Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mwanzo 1:2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Kwa Sura hii inamaanisha’ Roho Mtakatifu’ alikuwepo wakati wa uumbaji

Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Mastari wa 26 ametaja utatu mtakatifu na mstari wa 27 unamaanisha ni Mungu pekee ndie aliumba mwanadamu.

Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
* kwa hiyo Mungu mwenyewe ndio alimuumba Binadamu
 
Theolojia haimtaji Lilith na huyu Shetani anatajwa tu kama Shetani.

Mara baada ya kukifuta kile kizazi dunia ilibaki tupu na ukiwa, maana yake hakukuwa na kiumbe hai chochote kilichobakia, na hapo ndipo Roho wa Mungu ikabidi ashikilie kipindi hicho cha mpito.

Shetani hakuachwa atambe kama wengi wanavyodhani, ila wanadamu ndio walimpa upenyo wa kuingia huku kwetu, kawaida ya Mungu huvijaribu viumbe vyake vyote alivyovyipa utashi wa kuchagua jema na baya.

Na lake ni zuri tu, ni ili viumbe vyake vionyeshe upendo na utiifu kwa Mungu wao kama vikipewa nafasi ya kupewa kuasi, maana yake ni kuwa pasipo uhuru wa kuasi maana yake hakuna freewill.

Adam alipewa mtihani huo kumpima utiifu wake, bahati mbaya sana akalamba F.
Theolojia inadai kuwa baada ya kuona amechemka, akapanga kujiua, lakini Mungu akamzuia, lakini aliendelea kufanya majaribio kama matatu hivi ya kujiondoa uhai kwani alijua madhara aliyoyaleta kwa kizazi chake baada yake.

Ndipo ikabidi Mungu kupitia Neno(kama aivyokuwa anajulikana siku hizo) kutoa ahadi ya kuja kumuokoa baada ya siku kubwa 5500.

Adamu akajua ni siku 5500 za kibinadamu, kumbe ilikuwa ni miaka 5500.
Na baada ya miaka hiyo 5500, Neno akaja kama mtoto mdogo kwa jina la Yesu na akaja kufanya kama alivyofanya.

Kwa nini Shetani aache kutamba??

Shetani amekuwa na kawaida ya kuendeleza uasi kwa uumbaji wa Mungu toka huko mbinguni mpaka huku duniani, sasa hukumu yake ilikwishatolewa, ila moja ya maajabu ya Mungu ni kutokutekeleza hukumu zake hata kama ameshahukumu.
Huwa Mungu ana tabia ya kutoa muda fulani kwa waliohukumiwa, kabla ya hukumu zao kutekelezwa.

Mfano Adamu aihukumiwa kufa mara baada ya kula tunda, lakini hukumu ilikuja kutimia Adamu akiwa na miaka kama 930 hivi, hivyo hivyo kwa Kaini na wengineo.

Shetani naye ameshahukumiwa, kinachompa kiburi shetani ni ujinga wa wanadamu kuendelea kumfuata huko kuzimu ili awape nguvu(kumbuka Shetani alikuwa malaika wa ngazi ya Kerubi na alikuwa ametiwa mafuta, au ana upako wake).

Na huo upako wake ambao wanadamu wanautafuta ndio unaompa access ya kuja huku uraiani, wanamfuata awape upako wa kuwa maarufu kupitia jamii za siri kama freemasonry, kuwapa upako wa kuwa matajiri, kuwapa upako wa kiutawala kupitia makafara, kuwapa upako wa ulinzi kupitia sarakasi zote za giza.

Kama mwanadamu akiamua kuachana na shetani , shetani hawezi kutamba duniani.
Dunia iliumbwa kwa ajili ya wanadamu na si mashetani, sisi ndio wenye vihere here vya kumkaribisha humu duniani, na kwa kuwa ni king'ang'anizi akishakuja kuondoka ni shughuli kweli kweli.
Asante sana naomba niongee kwa ufupi sana kwamba kuna mstari mwembamba sana kati ya shetani na mwanadamu... Kiasi kwamba binadamu awaye yote hana nguvu wala utashi wa kumkwepa shetani.

Na huu ni unabii mkongwe sana.... Binadamu aliumbwa siku ya sita (666?) Namba ya mamlaka ya dunia(Lucifer).... Mungu akapumzika siku ya saba 7️⃣.... Kiroho hii ni namba ya ukamilifu wa mamlaka ya kimbingu na kiroho
 
Mwanzo 1:2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Kwa Sura hii inamaanisha’ Roho Mtakatifu’ alikuwepo wakati wa uumbaji

Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Mastari wa 26 ametaja utatu mtakatifu na mstari wa 27 unamaanisha ni Mungu pekee ndie aliumba mwanadamu.

Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
* kwa hiyo Mungu mwenyewe ndio alimuumba Binadamu
Mstari wa 27 unazua Maswali... Kwa mfano wa Mungu akaumba mwanaume (Adam) na mwanamke(....) Ni mwanamke gani huyu? Kwa vyovyote sio Hawa/Eva... Kwakuwa huyu alikuja baadae kabisa tena hakuumbwa bali alitengenezwa toka mifupani mwa Adam
 
Inaandikwa kwamba..... Basi Bwana Mungu akasema... NA TUUMBE MTU kwa mfano wetu.. Hapa Bwana Mungu hakuwa pekeyake... Kulikuwa na mamlaka kamili ya kiroho juu mbinguni yaliyokuwa yanaongozwa na Mungu mwenyewe
Tafsiri nyingine ni kwamba tayari huko mbinguni kulikuwa na maisha mengine ya kiroho mpaka walipojadiliana kuumba mtu mwenyewe mwili wa nyama
Uumbaji mwingine wote wa vitu na wanyama viliumbwa na Mungu mwenyewe... Kwa uweza wake mkuu wa kutamka tu na ikawa.... Ilipofika kwenye kuumba MTU ndio cabinet ya mbingu ikahusishwa!
Kwanini kwenye uumbaji wa MTU Mungu hakufanya maamuzi binafsi Kama kwa wanyama mimea na vingine vyote? Kuna ufunuo wa ajabu hapa... Ni kwa vile alitaka awepo mtu kwa mfano WAO
Shetani anatajwa kama malaika mkuu... K vyeo vya kisasa unaweza kusema katibu mkuu, waziri mkuu ama msaidizi mkuu..... Huyu kwa asilimia 95 hufahamu yote ya mkuu wake wa kazi kwakuwa ndio kama mtendaji mkuu
Kwenye uumbaji Mungu aliumba kila kimoja na kinyume chake... N mpaka wakati huu Hakukuwa na kitu kinaitwa dhambi japo kabla ya uumbaji nchi ilikuwa kiza tena totoro kiwa(ukiwa) na vilindi vya maji vikiwa vimetuama juu ya uso wa dunia...
Ni kwenye uumbaji pekee wa Adam ndio Mungu aliishirikisha Mamlaka yake (shetani?) Vingine vyote alifanya mwenyewe.... Na hata alipoona Adam yu mpweke bustanini... Kwa mamlaka yake binafsi akamtengenenezea Adam msaidizi (Hawa/Eva?)
Kwanini hapa haikushirikisha cabinet yake? Je lilith ndio shetani mwenyewe? Nini kilimuudhi shetani mpaka kuamua kwenda kumdanganya msaidizi wa Adam ale tunda la mti wa kati? Mti wa ujuzi wa mema na mabaya? Je ni kwa vile hakushirikishwa kwenye kumtengeneza? Wivu? Kisasi? Kwanini hakumwendea Adam? Au kwakuwa aliasi mbinguni na kufukuzwa?
Na baada ya hapo dhambi ikaingia ulimwenguni na shetani akapewa ufalme wa giza.... Ndio hapa kinyume cha mbingu kinakamilisha uumbaji wote kiroho....
Je huu ulikuwa unabii au mpango wa Mungu? Kwanini shetani ana role kubwa sana kwenye dhana nzima ya kukengeuka kwa dunia, Adam na upili wa kiumbaji?

Tutafakari kwa pamoja... Inawezekana kabisa shetani tumdhaniaye na nyoka tumwonaye ni vitu vingine kabisa tofauti na uhalisia wa dhana nzima ya Eden, uumbaji, uasi, tunda la mti wa kati nk
Sijawahi kuona andiko likimtambulisha shetani kama aliwahi kuwa malaika mkuu.
Vipi ndugu yetu unaweza kutusaidia hili andiko?
 
Sijawahi kuona andiko likimtambulisha shetani kama aliwahi kuwa malaika mkuu.
Vipi ndugu yetu unaweza kutusaidia hili andiko?
Hata mimi sijawahi bali inasemwa hivyo... Pengine kuna ambao wanaweza kuja na ithibati
 
