Malkia Elizabeth na Viongozi wa TAA, 1953

Malkia Elizabeth na Viongozi wa TAA, 1953

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MALKIA ELIZABETH NA VIONGOZI WA TAA 1953
Picha hiyo hapo chini ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth imenirudisha nyuma sana hadi mwaka wa 1953.

Nimeitazama hiyo picha ya viongozi awa wawili nikaamua kufungua kitabu cha Abdul Sykes niangalie nimeandika nini kuhusu Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth.

Siku chache zilizopita niliandika katika mtandao kuwa Nyaraka za Sykes zina jina la kila mtu alyehusika katika siasa za Tanganyika.

Kuna mtu alichukizwa na maneno yangu haya na akaniandikia maneno ya kifedhuli na kejeli lakini mimi kwa dhati na ukweli wa nafsi yangu nikawambia asidhani kuwa mimi natania nyaraka zile zina mambo mengi sana kuhusu harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa nilipoona picha hii ya Malkia akiwa na Mwalimu Nyerere wakati Malkia Elizabeth alipofanya ziara ya Tanzania mwaka wa 1979 nikasema hebu nifungue kitabu changu niangalie kuna nini kuhusu Malkia na Mwalimu Nyerere.

Ili uweze kupata historia yote vizuri inabidi nianze mwanzo wa maisha ya Julius Nyerere pale alipoingia katika siasa za Dar es Salaam na kuchaguliwa kuwa President wa TAA tarehe 17 April, 1953.

Tarehe 19 June, gazeti la Tanganyika Standard likachapa majina ya viongozi wa TAA kama ifuatavyo: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias, Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer, Ally K. Sykes Assistant Treasurer. Committee members Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Katika Nyaraka za Sykes kuna barua iliyoandikwa na kwenda kwa Malkia Elizabeth isiyokuwa na tarehe iliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwa kutawazwa kuwa Malkia wa Uingereza.

Katika barua hii jina la Dome Budohi ndilo linaloonekana kama Katibu Mkuu badala ya jina la Kasella Bantu kama lilivyotokea katika Tanganyika Standard.

Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Yahya Othman na Dr. Ng’wazi Kamata waandishi wa kitabu cha maisha ya Julius Nyerere walipokuja kunihoji kuhusu Mwalimu niliwaonyesha barua hii.

Waliipenda sana na wakaniomba niwape nakala.

Nilipokuwa naiangalia picha hii ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth nikawa najiuliza kama Malkia anakumbuka kuwa aliandikiwa barua na Mwalimu Nyerere mwaka wa 1953 akimpongeza kwa kutawazwa kuwa Malkia.
Sijui kama Malkia anaikumbuka barua hii.

Lakini nina uhakika ukienda Rhodes House Oxford barua hii itakuwapo.

Sasa tuje kwa Ally Sykes na ziara hii ya Malkia Tanzania mwaka wa 1979.

Ubalozi wa Uingereza ulifanya dhifa nyumbani kwake kwa heshima ya Malkia.
Ally Sykes ananihadithia.

Katika dhifa ile Julius Nyerere alikuwapo na mgeni wake na katika walioalikwa alikuwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab.
Miaka mingi ilikuwa imepita na Ally Sykes, Bi. Zainab na Nyerere walikuwa hawajaonana kwa muda mrefu sana.

Walipokutana uso kwa uso Nyerere alimwambia Ally Sykes, ‘’Ally hawa Waingereza unakuja katika shughuli zao lakini shughuli zetu huonekani.’’

Ally Sykes akajibu, ‘’Hawa wananialika nyinyi hamnialiki mimi.’’

Mwalimu akacheka akamgeukia Bi.Zainab akamwambia, ‘’Bi. Zainab Ally hajabadilika karibu wewe Msasani.’’

Ally Sykes akaniambia baada ya siku ile hawakupata kuzungumza hadi Nyerere anakufa ingawa iko siku walikuwa ndege moja na viti jirani wote wakielekea London.

Hakuna kati yao aliyefanya juhudi ya kumsogelea mwenzake kumsalimu.
Hawa ni wanachama wawili ambao kadi zao za TANU zilifuatana.

Kadi no 1 Territorial President Julius Kambarage Nyerere kadi no.2 Ally Kleist Sykes.

