Mama Kanumba afurahia mpaka machozi hukumu ya Lulu, asema anaenda makaburini moja kwa moja kumzika rasmi

Mama Kanumba afurahia mpaka machozi hukumu ya Lulu, asema anaenda makaburini moja kwa moja kumzika rasmi

Hakika!! Nakubaliana na wewe. Hapa najiuliza maswali mengi tu - ningekuwa mie ndio Lulu - ningeshukuru kua bora ni hio miaka miwili kuliko kifungo cha maisha, au?? Ningekuwa mama Kanumba - hio miaka miwili inatosha kweli au???
😕😕

Jela ni jela tu hata hii miaka miwili ni mingi sana,cha msingi Lulu na wakili wake wakae watuli,wanaweza chomoka kwa msamaha wa rais,lakini wakianza fujo,mara zakukata rufaa,wanaweza kumbana na mkazio mzito tena
 
Haya mambo magumu mpaka yakupate ndio utaelewa!!!!
Mkuu umenena vyema naona humu watu wana comment wawezavyo kana kwamba wao wana guarantee na maisha yao badae, ni kumuomba Mungu atuepushe
 
Rais anaweza kumtoa..

Japo hata kama asipompa huo msamaha hatokaa zaidi ya mwaka huyo....ila ingekuwa mtoto wa dhalili huku asingetoka mpk atoke madarakani.
 
yule mchungaji anayesema kanumba anatumikishwa na free mason, yuko wapi aje atoe utetezi humu, wasije wakamchukua na huyo lulu, lulu imemkuta bahati mbaya, yule aliyempigia simu usiku siku ya tukio keshajulikana?
 
Tatizo langu sio sheria kuamua.Tatizo langu ni kwa nini afurahie Lulu kufungwa wakati mwanae harudi.

Sheria imechukua mkondo wake ni sawa, lakini sioni sababu ya mama kanumba kufurahi ndo maana namwona Jingajinga.
Mna uhakika gani kuwa kafurah, uchungu wa mwana aujuae mzazi jmn mwanae hatorud lkn atapata amani ya moyo kidogo kuona kuwa at least sheria imefuatwa.
 
Kurufahi kumenipa shaka kidogo na mtu aliua bila kusudi??
Okay wacha tu sheria ifate mkondo wake
 
masikini!hata haisaidii
Hukumu haitamfufua Kanumba lakini sheria lazima ichukue mkondo wake ndio maana zipo Mahakama duniani kote otherwise tungechinjana kama mbuzi.
Hata hivyo mahakama imemhurumia sana nchi za ulimwengu wa kwanza hukumu yake ingekuwa 10+ akitoka hawezi kupata kazi ataanza kila kitu upya. Mara nyingi hata jamii itakutenga utakuwa mpweke na mara nyingi wengi wao hukata tamaa ya maisha.
Ukihukumiwa kwa kosa la kuua kwa kukusudia au kutokukusudia Maisha yako yanabadilika kuanzia hapo tofauti na aliyehukumiwa kwa kosa la kuiba etc.
 
Back
Top Bottom