Ninacho kupendea Mshana, mara nyingi hua unaleta HOJA fikirishi, well done brother.
Nichangie name ninavyo fahamu kidogo kuhusu hu uzi uliouleta; Ukisoma Biblia shetani (kabla ya kutupwa duniani alikua akiitwa Kerubi) hakua mkuu wa malaika kama watu wanavyo jaribu kufikiri, alikua mkuu wa Idara ya UIMBAJI, huko mbinguni inaitwa idara ya kusifu na kuabudu na Michael/Mikaeli yeye ni mkuu wa vita wakati Gabriel yeye ni mkuu wa kutoa habari; ukisoma kitabu cha Daniel nafikiri sura ya 7, malaika mmojawapo aliyetumwa kumletea habari Nabii Daniel anamwambia hivi Daniel, "....Ewe Daniel unaye pendwa sana...., maombi yako yalisikiwa tokea siku ile ulipo OMBA lakini yule mkuu wa UAJEMI alimzuia aliyetumwa nae Mikaeli mmojawapo wa wakuu..." hilo neno mmojawapo wa wakuu lina maana kwamba huko mbinguni wakuu wapo wengi! Again, hatuna hakika ni lini shetani alitupwa duniani, je ni baada ya uumbaji au kabla ya uumbaji!?

No body knows kwasababu kwanini huyu huyu shetani alimuijia HAWA pale bustanini na kumdanganya!? LEt su wait from the Bible scholar to explain more
 
Na ndio kuna kitu huwa wengine tunajiuliza...

Je ww mshana unaweza ukatengeneza gari lako mwenyewe kisha ukaanza kulipiga mawe kuliharibu... Au ndio utatafuta kila namna kulitunza na kuihakikishia ulinzi wa kudumu milele... Kumbuka una uwezo wa kulitimizia chochote kile... Mafuta endapo yataisha, ufundi endapo litaharibika,...

Kwanini Mungu aliweza kumpa uhuru shetani kumuharibu mwanaadamu akianza na Hawa/Eva bila Mungu kuulinda huo uharibifu kwakuwa alikuwa na mamlaka kamili...


Kaka jifunze kutoa mifano,yaani tolea mfano jambo ambalo linalingana na jambo kusudiwa.

Ukilinganisha uumbaji wa Allah na vitu vilivyo tengenzwa na binadamu.

Kwa ufinyu wa tafakuri ndio huwa kuna muda mnauliza maswali ya UONGO.
 
Inaandikwa kwamba..... Basi Bwana Mungu akasema... NA TUUMBE MTU kwa mfano wetu.. Hapa Bwana Mungu hakuwa pekeyake... Kulikuwa na mamlaka kamili ya kiroho juu mbinguni yaliyokuwa yanaongozwa na Mungu mwenyewe
Tafsiri nyingine ni kwamba tayari huko mbinguni kulikuwa na maisha mengine ya kiroho mpaka walipojadiliana kuumba mtu mwenyewe mwili wa nyama
Uumbaji mwingine wote wa vitu na wanyama viliumbwa na Mungu mwenyewe... Kwa uweza wake mkuu wa kutamka tu na ikawa.... Ilipofika kwenye kuumba MTU ndio cabinet ya mbingu ikahusishwa!
Kwanini kwenye uumbaji wa MTU Mungu hakufanya maamuzi binafsi Kama kwa wanyama mimea na vingine vyote? Kuna ufunuo wa ajabu hapa... Ni kwa vile alitaka awepo mtu kwa mfano WAO
Shetani anatajwa kama malaika mkuu... K vyeo vya kisasa unaweza kusema katibu mkuu, waziri mkuu ama msaidizi mkuu..... Huyu kwa asilimia 95 hufahamu yote ya mkuu wake wa kazi kwakuwa ndio kama mtendaji mkuu
Kwenye uumbaji Mungu aliumba kila kimoja na kinyume chake... N mpaka wakati huu Hakukuwa na kitu kinaitwa dhambi japo kabla ya uumbaji nchi ilikuwa kiza tena totoro kiwa(ukiwa) na vilindi vya maji vikiwa vimetuama juu ya uso wa dunia...
Ni kwenye uumbaji pekee wa Adam ndio Mungu aliishirikisha Mamlaka yake (shetani?) Vingine vyote alifanya mwenyewe.... Na hata alipoona Adam yu mpweke bustanini... Kwa mamlaka yake binafsi akamtengenenezea Adam msaidizi (Hawa/Eva?)
Kwanini hapa haikushirikisha cabinet yake? Je lilith ndio shetani mwenyewe? Nini kilimuudhi shetani mpaka kuamua kwenda kumdanganya msaidizi wa Adam ale tunda la mti wa kati? Mti wa ujuzi wa mema na mabaya? Je ni kwa vile hakushirikishwa kwenye kumtengeneza? Wivu? Kisasi? Kwanini hakumwendea Adam? Au kwakuwa aliasi mbinguni na kufukuzwa?
Na baada ya hapo dhambi ikaingia ulimwenguni na shetani akapewa ufalme wa giza.... Ndio hapa kinyume cha mbingu kinakamilisha uumbaji wote kiroho....
Je huu ulikuwa unabii au mpango wa Mungu? Kwanini shetani ana role kubwa sana kwenye dhana nzima ya kukengeuka kwa dunia, Adam na upili wa kiumbaji?

