Mambo ya Msingi Sana katika maisha

Mambo ya Msingi Sana katika maisha

(1) Ukipiga mihayo (yawning), chafya au kukohoa, funika mdomo na pua kwa mikono.

(2) Usiteme mate, kutapika, kupenga kamasi, wenzako wakiwa wanakula.

(3) Ukienda nyumbani kwa mtu, hususan rafiki, usitangaze madhaifu utakayoyaona. Mfano: Watoto wao wanashindia nguo zilizochanika.

(4) Rafiki yako unayeheshimiana naye, usiwe na namba ya simu ya mkewe ili kuepuka kutembea naye.

(5) Ukiacha kazi ofisini, usiwatukane former employers wako kwa maana katika maisha kuna leo na kesho.

(6) Ni vema ukapakua chakula kidogo kisha ukaongeza kuliko kupakua kingi alafu ukashindwa kukimaliza.

(7) Ukienda kwenye sherehe, hata kama wewe ni ndugu za karibu, usikae sehemu za VIP bila kukaribishwa. Ni aibu sana kuambiwa uondoke kwenye seat za VIP uende kwa wageni wa kawaida.

(8) Ukigundua spouse wa rafiki yako ana uhusiano wa nje ya ndoa, mfuate na mkanye ila usimwambie mumewe/mkewe.

(9) Mtu akikusaidia mara moja, usimgeuzi kitega uchumi cha kumuomba mara kwa mara. Kumbuka yeye pia ana majukumu yake binafsi.

(10) Ukiongea kwenye simu na mtu wa mbali sio vizuri kusema "fulani (Alex) nipo naye hapa ongea naye pia. Kama huyo Alex hajakuomba kuongea na mhusika basi kaa kimya.

(11) Ukipata mshahara mwisho wa mwezi, wape kidogo mfanya usafi pamoja na mpika chai hapo ofisini kwenu. Hao ndio informers na wanajua mengi ya hapo ofisini kwenu.

(12) Usiache kwenda likizo ya mapumziko kwa kuambiwa eti "tutakufidia kwa fedha hizo siku 28 za mapumziko". Afya yako ya akili ni kitu cha msingi sana.

(13) Ukienda ugenini kisha ukaachwa peke yako sebuleni, usishike chochote kama mwenyeji wako hayupo (ameenda kunununulia soda kwa mfano). Hata kama ni gazeti umelikuta hapo, subiri akirudi ndio umuombe.

ONGEZEA NA WEWE NDUGU YANGU......
Hii namba 12...Ndio ugonjwa mkubwa wa wakazi wa Daslam.....wataalam wanaita .....''Burnout".........
 
Yaani hotelini kabisa nimelipia hela halafu nibakishe chakula?
Mi hua nasafisha kila kitu, respect itakuja kwa ustaarabu mwingine
Ukiagiza chakula hotelini, kumaliza chakula kwenye sahani ni ishara ya heshima na shukrani kwa mlo waliokuandalia. Inaonyesha kuwa unathamini jitihada zao.

Hata hivyo, kama ni kwa ndugu yako pakua kile kinachokutosha, ikitokea umepakuliwa acha chakula kidogo kuonyesha umeshiba, Muhimu zaidi ni kuwa na adabu na kushukuru.
 
Jitahidi sana kutokuelezea shida zako kwa kila mtu labda zimekufika shingoni na kwa watu maalum
Usijionyeshe unapesa pesa inajionyesha yenyewe
Usiwakate watoto unaoona kabisa hii damu yako wala usiwatolee maneno machafu
Sasa mwanangu kwanini nisijionyeshe kama Nina pesa Ata kama Sina maana kwa mfano ata mahusiano huwezi Pata bila ya ku-brag docio(kujisifu) labda wa watu wengine ndugu, mke, na marafiki s vyema kujionesha kwamba na hapa ipo sana
 
(1) Ukipiga mihayo (yawning), chafya au kukohoa, funika mdomo na pua kwa mikono.

