Mambo usiyoyajua kuhusu Biblia

Mambo usiyoyajua kuhusu Biblia

Biblia ukiisoma usisome kwa kutumia sana ufahamu wa aliekufundisha hayo maandiko kama ni Mchungaji wako,Askofu wako au Muinjilisti wako au hata Sheikh wako.Katika Biblia tumepewa roho wa kweli atakae tufundisha ile kweli,ambayo haineni kwashauri lake ila shauri la MUNGU (YOHANA 16:13) kwasababu wanadamu woote asili yetu niya upotevu toka Kwa Adamu na Hawa,uzao wetu ulianzia njee ya Eden kwa upotevu.Yesu alikuja ili kuturudisha Eden(kwenye uwepo wa Mungu) lakini alipoondoka alituachia msaidizi wa kutupa ile kweli ambayo ni Roho wa Mungu
Biblia sio kitabu cha Wakristo ni kitabu cha kifalme toka Mwanzo mpaka Ufunuo,Yesu akuja kwa ajili ya wakristo Yesu alikuja kwaajili ya wanaomini injili yake ya ufalme wa mbinguni(Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili kila amuaminie asipotee YOHANA 3:16) Hivi ni wanao amini tu kile alichohubiri Yesu.
Yesu kwa maisha yake ya injili alihubiri juu ya ufalme wa Mbinguni tu
Mathayo 4:17
" Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia"

Na mifano yake katika injili yake ilikuwa ni ufalme wa Mungu/mbinguni umefanana....ufalme wa Mungu/Mbinguni umefanana.....ufalme wa Mungu/Mbinguni umefanana.... hivyo hivyo kwa sehemu kubwa ya mafundisho yake
Hivyo Yesu hakuja kuubiri ukristo duniani maana kwa maisha yake yoote hakuwai kuingia Kanisani aliingia katika Misikiti ya kiyahudi(Masinagogi) lakini hawakuyapokea mafundisho yake kabisa ndio maana alisema jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni akiwa na maana watu alio wahubiria wa misikitini wamemkataa na wamempokea watu wapembeni ambao kwasasa ndio Wakristo na makanisa yameanza baada ya kifo cha Yesu kupitia mitume wake,lakini baya zaidi nalo liona makanisani hawaubiri tena alichoubiri Yesu Kristo wanahubiri ya kwao na sio tena Ufalme wa Mungu japo wanatumia kitabu cha Kifalme.Yesu hakutaka mumuhubiri yeye alitaka tuhubiri u habari za ufalme kwanza kisha ndio habari zake au habari nyingine (utafteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa Mathayo 6:33)
Lakini hata Mtume Paulo mwenyewe alikuwa anawahubiria watu kwanza juu ya ufalme wa mbinguni ndio habari za Yesu zinafata

Matendo Ya Mitume 28:30-31

"Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea,akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu.
 
Biblia ukiisoma usisome kwa kutumia sana ufahamu wa aliekufundisha hayo maandiko kama ni Mchungaji wako,Askofu wako au Muinjilisti wako au hata Sheikh wako.Katika Biblia tumepewa roho wa kweli atakae tufundisha ile kweli,ambayo haineni kwashauri lake ila shauri la MUNGU (YOHANA 16:13) kwasababu wanadamu woote asili yetu niya upotevu toka Kwa Adamu na Hawa,uzao wetu ulianzia njee ya Eden kwa upotevu.Yesu alikuja ili kuturudisha Eden(kwenye uwepo wa Mungu) lakini alipoondoka alituachia msaidizi wa kutupa ile kweli ambayo ni Roho wa Mungu
Biblia sio kitabu cha Wakristo ni kitabu cha kifalme toka Mwanzo mpaka Ufunuo,Yesu akuja kwa ajili ya wakristo Yesu alikuja kwaajili ya wanaomini injili yake ya ufalme wa mbinguni(Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanae wa pekee ili kila amuaminie asipotee YOHANA 3:16) Hivi ni wanao amini tu kile alichohubiri Yesu.
Yesu kwa maisha yake ya injili alihubiri juu ya ufalme wa Mbinguni tu
Mathayo 4:17
" Tokea wakati huo Yesu alianza kuhubiri, na kusema, Tubuni; kwa maana ufalme wa mbinguni umekaribia"

