Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Inaandikwa kwamba, basi Bwana Mungu akasema. NA TUUMBE MTU kwa mfano wetu. Hapa Bwana Mungu hakuwa pekeyake... Kulikuwa na mamlaka kamili ya kiroho juu mbinguni yaliyokuwa yanaongozwa na Mungu mwenyewe.

Tafsiri nyingine ni kwamba tayari huko mbinguni kulikuwa na maisha mengine ya kiroho mpaka walipojadiliana kuumba mtu mwenyewe mwili wa nyama.

Uumbaji mwingine wote wa vitu na wanyama viliumbwa na Mungu mwenyewe. Kwa uweza wake mkuu wa kutamka tu na ikawa. Ilipofika kwenye kuumba MTU ndio cabinet ya mbingu ikahusishwa!

Kwanini kwenye uumbaji wa MTU Mungu hakufanya maamuzi binafsi Kama kwa wanyama mimea na vingine vyote? Kuna ufunuo wa ajabu hapa. Ni kwa vile alitaka awepo mtu kwa mfano WAO.

Shetani anatajwa kama malaika mkuu. Kivyeo vya kisasa unaweza kusema katibu mkuu, waziri mkuu ama msaidizi mkuu. Huyu kwa asilimia 95 hufahamu yote ya mkuu wake wa kazi kwakuwa ndio kama mtendaji mkuu.

Kwenye uumbaji Mungu aliumba kila kimoja na kinyume chake. N mpaka wakati huu Hakukuwa na kitu kinaitwa dhambi japo kabla ya uumbaji nchi ilikuwa kiza tena totoro kiwa (ukiwa) na vilindi vya maji vikiwa vimetuama juu ya uso wa dunia.

Ni kwenye uumbaji pekee wa Adam ndio Mungu aliishirikisha Mamlaka yake (shetani?) Vingine vyote alifanya mwenyewe. Na hata alipoona Adam yu mpweke bustanini. Kwa mamlaka yake binafsi akamtengenenezea Adam msaidizi (Hawa/Eva?)

Kwanini hapa haikushirikisha cabinet yake? Je, lilith ndio shetani mwenyewe? Nini kilimuudhi shetani mpaka kuamua kwenda kumdanganya msaidizi wa Adam ale tunda la mti wa kati? Mti wa ujuzi wa mema na mabaya? Je, ni kwa vile hakushirikishwa kwenye kumtengeneza? Wivu? Kisasi? Kwanini hakumwendea Adam? Au kwakuwa aliasi mbinguni na kufukuzwa?

Na baada ya hapo dhambi ikaingia ulimwenguni na shetani akapewa ufalme wa giza. Ndio hapa kinyume cha mbingu kinakamilisha uumbaji wote kiroho.

Je, huu ulikuwa unabii au mpango wa Mungu? Kwanini shetani ana role kubwa sana kwenye dhana nzima ya kukengeuka kwa dunia, Adam na upili wa kiumbaji?

Tutafakari kwa pamoja, inawezekana kabisa shetani tumdhaniaye na nyoka tumwonaye ni vitu vingine kabisa tofauti na uhalisia wa dhana nzima ya Eden, uumbaji, uasi, tunda la mti wa kati nk
 
Hiyo ni dhana moja inayoaminiwa na watu chini ya 1/3 ya world population.

Sidhani kama wachina na wahindi wanaamini hiyo nadharia mkuu, anyway ni nadharia tuliyolishwa kwa miaka mingi sasa kuna haja ya kuijadili kama ulivyoileta ili tuamue kama tuendelee nayo ama tuipuuze.
 
Hiyo ni dhana moja inayoaminiwa na watu chini ya 1/3 ya world population.

Sidhani kama wachina na wahindi wanaamini hiyo nadharia mkuu, anyway ni nadharia tuliyolishwa kwa miaka mingi sasa kuna haja ya kuijadili kama ulivyoileta ili tuamue kama tuendelee nayo ama tuipuuze.
Kwa hawa uliwataja wanaingia kwenye dhana na mbingu na kuzimu. Mema na mabaya. Malaika na mapepo. Yaani nao wanaamini katika uwili.
 
Mkuu hapo ngoja na mimi nitoe mawazo yangu kutokana na dhehebu langu tulivyofunzwa Shetani alikuwa malaika kama ulivyoeleza pia aliumbwa kwa madini mbalimbali ya kuvutia. Na alikuwa na mamlaka kuliko malaika wote. Sasa wakati anaumbwa mwanadamu shetani hakushirikishwa hivyo moja ya vitu vilivyopelekea aanze kampeni yake ya uhamasishaji usaliti na uasi.

