Mama Samia Suluhu wakumbuke watumishi wa CCM wanaoteseka kwa dhiki haswa wale wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM

Mama Samia Suluhu wakumbuke watumishi wa CCM wanaoteseka kwa dhiki haswa wale wa Jumuiya ya Wazazi ya CCM

DATAZ

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2012
Posts
3,799
Reaction score
10,196
Naamini sijakosea kukuita Mwenyekiti mpya wa CCM, leo siku moja kabla ya uthibitisho wako. Naamini utakuwa ndiye tena kwa kura zoote, ni suala la muda tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti naomba nikueleze kuwa wako waliokuwa watumishi ndani ya CCM na hasa katika shule zilizokuwa chini ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM ambao wako hoi kimaisha, na wengine wameshakufa ili hali haki zao hawajapata. Wengi hawajipwa haki zao za NSSF, MISHAHARA NA VIINUA MGONGO hadi katika uzee wao.

Hawa nao ni watoto wako kama Mama na Kiongozi katika Chama. Wewe ndiye wakufuta machozi yao na dhiki yao kwani naamini Mungu amekuleta kwa kusudi.

Chonde chonde Mheshiwa Mama Mwenyekiti, wakumbuke watu hawa kwani wametoa mchango wao kwa chama na taifa na sasa wanaugulia kwa njaa na dhiki za maisha ili hali haki zao zinajulikana.
 
Dah! Ni Kwa muda gani wameishi kwenye dhiki namna hiyo?
Nalog off
 
Mambo ya chama sio Ajira za kujitolea
Ni moyo wako kusaidia jamii
Waendelee kujitolea uzalendo kwanza
 
Mbona mwendazake hamjawahi kumwambia haya mambo nyie si mna kodi majengo shule viwanja sasa mnalialia nini, tulieni mama afanye kazi ana mambo muhimu ya watumishi wa umma kwanza
 
Naamini sijakosea kukuita Mwenyekiti mpya wa CCM, leo siku moja kabla ya uthibitisho wako. Naamini utakuwa ndiye tena kwa kura zoote, ni suala la muda tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti naomba nikueleze kuwa wako waliokuwa watumishi ndani ya CCM na hasa katika shule zilizokuwa chini ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM ambao wako hoi kimaisha, na wengine wameshakufa ili hali haki zao hawajapata. Wengi hawajipwa haki zao za NSSF, MISHAHARA NA VIINUA MGONGO hadi katika uzee wao.

Hawa nao ni watoto wako kama Mama na Kiongozi katika Chama. Wewe ndiye wakufuta machozi yao na dhiki yao kwani naamini Mungu amekuleta kwa kusudi.

Chonde chonde Mheshiwa Mama Mwenyekiti, wakumbuke watu hawa kwani wametoa mchango wao kwa chama na taifa na sasa wanaugulia kwa njaa na dhiki za maisha ili hali haki zao zinajulikana.
Rais anamajukumu mengi sana kitaifa muhimu sana kuliko hao ulio wataja.
 
Mbona mwendazake hamjawahi kumwambia haya mambo nyie si mna kodi majengo shule viwanja sasa mnalialia nini, tulieni mama afanye kazi ana mambo muhimu ya watumishi wa umma kwanza
Hongera sana mkuu kwa mchango wenye nia ya kulijenga taifa
 
Mambo ya chama sio Ajira za kujitolea
Ni moyo wako kusaidia jamii
Waendelee kujitolea uzalendo kwanza
Kwanza ni waporaji wa mali za watanzania kama vile kujimilikisha viwanja
 
Kwanza ni waporaji wa mali za watanzania kama vile kujimilikisha viwanja
Hapa tunazungumzia mamia ya watumishi wasio na hatia. Hao wapora viwanja si mahala pao hapa
 
Huyu mtu mmoja anasumbuliwa toka kila upande, haya mambo ya uenyekiti wa chama awaachie wengine abaki na mambo ya kitaifa tu.
 
awasaidie kwa pesa za ccm au kwa kodi za watanzania wote?
CCM ina vyanzo vingi vya mapato. Ni hekima na busara tu vilikosekana hadi kuacha watu wasio na hatia katika mateso makubwa
 
Huyu mtu mmoja anasumbuliwa toka kila upande, haya mambo ya uenyekiti wa chama awaachie wengine abaki na mambo ya kitaifa tu.
Uenyekiti ni taasisi kama ilivyo kwa Uraisi.
 
Chonde chonde Mheshiwa Mama Mwenyekiti, wakumbuke watu hawa kwani wametoa mchango wao kwa chama na taifa na sasa wanaugulia kwa njaa na dhiki za maisha ili hali haki zao zinajulikana.
Sema ukiwakuta wanaisifia CCM dah utadhani wanaishi peponi na wewe ndio uko peke yako jehanamu. Sema wana ujasiri wa hali ya juu.

Siwezi kutetea kitu wakati naumia, yaani baadae mkiwa wawili anakufuata anakukopa, unabaki unashangaa tu
 
Wapinzani na Watanzania wanaojitambua pamoja na dhiki zao lakini naamini wanaishi maisha ya amani na furaha zaidi kuliko pro-ccm
 
Naamini sijakosea kukuita Mwenyekiti mpya wa CCM, leo siku moja kabla ya uthibitisho wako. Naamini utakuwa ndiye tena kwa kura zoote, ni suala la muda tu.

Mheshimiwa Mwenyekiti naomba nikueleze kuwa wako waliokuwa watumishi ndani ya CCM na hasa katika shule zilizokuwa chini ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM ambao wako hoi kimaisha, na wengine wameshakufa ili hali haki zao hawajapata. Wengi hawajipwa haki zao za NSSF, MISHAHARA NA VIINUA MGONGO hadi katika uzee wao.

Hawa nao ni watoto wako kama Mama na Kiongozi katika Chama. Wewe ndiye wakufuta machozi yao na dhiki yao kwani naamini Mungu amekuleta kwa kusudi.

Chonde chonde Mheshiwa Mama Mwenyekiti, wakumbuke watu hawa kwani wametoa mchango wao kwa chama na taifa na sasa wanaugulia kwa njaa na dhiki za maisha ili hali haki zao zinajulikana.


Waache waonje joto la jiwe , si walishabikia udhalimu, matunda yake ndio hayo na wayale tu
 
Back
Top Bottom