Mama Diamond: Diamond hakuja kwenye msiba wa Godzilla kwa sababu angesababisha vurugu na watu wange zimia.

Au Juma Nature qibratan
 
Acha uongo msiba wa kanumba watu walizimia kisa wingi wa watu ambao ulikuwapo tokea hata diamond hajaja na.pale watu walienda kumuaga kanumba si kumuona Diamond, kipindi hicho diamond bado sana hajawa famous kiasi hiki, na hiyo april 2012 watu walikuwa wanamkubali sana Kanumba
 
We pimbi kweli; kuna mahali niliposema watu walizimia?! NImesema kwenye msiba wa Kanumba watu walikuwa wengi sana lakini walikuwa wametulia! Alipotokea Diamond, ndipo ikaanza mshike mshike hadi polisi wakalazimika kuingilia kati na kumsindikiza Diamond alipokuwa amepangiwa kukaa lakini ilishindikana! Video hii hapa wakati Diamond anawasili msibani!!
Halafu unaonekana wala sio mtu wa burudani! Yaani 2012 Diamond alikuwa hafahamiki?! You can't be serious! Hivi tangu atoke Nenda Kamwambie mwaka 2009 hadi 2012 Diamond alikuwa ametoa hit ngapi ambazo zilishamtengenezea history?
 
Hakuwa maarufu kiivyo alafu hakuna haja ya kunitukana, nakwambia umaarufu wa diamond mwaka 2012 haukuwa mkubwa sana kama mwaka 2014 na kuendelea, Diamond mwaka 2012 bado hajatoa hata ile Kesho , hata nyimbo nyingine kali kali, Diamond ni maarufu tokea 2014 zaid, miaka hiyo alikuwa kama Zilla tu
 
Kwa kanumba ni kweli mond alivuruga utulivu! Kama kitu mtu hukijui ni bora ukae kimya
 
Aiseeee nakumbuka kwa kanumba kweli jamaa alivuruga kweli pale leaders mpaka wakamuondoa mama mtu anaweza kuwa sahihi kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
diamond ana nyota kali sana.. nakumbuka mzumbe mwaka 2010 ilipigwa mbagalaaa wakati wa break ya semina.... tulikuwa kwenye semina ya mambo ya ethics.. ukumbi ukavurugika.. kila mtu anataka aimbe na kucheza mbagala
 
Kama mnasema hakuwa na umaarufu kanumba alifarik 2012 kama sijakosea nadhani hiki kipindi ndo umaarufu wa diamond ulianza kuja juu narecall tu jamaa alivotokeaga msibani leaders daaaah ilikuwa taflan ila wasanii wengine ilikuwa fresh tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya kulia lia kwamba umetukanwa, nadhani ulitakiwa kwanza uwe na adabu wakati wa kuwajibu wenzako! How come unaibuka from nowhere na kuniita muongo?! Ulishindwa kutumia lugha ya kiungwana?!

Na kama hakuwa na huo umaarufu, sasa kwanini hadi polisi akaingilia kati na kumsindikiza sehemu aliyotakiwa kukaa?! Au huna bundle ya kutosha na kwahiyo umeshindwa kuangalia hiyo video? Kama hiyo umeona ni ndefu, hebu iangalie hii Twangala akimuhoji Diamond kufuatia kushindwa kwake kwenda kutoa salamu za mwisho kwa Marehemu Kanumba:
-

Narudia, wewe sio mfuatiliaji wa muziki! Hiyo beyond 2014 ni Diamaond kutoka international lakini by 2012 tayari alishakuwa mkubwa sana East Afrika! Kesho aliitoa mwishoni mwa 2012 lakini kwavile jina lake lilishakuwa kubwa, Avril akaamua kucheza as a vixen for free, tena ni mwenyewe ndie alitaka awepo kwenye video! May 2012 Diamond alienda kutumbuiza Big Brother kwenye eviction show; sasa kama hakuwa maarufu alipata vp hiyo show?

And by that time, tayari alishaachia hits kama Nenda Kamwambie, Mbagala, Nitarejea, Moyo Wangu, Mawazo na zingine kadhaa!!! Inawezekana wewe ulianza kumfuatilia baada ya kutoka na My Number 1 Remix ambayo ndiyo ilimpeleka international lakini Tanzania na EA tayari alishakuwa mkubwa sana kiasi cha kuchukuwa Nzumari Awards kule Kenya!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…