Mamlaka, Jengeni maeneo ya watu kupumzika na kuhuisha akili zao

Mamlaka, Jengeni maeneo ya watu kupumzika na kuhuisha akili zao

ERoni

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2013
Posts
48,052
Reaction score
104,677
Wakuu,

Ni ajabu sana kuona miji midogo ndani ya majiji haina sehemu zenye utulivu kwa ajili ya watu kupumzika na kutembea, huku wakicheza na watoto wao, wakinywa soft drinks na bites, wakipiga picha na kupumzisha mafuvu yao.

Mji mdogo kama Mbezi-Kimara, kutwa ni shughuli za kiuchumi zinaendelea, kuanzia maduka makubwa hadi wanaopanga nyanya stand, huduma za usafirishaji hadi huduma zetu pendwa usiku wa manane maeneo tofauti kama kwa Gody, kwa Robert(Ngao Pub) na njia ya Kinyerezi.

Sasa kwa nini kusiwe na maeneo ya watu kupumzika, yatengenezwe vizuri, yahudumiwe kwa usafi yavutie wenyeji na wageni? Hizi open spaces nyingi zimegeuzwa maeneo ya biashara ndogondogo.

Watanzania nadhani hatuna huu utamaduni, tukitaka kutoka basi it's either tukutane bar, beach na wengine wetu guest😀, sio kila mtu anapenda kukutana bar. Lakini kuna namna tunaweza kujenga na kutengeneza maeneo mahususi watu wakakaa na kupumzika, kuongea, kupanga na kupangua mambo yao. Mbona hapo Zanzibar kuna sehemu zimejengwa vizuri tu, huku bara sisi tunashindwa nini?

Napendekeza eneo linalotizamana na Magufuli Stand, katikati ya barabara kuu na Stand kuu kuwe na recreation space, ijengwe vizuri, ivutie wageni na wenyeji, yaani sisi tunakuwa wala vumbi tu mda wote kweli? Sio Mbezi tu, sehemu zote za miji yetu zinahitaji kuwa na mandhari za kuvutia wageni na wenyeji, tuache uchafu jamani, miji yetu ni michafu sana, haivutii, inaongezea watu stress.

Kwani wenye nchi huwa hawasafiri wakaona wenzetu wanafanyaje huko kwao?

Screenshot_20221020-110217_Chrome.jpg
 
Wakuu,
Ni ajabu sana kuona miji midogo ndani ya majiji haina sehemu zenye utulivu kwa ajili ya watu kupumzika na kutembea, huku wakicheza na watoto wao, wakinywa soft drinks na bites, wakipiga picha na kupumzisha mafuvu yao.

Mji mdogo kama Mbezi-Kimara, kutwa ni shughuli za kiuchumi zinaendelea, kuanzia maduka makubwa hadi wanaopanga nyanya stand, huduma za usafirishaji hadi huduma zetu pendwa usiku wa manane maeneo tofauti kama kwa Gody, kwa Robert(Ngao Pub) na njia ya Kinyerezi.

Sasa kwa nini kusiwe na maeneo ya watu kupumzika, yatengenezwe vizuri, yahudumiwe kwa usafi yavutie wenyeji na wageni? Hizi open spaces nyingi zimegeuzwa maeneo ya biashara ndogondogo.

Watanzania nadhani hatuna huu utamaduni, tukitaka kutoka basi it's either tukutane bar, beach na wengine wetu guest[emoji3], sio kila mtu anapenda kukutana bar. Lakini kuna namna tunaweza kujenga na kutengeneza maeneo mahususi watu wakakaa na kupumzika, kuongea, kupanga na kupangua mambo yao. Mbona hapo Zanzibar kuna sehemu zimejengwa vizuri tu, huku bara sisi tunashindwa nini?

Napendekeza eneo linalotizamana na Magufuli Stand, katikati ya barabara kuu na Stand kuu kuwe na recreation space, ijengwe vizuri, ivutie wageni na wenyeji, yaani sisi tunakuwa wala vumbi tu mda wote kweli?
Sio Mbezi tu, sehemu zote za miji yetu zinahitaji kuwa na mandhari za kuvutia wageni na wenyeji, tuache uchafu jamani, miji yetu ni michafu sana, haivutii, inaongezea watu stress.

Kwani wenye nchi huwa hawasafiri wakaona wenzetu wanafanyaje huko kwao?
Sawa nitawajengea sehemu ya kuhuisha akili zenu Wananchi wangu.
 
Maeno ya Temeke - karibu na hospitali, Mnazi mmoja - lumumba, Magomeni - karibu na kanisa la KKT, kulikuwa na bustani za watu kupumzika. Tatizo ni utunzani wa maeneo hayo na pia baadhi hawaendi maeno hayo kwa nia njema bali ovu
 
Utaratibu huo kihistoria toka wakat wa mkoloni na mpaka uhuru umekuwa ukiendelea.
Parks ni maeneo muhimu hata kuwepo kwenye kila master plans.
Kwa mfano eneo la botanical Garden ambalo lilitengwa mahusus toka enz za mjeruman kuwa sehem ambayo itakua ya miti ya asil ya ukanda wa pwan na pia ni eneo zuri kupumzikia.
Leo botanical gareden pale shaban Roberts limekua masikitiko makubwa sana. Lina uzio lakin kwanin lisiboreshwe mandhar ikawa nzur.ikawa wat jion wana jogging kule baharin na.pale pakawa angalau hata weekend carnivals? Ice cream families pop corn na exhibition mbalimbali?
 
