Mama wa pacha waliotenganishwa asimulia alivyoambiwa amezaa laana, adai baba mtu alimtelekeza

Mama wa pacha waliotenganishwa asimulia alivyoambiwa amezaa laana, adai baba mtu alimtelekeza

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
pic.jpg

Siku tatu sasa tangu pacha Rehema na Neema waliokuwa wameungana kufanyiwa upasuaji na kutenganishwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), mama mzazi wa pacha hao, Amina Amos amesimulia visa na mikasa aliyokumbana nayo baada ya kujifungua pacha hao.

"Niliambiwa nimezaa laana, nimeleta mkosi, kwenye jamii yangu wapo walionitenga, nikawa najiuliza marafiki zangu wamepata watoto lakini mbona hawapo kama wangu?!.. nilijiuliza mno kwa nini mimi?" amefunguka Amina.

Ni mara ya kwanza mama huyo mwenye umri wa miaka 17 kuzungumza na waandishi wa tangu alipofika Muhimbili na hadi pacha wake hao kufanyiwa upasuaji wa ubingwa wa juu ulioandika historia mpya kwa Tanzania Julai mosi, 2022.

"Nimepitia changamoto nyingi lakini sasa hivi nina furaha kwa sababu napata mahitaji ya watoto hapa Muhimbili wamenipa msaada mkubwa na nimelelewa vizuri pamoja na Wanangu.

"Namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa kuwawezesha wataalamu kufanikisha upasuaji wa pacha wangu. Napenda kushukuru Taifa letu na Muhimbili kwa kuweza kutenganishia pacha wangu salama pamoja na madaktari wote wa ndani na nje ya nchi.

"Nashukuru sana wauguzi wa kitengo cha PIKU (wodi maalum ya kulaza watoto wachanga wenye umri kuanzia miezi 28 hadi miaka 14), wamenilea vema na wanangu na wamenisaidia sana."

Amesema baba wa watoto hao alimtelekeza baada ya kuona watoto wameungana

pongezi.JPG
Ameongeza kuwa kizungumkuti alichonacho sasa ni namna gani atakavyowalea pacha wake baada ya kutoka hospitalini hapo pindi watakapopewa ruhusa, akidai baba watoto wake amemtelekeza.

"Mwanzo mtihani niliokuwa nao ni jinsi gani nitawalea wakiwa wameungana, wametenganishwa sasa nina furaha na nashukuru sana lakini sasa naanza kujiuliza nikitoka hapa itakuwaje?"

Akizungumza, Katibu Mkuu wa Wizata ya Afya, Profesa Abel Makubi aliyefika hospitalini hapo kumjulia hali mama huyo pamoja na pacha wake, kwanza amekemea tabia ya unyanyapaa kwa watu waliopata watoto wenye changamoto kama ilivyo kwa pacha hao.

"Nimewaona pacha wanaendelea vizuri baada ya upasuaji, tuzidi kuwaombea kwa Mwenyezi Mungu ili hali zao zizidi kuimarika zaidi, lakini bado kunaonekana kuna unyanyapaa katika jamii kwa watoto hawa.

"Serikali itaendelea ku-support malezi/makuzi yao kwa kuwa tumeanza nao, lakıni pla natoa rai kwa wadau wengıne waje tushirikiane pamoja kuhakikisha wanapata lishe vizuri, wakue na waendelee na maisha yao," - Profesa Makubi

Pamoja na hayo, Profesa Makubi amewasilisha salamu za pongezi kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu kwa jopo la wataalamu waliofanikisha upasuaji huo.

"Mh. Rais Samia Suluhu na Mhe Ummy Ally Mwalimu Waziri wa afya, wanatoa pongezi sana kwa watalaamu wetu nchini wakishirikiana na wale wa chuo kikuu cha Bahrain kwa kufanikisha 'operation' kubwa ya upasuaji wa pacha hawa," amewasilisha salamu hizo.

Akizungumza, Mkuu wa Kitengo cha Watoto Muhimbili na Daktari Bingwa wa Upasuaji Watoto, Zaitun Bokhari ameshukuru wamepokea salamu za Rais Samia na Waziri Ummy.

"Tunaishukuru Serikali kwa sababu imefanya kazi kubwa kuwekeza katika miundombinu, imeimarika na leo tumeweza kutanya upasuaji huu.

"Hawa wataalamu wenzetu walipokuja na kuona miundombinu yetu, waliona ipo vizuri na wakasema tunaweza kufanya hapa hapa," amebainisha.

Upasuaji huo ni wa tatu kufanyika nchini na umefanyika kwa mafanikio makubwa na kuandikia Tanzania historia mpya.


