Mambo mengine utayaelewa siku ukiwa muhusika, kwa sasa utaona kama vile hawajui kutumia vizuri nafasi zao

Mambo mengine utayaelewa siku ukiwa muhusika, kwa sasa utaona kama vile hawajui kutumia vizuri nafasi zao

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2024
Posts
344
Reaction score
926
Inawezekana kuna watu unawaona wa ajabu sana, unaona kama ungepewa uhusika wao basi ungefanikiwa ndani ya dakika moja 😊 Inawezekana ikawa kweli wapo kwenye nafasi wasizojua kuzitumia vyema au ikawa sio kama uonavyo ukiwa sio muhusika.

Kuna watu wakikusimulia utaona kama vile wanakutisha hivi, yawezekana ikawa kweli wanakutisha au wakawa wanakupa ukweli ambao kwako unaona haiwezekani kwa sababu bado hujawa muhusika.

Mambo sio magumu ila pia sio rahisi lakini majibu sahihi utayapata siku ukiwa muhusika lakini kwa tahadhari tu ni kuwa sio wahusika wote ni wavivu au hawajui kutumia nafasi zao vizuri bali kuna mengi ambayo ukiwa nje ya mchezo huyaoni na ukitaka ufurahie mchezo jiandaye kutokata tamaa kirahisi kwani mchezo huwa hautaki jamii ya wakata tamaa kirahisi.

Ukianza kulipwa mshahara ndio utajua hautoshi ila ukiwa nje ya mfumo utaona watu wana mishahara mikubwa ila hawajui kuitumia.

Ukimaliza shule ukawa mtaani ndio utajifunza kuwaheshimu waliopo mtaani kwa miaka mitano bila kulia lia njaa.

Usiwe mtu wa kuhukumu sana ukiwa nje ya mchezo bali ukiona ni kama hawatumii vizuri nafasi zao wewe tumia kama funzo ili siku ukiwa muhusika basi utumie vizuri nafasi yako.

Mwanasayansi Saul kalivubha.
Fikia Ndoto Zako.
 
kweli kabisa hapo zamani tulikuwa tunamsema sana shetani ila sasahivi sisi ndo tumegeuka kuwa shetani!!.

haka ka dunia kitu kama hujui kiache kama kilivyo kwanza anaekijua ndo anaweza kukibadili!,ukiwa nje ya mfumo wa mapenzi unaona wanaolia wanaigiza! ukiingia ndani tu ukakutana na wapenzi wakurupuaji utalia yale machozi yanayokimbilia kwenye masikio hata uwe umesimama yanaenda masikioni tu!..🤣
 
kweli kabisa hapo zamani tulikuwa tunamsema sana shetani ila sasahivi sisi ndo tumegeuka kuwa shetani!!.

haka ka dunia kitu kama hujui kiache kama kilivyo kwanza anaekijua ndo anaweza kukibadili!,ukiwa nje ya mfumo wa mapenzi unaona wanaolia wanaigiza! ukiingia ndani tu ukakutana na wapenzi wakurupuaji utalia yale machozi yanayokimbilia kwenye masikio hata uwe umesimama yanaenda masikioni tu!..🤣
Walio nje ya mchezo huwa wanaona wachezaji wote hawajui kuliko wao
 
Back
Top Bottom