Mama wa Rayvany anauza mbogamboga na Mama wa Martha anauza Juice. Maisha ya wasanii ni magumu sana

Mapema yote hii umeamka na maisha ya Watu kichwani mwako? Sidhani kama Leo utapa nafasi ya kutafakari maisha yako na hatima ya familia yako!
Wao si ndio wanawake maisha yao tuyajue mitandaoni? Sada endelea na Show Off harafu ukibroke uone kama tutaacha kukusema.

Kama unayaonesha hadharani inakuwaje usitake.kusemwa hadharani?
 
Uko sahihi. Wa kuwaboreshea ni watoto.
Wawawekee mazingira mazuri ya kuuza vitu fresh kulingana na dunia ya sasa.
 
Mama wa Rayvanny ni mlokole . Huwa hataki pesa za mwanae sababu anaamini ni pesa ambazo zimepatikana kwa njia za kishetani na hazina upako ndani yake.

Anauishi mstari wa Biblia unaosema ; "Heri walio maskini wa Roho maana ufalme wa mbinguni ni wao."
 
Hapo umemaliza Mkuu! 👏👏👏
 
Kuuza mboga sokoni kuna tatizo gani??
 
Bimkubwa ana watoto wanne wakiume wote tunajiweza. Ila kila siku jioni anapika mikate anauza ambapo faida yake kwa siku ni kama 6000. 6000Tsh ndio faida yake kwa siku pesa ambayo anaiweza kuipata bila kufanya kazi,ila anaskia raha kuifanya ile kazi yake na kuzalisha kipato chake hata kama kidogo.
 
Afu watu hawajui, Bustani za mboga zina hela balaa, nilishawahi fanya,
Ila mie walikua wanakuja bustanini wenyewe walanguzi, pesa nayopata hadi mwenyewe siamini.

Ni biashara nzuri yenye hela hatarii, mchicha, tembele, pitiku, sukuma wiki, mnafu, Chinese, spinach, etc
 
umenena mkuu
 
Uko sahihi. Wa kuwaboreshea ni watoto.
Wawawekee mazingira mazuri ya kuuza vitu fresh kulingana na dunia ya sasa.
Si lazima mtoto aboreshe, mama anaingiza pesa kila siku hapo hizo pesa zitumike kuboresha na mtoto ampe mama idea na jina lake aliingiza kwenye biashara ya mama mambo yanaenda..... Unajua mboga mboga kufunga faida ya 20000 ni kawaida!!
 
Wasanii wa Tz ukiachana na showoff zao, Ila kiufupi wana maisha magumu Sana .

Mama wa Rayvanny yupo mbeya sokoni anauza Mboga za majani za reja reja.

Na mama yake Martha anaokota machupa na kuuza juice.


This industry is all about shit.
Si kila mzazi hupenda kumtegemea mwanae akiwa na nguvu.Wengine ni hulka yao kufanya kazi teache hizo mindset
 
Watu hawaelewi tu... Bustani Ina hela mdogo wangu.,... Wamekalili mpaka wafungue maduka Kodi kubwa wakae kupiga picha hapo. Wakati chinese, spinach ,sukuma wiki unavuna miezi mitatu na ukipanda ni siku 21 tu unaanza kuchukua maokoto.
 
Wasanii wa Tz ukiachana na showoff zao, Ila kiufupi wana maisha magumu Sana .

Mama wa Rayvanny yupo mbeya sokoni anauza Mboga za majani za reja reja.

Na mama yake Martha anaokota machupa na kuuza juice.


This industry is all about shit.
Kufanya kazi ni baraka, kufanya kazi ni lazima

Tangu kuumbwa kwa dunia Mungu alimwamrisha binadamu afanye kazi!

Na ndio maana alimpa Bustani ailime na kuitunza!

Kazi ni lazima haijalishi una pesa ngapi unless una afya isiyo njema au umri mkubwa
 
Kuna wazazi wanapenda kazi ili kulinda identities zao. Kuwapa pesa sio kigezo cha kuacha kazi zao.

Ila kuna wazazi ambao watoto hawajali kabisa kama wapo na pengine wanahitaji ukaribu wao.

Mara nyingi watoto wanakuwa busy hasa na mapenzi ya kutambulika, kuliko kuangalia wametokea wapi.

Diamond hamsahau mama yake na nahisi kama ana tofauti kubwa na wasanii wengi sana
 
Vipi kuhusu baba yake?
 
Watu hawaelewi tu... Bustani Ina hela mdogo wangu.,... Wamekalili mpaka wafungue maduka Kodi kubwa wakae kupiga picha hapo. Wakati chinese, spinach ,sukuma wiki unavuna miezi mitatu na ukipanda ni siku 21 tu unaanza kuchukua maokoto.
Labda wanaidharau jinsi ilivyo kazi enyewe, ila wangejua maokoto yako hapo wasingesema.

Wawaache wamama wa watu wajitafutie pesa zao wenyewe.
 
nafikiri tatizo sio biashara ya mbogamboga shida hawa wasanii wanatabia ya kuigiza maisha na kutengeneza picha flani kwa watu kwamba maisha wameyapatia kumbe sio ualisia jambo ambalo ndio usani wenyewe na watu hawaelewi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…