Screenshot_20220222-135528_Facebook.jpg
 
MALKIA ELIZABETH NA VIONGOZI WA TAA 1953
Picha hiyo hapo chini ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth imenirudisha nyuma sana hadi mwaka wa 1953.

Nimeitazama hiyo picha ya viongozi awa wawili nikaamua kufungua kitabu cha Abdul Sykes niangalie nimeandika nini kuhusu Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth.

Siku chahe zilizopita niliandika katika mtandao kuwa Nyaraka za Sykes zina jina la kila mtu alyehusika katika siasa za Tanganyika.

Kuna mtu alichukizwa na maneno yangu haya na akaniandikia maneno ya kifedhuli na kejeli.lakini mimi kwa dhati na ukweli wa nafsi yangu nikawambia asidhani kuwa mimi natania nyaraka zile zina mambo mengi sana kuhusu harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa nilipoona picha hii ya Malkia akiwa na Mwalimu Nyerere wakati Malkia Elizabeth alipofanya ziara ya Tanzania mwaka wa 1979 nikasema hebu nifungue kitabu changu niangalie kuna nini kuhusu Malkia na Mwalimu Nyerere.

Ili uweze kupata historia yote vizuri inabidi nianze mwanzo wa maisha ya Julius Nyerere pale alipoingia katika siasa za Dar es Salaam na kuchaguliwa kuwa President wa TAA tarehe 17 April, 1953.

Tarehe 19 June, gazeti la Tanganyika Standard likachapa majina ya viongozi wa TAA kama ifuatavyo: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias, Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer, Ally K. Sykes Assistant Treasurer. Committee members Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Katika Nyaraka za Sykes kuna barua iliyoandikwa na kwenda kwa Malkia Elizabeth isiyokuwa na tarehe iliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwa kutawazwa kuwa Malkia wa Uingereza.

Katika barua hii jina la Dome Budohi ndilo linaloonekana kama Katibu Mkuu badala ya jina la Kasella Bantu kama lilivyotokea katika Tanganyika Standard.

Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Yahya Othman na Dr. Ng’wazi Kamata waandishi wa kitabu cha maisha ya Julius Nyerere walipokuja kunihoji kuhusu Mwalimu niliwaonyesha barua hii.

Waliipenda sana na wakaniomba niwape nakala.

Nilipokuwa naiangalia picha hii ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth nikawa najiuliza kama Malkia anakumbuka kuwa aliandikiwa barua na Mwalimu Nyerere mwaka wa 1953 akimpongeza kwa kutawazwa kuwa Malkia.
Sijui kama Malkia anaikumbuka barua hii.

Lakini nina uhakika ukienda Rhodes House Oxford barua hii itakuwapo.

Sasa tuje kwa Ally Sykes na ziara hii ya Malkia Tanzania mwaka wa 1979.

Ubalozi wa Uingereza ulifanya dhifa nyumbani kwake kwa heshima ya Malkia.
Ally Sykes ananihadithia.

Katika dhifa ile Julius Nyerere alikuwapo na mgeni wake na katika walioalikwa alikuwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab.
Miaka mingi ilikuwa imepita na Ally Sykes, Bi. Zainab na Nyerere walikuwa hawajaonana kwa muda mrefu sana.

Walipokutana uso kwa uso Nyerere alimwambia Ally Sykes, ‘’Ally hawa Waingereza unakuja katika shughuli zao lakini shughuli zetu huonekani.’’

Ally Sykes akajibu, ‘’Hawa wananialika nyinyi hamnialiki mimi.’’

Mwalimu akacheka akamgeukia Bi.Zainab akamwambia, ‘’Bi. Zainab Ally hajabadilika karibu wewe Msasani.’’

Ally Sykes akaniambia baada ya siku ile hawakupata kuzungumza hadi Nyerere anakufa ingawa iko siku walikuwa ndege moja na viti jirani wote wakielekea London.

Hakuna kati yao aliyefanya juhudi ya kumsogelea mwenzake kumsalimu.
Hawa ni wanachama wawili ambao kadi zao za TANU zilifuatana.

Kadi no 1 Territorial President Julius Kambarage Nyerere kadi no.2 Ally Kleist Sykes.

