Mambo muhimu ya kuzingatia katika uendeshaji wa kampuni

Mambo muhimu ya kuzingatia katika uendeshaji wa kampuni

Ndugu niliweka hapo juu kusajili zaidi ya 50m mtaji ni Tshs 440,000/ Hapo iwe billion au hata Trillion bei ni hiyo

Trade mark naomba tembelea website hii ya brela wameeleza taratibu zote na mpaka bei zake
BRELA ila ukitaka kufanya hili ushauri wangu ni vyema kutafuta mwanasheria mbobezi kwenye eneo hilo naamini utanufaika zaidi kuliko kutaka kufanya mwenyewe.
Mkuu unamaanisha kusajili Trademarks tu mpaka nitafute mwanasheria tena ?
 
A registered company inaweza kufanya biashara popote. Utaratibu ulipo sasa ukifungua branch unaenda TRA wanakupa form ya kujaza ili ujulikna ulipo na kupata Tax clareance kwa ajili ya kupata leseni kwenye halmashauri husika

Habari,nahitaji kufungua branch ya kampuni mkoa mwingine taratibu zikoje?
 
Mkuu nikibadilisha directors Brela nalazimika kuwataarifu tra?
 
Tra wanatunza Tax file ni vizuri wakiwa na updated file ya Director wako. Tena hapa umenikumbusha kitu kingine kimoja ambacho watu wengi wenye makampuni huwa hawakifanyi wakati wanapeleka returns zao TRA. Ni swala la director returns kila kampuni inalazimika kupeleka mapato ya ma director wake kwa mwaka husika hapa zinatakiwa kuaambatana na hesabu za mwaka. Kwa hiyo hata kama hutaki kupeleka siku hiyo unapobadilisha utatakiwa kupeleka miezi sita baada ya kufunga hesabu zako za mwaka.

Mkuu nikibadilisha directors Brela nalazimika kuwataarifu tra?
 
A registered company inaweza kufanya biashara popote. Utaratibu ulipo sasa ukifungua branch unaenda TRA wanakupa form ya kujaza ili ujulikna ulipo na kupata Tax clareance kwa ajili ya kupata leseni kwenye halmashauri husika
Thanx Nyumbalo,na je iwapo director wa kampuni kapata matatizo yeye kama yeye na kushikiliwa mahabusu kwa muda mrefu kampuni inaweza kuendelea na kazi zake bila yeye?
 
Asante mkuu, nitasoma vizuri nikitulia.
 
Hii shida ipo sana na kuajiri mhasibu wengi wanataka mshahara mkubwa, kwaiyo nifanyaje mkuu?
 
Karibu sana

QUOTE="BIGstallion, post: 24812471, member: 387074"]Nzuri sana,[/QUOTE]
 
Kaka kwa technologia ilipofika sasa unaweza kuwa na mhasibu part time anakuja anatoa ushauri anapita mara moja au mbili kwa mwezi kuhakikisha kuwa vitabu vyako vimekaa vizuri. Then Auditing inafanyika mwisho wa mwaka na reports inaandaliwa. Ila ukiwa na kampuni ki ukweli huwezi kuepuka garama ni vizuri kijipanga mapema.

Hii shida ipo sana na kuajiri mhasibu wengi wanataka mshahara mkubwa, kwaiyo nifanyaje mkuu?
 
Asante sana mkuu kwa elimu....hapo kwenye fine ya kutokufill returns binafsi sikwepi...
 
Mkuu kwa uelewa wangu mdogo, mambo ya copyrights yanakuwa issued na COSOTA (Copyright Society of Tanzania) kwa upande wa Tanzania bara ila kwa Zanzibar ni COSOZA, pili kwa kipengele cha patents registration/recognition hii inatolewa na serikali kupitia BRELA ikishirikisha ARIPO na WIPO ili kuhakikisha hiyo pantent haijawahi kuwa registered elsewhere duniani. Pia zingatia kwamba patent inakuwa registered for a certain life time, muda huo ukiisha hiyo pantent inakuwa public hivyo yoyote ataweza kuitumia either for private uses au commercial gains.
Asante sana mkuu
 
Hili lilijadiliwa page ya kwanza haya hii hapa kwa faida yako.

Kusajili kampuni inakuwezesha kuwa na mtu mwingine zaidi ya wewe. Maana kampuni ni kitu kamili ( Entity) na sheria nyingi za kodi zinaonyesha kulinda zaidi kampuni zaidi kuliko aina nyingine za biashara. Yani zile za watu binafsi (Sole Proprietor ) au zile za Ubia (Partnership).

Kwa kuwa kampuni inaweza kushitaki na kushitakiwa ( Entity) na hivyo kuwezesha kuwa na ukomo kwa hisa zake tu ( Limited to its share) na hivyo inaweka cover fulani kuliko aina nyingine. Na faida nyingine kubwa ni uwezo wa kutoa matumizi ya biashara katika faida unayotengeneza.

Na huo uhuru wa kuweza kukadiria kodi mwanzoni wa mwaka tofauti ya ile ambayo biashara nyingine unakadiriwa tu then unalipa. Ila uhuru huo unalimit usije ukapungua zaidi ya 20% unaweza kukutana na penalty.
ukitaka kusoma zaidi unaweza kutembelea link hii Advantages and Disadvantages of the Corporate Form of Business

naomba unieleweshe faida na hasara za kufungua kampuni as a sole proprietor na partnership
 
Hujafile zipi TRA au Brela jitahidi ufanye mapema inavyowezekana inakupunguzia garama za kuendesha biashara

QUOTE="Ntolonyonyo, post: 24815975, member: 301298"]Asante sana mkuu kwa elimu....hapo kwenye fine ya kutokufill returns binafsi sikwepi...[/QUOTE]
 
Nashauri waweke hisa kuwa kubwa ila issued iendane na hali ya mtu ili wakati wa kuongeza unaongeza kwenye issue ambayo ni process rahisi kuliko kuchange memerts yote kwa ajili ya kuongeza hisa. Naamini 500m to 1 B ni range nzuri. Halafu ukanzia na kuissue 5m to 10 m sio mbaya
Noted ntakutafuta for more details ubarikiwe sana,
 
Back
Top Bottom