Mama Kanumba: Lulu ameenda miaka 2 jela na atatoka, Kanumba hatarudi tena

Mama Kanumba: Lulu ameenda miaka 2 jela na atatoka, Kanumba hatarudi tena

Kama kanumba asingekufa angefungwa jela miaka 30 au zaidi kwa kutembea na binti wa Chini ya miaka 18
Alishafikisha miaka18si alikuwa mpaka na leseni?uwongo mwinginee hauna maana.
 
Huyu mama ni mnafiki mpaka malaika waovu wanashangaa.
Hivi na utu uzima wake anadhubutu kuongea hayo matapishi mbele za watu? Haoni aibu mwanae kutembea na katoto kadogo hakajavuka hata miaka 18?
Kuna mambo mengine kama mtu mzima wapaswa kuyapuuzia tuu vinginevyo wajitaftia laana.
 
Alishafikisha miaka18si alikuwa mpaka na leseni?uwongo mwinginee hauna maana.
Hakuwa na miaka 18 wakati yanatokea
d58eaf75a48f51021096da1dec83b43c.jpg

Alishafikisha miaka18si alikuwa mpaka na leseni?uwongo mwinginee hauna maana.
 
Natamani ungejua yote anayopayuka huyu mama
Pamoja na yote mkuu lakini kwa sasa hivi hisia zake zipo juu sana hata zimezuia uwezo wa ubongo wake kufanya kazi vizuri.....kwa hiyo amepoteza udhibiti wa matendo yake na maneno yake........( namtazama katika nadharia ya uchungu wa mwana )......
 
Huyu mama anarohombaya sana, anaposema luluatarudi kanumbaharudi inamaana anataka wamuue lulu au?
 
e5459bab547d52237be2d010e50a49b2.jpg

Siku moja baada ya Elizabeth Michael 'Lulu' kuhukumiwa kifungo cha kutumikia jela miaka miwili kwa kosa la kuua bila kukusudia, mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Frora Mutegoa amesema wanaombeza kwa kuishukuru mahakama wamuache kwa hakuna mwenye uchungu zaidi yake.

Jana baada ya Mahakama Kuu kumtia hatiani mwigizaji huyo na kumpa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela, Mama Kanumba aliishukuru mahakama akisema imetenda haki jambo ambalo lilizusha gumzo wengi wakisema hakupaswa kufurahia adhabu hiyo.

Akihojiwa na waandishi wa habari nje ya mahakama kuu jijini Dar es salaam jana Jumatatu baada ya hukumu kutolewa alisema anashukuru kwa kuwa haki imetendeka na kwamba atakwenda kumzika rasmi mtoto wake.

Hata hivyo, Mwananchi leo Jumanne amesema asibezwe kwa kauli hiyo kuwa hakuna anayejua uchungu anaoupata kila siku.

"Mimi sijui kama ninafurahia kama wanavyodai, waulize kwamba, yeye Lulu alipokufa mwanangu Kanumba alifurahia? Mimi ni mkristo, sipendi kuona baya likimfika binadamu mwenzangu, lakini Lulu ameenda miaka miwili jela na atarudi, je mwanangu atarudi lini? nitamwona wapi tena"? Amehoji.
Na yeye,ajihoji,mwanae alitenda sahihi? Na yeye kama mzazi alichukua hata gani Kabla ya mauti kumfika mwanae?
 
Tunatofautiana mitazamo tu yeye angeruhusu moyo tu ukubali sababu huwezi shindana na nature zaid tumuombee tu kanumba tuamini ipo siku tutaonana nae sie ni wapangaji tu wa dunia hii hapa sio kwetu
Anamsingizia mtoto wa watu bila sababu. Anayetoa na kuchukua uhai ni Mwenyezi Mungu peke yake. Aachane na Lulu. Kanumba naye ana makosa yake. Tusameheane ili maisha yasonge.
 
