Mama hamtaki Mpenzi wangu

Mama hamtaki Mpenzi wangu

Ungekuwa ni dada yangu unaolewa na mtu mwenye sifa kama hizo hapo juu ningesikitika. Umetaja sifa za mtu ambaye huwa namkwepa kuwa rafiki yangu wa kutafuta mishe mtaani na jioni kila mmoja kwake, sasa wewe unaenda kumfanya mumeo wa kuishi nae nyumba moja.
 
Habari za saa hii wana Jf
Naomba msaada wenu wa mawazo juu ya swala hili, kama kichwa cha habari kinavyojieleza;
kwa miezi mi3 hii nmekua na mahusiano ya kimapenzi na kijana karibu na maeneo ninayoishi,
  • mimi binti wa 28 yrs Mpenzi ana 38 aliwahi kuishi na mwanamke kwa miaka kadhaa zamani akaachana na mwanamke wake baada ya kuachishwa kazi ( kampuni ilifilisika)
  • Kwasasa ana biashara zake
-wote tumeishia 0- level kielimu
-anataka kunioa pale nikiridhia

sasa tatizo linaanza baada ya mama kuhisi uhusiano baina yetu, anasema kijana hafai kwanza
-ana vuta bangi/pombe
-Hajui kuvaa sio mtanashati
- aliwahi kuishi na mwanamke
-anatoka familia ya kawaida kama yetu kwahiyo hafai hatanisaidia chochote
- hana mvuto mbele za watu
-hana Cv nzuri hata nikimtambulisha
- anahisi kaniroga ndo mana nmekua nae kimahusiano
-kwanza anakaa maeneo ya karibu na nyumbani
-hana hadhi ya kuwa na mimi
sababu ni nyingi!!

Kwa kuliona hilo tukaamua basi ahame makazi tayari kashahama, mazingira yote tumeyafanya yawe mapya,kwa kila kitu cha hadhu anayoitaka mama,nmeshambadilisha huo muonekano kwa kiasi chake ili afanane na anavyotaka mama ila naona pamoja na kutaka aridhike ila kila siku anaanzisha sababu mpya ya kumkataa anasema anajitutumua tu ili anipate na pombe ameacha anipate akishanioa ntapata shida mana atarudi kwenye mambo yake yote!! Pia namdhalilisha kwa wamama wenzie kwa kuwa na mahusiano na jamaa
- mama anasema yuko tayari kwenda kwa mganga yoyote akavunje mahusiano mana kwanza jamaa atakua kaniroga sio kawaida.

Sasa hapo nifanyaje wakuu? maana naona nachanganyikiwa kila siku anaanzisha jambo jipya! ilihali nmemwambia mimi mwenyewe sijasoma! kazi sina wala bishara yoyote na kijana wa watu ameridhia ana fanya kila jukumu lake bila kinyongo ila mama anasema anafanya mana hana hadhi ya kuwa na ww ndo mana inabidi afanye tu...
Kinachoniumiza ni hakuna siku amewahi niuliza changamoto za maisha yangu ya mahusiano. nmejaribu kumwambia wachumba wakija wakijua sijasoma/sina kazi wanagairi haelewi.. anasema umerogwa wewe
nikiomba space nitulize kichwa sipewi naambiwa mpaka utanielewa...
nmepata feeling mama angu ni Toxic /narcissistic mom ila nikieleza hisia zangu yeye ana cheka ndo ananiona kama mpuuzi..
maana mimi nmemwambia kwanini tusimwachie Mungu tu kama Mungu hajapanga tutaachana tu ila kwa ridhaa yetu mengine tutarekebishana sitaki uwe kama unanipangia maisha ila haelewi kabisa , niko njia panda maana maisha nayaona machungu kabisa ni mimi ndo tatizo au mama? nishaurini wakubwa kabla sijashuka presha nikazimika mana bi mkubwa kasema kama ntakufa nife mana ndo ilivyopangwa.
Mkuu, tunaingia kwenye mahusiano na watu ambao ni sisi ndio tunawaelewa na kuwafahamu undani wao. Kisha ndio tunawashirikisha wengine, mfano wazazi na familia.

Wewe ndio unamfahamu huyo jamaa Kwa undani sana. Ni mlevi, mvuta bangi ila still umemkubali, may b kuna vitu ambavyo umeviona kwake.

