Mali za umma zinapouzwa, watumishi wa Serikali wasiruhusiwe kununua sababu si walipa kodi

Hiyo ni kodi. Kwa sababu kama kulikuwa hakuna kitu kwenye hazina huyu akitozwa kutakuwa na kitu. Lakini kama hakuna kitu kwenye hazina huwezi pata kodi toka kwa mtumishi.

Maana mtumishi anategemea apate pesa toka hazina, kisha akatwe irudi hazina.
 
Kilichoandikwa kwenye PAYE kwenye pay slip ni kitu gani?
 
Kilichoandikwa kwenye PAYE kwenye pay slip ni kitu gani?
Unaweza ita vyovyote. Hata wabunge, mawaziri na Rais huwa wanatoka hadharani na kusema wanalipa kodi. Ila kiukweli hawalipi hata mia.
 
Hiyo ni kodi. Kwa sababu kama kulikuwa hakuna kitu kwenye hazina huyu akitozwa kutakuwa na kitu. Lakini kama hakuna kitu kwenye hazina huwezi pata kodi toka kwa mtumishi.

Maana mtumishi anategemea apate pesa toka hazina, kisha akatwe irudi hazina.
Haya twende mbele mfanyabiashara kamuuzia mfanyakazi wa Serikali bidhaa mfanyakazi akalipua chake

Tuchukulie huyo mfanyabiashara anauza simenti stock imeisha mfanyabiashara akachukua ile pesa kalipwa na mfanyakazi wa Serikali akaenda kununua simenti kiwandani ambapo kiwanda kinalipa kodi kodi kwa mzigo kimeuza.Ni sahihi kiwanda kukiita kilipa kwenye huo mzigo mfanyabiashara kanunua kupitia pesa ya mfanyakazi wa Serikali aliyenunua simenti kwake?
 
Mishahara yao inatokana na kodi. Sasa atatumiaje pesa ya kodi kulipa kodi? Ataongeza chochote kwa kulipa kodi kwa kutumia kodi? Watumishi wote kuanzia Rais, hawatakiwi kupewa nafasi ya kununua mali za umma zilizopatikana kwa kutumia kodi.
The way unavyoandika utadhani hao watumishi wa umma wanakaa tu nyumbani hawafanyi kazi yoyote ila kila mwisho wa mwezi wanalipwa!! Mpumbavu kweli wewe
 
Mishahara yao inatokana na kodi. Sasa atatumiaje pesa ya kodi kulipa kodi? Ataongeza chochote kwa kulipa kodi kwa kutumia kodi? Watumishi wote kuanzia Rais, hawatakiwi kupewa nafasi ya kununua mali za umma zilizopatikana kwa kutumia kodi.
Mshahara ni mapato unalipwa baada ya kufanya kazi Kwa mwezi hawapewi bure wameufanyia kazi
 
Utalipaje kodi kwa kutumia pesa ya kodi. Watumishi mishahara yao inategemea watu wengine walipe kodi. Kwa hiyo yale makato yao hayaongezi chochote kwenye kodi ya nchi.
Kwa uwezo mdogo ulio nao unadhani mishahara wanayolipwa watumishi huwa in bure. Kazi wanazofanya zinatakiwa wafanye bure.
 
Usiende mbali. Assume nchi ndiyo inaanza from scratch. Haina hata mia. Lakini ina watumishi wa umma, wafanyabiashara, wakulima na wataalamu wengine. Ni watu gani watafanya kuwe na chochote kwenye hazina ya nchi kupitia kodi? Katika wote hao, ni nani ambaye hatachangia kodi? Utaona kuwa ni mpaka wafanyabiashara, wakulima, na watu wengine watozwe kodi ndipo mtumishi wa umma anapata mshahara. Sasa atachukuaje sehemu ya kodi na kusema analipa kodi?
 
The way unavyoandika utadhani hao watumishi wa umma wanakaa tu nyumbani hawafanyi kazi yoyote ila kila mwisho wa mwezi wanalipwa!! Mpumbavu kweli wewe
Wanafanyakazi na wanalipwa kutokana na kazi yao. Ila hawalipi kodi. Badala yake wanakula kodi. Mtumishi wa umma anatumia kodi kama ambavyo kodi inatumika kujenga barabara.
 
Hiyo ni kodi. Kwa sababu kama kulikuwa hakuna kitu kwenye hazina huyu akitozwa kutakuwa na kitu. Lakini kama hakuna kitu kwenye hazina huwezi pata kodi toka kwa mtumishi.

Maana mtumishi anategemea apate pesa toka hazina, kisha akatwe irudi hazina.
Mfanyakazi ni mfanyabiara sekta binafsi anauza labour yake au nguvu kazi yake kwa Serikali kama ambavyo mfanyabiashara wa tenda serikalini

Anaiuzia Serikali nguvu zake

Mtaji wa maskini nguvu zake

Tofauti na wa mitaani ni moja tu mfanyakazi wa Serikali ana ofisi permanent majengo ya Serikali

Lakini ni mfanyabiara private muuza labour hours zake kwa mkataba wa kulipana kila mwezi kwa kazi anafanya

Ndio maana huwa kuna mikataba ya ajira kama ilivyo mikataba ya tenda
 
Mfanyabiashara ni nani?
 
Mfanyabiashara ni nani?
Ni yeyote anayeyeuzia Serikali chochote iwe bidhaa au huduma akiwemo mfanyakazi wa Serikali ni mfanyabiara anaiuzia Serikali huduma kwa makubaliano ya malipo ya kila mwezi ndio maana hukatwa kodi wakati kuajiriwa na Serikali

Serikali inatambua wafanyakazi kama wafanyabiashara binafsi
 
Ndiyo maana nikasema mfanyabiashara wa tenda za serikali na mtumishi wa serikali hawana tofauti.
 
Uko sahihi

Ndio maana Serikali huwakata kodi wafanyakazi wa Serikali.
Wafanyakazi na watu wa tenda za serikali hawaongezi chochote kwenye kodi ya nchi. Ni mkulima, na mchimbaji na mvuvi nk ndiyo wanaongeza kitu. Huwezi tumia pesa ya kodi kulipa kodi.
 
Unaweza ita vyovyote. Hata wabunge, mawaziri na Rais huwa wanatoka hadharani na kusema wanalipa kodi. Ila kiukweli hawalipi hata mia.
Inafikirisha, hiyo ni kodi bhana.

Tukianza kudadavua, mlipa kodi atabakia ni raia mvuja jasho wa chini kabisa anayelipa kodi kwa njia ya Vat katika kuendesha maisha yake ya kila siku.

Kwa tafsiri yako hiyo wafanyakazi na wafanya biashara wote hawalipi kodi sasa.

Maana yake ni kwamba, wafanya kazi wanalipiwa pesa za kulipa kodi na wafanya biashara wanalipiwa pesa za kulipia kodi kwa njia ya Vat za walala hoi.
 
Pengine ndiyo maana huwa wanasema mfanyabiashara ni mkasanyaji wa kodi ya serikali. Aliyenunua ndiye kalipa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…