watatunzwaje na wataishi vipi. Na je huko wanakoenda wana maisha gani. Na je in case yule mama akaolewa au yule baba ambaye amebaki na watoto akaoa je maisha ya wale watoto na matunzo yao yakoje.
Watu wanawaza mengine kabisa ya mali na mgawanyo wake bila kufikiria wale watoto. Ni wazazi wachache sana wanaoenda kuomba custody ya mtoto au kuwaombea watoto maisha. (Niko off topic ila nayo ni katika kufikiria watoto ambao wanajikuta wazazi wao wametengana na wanaingia kwenye maisha mapya)
..nawasifu kina mama katika hili, ni mahodari sana kusamehe kila kilichomo ili wabakie na mtoto/watoto wao.
Mkuu, Tulizo haitaji kuja kwenye huo ulimwengu kwani amekulia kwenye huo ulimwengu.
Binafsi, Kuna mengi mabaya ambayo nayakumbuka hadi sasa, nami nimeapa kuwa nitafanya kila lililo ndani ya uwezo wangu kuepusha watoto wangu kuingia kwenye maisha kama haya ya wazazi wa kambo wasio thamini viumbe wengine ..Hebu fikiri unalelewa na mzazi wa kambo ambaye yuko tayari kuzima Jiko la kupikia, kumnunulia chips mtoto wake na kuacha watoto wengine wakiangalia kwa uchungu au kusubiri kurushiwa vipande vya mabaki na mdogo wao kama mbwa uliza kisa ...baba yao kasahau kuacha hela ya chakula na Mama wa kambo ingawa anayo hela lakini hawezi kuchezea hela yake kulisha watoto wa mtu mwingine.
Picha kama hii inaweza kukaa akilini hadi unakufa.. na inarudi kila unaposoma thread kama hizi..
My apologies..a bit out of topic..
...dahh, mkuu Tulizo pole sana kwa kupitia hayo, wala hujaenda off topik...haya ndio tunayoyazungumzia hapa.
Inauma sana kwakweli.
asante BAK.... mie mwanzoni nilikuwa najiuliza naanzia wapi malezi na huyu binti yangu, ictoshe alikuwa ametoka kwenye malezi ya mama yake mzazi sasa naanzia wapi, hapo bado nilikuwa cna mtoto, nilikuwa namlea kwa hofu kweli ndugu wa mama yake walisema mengi, nitawezaje wakati mie bado cjui uchungu wa mtoto cjui nn na nn, lakini nilifanikiwa kwa msaada wa msukuma, ndio mana nasemaga binti yangu wa kwanza, huwezi kujua kabisa kama sio wangu, tunaenda sawa sana mpaka raha......
...naaam, ndivyo ilivyo. Naamini kwa ushirikiano utaopewa na mama/baba mzazi wa huyo mtoto unaweza mlea vizuri sana mtoto kwani mzazi ndiye anayejua mengi tangu huko walikotokea. Tatizo ni pale mzazi asipokupa ushirikiano kwenye malezi ya mwanae,...yaani sawa na yule anayekwambia achana nae huyu ana mama yake!...wanaume wengi wana kaujinga hako kwa kudhani anampendezesha mkewe kumbe anapenyeza mianya ya mtoto kuteseka.
hapo ndio kuna ule usemi wa kiswahili ukipenda boga.....mie niliemkuta kama ninaemlea sasa cna shaka but kwa sasa aniletee mtoto chini wa umri wa mwanangu wa mwisho hiyo atanisamehe, sioni sababu ya mwanamke kukataa mtoto wa mume wake aliemkuta, hapo hakuna upendo kabisa kabisa.
...japo inauma hiyo scenario, lakini je? Vipi iwapo mama mtoto huyo alifariki wakati wakujifungua? au alimtelekeza mtoto mlangoni kwa baba yake akatoweka? ...najua kuna ugumu sana wa ulezi huo lakini bado nataka kuamini unao moyo wa huruma kwa huyo malaika asiye na kosa maskini.