Nilijitahidi kuhoji zaidiii "Na tumuumbe mtu kwa mfano wetu" hii kauli Mungu alikuwa na nani? Nilipewa ufafanuzi kuwa kulikuwa na Mungu Baba(Power), Mungu mwana na Mungu roho mtakatifu.

Hivyo Baada ya shetani kufurushwa kwa kushindwa mapambano yeye na theluthi ya malaika aliowashawishi akatupwa huku duniani na ole ikatolewa kwa wote waliokuwa huku duniani.

Sasa hii mada imekuja wakati muafaka zaidi ili kupata mwanga zaidi maana hapa kwenye Creation pana maelezo tofauti sana na kuna wakati hapaitaji kabisa uwe religious.

Asante mkuu mshana
 
Kwa mujibu huo Mungu kukaa na cabinet yake kisha kuleta hoja ya aidha aumbe kiumbe chenye kufanana nao.

Hii inaonesha hakuwa na maamuzi ya moja kwa moja katika kila jambo. Ama kama alikuwa alikuwa na alikuwa na mamlaka ya kufanya chochote bila kuwepo kwa ushauri wa cabinet yake lakini aliamua ashirikishe cabinet yake. Basi yeye ni mwenye busara sana.

Je, vipi kama angepata upinzani baada ya kuwasilisha ombi lake.

Je, ni wote kwenye cabinet walikubali wazo lake.
 
Ukisoma kwa umakini Mwanzo sura ya kwanza mstari wa kwanza utagudundua kuwa kulikuwa na maisha kabla ya uumbaji huu wa dunia ya sasa uliopo.

Na baadhi ya theolojia za Kikristo zinataja kuwa Mungu kabla ya kumuumba Adam na kizazi chake aliwahi kuumba kizazi kingine, ila kilijivuruga sana, hivyo akaamua kukifutilia mbali na hivyo kupelekea nchi kuwa giza na ukiwa na Roho Mtakatifu akapewa jukumu a kuishikilia dunia kwa muda mpaka pale Uumbaji mpya utakapofanyika.

Kwa muktadha wa theolojia hiyo ni kuwa mara baada ya Mungu kutaka kurudisha uumbaji upya kutokana na uumbaji wa kwanza kufutiliwa mbali, ilibidi kukaa kikao mbinguni kupitisha maazimio ya kumuumba mwanadamu wa sasa na kizazi chake, na hili lilileta mvutano sana.

Wengi wa malaika na viumbe vya mbinguni vilipinga wazo hili kwa hoja kuwa so long as Shetani bado yupo, haina maana ya kuleta upya kizizi kingine maana yatatokea yale yale ya kizazi cha kwanza.

Lakini theolojia hiyo haisemi kwa nini Mungu pamoja na hoja nzuri ya malaika zake aliamua kumuumba Adamu japo alijua kabisa kuwa angeyarudia makosa yale yale ya watangulizi wake.

Ikumbukwe pia kuwa Mungu amekuwa na kawaida ya kukaa vikao na malaika wake, kama inavyoonekana kwenye Biblia.

Mfano , wakati Mungu anataka kumuhukumu Mfalme katili sana wa Israel aliyejulikana kama Ahabu kilikaa kikao na majadiliano yakawepo ya jinsi ya kumdanganya Mfalme aende vitani ili auwawe ili neno la nabii Eliya litimie, habari hii inapatikana katika 1Wafalme 22:19-23.

Pia wakati Ayubu anaundiwa zengwe ili kujaribiwa kwa majipu yale kiliwahi kukaa kikao Mbinguni na inaonekana Shetani alipeleka hoja zake Mbinguni japo za uchongezi ili kumshitaki Ayubu ajaribiwe.

Pia kimewahi kukaa kikao kati ya Mungu na Wajumbe wake cha nani atumwe kuja duniani kuwaokoa wanadamu, wajumbe kwa kujua uzito wa kazi mbele yao walikaa kimya, ndipo Yesu akasema nitume mimi.

Pia kwenye kitabu cha Ufunuo 5:1 inaonekana kulikuwa kikao mbinguni kati ya Mungu na wajumbe wake cha kuangalia ni nani aliyekuwa na uwezo wa kufungua document moja iliyokuwa ina siri nzito sana, na wajumbe wote wakakosa qualifications , mpaka Yesu mwenyewe alipoamua kufungua document hiyo.

