Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Kwa mujibu huo Mungu kukaa na cabinet yake kisha kuleta hoja ya aidha aumbe kiumbe chenye kufanana nao.

Hii inaonesha hakuwa na maamuzi ya moja kwa moja katika kila jambo. Ama kama alikuwa alikuwa na alikuwa na mamlaka ya kufanya chochote bila kuwepo kwa ushauri wa cabinet yake lakini aliamua ashirikishe cabinet yake. Basi yeye ni mwenye busara sana.

Je, vipi kama angepata upinzani baada ya kuwasilisha ombi lake.

Je, ni wote kwenye cabinet walikubali wazo lake.
Ule ushauri alioomba ndo unamgharimu mpaka leo, pengine angemuumba pekee yake yasingetokea haya.Binaadam amekuwa msumbufu kwa mungu.
 
Mwanzo 1:2 Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu, na giza lilikuwa juu ya uso wa vilindi vya maji; Roho ya Mungu ikatulia juu ya uso wa maji.

Kwa Sura hii inamaanisha’ Roho Mtakatifu’ alikuwepo wakati wa uumbaji

Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi.

Mastari wa 26 ametaja utatu mtakatifu na mstari wa 27 unamaanisha ni Mungu pekee ndie aliumba mwanadamu.

Mwanzo 1:27 Mungu akaumba mtu kwa mfano wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.
* kwa hiyo Mungu mwenyewe ndio alimuumba Binadamu
Roho mtakatifu ni kama kusema mama anaupiga mwingi.Ni ile nguvu ya kiutendaji ya Mungu.
 
Nimerudia huu uzi wa miaka zaidi ya minne na kusoma comment zangu nikajikuta najihubiria! Wakati mwingine unaweza kuandika jambo na baadae ukisoma unaweza kukana mwandishi si wewe!
 
Nimerudia huu uzi wa miaka zaidi ya minne na kusoma comment zangu nikajikuta najihubiria! Wakati mwingine unaweza kuandika jambo na baadae ukisoma unaweza kukana mwandishi si wewe!
Kichwa kikiwa na utulivu lazima utakachoandika kitakushangaza hata wewe mwenyewe siku ukija kurudia kukisoma
 
Back
Top Bottom