Tutafakari kwa pamoja... Inawezekana kabisa shetani tumdhaniaye na nyoka tumwonaye ni vitu vingine kabisa tofauti na uhalisia wa dhana nzima ya Eden, uumbaji, uasi, tunda la mti wa kati nk


Tukio hili pia limezungumzwa katika Qur'an ila tofauti na upande wako.

Kabla sijaelezea kile ninacho taka nikielezee,naomba unipe ufafanuzi kidogo kutokana na kaulli yako "...Shetani anatajwa kama malaika mkuu" . Hapa sijaelewa kidogo. Yaani anatajwa na nani kama malaika mkuu ?
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Tukio hili pia limezungumzwa katika Qur'an ila tofauti na upande wako.

Kabla sijaelezea kile ninacho taka nikielezee,naomba unipe ufafanuzi kidogo kutokana na kaulli yako "...Shetani anatajwa kama malaika mkuu" . Hapa sijaelewa kidogo. Yaani anatajwa na nani kama malaika mkuu ?
Nimeulizwa pia na mdau mmoja hapo juu nikakosa jibu vivyo naomba uendelee
 
Kuna wakati kuyafikiria baadhi ya Mambo Aliyoyanya MUNGU hasa hili LA Uumbaji na lile LA MUNGU ni nani?? Ana umbo?? Ni Jinsia gani?? Anaishi wapi? Kwa Nini Aliruhusu Dhambi?

Kwa nini Aliruhusu shetani Autawale ulimwengu?? Itoshe tu kubaki ktk Imani zetu AKILI ZA MUNGU HAZICHUNGUZIKI.
 
Theolojia haimtaji Lilith na huyu Shetani anatajwa tu kama Shetani.

Mara baada ya kukifuta kile kizazi dunia ilibaki tupu na ukiwa, maana yake hakukuwa na kiumbe hai chochote kilichobakia, na hapo ndipo Roho wa Mungu ikabidi ashikilie kipindi hicho cha mpito.

Shetani hakuachwa atambe kama wengi wanavyodhani, ila wanadamu ndio walimpa upenyo wa kuingia huku kwetu, kawaida ya Mungu huvijaribu viumbe vyake vyote alivyovyipa utashi wa kuchagua jema na baya.

Na lake ni zuri tu, ni ili viumbe vyake vionyeshe upendo na utiifu kwa Mungu wao kama vikipewa nafasi ya kupewa kuasi, maana yake ni kuwa pasipo uhuru wa kuasi maana yake hakuna freewill.

Adam alipewa mtihani huo kumpima utiifu wake, bahati mbaya sana akalamba F.
Theolojia inadai kuwa baada ya kuona amechemka, akapanga kujiua, lakini Mungu akamzuia, lakini aliendelea kufanya majaribio kama matatu hivi ya kujiondoa uhai kwani alijua madhara aliyoyaleta kwa kizazi chake baada yake.

Ndipo ikabidi Mungu kupitia Neno(kama aivyokuwa anajulikana siku hizo) kutoa ahadi ya kuja kumuokoa baada ya siku kubwa 5500.

Adamu akajua ni siku 5500 za kibinadamu, kumbe ilikuwa ni miaka 5500.
Na baada ya miaka hiyo 5500, Neno akaja kama mtoto mdogo kwa jina la Yesu na akaja kufanya kama alivyofanya.

Kwa nini Shetani aache kutamba??

Shetani amekuwa na kawaida ya kuendeleza uasi kwa uumbaji wa Mungu toka huko mbinguni mpaka huku duniani, sasa hukumu yake ilikwishatolewa, ila moja ya maajabu ya Mungu ni kutokutekeleza hukumu zake hata kama ameshahukumu.
Huwa Mungu ana tabia ya kutoa muda fulani kwa waliohukumiwa, kabla ya hukumu zao kutekelezwa.

Mfano Adamu aihukumiwa kufa mara baada ya kula tunda, lakini hukumu ilikuja kutimia Adamu akiwa na miaka kama 930 hivi, hivyo hivyo kwa Kaini na wengineo.

Shetani naye ameshahukumiwa, kinachompa kiburi shetani ni ujinga wa wanadamu kuendelea kumfuata huko kuzimu ili awape nguvu(kumbuka Shetani alikuwa malaika wa ngazi ya Kerubi na alikuwa ametiwa mafuta, au ana upako wake).

