Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Mama mkwe hataki niolewe na mwanaye kisa mimi ni Mchaga

Baba mkwe alishatangulia mbele ya haki kabaki tu mama mkwe
Basi jitahidini huyu mama apelekwe kwa wazee... ukiweza pata kaka wa huyu mama au mjomba wa mchumba wako pia akiwa upande wenu mtalimaliza hili. Mwambie mchumba wako akaongee na mjomba wake mkubwa kama yupo.
 
Miss chaga hujaolewa hadi leo?
Miss chagga ni mwnamke wa ajabu kweli. Ni wife material hakuna mfano nakuhakikishia. Kiuhalisia alivyo ni tofauti na anavyojionesha hapa JF. Kwa bahati namfahamu tangu akiwa kinda
 
Ushauri hapa utapata mwingi tu tena usiofaa na unaofaa ila all in all majibu ya maombi yetu yanatoka kwenye Biblia,nakushauri OMBA OMBA OMBA kama hii ndoa ipo itafungwa tu hata kama ikisogezwa mpaka mwakani maana wewe si mchaga wa kwanza kuolewa wala hutokua wa mwisho,haya mambo hutokea pindi mnapokua kwenye process ya kufunga ndoa shetani hutafuta kujiinua maana Ndoa ni ibada na hataki ikamilike kwenu so lia na Mungu wako atakushindia jaribu lako pia ongea na wazazi wako itakusaidia kutua mzigo na uchungu moyoni na naimani utapata ushauri mzuri na wakiutuuzima...Pole


Kingsmann

Sent from my Redmi Note 8 Pro using JamiiForums mobile app
 
Ukiwa na shughuri ya ndoa mambo mengi Sana walengwa ukutana nayo na hapo bado changamoto zitakuja nyingi Sana ambazo unaweza ukajiuliza maswali mengi Sana na ukakufuru apo binadamu Hana nafasi katika ushauri dili na Mungu tu funga hata siku tatu mwambie Mungu Kama huyu mwanaume ni wangu nipe Kama cyo wangu naomba aondoke Mungu ujibu usitetereke na aibu pambana na Mungu wako afu mpenzi wako mwache amue yeye afanyaje usimforce afanye hvyo na usije ukabeba mimba omba Kwanza afu utulie Mungu afanye kazi yake.
 
uzoefu ni kwamba mkifikia hatua ya kupata nyumba, gari na kitega uchumi endelevu mkeo anaanza kukuwekea steel wire kwenye chakula ndan ya miaka 5 unakufa kwa saratan ya utumbo!
aisee... hatari sana[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Ukiwa legelege lazima iwe hivyo! Halafu usisahau mchagga huwa anaondoka na mguu mmoja na mwingine unabaki kwao. Ukiwa ngangari kama sie wananyoka ila ujiweze kielimu na kimapato (hapo ungangari wako utakuwa na maana)
Sasa hayo ni mahusiano au vita....?!

Yaani taabu yote hiyo ni kumlazimisha mtu kuishi na mimi atumie pesa zangu na kuishi katika miliki yangu...... Upuuzi wa karne kwakweli.
 
Kusema kweli mikoa ya Mbeya na Iringa kwenu ukisema unaoa uchagani hakuna anayekuelewa.....sijui wachaga waliwafanya nini wazee wetu, nimeishi mikoa yote, wazee wengi wamewasusia watoto wao Proposal za kuoa uchagani

Una uhakika?
 
Sasa hayo ni mahusiano au vita....?!

Yaani taabu yote hiyo ni kumlazimisha mtu kuishi na mimi atumie pesa zangu na kuishi katika miliki yangu...... Upuuzi wa karne kwakweli.
Wewe unatafuta mke au malaika! Kama hutaki kuwa ngangari kwa mwanamke yeyote USIOE, sie tuna uzoefu
 
Ila wachaga nyinyi wenyewe hamu aminiani,mimi kuna rafiki yangu mmoja ni mwalimu wa shule ya primary niliyo soma mimi aliniambia husithubutu kuoa uchagani mpaka nilimshangaa.
 