Source: Matukionamaisha.blogspot.com


Pia soma >>
Muhimbili yasema upasuaji wa watoto pacha umefanyika kwa mafanikio
Watoto pacha walioungana kufanyiwa upasuaji Muhimbili, leo Julai 1, 2022
 
Baba wa mapacha aliye watelekez kwa sasa kama na mwona anavyo tafta mbinu ya kujirudi kwa wanaye baada ya kusikia wametenganishwa
 
Baba wa mapacha aliye watelekez kwa sasa kama na mwona anavyo tafta mbinu ya kujirudi kwa wanaye baada ya kusikia wametenganishwa
Sure, huko alipo anaona soni sana, hata ndugu nk wote wanapata soni kubwa sana but jamaa arudi aombe poo kwa mama watoto, ndg na jamaa maisha yasonge japo hata bila huyo jamaa tayari watoto wataishi kwa 10 percent kutoka hazina.
 
Mambo ya siasa yanachanganya sana.
Sasa yule katibu wa CCM alipeleka taarfa gani na alienda kukagua nini.
Huyu Makubi ni Professor na Katibu mkuu wa wizard ya Afya,
Kapeleka salamu za Mama yake aliyemteua ni sawa, sasa na Najiuliza yule alipeleka salamu za tweeter?
Wana siasa kwa kiki...
Yaan uchawa kila sehemu huu sasa sio uchawa ni uchawi.
Wasije Watoto watachelewa kupona maana wengine wana macho maovu ktk nchi hii.
 
Kasepa hataki laana eti...

Hizi mila potofu zinanyanyasa sana wanawake wakijifungua mapacha na walemavu wa ngozi yaani albino
Nimekumbuka evil forest walikokuwa wanatupwa mapacha kwenye kile kitabu cha things fall apart
 
Miaka 17?
Unashangaa nini miaka 17 kuitwa mama kwa mazingira ya kijijini, Hujui kama watoto wa kike wanaanza darasa la kwanza na miaka 5 mpaka 7? Hujui kama watoto wa kike huvunja ungo kuanzia miaka 9? Twende sawa kwanza kama alianza darasa la kwanza na miaka 7 atamaliza la saba na miaka 14, hakuchaguliwa kwenda sekondari atakuwa na nini kilichobaki zaidi ya kuolewa? Huoni kajitunza sana toka miaka 9 mpaka 17? Tumwombee kwa Mungu watoto wake zikawe nyota zinazongára ili huyo baba na ukoo wake wajue kuwa Mungu ni mkubwa kuliko ukoo wa watu fulani. Mungu wabariki Rehema na Neema wana stori ndefu ya kuja kuisimulia dunia.
 
Miaka 17?kumbe jamaa alibaka sasa
... huyo mdada mjanja sana! Baada ya baba mtu kumkimbia kaona namna ya kumwingiza kingi (kumkomoa) ni kushusha umri wake to 17 ili msela automatically aingie kwenye kesi ya kubaka! Hata kama itathibitishwa vinginevyo hapo baadaye, jamaa atakuwa ameonja joto!
 
Unashangaa nini miaka 17 kuitwa mama kwa mazingira ya kijijini, Hujui kama watoto wa kike wanaanza darasa la kwanza na miaka 5 mpaka 7? Hujui kama watoto wa kike huvunja ungo kuanzia miaka 9? Twende sawa kwanza kama alianza darasa la kwanza na miaka 7 atamaliza la saba na miaka 14, hakuchaguliwa kwenda sekondari atakuwa na nini kilichobaki zaidi ya kuolewa? Huoni kajitunza sana toka miaka 9 mpaka 17? Tumwombee kwa Mungu watoto wake zikawe nyota zinazongára ili huyo baba na ukoo wake wajue kuwa Mungu ni mkubwa kuliko ukoo wa watu fulani. Mungu wabariki Rehema na Neema wana stori ndefu ya kuja kuisimulia dunia.
Acha hadithi ndeefu mara ungo mara kijijini, sheria ya mtoto na penal code zinasemaje kama si ubakaji?
 
Acha hadithi ndeefu mara ungo mara kijijini, sheria ya mtoto na penal code zinasemaje kama si ubakaji?
Sheria inatambua mtoto miaka 18, sheria hiyo hiyo inaruhusu msichana kuolewa akiwa na miaka 14 nionyeshe amendment ya hiyo code.
 
Acha hadithi ndeefu mara ungo mara kijijini, sheria ya mtoto na penal code zinasemaje kama si ubakaji?
usikimbilie kutaja sheria kaisome kwanza ndo urudi ikiwa hairuhusu msichana kuolewa chini ya miaka 18
 
usikimbilie kutaja sheria kaisome kwanza ndo urudi ikiwa hairuhusu msichana kuolewa chini ya miaka 18
Unafahamu tafsiri sahihi ya kifungu cha 13 cha sheria ya ndoa na lengo la bunge kukitunga? Au unabwabwaja tuu, unafikiri kama tafsiri yake ilikuwa ni ya Plain rule ( Litera legis) bunge lingepitisha sheria nyingine baafaye ambayo ukisoma plainly utadhani kuwa ina kinzana? Je ! Hata kama kama ingekuwa hivyo kwenye suala la mtoto sheria sheria ya mtoto ina stand
 
Back
Top Bottom