Tembelea pugu forest, kuna bamboo trees za maana na camping pia, ukikaa kule akili inajifomati kabisa.....usiache kuja kunishukuru 😉
 
Aisee Dar kila sehemu pesa 😂😂😂😂..Ukikaa ovyo ovyo kweny maeneo ya biashara za watu unaleteaa menu uchague hata kinywaji ukizingua unatimuliwa..

Ila naona kigamboni Pako poa kwa hayo maeneo especially ule usawa wa beach zake ..
 
Kwani wenye nchi huwa hawasafiri wakaona wenzetu wanafanyaje huko kwao?

Halafu sisi swala la ustaarabu ni sifuri hatujastaarabika kabisa, sehemu kama hizo tukijengewa itakua ndio sehemu ya kuvutia bangi, kutupa taka watu watakaa hapo wale watupe mabaki ya vyakula na machupa ya plastic, asubuhi utakuta condom zilizotumika, watu watakojoa watapupu hapo hadi basi...hizi vurugu ndio tumezizoea 😁
 
mwembeyanga (bornthere) zamani ilikuwa park nzuri ikabadilika kuwa maficho ya wa wahuni na ukabaji mixer kuvuta bangi.

lakini naona sasahivi wanafanya maboresho tena, ningependekeza wangetoa na elimu jinsi ya kutumia lile eneo tujione kama mbele
 
parks zipo lakin zinapotea kwasababu ya ustaarabu duni wa watanzania, sanasana uchafu
Kwa hiyo kumbe shida yetu kubwa ni ustaarabu? Tumekuwa watu wa hovyo kiasi hiki, au ni muendelezo wa watu masikini hawawezi kutunza hata mazingira yao?

Hivi hii inaweza kuwa sababu ya umasikini wetu?
 
Halafu sisi swala la ustaarabu ni sifuri hatujastaarabika kabisa, sehemu kama hizo tukijengewa itakua ndio sehemu ya kuvutia bangi, kutupa taka watu watakaa hapo wale watupe mabaki ya vyakula na machupa ya plastic, asubuhi utakuta condom zilizotumika, watu watakojoa watapupu hapo hadi basi...hizi vurugu ndio tumezizoea [emoji16]
Mkuu, hapa sasa ndio naanza kuelewa. Kumbe pamoja na yote shida yetu kubwa ni kukosa ustaarabu? Hili linaumiza, mbona miaka hiyo Zanzibar(sijui siku hizi) kulikuwa na maeneo mazuri watu wanakaa na kupiga story, wanaenjoy. Tumekuwaje watu wa hovyo namna hii?
 
Wakuu,
Ni ajabu sana kuona miji midogo ndani ya majiji haina sehemu zenye utulivu kwa ajili ya watu kupumzika na kutembea, huku wakicheza na watoto wao, wakinywa soft drinks na bites, wakipiga picha na kupumzisha mafuvu yao.

Mji mdogo kama Mbezi-Kimara, kutwa ni shughuli za kiuchumi zinaendelea, kuanzia maduka makubwa hadi wanaopanga nyanya stand, huduma za usafirishaji hadi huduma zetu pendwa usiku wa manane maeneo tofauti kama kwa Gody, kwa Robert(Ngao Pub) na njia ya Kinyerezi.

Sasa kwa nini kusiwe na maeneo ya watu kupumzika, yatengenezwe vizuri, yahudumiwe kwa usafi yavutie wenyeji na wageni? Hizi open spaces nyingi zimegeuzwa maeneo ya biashara ndogondogo.

Watanzania nadhani hatuna huu utamaduni, tukitaka kutoka basi it's either tukutane bar, beach na wengine wetu guest😀, sio kila mtu anapenda kukutana bar. Lakini kuna namna tunaweza kujenga na kutengeneza maeneo mahususi watu wakakaa na kupumzika, kuongea, kupanga na kupangua mambo yao. Mbona hapo Zanzibar kuna sehemu zimejengwa vizuri tu, huku bara sisi tunashindwa nini?

Napendekeza eneo linalotizamana na Magufuli Stand, katikati ya barabara kuu na Stand kuu kuwe na recreation space, ijengwe vizuri, ivutie wageni na wenyeji, yaani sisi tunakuwa wala vumbi tu mda wote kweli?
Sio Mbezi tu, sehemu zote za miji yetu zinahitaji kuwa na mandhari za kuvutia wageni na wenyeji, tuache uchafu jamani, miji yetu ni michafu sana, haivutii, inaongezea watu stress.

Kwani wenye nchi huwa hawasafiri wakaona wenzetu wanafanyaje huko kwao?

View attachment 2392589
NA HILI NALO MKALITAZAME
 
Back
Top Bottom