Kimsingi suala la vikao mbinguni ni la kawaida sana, tatizo linakuwa ni moja tu kuwa wajumbe wa vikao huwa hawatajwi, anatajwa mwenyekiti wa kikikao pekee ambaye ni Mungu, na hii inatokana na mfumo wa utawala wa Kimbingu kuwa wa Kifalme.

Kawaida ya mfalme ni kubeba sifa zote hata kama watendaji wake ndio wamefanya maana mamlaka ya kiutendaji ya watendaji hao inatoka kwa Mfalme mwenyewe.

Kwa hiyo suala la uumbaji wa Adamu lilikuwa ni mwendelezo wa vikao hivyo hivyo, tatizo ni kuwa wajumbe wa vikao hawakutajwa, ila ukisoma Bibia kwa umakini utagundua kuwa waliokuwa wanazungumza katika kikao hicho walikuwa na cheo cha Uungu.

Kibiblia wenye cheo cha Uungu kwa mbinguni wako watatu, Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.
Kwa duniani cheo cha Uungu kipo kwa Shetani(Yesu alimuita Mungu wa dunia hii), Musa pia aliwahi kupewa cheo hicho, akawa kama Mungu kwa Farao na Haruni kuwa Nabii wake.

Kwa mantiki hiyo, kama kikao kile cha uumbaji kilikaa mbinguni bila shaka walikuwa watatu waliokaa ambao ni Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.

Na hapo ndipo inapokuja kauli ya tumfanye mtu kwa sura yetu na mfano wetu.
 
Mkuu hapo ngoja na mimi nitoe mawazo yangu kutokana na dhehebu langu tulivyofunzwa Shetani alikuwa malaika kama ulivyoeleza pia aliumbwa kwa madini mbalimbali ya kuvutia. Na alikuwa na mamlaka kuliko malaika wote. Sasa wakati anaumbwa mwanadamu shetani hakushirikishwa hivyo moja ya vitu vilivyopelekea aanze kampeni yake ya uhamasishaji usaliti na uasi.

Nilijitahidi kuhoji zaidiii "Na tumuumbe mtu kwa mfano wetu" hii kauli Mungu alikuwa na nani? Nilipewa ufafanuzi kuwa kulikuwa na Mungu Baba(Power), Mungu mwana na Mungu roho mtakatifu.

Hivyo Baada ya shetani kufurushwa kwa kushindwa mapambano yeye na theluthi ya malaika aliowashawishi akatupwa huku duniani na ole ikatolewa kwa wote waliokuwa huku duniani.

Sasa hii mada imekuja wakati muafaka zaidi ili kupata mwanga zaidi maana hapa kwenye Creation pana maelezo tofauti sana na kuna wakati hapaitaji kabisa uwe religious.

Asante mkuu mshana
Asante sana kuna kitu kinaacha Maswali mengi kumhusu shetani. Je, huyu ni mbeba maono? Kwanini baada ya kuasi mbinguni akapewa access na mamlaka ya kuingia Eden?

Katika utatu mtakatifu. Shetani sio sehemu yake. Lakini anakuja baadae kuasi na kufukuzwa mbinguni huku akipewa ukuu wa anga. Anafanya mabaya na maovu mengi lakini hawezi kuangamizwa. Anaomba hata ruhusa na anapewa kibali cha kumtesa Ayubu (kwa sababu tu ya imani yake thabiti kwa Mungu). Shetani anaweza kuwa sehemu kubwa ya unabii.
 
Nahtaji kufahamU kipi kilitangulia kati ya hvi? shetan kutupwa kwny mamlaka ya giza au shetan kumuongopea mwanamke?

Lakn pia nadhan aliamua kushirikisha cabinet yake juu ya uumbaji wa adam mana am sure ilihtaji skills kubwa zaid na pia ndo kwa mara ya kwanza ilibid aumbwe kiumbe kwa udongo na nyama, lakn hakuitaj sana msaada kumtengeneza mwanamke mana ilikua ni inshu ya kupga copy na kuweka jinsia tu.
 
Kwa mujibu huo Mungu kukaa na cabinet yake kisha kuleta hoja ya aidha aumbe kiumbe chenye kufanana nao... Hii inaonesha hakuwa na maamuzi ya moja kwa moja katika kila jambo. Ama kama alikuwa alikuwa na alikuwa na mamlaka ya kufanya chochote bila kuwepo kwa ushauri wa cabinet yake lakini aliamua ashirikishe cabinet yake. Basi yeye ni mwenye busara sana.