Na mifano yake katika injili yake ilikuwa ni ufalme wa Mungu/mbinguni umefanana....ufalme wa Mungu/Mbinguni umefanana.....ufalme wa Mungu/Mbinguni umefanana.... hivyo hivyo kwa sehemu kubwa ya mafundisho yake
Hivyo Yesu hakuja kuubiri ukristo duniani maana kwa maisha yake yoote hakuwai kuingia Kanisani aliingia katika Misikiti ya kiyahudi(Masinagogi) lakini hawakuyapokea mafundisho yake kabisa ndio maana alisema jiwe walilolikataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembeni akiwa na maana watu alio wahubiria wa misikitini wamemkataa na wamempokea watu wapembeni ambao kwasasa ndio Wakristo na makanisa yameanza baada ya kifo cha Yesu kupitia mitume wake,lakini baya zaidi nalo liona makanisani hawaubiri tena alichoubiri Yesu Kristo wanahubiri ya kwao na sio tena Ufalme wa Mungu japo wanatumia kitabu cha Kifalme.Yesu hakutaka mumuhubiri yeye alitaka tuhubiri u habari za ufalme kwanza kisha ndio habari zake au habari nyingine (utafteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine mtazidishiwa Mathayo 6:33)
Lakini hata Mtume Paulo mwenyewe alikuwa anawahubiria watu kwanza juu ya ufalme wa mbinguni ndio habari za Yesu zinafata

Matendo Ya Mitume 28:30-31

"Akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea,akihubiri habari za ufalme wa Mungu, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo, kwa ujasiri mwingi, asikatazwe na mtu.
Very right ✅

Naomba kuuliza maana ya ufalme wa Mungu, na je umekwisha kuja au bado.
Na unapatikana wapi?
 
Very right ✅

Naomba kuuliza maana ya ufalme wa Mungu, na je umekwisha kuja au bado.
Na unapatikana wapi?
Asante King Jim
Umeuliza maswali 3
Ufalme Wa Mungu nini? Kwa ufupi na urahisi ili unielewe pia kwa mifano toka katika Biblia
Ufalme wa Mungu ni kujua kusudi la Mungu kumuumba mwanadamu na kuliishi hilo kusudi.Na makusudi hayo ni UPENDO na KUTAWALA(ufalme)

Swali la Pili
Je? Umekwisha kuja
Jibu ni ndio umekwisha kuja baada ya Adam kuupoteza,Mungu aliupenda tena ulimwengu akamtoa mwanae wa pekee Yesu Kristo ndie alie kuja nao kwa mala ya pili.
Kumbuka Ufalme ni utawala wa kimungu,Mungu alipo ongea na nafsi yake katika MWANZO 1:26 alisema

Mwa 1:26 SUV
Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.
👆 hapa Mungu alimpa Mwanadamu ufalme hapa duniani ila kuongezea kuna ufalme wa duniani na Mbinguni,Mungu alitaka ufalme wake hapa duniani uwakilishwe na mwanadamu sio shetani.Lakini ufalme huu tulio pewa wanadamu aliupoteza Adam kwa kutenda dhambi kuto tii.Ufalme tukanyang'anywa.
Nabii wa kwanza kutabilii juu ya ujio wa Yesu Kristo alikuwa nabii Isaya,aliwashuhudi watu kuwa ufalme utarudi tena kupitia mtoto mwanaume ambae tutapewa
ISAYA 9:6
"Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani."
Ndio maana Maisha ya Yesu hakunyama juu ya habari njema ya ufalme,aliingia kwenye misikiti ya kiyahudi yote ya Galilaya (Masinagogi)

MATHAYO 4:23
"Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri Habari Njema ya ufalme, na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu."

Lakini kote huko hawakumsadiki wala kumuamini,nyumba zote za ibada ila alipokuwa akihubiri njee ya misikiti alipata watu wengi walio muamini ambao ndio leo wanaitwa wa kristo,ndio maana anasema jiwe walilo likataa waashi limekuwa jiwe kuu la pembe,waashi kwa lugha ya kufikirisha aliona kama wajuaji maana walimkosoa sana kwasababu wao waliamini katika sheria yaani torati na maandishi ya manabii
Hapa 👇 anawaambia

LUKA 16:16
Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu.

Lakini itoshe kukuambia kuwa ufalme wa Mungu upo Duniani na Mbinguni pia upo,katika sala ya Bwana Yesu akiwafundisha wanafunzi wake kuna pahala anasema "Baba yetu ulie mbinguni jina lako litukuzwe,UFALME wako uje ina maana ufalme upo hapa hapa ila pia

LUKA 17:20-21
Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza; wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.

SWALI LA 3
Unapatikana wapi?
Hapa ni kama nimeisha kujibu.Pale unajitia nia ukiongozwa na roho mtakatifu ambae ndie msaada wetu atakae tuongoza katika ile kweli pia ukajitia nia hasa katika kumjua Mungu kupitia maandiko utakalo liskia kwa mchungaji wako,Askofu wako au mwinjilisti wako usiishie kulimeza tu! Tafuta ukweli wake maana kusududi lako analijua MUNGU TU ila wanadamu wote wanayokwambia ni kama maoni yao juu yako na maisha yako mkweli ni Mungu.Biblia inasema wanadamu wote ni waongo ila Mungu pekee ndio mkweli

WARUMI 3:4

Hasha! Mungu aonekane kuwa amini na kila mtu mwongo

👆 Ningependa hata haya niliyo kwambia pata nafasi ukiongozwa na roho mtakatifu kuyahakiki.
 
Back
Top Bottom