pCpCp RICH THINKER
Senior Member
- Apr 5, 2021
- 121
- 103
Una mpango wa kusoma Short Course V.E.T.A ? Na ni mtu mwenye majukumu yako?!
Basi, tambua:
1. Utalazimishwa kuvaa sare. Hauko tayari kuvaa sare mazingira yako ni magumu. Hakuna cha 'bring-bring' wala nini!
2. Utanyoa Kama mtoto, kama mwanafunzi haswaa. Kama unauchebe, uchebe wako utaambiwa 'kakate ndevu' na kama mke wako anaupenda 'mustachi'; rafiki yangu utaambiwa “chagua V.E.T.A ama mkeo”.
3. Usilete habari za 'udigrii', 'u-pHD', uzamili wala u-astashahada. Jifanye hujui, jifanye darasa la saba hata Kama una shahada ya uzamivu. “Don't outshine your teachers”.
4. Utapaswa kujibu Kama madesa ya Mwalimu yanavyo sema na si vinginevyo. Ujuaji hautakiwi, hata kwa mambo unayojua ya mtaa, tulia; ' aliye na kisu ndio anaamua keki aikate vipi'
5. Hutaruhusiwa kufuga rasi, a.k.a 'dread', kunyoa kidugu, kufuga kucha n.k Hiyo ni ishara ya uhuni. Wadada wote wasuke twende kilioni ama wanyoe ama nywele fupi fupi.
6. Utasalimia watu na stafu wote, hata kama unawazidi umri Salam kwa mwanafunzi ni moja tu nayo ni “shikamoo”; usile mambo ya “za saizi!” na salamu unazozijua wewe! Hutaki tafuta chuo chako.
7. Hutaruhusiwa kutumia simu ukiwa darasani. “Simu utazima ukiwa darasani, na ukikamatwa nayo siku utakayoichukua siifahamu!”
8. Utapewa adhabu kama kawaida, kuzibua mifereji kumwagia maji, ikiwezekana kung'oa visiki, ukizingua. Kwa ufupi unaambiwa “ukiingia humu hata kama una pHD; unaiacha getini”
9. Habari za ujuaji na ‘harakati za hovyo’ hazitakiwi kwa sababu “hujalazimishwa kuja V.E.T.A”
10. Ukikiuka kati ya hayo tisa, maana yake uko tayari kufukuzwa hatakama unafadhiliwa na Ofisi ya waziri mkuu
Basi, tambua:
1. Utalazimishwa kuvaa sare. Hauko tayari kuvaa sare mazingira yako ni magumu. Hakuna cha 'bring-bring' wala nini!
2. Utanyoa Kama mtoto, kama mwanafunzi haswaa. Kama unauchebe, uchebe wako utaambiwa 'kakate ndevu' na kama mke wako anaupenda 'mustachi'; rafiki yangu utaambiwa “chagua V.E.T.A ama mkeo”.
3. Usilete habari za 'udigrii', 'u-pHD', uzamili wala u-astashahada. Jifanye hujui, jifanye darasa la saba hata Kama una shahada ya uzamivu. “Don't outshine your teachers”.
4. Utapaswa kujibu Kama madesa ya Mwalimu yanavyo sema na si vinginevyo. Ujuaji hautakiwi, hata kwa mambo unayojua ya mtaa, tulia; ' aliye na kisu ndio anaamua keki aikate vipi'
5. Hutaruhusiwa kufuga rasi, a.k.a 'dread', kunyoa kidugu, kufuga kucha n.k Hiyo ni ishara ya uhuni. Wadada wote wasuke twende kilioni ama wanyoe ama nywele fupi fupi.
6. Utasalimia watu na stafu wote, hata kama unawazidi umri Salam kwa mwanafunzi ni moja tu nayo ni “shikamoo”; usile mambo ya “za saizi!” na salamu unazozijua wewe! Hutaki tafuta chuo chako.
7. Hutaruhusiwa kutumia simu ukiwa darasani. “Simu utazima ukiwa darasani, na ukikamatwa nayo siku utakayoichukua siifahamu!”
8. Utapewa adhabu kama kawaida, kuzibua mifereji kumwagia maji, ikiwezekana kung'oa visiki, ukizingua. Kwa ufupi unaambiwa “ukiingia humu hata kama una pHD; unaiacha getini”
9. Habari za ujuaji na ‘harakati za hovyo’ hazitakiwi kwa sababu “hujalazimishwa kuja V.E.T.A”
10. Ukikiuka kati ya hayo tisa, maana yake uko tayari kufukuzwa hatakama unafadhiliwa na Ofisi ya waziri mkuu