Je, vipi kama angepata upinzani baada ya kuwasilisha ombi lake.

Je, ni wote kwenye cabinet walikubali wazo lake.
Mamlaka ya cabinet yaliridhia kwa pamoja wazi la kuumba mtu kwa mfano wao. Shida au unabii inaanzia pale Mwenyezi Mungu anapoamua kwa mamlaka aliyonayo kumtengeneza Hawa. 'NITAKUNGENGENEZEA MSAIDIZI' hapa malaika mkuu hakushirikishwa wala cabinet.
 
Asante sana kuna kitu kinaacha Maswali mengi kumhusu shetani. Je, huyu ni mbeba maono? Kwanini baada ya kuasi mbinguni akapewa access na mamlaka ya kuingia Eden?

Katika utatu mtakatifu. Shetani sio sehemu yake. Lakini anakuja baadae kuasi na kufukuzwa mbinguni huku akipewa ukuu wa anga. Anafanya mabaya na maovu mengi lakini hawezi kuangamizwa. Anaomba hata ruhusa na anapewa kibali cha kumtesa Ayubu (kwa sababu tu ya imani yake thabiti kwa Mungu). Shetani anaweza kuwa sehemu kubwa ya unabii.
Na ndio kuna kitu huwa wengine tunajiuliza.

Je, wewe mshana unaweza ukatengeneza gari lako mwenyewe kisha ukaanza kulipiga mawe kuliharibu. Au ndio utatafuta kila namna kulitunza na kuihakikishia ulinzi wa kudumu milele. Kumbuka una uwezo wa kulitimizia chochote kile. Mafuta endapo yataisha, ufundi endapo litaharibika.

Kwanini Mungu aliweza kumpa uhuru shetani kumuharibu mwanaadamu akianza na Hawa/Eva bila Mungu kuulinda huo uharibifu kwakuwa alikuwa na mamlaka kamili.
 
@ Mshana Jr. Naomba kushare vitu viwili nilivyokuwa na uelewa navyo.

1. Kuna kipindi nikiwa nasoma kwa mzee Madiba, chuo flani maarufu katika mji mkuu wao, walinijia wasichana kama wa3 hivi na kuniomba wanihubirie, so niliwakubalia. Wakaanza mahubiri na huo mstari unaosema na tuumbe mtu kwa mfano wetu.

Point yao ni kama unavyosema wewe kulikuwa na zaidi ya Mungu muda huo. Na wakaenda mbali zaidi na kusema kuwa kama waliumba Adam na Hawa, basi kulikuwa na jinsia ya kike vilevile, hivyo Mungu alikuwa anashauriana na mke wake. Kwa imani yao wao ni kuwa Mungu alikuwa na mke ndio maana aliumba mume na mke. Wakamlizia kwa kunikaribisha katika kanisa lao. Hivyo utaona hili suala linasumbua sio sisi tu.

2. Ni kuwa katika imani ya kiislam, Mungu kutumia neno linalo onyesha wingi ni katika kutaka kuonyesha utukufu na ukubwa wake. So kwao hilo alina maana kuna miungu mingi au wasaidizi ila ni utukufu na ukubwa wake.
Kwa majibu mazuri zaidi ya kutoka katika vitabu, tuombe wenye elimu zaidi ya hivi vitu watusaidie kwa pande zote mbili.
 
Ukisoma kwa umakini Mwanzo sura ya kwanza mstari wa kwanza utagudundua kuwa kulikuwa na maisha kabla ya uumbaji huu wa dunia ya sasa uliopo.

Na baadhi ya theolojia za Kikristo zinataja kuwa Mungu kabla ya kumuumba Adam na kizazi chake aliwahi kuumba kizazi kingine, ila kilijivuruga sana, hivyo akaamua kukifutilia mbali na hivyo kupelekea nchi kuwa giza na ukiwa na Roho Mtakatifu akapewa jukumu a kuishikilia dunia kwa muda mpaka pale Uumbaji mpya utakapofanyika.

Kwa muktadha wa theolojia hiyo ni kuwa mara baada ya Mungu kutaka kurudisha uumbaji upya kutokana na uumbaji wa kwanza kufutiliwa mbali, ilibidi kukaa kikao mbinguni kupitisha maazimio ya kumuumba mwanadamu wa sasa na kizazi chake, na hili lilileta mvutano sana.
Wengi wa malaika na viumbe vya mbinguni vilipinga wazo hili kwa hoja kuwa so long as Shetani bado yupo, haina maana ya kuleta upya kizizi kingine maana yatatokea yale yale ya kizazi cha kwanza.