Na huo upako wake ambao wanadamu wanautafuta ndio unaompa access ya kuja huku uraiani, wanamfuata awape upako wa kuwa maarufu kupitia jamii za siri kama freemasonry, kuwapa upako wa kuwa matajiri, kuwapa upako wa kiutawala kupitia makafara, kuwapa upako wa ulinzi kupitia sarakasi zote za giza.

Kama mwanadamu akiamua kuachana na shetani , shetani hawezi kutamba duniani.
Dunia iliumbwa kwa ajili ya wanadamu na si mashetani, sisi ndio wenye vihere here vya kumkaribisha humu duniani, na kwa kuwa ni king'ang'anizi akishakuja kuondoka ni shughuli kweli kweli.
Theology ni uwanja mpana sana naanza kupata idea sasa ya vitu tofauti kuhusu uumbaji.
 
Mstari wa 27 unazua Maswali... Kwa mfano wa Mungu akaumba mwanaume (Adam) na mwanamke(....) Ni mwanamke gani huyu? Kwa vyovyote sio Hawa/Eva... Kwakuwa huyu alikuja baadae kabisa tena hakuumbwa bali alitengenezwa toka mifupani mwa Adam

Kwa uelewa wangu kwenye kitabu cha Mwanzo sura ya kwanza vitu vilitengenezwa katika ulimwengu wa Roho (Created) ; kwenye sura ya pili inaelezea vitu jinsi vilivyotokea katika ulimwengu wa nyama( Formed)

Nikupe mfano, kwenye Mwanzo sura ya kwanza wanyama na mimea waliumbwa kwenye Ulimwengu wa kiroho (Created)- Mwanzo 1:24-25, kabla ya Binadamu ( Human Kind)- Mwanzo 1:27

Kwenye sura ya pili wakati wa vitu kuonekana katika Ulimwengu wa nyama ( Formation) Binadamu alianza - Mwanzo 2:7 kabla ya wanyama na mimea-Mwanzo 2:19 BWANA Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.

Kwa hiyo uumbaji wa sura ya Pili ni katika ulimwengu wa kimwili kiroho ulishafanyika kama sura ya kwanza inavyoeleza
 
Theology ni uwanja mpana sana naanza kupata idea sasa ya vitu tofauti kuhusu uumbaji.
Kwa uelewa wangu kwenye kitabu cha Mwanzo sura ya kwanza vitu vilitengenezwa katika ulimwengu wa Roho (Created) ; kwenye sura ya pili inaelezea vitu jinsi vilivyotokea katika ulimwengu wa nyama( Formed)

Nikupe mfano, kwenye Mwanzo sura ya kwanza wanyama na mimea waliumbwa kwenye Ulimwengu wa kiroho (Created)- Mwanzo 1:24-25, kabla ya Binadamu ( Human Kind)- Mwanzo 1:27

Kwenye sura ya pili wakati wa vitu kuonekana katika Ulimwengu wa nyama ( Formation) Binadamu alianza - Mwanzo 2:7 kabla ya wanyama na mimea-Mwanzo 2:19 BWANA Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.

Kwa hiyo uumbaji wa sura ya Pili ni katika ulimwengu wa kimwili kiroho ulishafanyika kama sura ya kwanza inavyoeleza
Tuna members wana ufahamu wa juu sana kwenye haya mambo bahati mbaya taifa halina sera wala kipaumbele kwenye elimu ya kiroho... Kuna mijadala hapa michango yake inavutia na imebeba madini hasa..
 
Nimeulizwa pia na mdau mmoja hapo juu nikakosa jibu vivyo naomba uendelee


Kwetu sisi wislamu tukio hili,ila kwa maelezo haya.

Allah hakufanya majadiliano kwa maana ya kutaka ushauri sababu yeye anajua yale ambayo malaika walikuwa hawajui,tukio ni refu ila hapa naelezea kwa ufupi.

Allah aliyejuu aliwaita malaika na ndani yake alikuwemo Azaziri/Aba Sajida (Mwingi wa kusujudu) maarufu kama SHETANI WA KIJINI. Kisa chake ni kirefu cha kwanini naye alijumuishwa pamoja na malaika.

Allah aliwaambia malaika ya kuwa anataka kuweka kiongozi (Khalifa) duniani. Wakahoji "Ewe Mola wetu unataka kuweka kiumbe amacho kitaleta ufisadi katika ardhi". Allaha akawijibu "Mimi ninayajua yale msiyo yajua nyinyi".