Binti, kikubwa uwe umempenda kweli na ujitoe kuolewa na huyo mmakuwa wako. Mimi nke yangu ni Chagga kama wewe, wazazi wakati naoa hasa mama alikataa akisema ukioa mchagga utaenda kujenga kwao na bla bla. Nikamwambia wangu hayuko hivyo. Nikaoa mchagga wangu na sasa tuna mtoto ni zaidi ya umri wako. Kingine, kwa sasa yeye ndiye kipenzi cha mama ingawa wadogo zangu wameoa kabila letu ila hawamjali kama nke wangu anavyomjali. Kuna siku nilimuuliza kama anakumbuka alivyokuwa anasema, akasema ni maneno ya watu.

Zidisha kumleta mama mkwe karibu. Mfano ondoka huko ulipo ukae naye wiki moja alipo utaona atakavyobadilika mama mkwe wako to be
mkuu kipimo cha mke mzuri ambaye umeamua kumuoa licha ya wazazi kukataa ni baada au kabla ya hiyo ndoa yenu

mwanamke au mwanaume yeyote yule anayejielewa hawezi kukubali kumtenganisha na mume au mke wake na wazazi na ndugu kwa ujumla au kukubali kuona mume au mke wake anacut the ties na ndugu/wazazi wake,ukiona anaunga mkono wewe kucut the ties na wazazi/ndugu zako jua kabisa hapo umepata koroma na hata bila kuambiwa wewe jiondoe upesi

kwa hiyo huyo wa kwako ni mzuri kwa asili ndo maana amekuwa favourite ya kwenu, kwa hiyo wa kwenu walimkataa mwanzoni kwa myth tu bila kujali utu wake yeye kama yeye na yeye ndo akawaproove wrong,

sasa tulio wengi huwa tunafeli kuwaproove wrong wale waliotukataa au labda waliotukataa waliona uhalisia wetu na sisi tuliopenda tukapofushwa na mapenzi na baadae tukaanza kujutia maamuzi yetu na kuona sababu halisi za kwa nini wazazi au ndugu zetu walituonya kuhusu watu hao, na ndo hapo inabakiaga aliambiwaga lakini hakusikia
 
Maamuzi anayo mumeo mtarajiwa(mchumba).

Ila angalia miaka 30 mbele, usipokubalika wewe ujue hata wanao, wajukuu wa mama mkwe wako hawatakubalika.

Kama amani hakuna usilazimishe, japo wanaume ni wachache ila bado wako wengi duniani.

Kama una roho ya kupambana ingia ulingoni olewa, ila usilazimishe sasa hivi halafu baada ya miaka 2 ukimbie ndoa kuwa mama mkwe sio... dalili umeziona mapemaaa.

Mapenzi yatakuumiza, ukiyapuuza uliyempenda sana pia unamsahau vilevile na anakuja mwingine anakava nafasi ya jamaa.

NB: Kiukweli nimesoma kichwa cha uzi tuu, uzi wenyewe sijausoma [emoji12][emoji12]
Nadhani huu ni mtizamo,nami nitoe mtazamo wangu;
Kwanza ndoa maana yake ni nini?ni mahusiano ya hiyari baina ya ridhaa ya wawili.
Kwa muktadha wa jamii za kiafrica,ndugu wamekuwa wakipotosha "Taint" maana halisi ya ndoa na tafsiri yake hapo juu kwa kuingiza mitazamo yao kwenye mtazamo wa mtu aleyefanya maamuzi kwa kujiridhisha kwa mengi,nasikitika kusema,huu ni unyanyapaa wa mtu kujiamulia na mawazo yake kuheshimiwa.
Ki uhalisia,Mama mkwe,Baba mkwe na ndugu wengine wote, "hawatakiwi kumpenda mwenza"...wanatakiwa wamkubali! Maana wewe ulishampenda,kazi yao ni kumkubali na kuheshimu maamuzi yako,otherwise; Upande wako wanakujua; We mjinga,huna maamuzi,umelelewa bila misingi ya malezi bora na ya kujitegemea,hapo wanaweza wakakumudu!
Wazazi, tatizo la hili suala,sio makabila wala rangi au nini,,tatizo ni nyie wenyewe mmewaleaje watoto kuwa wawajibikaji kwenye maisha kiujumla,mathalani; Kielimu,Kiimani, Kijamii, Kiuchumi etc.
Huko ni kujificha kwenye makosa yenu ya msingi kwa kiraka cha; kabila flani,dini gani,rangi gani etc.
Lazma vijana walelewe vyema,na waachiwe uhuru na experience ya ulimwengu unakwenda ksai sana na mabadiliko ya haraka.
 
