Mambo gani ya fedheha umewahi kufanya kwasababu ya kufulia (kukosa Hela)?

Kutembelea minadani huku unaangalia chini kama kuna mtu alidondosha ka hela
hii ilinikuta nilipita kwenye kijiwe cha boda boda,nikaigumia 2000 imechokaa,imkunjwa kunjwa,nikaiokota nikiwa nashukuru kwa Mungu hatua chache mbele,naskia naitwa brazaa.
samahani hiyo 2k ni yangu nimeangusha pale nilikuwa natoa mfukoni nyingine hizi hapa zilikuwa 4k.

kwa udadisi nikamuuliza unajua ni shingapi??akaitaja mpaka hali yake[emoji23][emoji23],kinyoonge nikampa.
 
Home hamna kitu na nina Mtoto na mke jioni nikapata jero nikanunua vidagaa SASA inshu ikaja gas imeisha, mkaa hakuna SASA alternative ni kupika kuni hapo kuni nazo sjui napata wapi. Hapo ni Saa mbili usiku mchana na asubuhi sijala Ila mtoto alikorogewa uji Tu.

Basi wakati narudi home na kamfuko changu cha dagaa nikapita mahali nikaona limeza lipo road nikaona linafaa Kwa kuni nikabeba huyooo daaah mara nakutana na jamaa mmoja akanisimamisha akanambia meza Ile ni yake na mjomba wake huwa wanafanyia biashara kwahiyo Mimi ni mwizi akampigia simu HUYO mjomba wake kumpa taarifa ya wizi.

Yule mjomba wake akamwambia tukutane pale nilipoichukua Ile meza kweli tukarudi mpaka pale halafu ni barabarani nashukuru kulikuwa na kagiza basi tumesubiri wee Yule mjomba mtu akapiga simu nikapewa niongee naye akawa ananiambia niseme Mimi ni mwizi au nipelekwe polisi basi nikakiri ndivyo nimeiba bs ye akasema kapata emergency kwahiyo hiyo meza ipelekwe kwake nikabebeshwa tena mpk Kwa HUYO mjomba wake kesi ikawa imeisha yaani sitasahau sema ni zamani sana.
 
Aisee wanaume huwa tunahustle sana kumake mambo yawe sawa...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…