View attachment 2127281
Nina hakika hapa kuna photoshop; picha ya Nyerere mwaka 1953 hawezi kua hivo, alikua kijana sana. Hapa teknolojia imefanyika
 
Shukrani sana mzee wetu binafsi najifunza mengi kupitia maandiko yako.
 
MALKIA ELIZABETH NA VIONGOZI WA TAA 1953
Picha hiyo hapo chini ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth imenirudisha nyuma sana hadi mwaka wa 1953.

Nimeitazama hiyo picha ya viongozi awa wawili nikaamua kufungua kitabu cha Abdul Sykes niangalie nimeandika nini kuhusu Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth.

Siku chahe zilizopita niliandika katika mtandao kuwa Nyaraka za Sykes zina jina la kila mtu alyehusika katika siasa za Tanganyika.

Kuna mtu alichukizwa na maneno yangu haya na akaniandikia maneno ya kifedhuli na kejeli.lakini mimi

Mwenye kaunda suti nyeupe na miwani myeusi hapo mbele ni nani?!
 
Nina hakika hapa kuna photoshop; picha ya Nyerere mwaka 1953 hawezi kua hivo, alikua kijana sana. Hapa teknolojia imefanyika
Ukisoma huelewi, au ni "denial minds" tu? Kila unachokisoma au kukiona kimeandikwa na Mohamed Said basi kwenye "mind" yako (if any) ushajiwekea kukikataa na kukipinga tu. Matokeo yake hata ukweli mnaukataa.

Soma vizuri, hiyo ameandika ni picha ya 1979, picha hiyo ndiyo imemkubusha Malkia alivyokuja 1953 na picha aliopiga na Wazee wa TANU.

Sasa Photoshop ya nini na hiyo ni 1979?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Ukisoma huelewi, au ni "denial minds" tu? Kila unachokisoma au kukiona kimeandikwa na Mohamed Said basi kwenye "mind" yako (if any) ushajiwekea kukikataa na kukipinga tu. Matokeo yake hata ukweli mnaukataa.

Soma vizuri, hiyo ameandika ni picha ya 1979, picha hiyo ndiyo imemkubusha Malkia alivyokuja 1953 na picha aliopiga na Wazee wa TANU.

Sasa Photoshop ya nini na hiyo ni 1979?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
Mbona umepaniki bimkubwa? Nani kakwambia maandishi ya mzee huaga nayapinga???? Usikariri mama; hata hivyo mzee Mohamed ni babu, kumchangamsha babu ni haki yetu ya msingi kabisa, kama wewe tu, nikikuchangamsha au hata kukufata inbox ni haki yetu ya msingi mama, so just cool down mama cause mzee mwenyewe aliisha nijibu kuhusu comment yangu long time ago
 
Mbona umepaniki bimkubwa? Nani kakwambia maandishi ya mzee huaga nayapinga???? Usikariri mama; hata hivyo mzee Mohamed ni babu, kumchangamsha babu ni haki yetu ya msingi kabisa, kama wewe tu, nikikuchangamsha au hata kukufata inbox ni haki yetu ya msingi mama, so just cool down mama cause mzee mwenyewe aliisha nijibu kuhusu comment yangu long time ago
Mazindu...
Wewe ni mwanangu kwa umri wako na wangu.

Wanao sasa ndiyo wajukuu zangu.

Nakwambia haya kukusaidia uweze kuliweka kila jambo mahali pake.

Kinyume cha hapo utafanya mambo yasiyopendeza.

Unadhani wewe unaweza kunitania kwa kuwa mimi ni "babu" ilhali si sawa mimi kwako ni baba kwa hiyo unastahili kunipa heshima ya baba sawa na baba yako aliyekuzaa.

Hizi ndizo mila zetu.
 
Mazindu...
Wewe ni mwanangu kwa umri wako na wangu.

Wanao sasa ndiyo wajukuu zangu.

Nakwambia haya kukusaidia uweze kuliweka kila jambo mahali pake.

Kinyume cha hapo utafanya mambo yasiyopendeza.

Unadhani wewe unaweza kunitania kwa kuwa mimi ni "babu" ilhali si sawa mimi kwako ni baba kwa hiyo unastahili kunipa heshima ya baba sawa na baba yako aliyekuzaa.

