Leo nimesikiliza kipindi cha matukio WAPO FM nimepatwa na msituko mkubwa. Reporter alikuwa mmoja wa wateja wa babu. Ilipofika zamu yake ya kuhudumiwa aliamua kumuuliza babu maswali machache. Kwanza alimwomba amwonyeshe huo mti anaotumia, akaoneshwa. Lakini akapewa na tahadhari kwamba mti huo una sumu kali sana, na kwamba kama atakwenda kunywa mwenyewe tofauti na pale kwa yule babu mauti yanaweza kumkuta. Masharti ni kunywa dawa inayotolewa na babu, tena chini ya mti uleule uliopo nyumbani kwa babu. Ukisogea hata mita tano tu kutoka kwenye mti huo basi dawa ina-expire na kuwa sumu.
Hebu sasa tumjadili huyo mungu aliyepo chini ya mti wa kutolea dozi hapo Loliondo.
MARKO 13
13:22 Maana watatokea kina Kristo wa uongo na manabii wa uongo, watafanya ishara na maajabu, ili kuwapotosha wateule wa Mungu, kama ikiwezekana.
13:23 Lakini ninyi jihadharini. Mimi nimewaambieni mambo yote kabla hayajatokea.