Sasa tukirudi katika suala la kwanini Shetani wa kijini alifukuzwa ? Yeye alifukuzwa kwa tabia yake chafu ya kiburi pale walipoambiwa ya kuwa msujudieni Adamu (Kwa maana ya kuwa wampe heshima). Shetani alikaidi agizo hili hali ya kuwa malaika walitii. Shetani alikaidi kwa kusema "Nitamsujudiaje kiumbe kilcho umbwa kwa udongo hali ya kuwa mimi nimeumbwa kwa moto". Yaani Shetani wa kijini yeye alijiona bora kuliko Adamu.

Faida: Shetani ni sifa kama ilivyo sifa ya uzuri,ubaya,wizi na kadhalika. Shetani anaweza kuwa binadamu au jini.

Allah ndie anayejua zaidi na mkamilifu ni yeye.
 
Kwetu sisi wislamu tukio hili,ila kwa maelezo haya.

Allah hakufanya majadiliano kwa maana ya kutaka ushauri sababu yeye anajua yale ambayo malaika walikuwa hawajui,tukio ni refu ila hapa naelezea kwa ufupi.

Allah aliyejuu aliwaita malaika na ndani yake alikuwemo Azaziri/Aba Sajida (Mwingi wa kusujudu) maarufu kama SHETANI WA KIJINI. Kisa chake ni kirefu cha kwanini naye alijumuishwa pamoja na malaika.

Allah aliwaambia malaika ya kuwa anataka kuweka kiongozi (Khalifa) duniani. Wakahoji "Ewe Mola wetu unataka kuweka kiumbe amacho kitaleta ufisadi katika ardhi". Allaha akawijibu "Mimi ninayajua yale msiyo yajua nyinyi".

Sasa tukirudi katika suala la kwanini Shetani wa kijini alifukuzwa ? Yeye alifukuzwa kwa tabia yake chafu ya kiburi pale walipoambiwa ya kuwa msujudieni Adamu (Kwa maana ya kuwa wampe heshima). Shetani alikaidi agizo hili hali ya kuwa malaika walitii. Shetani alikaidi kwa kusema "Nitamsujudiaje kiumbe kilcho umbwa kwa udongo hali ya kuwa mimi nimeumbwa kwa moto". Yaani Shetani wa kijini yeye alijiona bora kuliko Adamu.

Faida: Shetani ni sifa kama ilivyo sifa ya uzuri,ubaya,wizi na kadhalika. Shetani anaweza kuwa binadamu au jini.

Allah ndie anayejua zaidi na mkamilifu ni yeye.
@zurri iko vizuri ila umefupisha mno maelezo ukiweza ingia deep kidogo... Hasa kwenye suala la shetani jini kuumbwa kwa moto... Je jini na shetani jini wana tofauti gani?
 
Ninacho kupendea Mshana, mara nyingi hua unaleta HOJA fikirishi, well done brother.
Nichangie name ninavyo fahamu kidogo kuhusu hu uzi uliouleta;

Ukisoma Biblia shetani (kabla ya kutupwa duniani alikua akiitwa Kerubi) hakua mkuu wa malaika kama watu wanavyo jaribu kufikiri, alikua mkuu wa Idara ya UIMBAJI, huko mbinguni inaitwa idara ya kusifu na kuabudu na Michael/Mikaeli yeye ni mkuu wa vita wakati Gabriel yeye ni mkuu wa kutoa habari; ukisoma kitabu cha Daniel nafikiri sura ya 7, malaika mmojawapo aliyetumwa kumletea habari Nabii Daniel anamwambia hivi Daniel, "....Ewe Daniel unaye pendwa sana...., maombi yako yalisikiwa tokea siku ile ulipo OMBA lakini yule mkuu wa UAJEMI alimzuia aliyetumwa nae Mikaeli mmojawapo wa wakuu..." hilo neno mmojawapo wa wakuu lina maana kwamba huko mbinguni wakuu wapo wengi!

Again, hatuna hakika ni lini shetani alitupwa duniani, je ni baada ya uumbaji au kabla ya uumbaji!?

No body knows kwasababu kwanini huyu huyu shetani alimuijia HAWA pale bustanini na kumdanganya!? LEt su wait from the Bible scholar to explain more
Mikael ndie anatajwa kuwa malaika mkuu. Shetani yeye kabla ya hili jina la uovu alitajajwa kama kerubi afunikae.

Ukiangalia shauku ya shetani iliyomfanya afukuzwe mbinguni kwa kichapo cha Mikael ni kukaaa juu ya mkutano wa watu wa Mungu na aabudiwe kama yeye ndio Mungu mkuu muumba wa yote.

Na ni kama kwetu sisi binadamu na sii mbinguni ni kama amefanikiwa kwa kiwango kikubwa. Watu wa dini humtaja Mungu lakini matendo yao yanamaanisha kitu kingine.