Hizi ndizo mila zetu.
Mzee wangu uko sawa kabisa; hata hivyo uliisha nijibu siku za mwanzoni kabisa, sema bimkubwa kakumbushia issue ambayo wewe uliisha nipa ufafanuzi. Wewe ni kama baba yangu kabisa, hilo wala sikatai yaani. Heshima kwako, tupo kujifunza
 
Mzee zangu uko sawa kabisa; hata hivyo uliisha nijibu siku za mwanzoni kabisa, sema bimkubwa kakumbushia issue ambayo wewe uliisha nipa ufafanuzi. Wewe ni kama baba yangu kabisa, hilo wala sikatai yaani. Heshima kwako, tupo kujifunza
Mazindu ...
Jingine ni jifunze kuandika kwa adabu.
Hii inakupa mosi wewe mwenyewe heshima; na pili inafanya mjadala ustawi na kupendeza.

Haya yakikaa sawa ndipo tija inapatikana na tunaelimika.
 
Mbona umepaniki bimkubwa? Nani kakwambia maandishi ya mzee huaga nayapinga???? Usikariri mama; hata hivyo mzee Mohamed ni babu, kumchangamsha babu ni haki yetu ya msingi kabisa, kama wewe tu, nikikuchangamsha au hata kukufata inbox ni haki yetu ya msingi mama, so just cool down mama cause mzee mwenyewe aliisha nijibu kuhusu comment yangu long time ago
Naona yamekuingia.
 
MALKIA ELIZABETH NA VIONGOZI WA TAA 1953
Picha hiyo hapo chini ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth imenirudisha nyuma sana hadi mwaka wa 1953.

Nimeitazama hiyo picha ya viongozi awa wawili nikaamua kufungua kitabu cha Abdul Sykes niangalie nimeandika nini kuhusu Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth.

Siku chahe zilizopita niliandika katika mtandao kuwa Nyaraka za Sykes zina jina la kila mtu alyehusika katika siasa za Tanganyika.

Kuna mtu alichukizwa na maneno yangu haya na akaniandikia maneno ya kifedhuli na kejeli.lakini mimi kwa dhati na ukweli wa nafsi yangu nikawambia asidhani kuwa mimi natania nyaraka zile zina mambo mengi sana kuhusu harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Sasa nilipoona picha hii ya Malkia akiwa na Mwalimu Nyerere wakati Malkia Elizabeth alipofanya ziara ya Tanzania mwaka wa 1979 nikasema hebu nifungue kitabu changu niangalie kuna nini kuhusu Malkia na Mwalimu Nyerere.

Ili uweze kupata historia yote vizuri inabidi nianze mwanzo wa maisha ya Julius Nyerere pale alipoingia katika siasa za Dar es Salaam na kuchaguliwa kuwa President wa TAA tarehe 17 April, 1953.

Tarehe 19 June, gazeti la Tanganyika Standard likachapa majina ya viongozi wa TAA kama ifuatavyo: J.K. Nyerere, President; Abdulwahid Sykes, Vice-President; J.P. Kasella Bantu, General Secretary; Alexander M. Tobias, Waziri Dossa Aziz, Joint Minuting Secretary; John Rupia, Treasurer, Ally K. Sykes Assistant Treasurer. Committee members Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.

Katika Nyaraka za Sykes kuna barua iliyoandikwa na kwenda kwa Malkia Elizabeth isiyokuwa na tarehe iliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwa kutawazwa kuwa Malkia wa Uingereza.

Katika barua hii jina la Dome Budohi ndilo linaloonekana kama Katibu Mkuu badala ya jina la Kasella Bantu kama lilivyotokea katika Tanganyika Standard.

Prof. Issa Shivji, Prof. Saida Yahya Othman na Dr. Ng’wazi Kamata waandishi wa kitabu cha maisha ya Julius Nyerere walipokuja kunihoji kuhusu Mwalimu niliwaonyesha barua hii.

Waliipenda sana na wakaniomba niwape nakala.

Nilipokuwa naiangalia picha hii ya Mwalimu Nyerere na Malkia Elizabeth nikawa najiuliza kama Malkia anakumbuka kuwa aliandikiwa barua na Mwalimu Nyerere mwaka wa 1953 akimpongeza kwa kutawazwa kuwa Malkia.
Sijui kama Malkia anaikumbuka barua hii.

