Malipo ya ving'amuzi yawe kwa namna mtumiaji anavyotumia

Malipo ya ving'amuzi yawe kwa namna mtumiaji anavyotumia

albert_daud

Member
Joined
Aug 26, 2015
Posts
21
Reaction score
26
Tanzania ni moja ya nchi ambazo huduma za kununua na kulipia ving'amuzi zinafanyika kwa kasi sana, hasa baada ya ushindani kuongezeka miaka kadhaa nyuma kutoka kampuni moja ambayo ilitawala soko kupata ushindani kutoka kwenye kampuni mpya zilizoanzishwa hasa moja ambayo ukuaji wake umechangiwa kwa kiasi kikubwa na kuonyesha na mpira wa ndani na tamthilia na nyingine kutokana na gharama zake kuwa nafuu na kuenea maeneo mengi ya nchi.

Wote tutakubaliana kwamba ushindani uliopo kwa namna fulani umeleta nafuu kwenye gharama za kulipia visimbuzi vyetu ukiachana na gharama za awali kabla ya ushindani sasa tumekua tukishuhudia ofa mbalimbali makampuni yakishindana yote kuonyesha wapi wanahuduma nzuri na zinapatikana kwa bei rahisi.

Turudi kwenye Hoja yangu ya msingi "MALIPO YA VING'AMUZI YAWE KWA NAMNA MTUMIAJI ANAVYOTUMIA"
tumekua tukipata huduma kwa kulipia visimbuzi vyetu kwa muda fulani "wengi kila mwezi" lakini tumekua tukipata changamoto kwamba kama umelipia kifurushi cha mwezi basi haijalishi kama kwa mwezi huo umetumia mara ngapi.

Mfano: Unaweza lipia kifurushi leo lakini bahati mbaya umepata safari mwezi mzima au hata masiku kadhaa hauko nyumbani au hata kutumia kifurushi chako kwa njia simu au kifaa chochote, lakini ukifika ule muda wa kifurushi kuisha basi kinaisha unalazimika kununua tena.

Kwanini usiwepo utaratibu wa malipo ya vifurushi yatokane na muda ambao mtumiaji kalipia, kama kalipia kifurushi cha mwezi basi isiwe kwa maana ya kuhesabu tarehe bali iwe kwa maana ya matumizi yake.

Teknolojia sasa imekua naimani inawezekana kabisa kila king'amuzi kuonyesha kimekua wazi kwa matumizi kwa muda gani.

Kwa maana inaweza kuwa king'amuzi kiuzwe kwa mfumo wa masaa na masaa hayo yanahesabika pale tu king'amuzi kinapokuwa kimewasha au kama mfumo huu huu wa week au mwezi basi kuhesabu matumizi yake iwe ni pale ambapo ambapo mteja anatumia.

Kwa maana nyingine iwe kama ambavyo sasa inafanyika kwenye umeme uniti za umeme zinatumia pale tu ambapo umeruhusu matumizi ya umeme, kama umeondoka hujaacha kifaa cha umeme kinafanya kazi basi ukirudi uniti zako unazikuta kama zilivyo unaendelea na matumizi.

Nawasilisha
Asanteni.
 
Ni kitu kizuri kwa upande wetu wateja. Japo kwa upande wa makampuni itawapunguzia sana mapato. Au eidha wapandishe bei
Utaratibu huu unamnyonya mteja... Kama tunaambiwa thamani fulani ya kifurushi ni kwa mwezi basi uhalisia uwe kwa matumizi halisi ya mteja
 
Mkuu, usipende kujiingiza kwenye unfamiliar territories, utapigwa vibaya sana,
 
Kuna watu wana akili za ajabu ajabu..sijui ni kukosa elimu ya biashara au ni ujinga.

1. Kampuni hizi ni za kibiashara siyo NGI za msaada. Ili ziendelee kutoa huduma ni lazima kwanza zirudishe gharama za uendeshaji (operations costs)

2. Pricing strategy ni fani. Kampuni huamua kuja na pricing tofauti tofauti ili kuhakikisha mteja au wateja walio wengi wananufaika na kampuni yenyewe ikanufaika.

Kwa mfano unajua gharama ya kupiga simu kama huna bando. Hebu jaribu kiweka 5000 kwenye simu halafu piga simu bila kununua bando uone utaongea kwa muda gani.


Ni kweli wanaweza kutoa option ya kulipa.kwa sekunde, dakika au saa...lakini ujue gharama yake itakuwa kubwa saaaaaana kuliko kulipa kwa mwezi.
 
Imekaa vizuri, naimani kama ulivyoeleza sasa hivi tuko katika teknolojia ya juu hivyo hilo huenda linawezekana kabisa.
Kama tulilalamika kuhusu vifurushi vya simu kuwa na kikomo cha matumizi wakaja kusema tumeiomba serikali/makampuni ya simu huduma ya kuhamisha vifurushi, sitashangaa na hili wakisema tumeomba kuwepo na uwezekano wa kuletewa visimbuzi vyenye uwezo wa kucheza ps2. Hii nchi hakuna kinachoendelea
 
Kuna watu wana akili za ajabu ajabu..sijui ni kukosa elimu ya biashara au ni ujinga.

1. Kampuni hizi ni za kibiashara siyo NGI za msaada. Ili ziendelee kutoa huduma ni lazima kwanza zirudishe gharama za uendeshaji (operations costs)

2. Pricing strategy ni fani. Kampuni huamua kuja na pricing tofauti tofauti ili kuhakikisha mteja au wateja walio wengi wananufaika na kampuni yenyewe ikanufaika.

Kwa mfano unajua gharama ya kupiga simu kama huna bando. Hebu jaribu kiweka 5000 kwenye simu halafu piga simu bila kununua bando uone utaongea kwa muda gani.


Ni kweli wanaweza kutoa option ya kulipa.kwa sekunde, dakika au saa...lakini ujue gharama yake itakuwa kubwa saaaaaana kuliko kulipa kwa mwezi.
Naomba nikwambie hili

Dstv na azam wapo kenya. Lakini una habari kwamba gharama za vifurushi vyao kwa mwezi ni ndogo sana ukilinganisha na gharama za Tanzania japo wao pia sarafu yao iko juu? Yani bei ya kifurushi Kenya ni nusu ya bei ya Tanzania. Unajua ni kwanini? Nchi yetu ina taasisi zisizojali maslahi ya mlaji.
 
Naomba nikwambie hili

Dstv na azam wapo kenya. Lakini una habari kwamba gharama za vifurushi vyao kwa mwezi ni ndogo sana ukilinganisha na gharama za Tanzania japo wao pia sarafu yao iko juu? Yani bei ya kifurushi Kenya ni nusu ya bei ya Tanzania. Unajua ni kwanini? Nchi yetu ina taasisi zisizojali maslahi ya mlaji.
Hivi idadi ya watumiaji haiathiri bei?
 
Back
Top Bottom