Mungu ni Roho na Adamu aliyeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu alikuwa vyote viwili mwanamme na mwanamke katika mwili mmoja na aliwaita jina lao Adamu.

Kwa mujibu wa biblia Mungu alipowatenga kutoka katika ule mwili mmoja na kuwa mwanamke na mwanamume ndipo kulikopelekea anguko. Shetani hakupitia kwa mwanamne kuuangusha uumbaji ila kwa mwanamke.

Kwa hili maandiko yanasema mwanaume hakuanguka ila mwanamke ndie aliyedanganywa na kuanguka kabisa. Kwa hiyo nine linamkataza mwanamke kumtawala wala kumfundisha mwanamume. Katika masuala ya kiroho ukimwona mwanamke mwenye mamlaka ya kiutendaji ni ishara moja kati ya nyingi za shetani kuendeleza himaya yake duniani.

Katika uumbaji wote wa Mungu viumbe wa kiume ndio warembo isipokuwa kwa binadamu mwanamke ndio mrembo. Katika viumbe wengine ngono ni kwa ajili ya kuendeleza uzao lakini kwa binadamu sii tu kuendeleza uzao bali pia ni starehe ya kudumu.

Hii inaweza kuleta suala la kufikiri ni nini nia ya ubunifu wa mwanamke katika uumbaji na ikiwa kwamba kuna kiumbe kingine kilishiriki katika huu ubunifu kikiwa na nia kinzani.

Kuna mengi kwa kwali ya kufikirisha na hasa ni kwa nini kila aliyezaliwa na mwanamke katika masuala ya kiroho ni sharti azaliwe tena upya kiroho?
Hata kama hakuna tendo lolote baya alilofanya hiyo haiwezi kumfanya awe sehemu ya ufalme wa Mungu hasa baada ya yeye kuweza kupambanua kati ya wema na ubaya.

Naamini bado mda upo ktk hii mada, wadau watakuja na post zenye changamoto tofauti.

Kwa kule juu niseme tuu malaika Gabriel kwa mujibu wa Daniel alikua malaika mkuu kwa taifa la Israel na tunaona alimwacha Malaika Mikael akipambana na mkuu wa taifa la uajemi. Hii inaweza kuonyesha kila anga la mahali katika dunia lina mkuu wao. Hakuna mahali ambapo malaka Gabriel aliwahi mletea mtu ujumbe nje ya waebrania.
 
Kwetu sisi wislamu tukio hili,ila kwa maelezo haya.

Allah hakufanya majadiliano kwa maana ya kutaka ushauri sababu yeye anajua yale ambayo malaika walikuwa hawajui,tukio ni refu ila hapa naelezea kwa ufupi.

Allah aliyejuu aliwaita malaika na ndani yake alikuwemo Azaziri/Aba Sajida (Mwingi wa kusujudu) maarufu kama SHETANI WA KIJINI. Kisa chake ni kirefu cha kwanini naye alijumuishwa pamoja na malaika.

Allah aliwaambia malaika ya kuwa anataka kuweka kiongozi (Khalifa) duniani. Wakahoji "Ewe Mola wetu unataka kuweka kiumbe amacho kitaleta ufisadi katika ardhi". Allaha akawijibu "Mimi ninayajua yale msiyo yajua nyinyi".

Sasa tukirudi katika suala la kwanini Shetani wa kijini alifukuzwa ? Yeye alifukuzwa kwa tabia yake chafu ya kiburi pale walipoambiwa ya kuwa msujudieni Adamu (Kwa maana ya kuwa wampe heshima). Shetani alikaidi agizo hili hali ya kuwa malaika walitii. Shetani alikaidi kwa kusema "Nitamsujudiaje kiumbe kilcho umbwa kwa udongo hali ya kuwa mimi nimeumbwa kwa moto". Yaani Shetani wa kijini yeye alijiona bora kuliko Adamu.

Faida: Shetani ni sifa kama ilivyo sifa ya uzuri,ubaya,wizi na kadhalika. Shetani anaweza kuwa binadamu au jini.

Allah ndie anayejua zaidi na mkamilifu ni yeye.
Mkuu zurri nina swali kidogo naomba ufafanuzi kwanini umesema SHETANI WA KIJINI?

pili, uyo Azazuri/Aba ndiye yule AZAZEL ambaye ni moja ya malaika 200 wanaotajwa katika kitabu cha HENOKO??
 