Wapendwa tumeongea mengi sana humu na kiukweli ni wazi kuwa mwenzetu anahitaji msaada na yuko njia panda na anapitia wakati mgumu sana kwa sasa

ila naomba tu nikumbushe kitu kimoja muhimu sana hapa duniani,kwani nimeona kuna wengine wanaongea katika namna ya wazazi nini banah as long as we umependa basi kazi imeisha

wapendwa naomba tukumbushane kuwa hata sisi ambao leo ndo tuko kwenye process ya kufunga ndoa ni wazazi watarajiwa ambao baadae tutakuwa na mabinti na vijana wetu ambao tungependa watusikilize na watuchukulie sisi kama part ya Maisha yao na watilie maanani maoni na maadili tuliyowapatia,jiulize wewe leo ni mzazi unamuonya mwanao kuhusu kuoa au kuolewa na mtu Fulani kwa sababu umeona wazi kuwa anaweza kumletea shida huko mbeleni,ungependa mwanao aitikieje? ungependa kumwacha mwanao ajiingize kwenye ndoa ambayo itamletea matatizo hapo baadae? au afanye chochote ambacho kitamsababishia shida hapo baadae?

actually sio kila sababu ambayo mzazi anaimpose ina maana au inaweza kutuletea shida kama tutaamua kwenda nayo kinyume,mf mzazi anamkataa mwanamke kwa sababu mbaya hana mvuto mtazaa watoto vituko,au labda hamtaki mwanaume kwa sababu ni masikini hana pesa,what the heck ?????????? Lakin kuna mambo ambayo wazai wetu wameona kwa sababu ya kuishi kwingi hivyo wanapojaribu kutupa opinion zao zenye mashiko na ambazo ni fact tujaribu kupima uzito wa yale wanayotuambia,kwa sababu mara nyingi maonyo ya wazazi huwa hayaanguki hivi hivi,esp kama ni facts.

My take kwako miss chuga kamwe usipuuze hisia za mama ya mume wako kwa sababu hata wewe kuna siku utakuja kuwa mama mwenye uchungu na upendo sana kwa kijana au binti yako,sidhani kama ungefurahia kuona kijana wako anacut ties na wewe au kupuuza vile unavyohisi kwa ajili ya mwanamke au mwanamume mwingine esp kama utakuwa na sababu za msingi za kutenda au kusema kwa namna moja ama nyingine.

kama unaamini unaweza kumproove wrong mama mkwe na kumfanya ajutie maamuzi ya kukutatalia kuolewa na kijana yake,basi jairibu kutumia hata watu wazima wamshawishi ili akubaliane na ndoa yenu hata kama ni kwa shingo upande ili baada ya hapo umuoneshe kuwa kijana wake hakukosea kukuchagua wewe kama mke

last option kama unaamini umedhamiria kujenga mji na huyo mume wako na unaamini una uwezo wa kurudisha uhusiano mzuri uliopo baina ya mama na mwanaye na kumprove wrong mama mkwe na kama umejaribu mbinu za kutumia watu wazima ikashindikana,basi kafungeni ndoa bomani na mashahidi wenu wawili tu bila kuhusisha upande wowote wa ndugu au wazazi kisha baada ya hapo uanze kazi ya kumrudisha mume wako na mama yake warudi kwenye good terms na kumuonesha kijana wao hakuksea kukuchagua wewe,na kamwe usiache kwani ukifanikiwa utakuwa the best mkwe ambaye wamewahi kuwa naye,na pengine wanaweza kuwa upande wako kuliko unavyotarajia kiasi hata wewe ukikosea wanaamini kijana wao ndo ana shida,mara nyingi ndoa ni kujisacrifice kwa ajili ya furaha ya mtu mwingine

tofauti na hapo usijjingize kwenye hiyo ndoa my dear,ni kweli ndoa ni ya watu wawili,lakini ndoa haipo kwa ajili ya kuwatenganisha na wazazi na ndugu au mahali tulipokulia,na kuna wakati tu katika maisha yetu mtawahitaji wazazi au ndugu au watu wowote zaidi ya ninyi wanandoa wenyewe,thats the fact of life,unaweza ukashangaa mkilazimisha bila bidi yoyote ya kushawishi wazzai hata huyo mumeo ikitokea ishu yoyote serious kati yenu anaweza akaongea maneno yakakuvunja moyo kabisa,utasikia anasema ndo maana mama yangu alikataa ndo mambo kama haya sasa najutia bora ningemsikilizaga mama yangu,