Lakini theolojia hiyo haisemi kwa nini Mungu pamoja na hoja nzuri ya malaika zake aliamua kumuumba Adamu japo alijua kabisa kuwa angeyarudia makosa yale yale ya watangulizi wake.

Ikumbukwe pia kuwa Mungu amekuwa na kawaida ya kukaa vikao na malaika wake, kama inavyoonekana kwenye Biblia.

Mfano , wakati Mungu anataka kumuhukumu Mfalme katili sana wa Israel aliyejulikana kama Ahabu kilikaa kikao na majadiliano yakawepo ya jinsi ya kumdanganya Mfalme aende vitani ili auwawe ili neno la nabii Eliya litimie, habari hii inapatikana katika 1Wafalme 22:19-23.

Pia wakati Ayubu anaundiwa zengwe ili kujaribiwa kwa majipu yale kiliwahi kukaa kikao Mbinguni na inaonekana Shetani alipeleka hoja zake Mbinguni japo za uchongezi ili kumshitaki Ayubu ajaribiwe.

Pia kimewahi kukaa kikao kati ya Mungu na Wajumbe wake cha nani atumwe kuja duniani kuwaokoa wanadamu, wajumbe kwa kujua uzito wa kazi mbele yao walikaa kimya, ndipo Yesu akasema nitume mimi.

Pia kwenye kitabu cha Ufunuo 5:1 inaonekana kulikuwa kikao mbinguni kati ya Mungu na wajumbe wake cha kuangalia ni nani aliyekuwa na uwezo wa kufungua document moja iliyokuwa ina siri nzito sana, na wajumbe wote wakakosa qualifications , mpaka Yesu mwenyewe alipoamua kufungua document hiyo.

Kimsingi suala la vikao mbinguni ni la kawaida sana, tatizo linakuwa ni moja tu kuwa wajumbe wa vikao huwa hawatajwi, anatajwa mwenyekiti wa kikikao pekee ambaye ni Mungu, na hii inatokana na mfumo wa utawala wa Kimbingu kuwa wa Kifalme.
Kawaida ya mfalme ni kubeba sifa zote hata kama watendaji wake ndio wamefanya maana mamlaka ya kiutendaji ya watendaji hao inatoka kwa Mfalme mwenyewe.

Kwa hiyo suala la uumbaji wa Adamu lilikuwa ni mwendelezo wa vikao hivyo hivyo, tatizo ni kuwa wajumbe wa vikao hawakutajwa, ila ukisoma Bibia kwa umakini utagundua kuwa waliokuwa wanazungumza katika kikao hicho walikuwa na cheo cha Uungu.

Kibiblia wenye cheo cha Uungu kwa mbinguni wako watatu, Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.
Kwa duniani cheo cha Uungu kipo kwa Shetani(Yesu alimuita Mungu wa dunia hii), Musa pia aliwahi kupewa cheo hicho, akawa kama Mungu kwa Farao na Haruni kuwa Nabii wake.

Kwa mantiki hiyo, kama kikao kile cha uumbaji kilikaa mbinguni bila shaka walikuwa watatu waliokaa ambao ni Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.

Na hapo ndipo inapokuja kauli ya tumfanye mtu kwa sura yetu na mfano wetu.
Nichukue kipengele kimoja cha maisha kabla ya kuumbwa Adam na kizazi kilichoteketezwa kama ilivyotokea kwa Sodoma na Gomora. Je, Huyu mwanamama Lilith asiyetajwa kwa jina lake hili kwenye Bible ni sehemu ya mabaki ya jicho kizazi kilichoteketezwa ama aliumbwa sawa na Adam kama baadhi ya maandiko nje ya Bible yanavyodai?

Na ni Kwanini shetani aliendelea kuachwa atambe?
 
Lugha ya mfano

Itawatoa povu Bure Tu
Sorry kama ni lugha ya mfano. Uhalisia wake ninini? Kumbuka hapa hatukosoi (hatuna uwezo huo) bali tunajenga mjadala wenye kuelimishana. Kwahiyo ishu ya kutoa povu sidhani kama hapa ni mahali pake sahihi
 
Nichukue kipengele kimoja cha maisha kabla ya kuumbwa Adam na kizazi kilichoteketezwa kama ilivyotokea kwa Sodoma na Gomora..... Je Huyu mwanamama Lilith asiyetajwa kwa jina lake hili kwenye Bible ni sehemu ya mabaki ya jicho kizazi kilichoteketezwa ama aliumbwa sawa na Adam kama baadhi ya maandiko nje ya Bible yanavyodai? Na ni Kwanini shetani aliendelea kuachwa atambe?
Theolojia haimtaji Lilith na huyu Shetani anatajwa tu kama Shetani.

