JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Mamlaka mbalimbali zimepewa madaraka kubwa katika kudhibiti maudhui na shughuli za kila siku za vyombo vya habari. Nguvu hizo, hasa kwa vyombo binafsi vya habari, zinaingilia uhuru wao wa uhariri na hivyo kuathiri kwa upana uhuru wa vyombo vya habari, kutoa maoni na kujieleza.
Mamlaka ya Polisi
Jeshi la Polisi limepewa mamlaka pana ya kufanya upekuzi kwenye chombo cha habari na kukamata kifaa chochote kilichoanzishwa, kuwekwa, au kuendeshwa kwa kukiuka matakwa ya Sheria hii. [Kifungu cha 60]
Vifaa vinavyotumika kuchapisha,kuzalisha au kuandaa habari havitoshikiliwa hadi tu pale ambapo askari anaona kuwa kuendelea kufanya kazi kwa kifaa husika kutazuia au kuharibu mchakato wa upelelezi
Upekuzi na ukamataji huo utazingaia Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai au sheria nyingine zinazosimamia masuala ya upekuzi na ukamataji
Mamlaka ya Polisi
Jeshi la Polisi limepewa mamlaka pana ya kufanya upekuzi kwenye chombo cha habari na kukamata kifaa chochote kilichoanzishwa, kuwekwa, au kuendeshwa kwa kukiuka matakwa ya Sheria hii. [Kifungu cha 60]
Vifaa vinavyotumika kuchapisha,kuzalisha au kuandaa habari havitoshikiliwa hadi tu pale ambapo askari anaona kuwa kuendelea kufanya kazi kwa kifaa husika kutazuia au kuharibu mchakato wa upelelezi
Upekuzi na ukamataji huo utazingaia Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai au sheria nyingine zinazosimamia masuala ya upekuzi na ukamataji
Upvote
0