(2) Usiteme mate, kutapika, kupenga kamasi, wenzako wakiwa wanakula.

(3) Ukienda nyumbani kwa mtu, hususan rafiki, usitangaze madhaifu utakayoyaona. Mfano: Watoto wao wanashindia nguo zilizochanika.

(4) Rafiki yako unayeheshimiana naye, usiwe na namba ya simu ya mkewe ili kuepuka kutembea naye.

(5) Ukiacha kazi ofisini, usiwatukane former employers wako kwa maana katika maisha kuna leo na kesho.

(6) Ni vema ukapakua chakula kidogo kisha ukaongeza kuliko kupakua kingi alafu ukashindwa kukimaliza.

(7) Ukienda kwenye sherehe, hata kama wewe ni ndugu za karibu, usikae sehemu za VIP bila kukaribishwa. Ni aibu sana kuambiwa uondoke kwenye seat za VIP uende kwa wageni wa kawaida.

(8) Ukigundua spouse wa rafiki yako ana uhusiano wa nje ya ndoa, mfuate na mkanye ila usimwambie mumewe/mkewe.

(9) Mtu akikusaidia mara moja, usimgeuzi kitega uchumi cha kumuomba mara kwa mara. Kumbuka yeye pia ana majukumu yake binafsi.

(10) Ukiongea kwenye simu na mtu wa mbali sio vizuri kusema "fulani (Alex) nipo naye hapa ongea naye pia. Kama huyo Alex hajakuomba kuongea na mhusika basi kaa kimya.

(11) Ukipata mshahara mwisho wa mwezi, wape kidogo mfanya usafi pamoja na mpika chai hapo ofisini kwenu. Hao ndio informers na wanajua mengi ya hapo ofisini kwenu.

(12) Usiache kwenda likizo ya mapumziko kwa kuambiwa eti "tutakufidia kwa fedha hizo siku 28 za mapumziko". Afya yako ya akili ni kitu cha msingi sana.

(13) Ukienda ugenini kisha ukaachwa peke yako sebuleni, usishike chochote kama mwenyeji wako hayupo (ameenda kunununulia soda kwa mfano). Hata kama ni gazeti umelikuta hapo, subiri akirudi ndio umuombe.

ONGEZEA NA WEWE NDUGU YANGU......
Namba 8 ni ngumu sana. Anaweza kukugeuzia kibao akakusemea kwa mumewe kuwa unamtaka. Kwa lugha rahisi anakuwahi kabla ww hujamsemea kwa mumewe
 
👉Point ya nyongeza. Ukikopeshwa na ukabahatika kuzipata fedha ndani ya muda usisubiri paka upigiwe ujiongeze rudisha hela ya watu

👉MTU akija kukukopa hela usimuulize ni ya kazi gani wewe mpe tu kama unayo.

👉Ukipanda kwenye basi jitahidi kumsalimia jirani utakaemkuta kwenye siti

👉Ukienda kusalimia, usikae sana watu wana bajeti zao
 
👉Point ya nyongeza. Ukikopeshwa na ukabahatika kuzipata fedha ndani ya muda usisubiri paka upigiwe ujiongeze rudisha hela ya watu

👉MTU akija kukukopa hela usimuulize ni ya kazi gani wewe mpe tu kama unayo.

👉Ukipanda kwenye basi jitahidi kumsalimia jirani utakaemkuta kwenye siti

👉Ukienda kusalimia, usikae sana watu wana bajeti zao
Safi sana mkuu
 
Sasa mwanangu kwanini nisijionyeshe kama Nina pesa Ata kama Sina maana kwa mfano ata mahusiano huwezi Pata bila ya ku-brag docio(kujisifu) labda wa watu wengine ndugu, mke, na marafiki s vyema kujionesha kwamba na hapa ipo sana
Pesa ya kujionesha itakupa mpenzi/mke na rafiki wa uongo. Pesa ikiisha hao wote watakukimbia. Trust me. I once went through all that.
 
Back
Top Bottom