Lakini nina uhakika ukienda Rhodes House Oxford barua hii itakuwapo.

Sasa tuje kwa Ally Sykes na ziara hii ya Malkia Tanzania mwaka wa 1979.

Ubalozi wa Uingereza ulifanya dhifa nyumbani kwake kwa heshima ya Malkia.
Ally Sykes ananihadithia.

Katika dhifa ile Julius Nyerere alikuwapo na mgeni wake na katika walioalikwa alikuwa Ally Sykes na mkewe Bi. Zainab.
Miaka mingi ilikuwa imepita na Ally Sykes, Bi. Zainab na Nyerere walikuwa hawajaonana kwa muda mrefu sana.

Walipokutana uso kwa uso Nyerere alimwambia Ally Sykes, ‘’Ally hawa Waingereza unakuja katika shughuli zao lakini shughuli zetu huonekani.’’

Ally Sykes akajibu, ‘’Hawa wananialika nyinyi hamnialiki mimi.’’

Mwalimu akacheka akamgeukia Bi.Zainab akamwambia, ‘’Bi. Zainab Ally hajabadilika karibu wewe Msasani.’’

Ally Sykes akaniambia baada ya siku ile hawakupata kuzungumza hadi Nyerere anakufa ingawa iko siku walikuwa ndege moja na viti jirani wote wakielekea London.

Hakuna kati yao aliyefanya juhudi ya kumsogelea mwenzake kumsalimu.
Hawa ni wanachama wawili ambao kadi zao za TANU zilifuatana.

Kadi no 1 Territorial President Julius Kambarage Nyerere kadi no.2 Ally Kleist Sykes.

Hii picha ni ya 1979 maana naona vijana kama SOKOINE pichani
 
Ukisoma huelewi, au ni "denial minds" tu? Kila unachokisoma au kukiona kimeandikwa na Mohamed Said basi kwenye "mind" yako (if any) ushajiwekea kukikataa na kukipinga tu. Matokeo yake hata ukweli mnaukataa.

Soma vizuri, hiyo ameandika ni picha ya 1979, picha hiyo ndiyo imemkubusha Malkia alivyokuja 1953 na picha aliopiga na Wazee wa TANU.

Sasa Photoshop ya nini na hiyo ni 1979?

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
Badala ya kutuletea umbeya huu, bora Mzee MS angejikita kusifia utanashati, utajiri na magari ya kifahari kama Mercedes Benz SE ya Sykes whoever (Can't tell the difference between them, and wouldn't care less which is which.) ya enzi hizo. Mzee mbeya wewe na mwongo, tunakujua vizuri. Tupe za Nyerere bila kumtaja Sykes. Kama kweli una weledi mkosoe Nyerere kwa lolote bila kuwataja hao Miungu Watu wako Sykes.
 
Badala ya kutuletea umbeya huu, bora Mzee MS angejikita kusifia utanashati, utajiri na magari ya kifahari kama Mercedes Benz SE ya Sykes whoever (Can't tell the difference between them, and wouldn't care less which is which.) ya enzi hizo. Mzee mbeya wewe na mwongo, tunakujua vizuri. Tupe za Nyerere bila kumtaja Sykes.
Umekurupuka hata huelewi yalipoanzia.

Tujuze baba au babu yako walikuwa wapi wakati watu wanadai Uhuru? Mohamed Said anatuwekea jinsi wazee wetu walivyokuwa mstari wa mbele tokea 1929 with proof.
 
Umekurupuka hata huelewi yalipoanzia.

Tujuze baba au babu yako walikuwa wapi wakati watu wanadai Uhuru? Mohamed Said anatuwekea jinsi wazee wetu walivyokuwa mstari wa mbele tokea 1929 with proof.
Walowezi Wazulu watawezaje kudai Uhuru wa nchi ambayo siyo yao?

Wazee wangu wameishi Tanganyika miaka elfu na elfu.

Unawezaje kudai Uhuru wa nchi ambayo siyo yako ilhali ukoo mzima mmeletwa Tanganyika na Wajerumani kama mercenaries/askari wa kukodi wa hao Wajerumani, halafu baadaye unalalamika mmewekwa nje kwenye historia rasmi ya nchi? Na majina ya Kijerumani mmeyang'ang'ania vilevile.
 
Back
Top Bottom