Ni ngumu kuolewa nae kama mama yako hataki, lakini pia ni ngumu kuachana nae kama moyo wako ndio umemchagua.

Nakushauri usipingane na Mama yako, lakini pia usikubaliane nae. Kwasasa hairisha ilo zoezi la utambulisho au urasimishaji hayo mahusiano yenu. Endeleeni hata kwa Siri, huku ukitafuta namna nzuri ya kuweza kumuaminisha Mama yako kuhusu huyo jamaa. Lakini pia itakupa muda zaidi wa kuendelea kufahamiana nae, maana miezi mitatu uliyojuana nae ni michachr mno, na ni rahisi mtu kuigiza.

With time, mkiwa serious ni rahisi mama kuwaelewa
 
kwasasa ni kama ameacha tangu nimkataze hajanywa na wala hakua mlevi ivyo ni mnywaji tu
- mama hakuchaguliwa baba
-ninae kaka angu ila hamfikii wa lolote kwenye kujituma mpaka maendeleo huyu jamaa yuko mbele sana
jamaa yeye amesema tumpe muda ajithibitishe kuwa ni sahihi na anajitahidi ila mama hamtaki
mpaka biashara anataka kunifungulia ila mama hataki
NIMESOMA COMMENT NYINGI ILA UKIONA HIYO MAMA YAKO ALISHALIWA NA HUYO JAMAA..NDO MAANA ANAWEKA VIPINGAMIZI VINGI SANA USIFANIKIWE.
 
nmeshamshirikisha mamdogo/bamdogo/dada na shangazi wote na wameongea nae jibu ni moja wao hawaoni shida yoyote kwa kijana wanataka kumpa muda ajithibitishe wanashangaa kwanini mama kama anaona anayoona asimuite akasema nae au kwanini asiche muda uongee,kama hata mimi sina haraka ya kuzaa/kuolewa/kuishi

walichogundua mama amekua mbaguzi tu kwamba hata kijana angekuwaje asingemtaka ni chuki yake tu binafsi sio fact
Kwa hio hakuna mtu mwingine anaeweza kumshauri mama abadirishe maamuzi yake kwamba kijana yumempa muda wa kumuangalia tumemuona, mjomba (kaka wa mama) mmemshirikisha maana kuna tamaduni mjomba akisema NO ni big NO hata ufanye nini mjomba akikugomea ndio imetoka hio kaka wa mama yako amesemaje km Shangazi yako amesema ndio mjomba anasemaje ili aongee na dada yake hapo waweke Mambo sawa,
 
Dear we km na huyo shemela mnapendana na mmeweka malengo ya dhati juu ya maisha yenu kwa pamoja endelea kuwa nae, achana na mbambamba za mama, kikubwa wee ni mtu mzima na unajua nn unafanyaa.

Mama mpe heshima yake km mzazi, mambo yako binafsi uamuzi uko kwako na ni haki yakoo. Kumbuka kuwa huyo jamaa unampenda wee na sio yeye, na hata kuishi utaishi nae wee sio yeye, na hata ya ndani zaidi utayajua wee sio yeye.

Kuwa huru na moyo wako kufuata hitaji lako lilipo, usiishi kwa kutaka kumridhisha huyo mama yako utapata tabu sanaaa, mambo mengine usikubali yeye atie mkono wake atakuharibia mipango yako.

Pambania furaha yako wee mwenyewee, sio kupambania furahaa ya mama yako, hilo ni yake yeye.

Nakusisitiza, fuata moyo wako, maisha ni vile wee unaamua, maisha yako binafsi ni juu yako ni hakii yakoo, hupaswi kuingiliwa.
 
Kumkosea heshima au kumuambia ukweli?? Huu Si unafiki sasa? Yaan bahati yake huyo mama hanihusu mbna ningemnyooshaa.

Niliwahi mchana makavu mama angu kisa suala km hili, ila sisi ilikua kwa Kaka.

Yaan nisivyopenda unafikii, mbna huyo mama angeeleza vizuri. Lol.
Sio rahisi kuongea kwa ukali na Bi Mkuwa au Mzee, unahitaji busara mno kuweza kuongea naye vitu ambavyo tayari wana majibu yao
 
Ndo nilitakaa niseme mie amuulize huyo mama ake, yeye kuwa na baba ake alichaguliwa au kwa ridhaa yake, wala hakuna heshima kuvunjwa anapaswa kumuuliza.
Nimemwambia huyu Muhanga kwamba inawezekana hata mama yake anavutiwa na huyo mpenzi wake lakini kama ni single parent family
 
Mama yako yuko sawa.