Inaandikwa kwamba..... Basi Bwana Mungu akasema... NA TUUMBE MTU kwa mfano wetu.. Hapa Bwana Mungu hakuwa pekeyake... Kulikuwa na mamlaka kamili ya kiroho juu mbinguni yaliyokuwa yanaongozwa na Mungu mwenyewe
Tafsiri nyingine ni kwamba tayari huko mbinguni kulikuwa na maisha mengine ya kiroho mpaka walipojadiliana kuumba mtu mwenyewe mwili wa nyama
Uumbaji mwingine wote wa vitu na wanyama viliumbwa na Mungu mwenyewe... Kwa uweza wake mkuu wa kutamka tu na ikawa.... Ilipofika kwenye kuumba MTU ndio cabinet ya mbingu ikahusishwa!
Kwanini kwenye uumbaji wa MTU Mungu hakufanya maamuzi binafsi Kama kwa wanyama mimea na vingine vyote? Kuna ufunuo wa ajabu hapa... Ni kwa vile alitaka awepo mtu kwa mfano WAO
Shetani anatajwa kama malaika mkuu... K vyeo vya kisasa unaweza kusema katibu mkuu, waziri mkuu ama msaidizi mkuu..... Huyu kwa asilimia 95 hufahamu yote ya mkuu wake wa kazi kwakuwa ndio kama mtendaji mkuu
Kwenye uumbaji Mungu aliumba kila kimoja na kinyume chake... N mpaka wakati huu Hakukuwa na kitu kinaitwa dhambi japo kabla ya uumbaji nchi ilikuwa kiza tena totoro kiwa(ukiwa) na vilindi vya maji vikiwa vimetuama juu ya uso wa dunia...
Ni kwenye uumbaji pekee wa Adam ndio Mungu aliishirikisha Mamlaka yake (shetani?) Vingine vyote alifanya mwenyewe.... Na hata alipoona Adam yu mpweke bustanini... Kwa mamlaka yake binafsi akamtengenenezea Adam msaidizi (Hawa/Eva?)
Kwanini hapa haikushirikisha cabinet yake? Je lilith ndio shetani mwenyewe? Nini kilimuudhi shetani mpaka kuamua kwenda kumdanganya msaidizi wa Adam ale tunda la mti wa kati? Mti wa ujuzi wa mema na mabaya? Je ni kwa vile hakushirikishwa kwenye kumtengeneza? Wivu? Kisasi? Kwanini hakumwendea Adam? Au kwakuwa aliasi mbinguni na kufukuzwa?
Na baada ya hapo dhambi ikaingia ulimwenguni na shetani akapewa ufalme wa giza.... Ndio hapa kinyume cha mbingu kinakamilisha uumbaji wote kiroho....
Je huu ulikuwa unabii au mpango wa Mungu? Kwanini shetani ana role kubwa sana kwenye dhana nzima ya kukengeuka kwa dunia, Adam na upili wa kiumbaji?

Tutafakari kwa pamoja... Inawezekana kabisa shetani tumdhaniaye na nyoka tumwonaye ni vitu vingine kabisa tofauti na uhalisia wa dhana nzima ya Eden, uumbaji, uasi, tunda la mti wa kati nk
Niaminivyo mimi Mungu huundwa na vitu vitatu kama ilivyo kwa Mtu(mfano wake). Mtu anaundwa na vitu vitatu 1. mwili (nyama na mifupa) 2.damu 3. uhai/pumzi/nafsi/ufahamu/roho hivyo na Mungu 1.Baba (pengine mwili) 2.Mwana (pengine damu) 3.Roho mtakatifu(uhai/pumzi/nafsi/ufahamu/roho).

Mungu ni very powerfull kuliko sisi/mtu hivyo yeye hivi vitatu vinavyomtengeneza vinaweza kujitenga na vikafanya shughuli kimpango wake kila kimoja bila kuleta madhara kwa Mungu.

Sisi ni mfano tu ndio maana sisi huwe ukatoa mwili kwenye damu bado ukabaki kuwa mtu? huwezi ukatoa ilepumzi ya uhai/ roho ukabaki kuwa mtu hivyohivyo kwenye damu.

kama ilivyo kwa Mungu ukifanya kitu chochote utakuwa umefanya ama mmefanya yote mawili kwenye nafsi yako yanawezekana mfano nikikimbia na kuwa nimekimbia ama tumekimbia (damu, mwili na roho).

unaweza kujiuliza kama ndivyo kwanini Mungu akafanya peke yake vitu vyote zeni kwa mwanadamu anaweka kikao ukweli ni hakuna kikao kilichokaa sababu ukisoma vizuri pale baada ya maneno tumuumbe mtu kwa mfano wetu, ukienda mbele kidogo utaona Mungu(baba, mwana na roho) akamuumba mwanadamu na sio wakamuumba mwanadamu otherwise kama wangekuwa ni watu tofauti basi wangesaidina kuumba pia kama walivyokubaliana mwanzo.
 
Back
Top Bottom