Mara baada ya kukifuta kile kizazi dunia ilibaki tupu na ukiwa, maana yake hakukuwa na kiumbe hai chochote kilichobakia, na hapo ndipo Roho wa Mungu ikabidi ashikilie kipindi hicho cha mpito.

Shetani hakuachwa atambe kama wengi wanavyodhani, ila wanadamu ndio walimpa upenyo wa kuingia huku kwetu, kawaida ya Mungu huvijaribu viumbe vyake vyote alivyovyipa utashi wa kuchagua jema na baya.

Na lake ni zuri tu, ni ili viumbe vyake vionyeshe upendo na utiifu kwa Mungu wao kama vikipewa nafasi ya kupewa kuasi, maana yake ni kuwa pasipo uhuru wa kuasi maana yake hakuna freewill.

Adam alipewa mtihani huo kumpima utiifu wake, bahati mbaya sana akalamba F. Theolojia inadai kuwa baada ya kuona amechemka, akapanga kujiua, lakini Mungu akamzuia, lakini aliendelea kufanya majaribio kama matatu hivi ya kujiondoa uhai kwani alijua madhara aliyoyaleta kwa kizazi chake baada yake.

Ndipo ikabidi Mungu kupitia Neno (kama aivyokuwa anajulikana siku hizo) kutoa ahadi ya kuja kumuokoa baada ya siku kubwa 5500.

Adamu akajua ni siku 5500 za kibinadamu, kumbe ilikuwa ni miaka 5500. Na baada ya miaka hiyo 5500, Neno akaja kama mtoto mdogo kwa jina la Yesu na akaja kufanya kama alivyofanya.

Kwa nini Shetani aache kutamba?

Shetani amekuwa na kawaida ya kuendeleza uasi kwa uumbaji wa Mungu toka huko mbinguni mpaka huku duniani, sasa hukumu yake ilikwishatolewa, ila moja ya maajabu ya Mungu ni kutokutekeleza hukumu zake hata kama ameshahukumu. Huwa Mungu ana tabia ya kutoa muda fulani kwa waliohukumiwa, kabla ya hukumu zao kutekelezwa.

Mfano Adamu aihukumiwa kufa mara baada ya kula tunda, lakini hukumu ilikuja kutimia Adamu akiwa na miaka kama 930 hivi, hivyo hivyo kwa Kaini na wengineo. Shetani naye ameshahukumiwa, kinachompa kiburi shetani ni ujinga wa wanadamu kuendelea kumfuata huko kuzimu ili awape nguvu (kumbuka Shetani alikuwa malaika wa ngazi ya Kerubi na alikuwa ametiwa mafuta, au ana upako wake).

Na huo upako wake ambao wanadamu wanautafuta ndio unaompa access ya kuja huku uraiani, wanamfuata awape upako wa kuwa maarufu kupitia jamii za siri kama freemasonry, kuwapa upako wa kuwa matajiri, kuwapa upako wa kiutawala kupitia makafara, kuwapa upako wa ulinzi kupitia sarakasi zote za giza.

Kama mwanadamu akiamua kuachana na shetani , shetani hawezi kutamba duniani. Dunia iliumbwa kwa ajili ya wanadamu na si mashetani, sisi ndio wenye vihere here vya kumkaribisha humu duniani, na kwa kuwa ni king'ang'anizi akishakuja kuondoka ni shughuli kweli kweli.
 
Na ndio kuna kitu huwa wengine tunajiuliza...

Je ww mshana unaweza ukatengeneza gari lako mwenyewe kisha ukaanza kulipiga mawe kuliharibu... Au ndio utatafuta kila namna kulitunza na kuihakikishia ulinzi wa kudumu milele... Kumbuka una uwezo wa kulitimizia chochote kile... Mafuta endapo yataisha, ufundi endapo litaharibika,...

Kwanini Mungu aliweza kumpa uhuru shetani kumuharibu mwanaadamu akianza na Hawa/Eva bila Mungu kuulinda huo uharibifu kwakuwa alikuwa na mamlaka kamili...
Ukifikiri sana utasema kwamba alikuwa hajiamini.
 
Back
Top Bottom