Mambosasa: Tumempuuza Mwamakula na kumuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana

Mambosasa: Tumempuuza Mwamakula na kumuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana

Huyo askofu uchwara kaamua kutumia hii njia ili kujiongezea umaarufu kanisani kwake ili kapu lijae

Pongezi kwa jeshi la polisi kumshughulikia na kumpuuza
Anamzidi Gwajima kwa huo uchwara? Binafsi namuunga mkono huyo Askofu Mwamakula kwa ujasiri wake wa kuwasemea Mamilioni ya Watanzania waliochoshwa na utawala kandamizi na wa kidikteta, kibabe, kikatili, kifisadi,kibaguzi ma wa kidhalimu unao fanywa na CCM.

Wala hahitaji umaarufu wowote! Zaidi anaonekana tu kama Mtu Shujaa machoni kwa Watanzania wengi Wazalendo na Wapenda Mabadiliko ya kweli ya kisiasa na kiuchumi nchini. Ni kweli tunahitaji Katiba Mpya na Tume Huru ya Uchaguzi ili tuone kama kweli nyinyi mi CCM mnapendwa na Watanzania, au mnashinda tu Uchaguzi kwa hila na ghiliba.
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi
Tumempuuza na kumwachia kwa dhamana. Kupuuza ni kwamba wamemuona mpuuzi au Hana maana sasa mpuuzi ana dhamana? Huyu ana mawili ni kumwachia bila masharti au kumuweka ndani, Bahati nzuri sio mvaa kanzu maana angesota gerezani hadi tukamsahau maana bila soni angetangazwa ni Alshabab
 
Sasa mlinda katiba asitake kusikia kitu cha kikatiba kwa misingi ipi? Sasa si wakatoe mapendekezo kuwa katiba imezingua hapo
 
Huyo askofu uchwara kaamua kutumia hii njia ili kujiongezea umaarufu kanisani kwake ili kapu lijae

Pongezi kwa jeshi la polisi kumshughulikia na kumpuuza
Wamuache tu aandamane. Hajui anapotoka wala anapokwenda
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi

wanatafuta mbinu za kuwa IGP ndiyo maigizo yote haya
 
Hivi mkienda kupekua watu nyumbani mnadhani mtakuta nini huo mfumo mlioiga ni mbaya kuwahi kutokea vitu ambavyo havieleweki mnavizingatia kweli mnaacha kupambana na Corona/ umasikini unaotuzunguka mpo busy na kauli za mtandaoni...
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi
Huyu Mzee ana hitilagu
 
unajua nchi hii watu mpaka watumwe ndio wafanye ujinga wao! jamani mambosasa kumpekua askofu unatafuta nini, biblia, joho lake au msalaba! sababu katiba mpya muhimu sana!
 
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limemuachia kwa dhamana Askofu Emmaus Mwamakula wa kanisa la Uamsho la Moravian baada ya kufanya upekuzi nyumbani kwake.

Taarifa za kushikiliwa Mwamakula zilitolewa na polisi jana Jumatatu Februari 15, 2021 kupitia mtandao wa kijamiii kabla ya Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kuthibitisha kumshikilia.

Akizungumza leo Jumanne Februari 16,2021 Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema baada ya jeshi hilo kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake limemuachia baada ya kutimiza masharti ya dhamana.

“Tumempuuza na baada ya kwenda kufanya upekuzi nyumbani kwake, mchana huu tumemuachia kwa dhamana baada ya kutimiza masharti,” amesema.

Awali polisi walieleza kumshikilia kumshikilia Mwamakula kutokana na taarifa aliyoichapisha mtandaoni iliyokuwa ikihamasisha wananchi wajitokeze kwa wingi kuandamana kushinikiza kudai katiba mpya jambo ambalo ni kinyume na taratibu na sheria za nchi.

Mwananchi
Huu uandishi wa kurudia-rudia kichwa cha habri huwa unanibore sana. Naamini wana taaluma ya uandishi ndivyo hufundishana huko vyuoni mwao lakini inakuwa kero kwa msomaji kwani unakuta paragraph zote nne ni kichwa cha habari kinarudiwa miwsho wa siku habari yenyewe fupi kama njugu.
 
Back
Top Bottom