Yaonesha wewe ndo unalazimisha kuolewa

Maana kama umembadilisha na kumwambia ahame naye akahama, huyo jamaa hajitambui.


Kwanza inakuwaje mwanaume una miaka 38 na huna hata mtoto?
 
Na hivyo vitu sio kivile, pombe ameacha tangu nimwambie mi pia staki hivyo vitu akishindwa kuacha tutakua tu casual amenielewa anayafanyia kazi hayo

ukimuuliza anasema umemtukana
Unazugwa tu.
Ukiolewa tu anaanza

Tabia ni kama ngozi, huibadilishi kamwe
 
Usithubutu kumuamini. Watu wasanii kwenye kutaka kufanikisha mambo yao. Usimlie yamini mlevi anayesema anafanyia kazi ulevi wake kwa ajili yako.
Pombe, Bangi, Sigara haziachwi kwa kuambiwa.
Watu wana Kansa ila wanaendeleza kutumia tu.

Hapo anazugwa atamkumbuka Mama yake
 
Lazimisha uolewe mkuu. Mwanakulitaka mwana kulipata,mtoto akililia wembe mpe

Yaani umembadilisha mazingira na kila kitu inaonekana jamaa ni mario
 
Hizo ni tabia mbaya mtu mvuta bangi ,mnywa pombe waga wanavijitabia wakilewa wengine husahau familia zao ,hela yote anamaliza kwenye pombe au nikuulize wewe binti yako utaeza muoza kwa mwanaume mwenye hizo character??

For me character count a lot ,sinaga ile atabadilika sijui akishanioa atabadilika wanabadilikaga for a mins once akikuoa mwendo ni ule ule
Kuna mifano kibao tu
Hapo bangi itoe sasa maana bangi kete 1 ni shilingi 300 unalewa tosha…Mtut atashindwa kuhudumia familia kisa kafirisiwa na miatatu?
 
Sio rahisi kuongea kwa ukali na Bi Mkuwa au Mzee, unahitaji busara mno kuweza kuongea naye vitu ambavyo tayari wana majibu yao
Yaan sio mie, bora nichukiwe ila kukubali unafiki hiyo hulka sina kwa kweli. Ukweli nitawaambia haijalishi watanionaje au watanifikiriaje sijali kikubwa mie unafiki nimeukataaa.

Tena kwa jambo langu binafsi ndo kabisaa nitawafurahishaa mbna. khaaaah
 
mwambie maisha yanataka "humble beginnings". Pengine atakuelewa
Yani ni mwamba miaka yote mama alikua anasema anatuweka kikao na mabinti wengine kuwa tunachagua sana mabwana, tunataka matajiri
tukipata wanaume wenye mapenzi ya kweli tuolewe haijalishi wana hali gani ila ukipata mwenye upendo unajenga maisha, nikamwambia nina mpenzi nmeanza nae kulala chini ila he took me for granted pia naogopaga kukuletea wakwe mana sina bahati sana na wanaume wazuri wazuri na hata mimi hawanivutiagi ila kwa historia yako unayosemaga unawapa kura za ndio vijana watanashati ila hawaoi tukawa tunaongeaga kawaida sometimes
sasa imetokea mtu aliokua anamsema ndio kanasa kwenye ndoano hamtaki kasahau yote
sasa
 
Ungekuwa ni dada yangu unaolewa na mtu mwenye sifa kama hizo hapo juu ningesikitika. Umetaja sifa za mtu ambaye huwa namkwepa kuwa rafiki yangu wa kutafuta mishe mtaani na jioni kila mmoja kwake, sasa wewe unaenda kumfanya mumeo wa kuishi nae nyumba moja.
Mtumiaji wa pombe
Bangi
Sigara
Ugolo

Hawaachi kamwe
 
mkuu princess ariana hapo kwenye pombe na bangi usipachukulie poa, hivyo vitu vina uraibu MNO na watu wana-struggle sana SANA kuacha.... Yawezekana sana anatumia bado, lakini kwa kujificha... Ni uraibu mbaya mno unaomaliza pesa na afya ya akili... nimeona mengi kwenye hii sekta
Mdogo wangu huyo Mama inawezekana ana mzimia mchumba wa mwanae. Hata kama ni mlevi au mvuta bangi sasa ndio mapenzi yamechukua nafasi awaache waendelee. Huyo Maza ni nongwa tu inamsumbua
 