haya mapenzi ni ya mwanzoni tu my dear,ndoa zina mengi marriage is not a bed of roses, inaweza ikafika point mkachokana jamaa anaweza amua hata kuoa mke mwingine kwa kisingizo tu mama yangu aliwahi kunikatalia ila nililazimisha tu ,na wakati huo ukose backup yoyote ile

usilazimishe kuna watu waliachwa siku ya ndoa yenyewe wanasubiria mume/mke kanisani haonekani hiyo aibu yake na maumivu yake hayawezi kufananishwa na hatua uliyofikia wewe,na bado baada ya muda mfupi tu wakapata wenzi wazuri na bora kuliko hao waliowaacha,

so please my dear usifanye maamuzi kwa kurupuka,omba sana mwongozo wa Mungu,tafakari na uchukue hatua,utakuja kuwa mama siku moja na labda ndipo utakapoweza kuzielewa vizuri Zaidi hisia za mama mkwe wako kwa sasa(esp kama ana sababu za msingi kuamua uamuzi wa namna hiyo na hajaamua kuweka wazi)
 
Relax usifanye maamuzi yatakayo kugharimu huko mbeleni

Kama mwanaume hana uhakika na upendo wake kwako basi hata ukibeba hiyo mimba itakua ni kujiongezea majanga wewe mwenyewe
 
Hahahahahahaaha akinipenda Mume inatosha au siyo
Mimi ninaamini ndoa ni ya kati ya watu wawili wanaopendana. Hao wa pembeni ni Ziada tu. Imeandikwa Mwanaume ataachaje na baba yake na ataambatana na mkewe na watakuwa mwili mmoja. Nimefurahi kuwa huyo kijana anakupenda sana na ninakuhakikishia hatokuangusha huyo. Shikaneni na pendaneni mpaka kieleweke. Fungeni ndoa yenu hiyo August 2021 kwa FURAHA zote. Asiyekutaka anywe sumu.
 
Acha tu Hawa wamama wakati mwingine sijui wanakuwaga wachawi wanapewa mashart uko watoto wao wasioe hata sielewi maana kaka ake naye amezaa na mdada wa uko kwao ika Bado mama naye hataki amuoe uyo dada anadai eti ana kiburi na wakati wameshazaa, Aya huyo mmakua mwenzao ana kiburi na Mimi huku ni mchaga yani hana jema hata kidogo hata na mimi ningekuwa mmakuwa Bado angesema labda Mimi mkorofi hakosi sababu ndomana mtoto wake amesema anamjua vizuri mama yake ndomana kachukua maamuzi magumu
Mimi mama mkubwa wangu Mnayakyusa aligoma kwenda kwneye sherehe ya mwanae kisa kaoa Mchagaa jamaa hata hakujali yanii[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Hadi leo wanadundaa alafu bro kafanikiwa kichiziii yani. Mama ake hajawahi kwenda kwa mwanae hata siku moja yani hataki hata kusikia!! Hapo bro alishazaa na wanawake watatu tofauti ambapo mama yake aliwakataa wawili huyu wa nne bro akasema liwalo na liwee yani

Sent from my SM-G611K using JamiiForums mobile app
 
Mkuu nikweli au ni story za vijiweni tu, lakini mbona mwanzo wa uchumba huwa wanakuwa na upendo mkubwa sana, maana nakumbuka nilibadilisha namba ya simu lakini haliweza kuja kunitafuta mkoa nilipo mpaka akanipata kwa picha tu
Duh aisee aliktafuta kwa picha mpaka akakupata,vipi mmeoana?
 
uzoefu ni kwamba mkifikia hatua ya kupata nyumba, gari na kitega uchumi endelevu mkeo anaanza kukuwekea steel wire kwenye chakula ndan ya miaka 5 unakufa kwa saratan ya utumbo!
Aisee imefika huku mkuu.Inaogopesha.
 
Back
Top Bottom