Mie nilikuwa nachukia mama yangu alikuwa ana tabia kwa mfano kama tunatembea naye njiani, akikutana na mtu pale alipokuwa anaanza kunitambulisha "HUYU NI MWANANGU WA 3 KUMZAA ANAITWA...."
Kuna siku alikuwa ametupanga mimi na ndugu zangu baada ya kutoka church, siku alisalisha padre mgeni, basi akaanza zake "PADRE HAWA NI WANANGU, WA KWANZA NI HUYU, WA PILI NI HUYU WA TATU NI HUY...." mie hapo hapo nikatoka nduki kukimbia kuelekea home, wakati bado angali anatutambulisha kwa father mgeni, alivyorudi nyumbani akanikuta, kilichonipata....... ngoja kwanza nitamalizia kesho
Yote kwa yote R.I.P mama yangu kipenzi