Mamlaka tazameni barabara ya Banana - Kitunda ili iweze kuwa msaada na si kero kwa wananchi

IbnBattuta

Senior Member
Joined
Feb 20, 2018
Posts
124
Reaction score
185
Wakuu Salaam,

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Barabara tajwa hapo juu amekuwa mwiba mkubwa sana kwa usafiri kwa wakazi wa Ukonga maeneo yanayozunguka Kitunda. Barabara ina hali mbaya sana na inachangia kwa kiasi kikubwa sana kuharibu vyombo vya usafiri vya wakazi wa maeneo hayo na hata kuchangia adha ya usafiri.

Tunaomba mamlaka husika ziangalie kwa jicho pana hii barabara ili iweze kuwa msaada na si kero kwa wananchi.

Ibn Battuta
 
Hamna mbunge eneo hilo au hata diwani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…