Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ni kweli hakuna kitu ambacho mzazi kinamuumiza kama kuona mwanae anafanya madudu.......kama mama kweli lazma utasikia tumbo la uzazi linauma....matendo mabaya ya mtoto yanaumiza sana kwa mzazi.....
Nasikia na hiyo mitihani hua anafeli tu
Hata kama angetamka kuwa anamkanya lulu kuhusu tabia yake, ila kitendo cha kuishi nyumba ambayo analipia hawara wa mtoto wako tena mume wa mtu ni uthibitisho tosha kuwa anahusika kumpotosha mwanae...
Ila kwa sasa familia nyingi tu mmoja kati ya mtoto kwenye familia akibahatika kupata mwanaume mwenye pesa, sidhani kama mzazi atamkataa huyo mwanaume haijalishi mume wa mtu au lah, huo udhaifu upo kwa wazazi wengi tu sana, pesa mbaya, kinachomponza lulu na mama yake ni UMAARUFU TU. kuna familia zinafanikiwa kupitia wanaume wa watoto au wanawake zao, ni kawaida sana kwa sasa ingawa kwa macho ya mungu haipendezi ila kibinadamu kwa kweli udhaifu kwenye pesa tunao
Inategemea!! mama muhuni anayemuuza mtoto wake hadharani kama afanyavyo mama Lulu,anaumia kwa lipi mwanae akisemwa kwa uovu aufanyao?!!! Mama anatakiwa kuumizwa na tabia mbaya za mwanae kabla yakuumizwa na maneno ya watu dhidi ya mwanae!! Mama Lulu anajiosha tu,ila ukweli anaujua-Lulu asipojiuza basi yeye(mama Lulu haendi chooni)
Ila me nikimkamatia huyu sifi aisee.
Kila kona Lulu lulu lulu,Who is Lulu by the way? wabongo wakiamua kumpa mtu kick utawapenda.Kwan magazeti wamempa kick gan mpya huyu Lulu?Mi ni mgeni jaman.
Kama alimulea na tabia hizo anamlaumu nani!!?
Yaani huyu mama kama angelijua huyo binti anaumiza mioyo ya wanawake wangapi hapa Tanzania angetubu na kumlilia Mungu, Pia akumbuke Mungu ni wa wote hivyo anapoona mtoto wake anaongelewa saana na watu anatakiwa achekeche kwanza asianze kulalamikikia watu na mitandao ya kijamii.
Angalie binti yake ameangukia wapi na amsaidie kwa upendo na ushauri, mtoto hajatimiza hata miaka 25 ana maisha ya mtu wa miaka 35, ajifikirie kwanza.
Halafu atakaje na kusubiri kulishwa na mtoto wake wa miaka 20 na halia anajua uwezo wake, mama anaonekana ni wamama wale wanaokaa kutegemea mabwana za watoto wake. Huyo Lulu angekua kaolewa mama asingekaa home kusubiri mkate kutoka kwa mkwewe, MAMA FANYA KAZI ACHA KUMTEGEMEA MTOTO AKUPE KILA KITU.
Huyo Lulu akifikisha miaka 30 wafanye sherehe ya kifamilia maana maisha yake ni sawa na mtu wa miaka 40 na yeye ana 20, akifika miaka 40 atakua na maisha ya mtu waa miaka 60. Amrudie Mungu.
Nirudieni mimi enyi wanadamu, dhambi zenu hata zikiwa nyekundu kama bendera nitazisafisha na mtakua weupe kama theruji na wala sitazikumbuka tena hizo dhambi zenu. LULU NA MAMA YAKE NAFASI IKO WAZI
Maneno uumba Lulu muda si mrefu atawafata aliowatanguliza.