Habari za saa hii wana Jf
Naomba msaada wenu wa mawazo juu ya swala hili, kama kichwa cha habari kinavyojieleza;
kwa miezi mi3 hii nmekua na mahusiano ya kimapenzi na kijana karibu na maeneo ninayoishi,
  • mimi binti wa 28 yrs Mpenzi ana 38 aliwahi kuishi na mwanamke kwa miaka kadhaa zamani akaachana na mwanamke wake baada ya kuachishwa kazi ( kampuni ilifilisika)
  • Kwasasa ana biashara zake
-wote tumeishia 0- level kielimu
-anataka kunioa pale nikiridhia

sasa tatizo linaanza baada ya mama kuhisi uhusiano baina yetu, anasema kijana hafai kwanza
-ana vuta bangi/pombe
-Hajui kuvaa sio mtanashati
- aliwahi kuishi na mwanamke
-anatoka familia ya kawaida kama yetu kwahiyo hafai hatanisaidia chochote
- hana mvuto mbele za watu
-hana Cv nzuri hata nikimtambulisha
- anahisi kaniroga ndo mana nmekua nae kimahusiano
-kwanza anakaa maeneo ya karibu na nyumbani
-hana hadhi ya kuwa na mimi
sababu ni nyingi!!

Kwa kuliona hilo tukaamua basi ahame makazi tayari kashahama, mazingira yote tumeyafanya yawe mapya,kwa kila kitu cha hadhu anayoitaka mama,nmeshambadilisha huo muonekano kwa kiasi chake ili afanane na anavyotaka mama ila naona pamoja na kutaka aridhike ila kila siku anaanzisha sababu mpya ya kumkataa anasema anajitutumua tu ili anipate na pombe ameacha anipate akishanioa ntapata shida mana atarudi kwenye mambo yake yote!! Pia namdhalilisha kwa wamama wenzie kwa kuwa na mahusiano na jamaa
- mama anasema yuko tayari kwenda kwa mganga yoyote akavunje mahusiano mana kwanza jamaa atakua kaniroga sio kawaida.

Sasa hapo nifanyaje wakuu? maana naona nachanganyikiwa kila siku anaanzisha jambo jipya! ilihali nmemwambia mimi mwenyewe sijasoma! kazi sina wala bishara yoyote na kijana wa watu ameridhia ana fanya kila jukumu lake bila kinyongo ila mama anasema anafanya mana hana hadhi ya kuwa na ww ndo mana inabidi afanye tu...
Kinachoniumiza ni hakuna siku amewahi niuliza changamoto za maisha yangu ya mahusiano. nmejaribu kumwambia wachumba wakija wakijua sijasoma/sina kazi wanagairi haelewi.. anasema umerogwa wewe
nikiomba space nitulize kichwa sipewi naambiwa mpaka utanielewa...
nmepata feeling mama angu ni Toxic /narcissistic mom ila nikieleza hisia zangu yeye ana cheka ndo ananiona kama mpuuzi..
maana mimi nmemwambia kwanini tusimwachie Mungu tu kama Mungu hajapanga tutaachana tu ila kwa ridhaa yetu mengine tutarekebishana sitaki uwe kama unanipangia maisha ila haelewi kabisa , niko njia panda maana maisha nayaona machungu kabisa ni mimi ndo tatizo au mama? nishaurini wakubwa kabla sijashuka presha nikazimika mana bi mkubwa kasema kama ntakufa nife mana ndo ilivyopangwa.
Kama mama anataka mme msomi mwenye hela na hadhi angemwandaa alafu akuozeshe .miaka 28 unasubiki msomi na mwenye hale itafika hatua utasema yoyote ilimradi mradi awe anapumua
 
Mdogo wangu huyo Mama inawezekana ana mzimia mchumba wa mwanae. Hata kama ni mlevi au mvuta bangi sasa ndio mapenzi yamechukua nafasi awaache waendelee. Huyo Maza ni nongwa tu inamsumbua
hata kama.... najaribu kusema tu uraibu wa pombe na bangi sio kitu cha kufumbia macho
 
Back
Top Bottom