Mama wa Rayvany anauza mbogamboga na Mama wa Martha anauza Juice. Maisha ya wasanii ni magumu sana

Wasanii wa Tz ukiachana na showoff zao, Ila kiufupi wana maisha magumu Sana .

Mama wa Rayvanny yupo mbeya sokoni anauza Mboga za majani za reja reja.

Na mama yake Martha anaokota machupa na kuuza juice.


This industry is all about shit.
Kwa hiyo mama zao wakiuza juice na mboga mboga ndio maisha ya wasanii yanakuwa magumu?

Au mtu akiwa msanii inatakiwa mama yake auze nini, magari?
 
Kwahiyo kuuza mboga mboga na juice ndio ugumu was maisha kwa tafsiri Yako sio!!?

Kwani wewe tafsiri ya maisha magumu na rahisi ni ipi!!?

Wewe naona ndio una matatizo man!
Hata kama ni maisha magumu, si ni ya mama zao?

Kwa hiyo wawalazimishe mama zao nao wawe wasanii?

Unaweza kumpangia maisha mkeo tu, siyo mama yako.
 
Ndo shida ya Utajiri "Mweusi" lazima mmoja kwenye familia yako ateseke!
 
...
 

Attachments

  • Screenshot_20241102-135058.png
    411.3 KB · Views: 1
Inawezakana wanatunzwa vizuri lakini sisi wenye mama zetu wanyakyusa tunawajua ni watata na wanapenda kujishughulisha ata kama anapata kila kitu na ukimforce aache shughuli zake atakwambia usiletee tena vipesa vyako yaan wana jeuri sijui ya dunia gani
 
Una uhakika huyo mama anaokota makopo?
 
Mbona kawaida Mzee,wajitafutia utaomba watoto mpaka lini au ww unataka wakajiuze.
Hapana Kuna kazi mara mbili ikiwa Mungu amekubarikia wewe let's say umekuwa C.E.O wa kampuni kubwa unalipwa vzr mamako na babako walikusomesha Kwa kuokota machupa... Kuuza Genge na kazi nyengine ndogondogo tunategemea ukivuka daraja uvuke na ulikuwa nao ulipokuwa kwenye shida .... Wafanye kazi lkn kidogo zenye kuwapumzisha na staha....
 
Bora muuza mboga mboga, ila muokota makopo anaweza kuwa mwehu ama akili zisiwe sawa kabisa

Siwezi kuwa na kipato cha uhakika halafu nikaruhusu mama Yangu akaokota makopo, aingie majalalani afungue makopo yenye mikojo eti kisa anatafuta... UONGO😭😭😭

siku ya msiba CV yake inasomwaje?😭😭😭
 
Wasanii wa Tz ukiachana na showoff zao, Ila kiufupi wana maisha magumu Sana .

Mama wa Rayvanny yupo mbeya sokoni anauza Mboga za majani za reja reja.

Na mama yake Martha anaokota machupa na kuuza juice.


This industry is all about shit.
Umiza kichwa kuhusu maisha yako
 
Wazazi lazima wafanye kazi wangali Bado na nguvu. Maisha ya mtoto siyo ya mzazi. Kila mmoja ana maisha yake. Mwenye uhitaji wa lazima wa kuhitaji msaada Kwa mwenzake atafuata utaratibu
 

Vipi kuhusu uboreshwaji wa Biashara? Kila mtu anapenda upgrade; ama?
 
Mbona ni maisha ya kawaida ya kiTanzania , ulitak aache asubr tuu apew wakt watoto nao wanasak future zAo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…