Kama kanumba asingekufa angefungwa jela miaka 30 au zaidi kwa kutembea na binti wa Chini ya miaka 18
kwa hiyo umeamini hiyo miaka iliyorudishwa nyuma? Muacheni Marehemu apumzike kwa amani.

Sheria ya ndoa inasema mwanamke anaweza kuolewa kuanzia miaka 16 ( wanasheria mnisahihishe kama sipo sahihi )sidhani kama angefungwa

w
 
Kama kanumba asingekufa angefungwa jela miaka 30 au zaidi kwa kutembea na binti wa Chini ya miaka 18
Huyo mama nae aacha ulalamishi usio na msingi. Huyo mwanae naye alikuwa na makosa.
 
basi kama ni hivyo kesi za kuua zingekuwa hazina maana maana hazirudishi uhai au za ubakaji maana haziondoi ukweli kwamba ubakaji ulitokea
 
Alipataje leseni ya udereva ilhali ni mtoto? Au magumashi

Na kama mazazi aliwezaje kumuruhusu kwenda Club usiku? Si kuonyesha tayari amepevuka.
Mimi mwenyewe nilipata leseni bila kufikisha umri unajifanya mgeni tz. Nenda pale tra na laki yako uone kama utaulizwa umri.
Kwenda club watoto wanaenda daily nimekwamvia hivi hata giggy kafikisha miaka 18 mwaka huu.
Wapo wengi vitoto vya shule vinaenda club kumbe ndiyo kwanza viko form 2.
Narudia tena, haijalishi aliwahi gongwa na mababu, haijalishi alianza gongwa akiwa chekechea, haijalishi ni kahaba, ili mradi tu hajafikisha umri wa miaka 18, huwezi jitetea kwa kitumia hoja hiyo.
Two wrongs don't makeup a right.
 
kwa hiyo umeamini hiyo miaka iliyorudishwa nyuma? Muacheni Marehemu apumzike kwa amani.

Sheria ya ndoa inasema mwanamke anaweza kuolewa kuanzia miaka 16 ( wanasheria mnisahihishe kama sipo sahihi )sidhani kama angefungwa

w
Ilikuwa miaka 14, Rebecca alienda mahakamani mwaka juzi kupinga hiyo sheria na ilikubaliwa sijajua kama imebadilishwa tayari.
Nakumbuka ilikuwa ni lazima wazazi wahusike kwenye ndoa hiyo siyo uzinzi uzinzi tu katoto kanabakwa bakea
 
Siku moja baada ya Elizabeth Michael 'Lulu' kuhukumiwa kifungo cha kutumikia jela miaka miwili kwa kosa la kuua bila kukusudia, mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Frora Mutegoa amesema wanaombeza kwa kuishukuru mahakama wamuache kwa kuwa hakuna mwenye uchungu zaidi yake.

Jana baada ya Mahakama Kuu kumtia hatiani mwigizaji huyo na kumpa adhabu ya kifungo cha miaka miwili jela, Mama Kanumba aliishukuru mahakama akisema imetenda haki jambo ambalo lilizusha gumzo wengi wakisema hakupaswa kufurahia adhabu hiyo.

Akihojiwa na waandishi wa habari nje ya mahakama kuu jijini Dar es salaam jana Jumatatu baada ya hukumu kutolewa alisema anashukuru kwa kuwa haki imetendeka na kwamba atakwenda kumzika rasmi mtoto wake.

Hata hivyo, Mwananchi leo Jumanne amenukuliwa akisema asibezwe kwa kauli hiyo kuwa hakuna anayejua uchungu anaoupata kila siku.

"Mimi sijui kama ninafurahia kama wanavyodai, waulize kwamba, yeye Lulu alipokufa mwanangu Kanumba alifurahia? Mimi ni mkristo, sipendi kuona baya likimfika binadamu mwenzangu, lakini Lulu ameenda miaka miwili jela na atarudi, je mwanangu atarudi lini? nitamwona wapi tena"? Amehoji.
Tuachane na mambo ya hisia ukweli ni kwamba Lulu alikuwa anabakwa.
 
Back
Top Bottom