TANZIA Malu Stonch (Nuhu) afariki Dunia. Alikuwa akitumbuiza jukwaani

TANZIA Malu Stonch (Nuhu) afariki Dunia. Alikuwa akitumbuiza jukwaani

View attachment 2956136Mwimbaji nyota wa FM Academia, Malu Stonch amefariki dunia baada ya kuanguka ghafla jukwaani.

Hali hiyo imetokea katika ukumbi wa Target Mbezi, Beach, Jumamosi usiku wakati mwimbaji huyo akiwa jukwaani anaimba wimbo wa "Hadija".

Inaelezwa kuwa wakati anaimba wimbo huyo, Malu Stonch alidondoka ghafla na kupoteza fahamu.

Baada ya kupatiwa huduma ya kwanza huku akiwa bado hajitambui, ndipo akakimbizwa Masana Hospital.

Mwanahabari na mdau mkubwa wa muziki, MC Petit aliyekuwa miongoni mwa waliomkimbiza Malu Stonch hospital, ameithibitishia Saluti5 kuwa mwimbaji huyo amefariki.

"Pale Masana walipompokea tu, wakatumbia tumpeleke Lugalo Hospital kwa kuwa mgonjwa wetu ameshafariki," ameeleza MC Petit.

"Tulipofika Lugalo nao wakatuthibitishia kuwa Malu Stonch amefariki na hivyo tukafanya utaratibu wa kumpeleka chumba cha kuhifadhi maiti," alifafanua zaidi MC Petit.

Pumzika kwa amani Malu Stonch.

Said Mdoe
7/4/2024
rip mwamba alikuwa jirani yangu pale ghorofa za utumish house magomeni alikuwa kuna wakongo walikuwa wanaishi pale miaka yote nilikuwa sijui kwamba ni muimbaji huyu jamaaa

Mara mwisho nimekuja kukutana nae goba kuna casino ndogo tukapiga story mbili tatu hapo goba casino ndogo texas walikuwa na project pale miezi kama mitano hivi imepita

Leo kafariki RIP.......
 
View attachment 2956136Mwimbaji nyota wa FM Academia, Malu Stonch amefariki dunia baada ya kuanguka ghafla jukwaani.

Hali hiyo imetokea katika ukumbi wa Target Mbezi, Beach, Jumamosi usiku wakati mwimbaji huyo akiwa jukwaani anaimba wimbo wa "Hadija".

Inaelezwa kuwa wakati anaimba wimbo huyo, Malu Stonch alidondoka ghafla na kupoteza fahamu.

Baada ya kupatiwa huduma ya kwanza huku akiwa bado hajitambui, ndipo akakimbizwa Masana Hospital.

Mwanahabari na mdau mkubwa wa muziki, MC Petit aliyekuwa miongoni mwa waliomkimbiza Malu Stonch hospital, ameithibitishia Saluti5 kuwa mwimbaji huyo amefariki.

"Pale Masana walipompokea tu, wakatumbia tumpeleke Lugalo Hospital kwa kuwa mgonjwa wetu ameshafariki," ameeleza MC Petit.

"Tulipofika Lugalo nao wakatuthibitishia kuwa Malu Stonch amefariki na hivyo tukafanya utaratibu wa kumpeleka chumba cha kuhifadhi maiti," alifafanua zaidi MC Petit.

Pumzika kwa amani Malu Stonch.

Said Mdoe
7/4/2024
Kwa ninavyowajua Wakongo ( Bandeko Nangai ) sasa hivi hii Bendi itaanza kufanya vyema na Kukubalika Kimuziki kwakuwa Shughuli imeshamalizika.
 
Rip Nuhu. Nakumbuka combination yake na Ndanda kosovo, Patcheko Mbongo, patcho mwamba, serge mwela ilikuwa balaa
 
Hawa jamaa kutoka Congo siamini kama wanatokaga kwao wakiwa wanamuziki kweli maana wakifika Bongo wanakuaga ving'ang'anizi hawataki kabisa kurudi kwao wanaishia kuzikwa hapo Kinondoni nahisi wanaogopa kurudi kwao kuishi maisha yao halisia wakati huku wanapata mtelezo.
Mkuu hao ni raia wa kawaida tu wakifika bongo wanajimwambafaai.,
.hawa wote nishakutana nao. Gisselle alikua mke wangu ni saloonist walikukua wanashinda kula na kusuka pale
King dodoo labuche alikua hakauki pale.
Nyoshi anamjua huyo mwanamke,,alivogongwa risasi karudi analia
 
Kuna mwamba mwingine king blaise alipata uchizi.
Kwenye dunia kigeugeu kaua sana..
Pablo masai tunae mtaani
 
Mkiwa na bando chungulieni sportfy kule kuna live za ngwasuma siio za nchi hii.
Kaandike tu rangi ya chungwa au dotnata utapata kilichopo live.
 
Juzi tu nilikuwa nasikiliza ngoma ya marehemu banza, kumekucha, ndani yupo ndanda kosovo na malu stoch, niliirudua si chini ya mara 10.
 
Back
Top Bottom