Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Mamlaka ya kiroho ndani ya mbingu - je, yalikuwa na pande mbili?

Uumbaji una maeneo mbali mbali uumbaji (kwa mujibu wa bible) labda tuanze na stage ya kwanza ambayo baadae bado haitakuwa ya kwanza, Mungu hajawahi kusema... (hakuna mahali iliposemwa Mungu aliumbaje roho (the holy trinity au malaika) Mungu aliumba mbingu na nchi stage 1.. ina maana gani mbingu ni universe na nchi ni Dunia hapo tunaona dunia ni sayari swali la kwanza sayari zipo ngapi? Alizuumba zote yeye Au galaxy zipo ngapi? Ok tuassume sayari ni dunia tu... turudi kwenye structure of the earth ni dude linaundwa na nitrogen, herium and other gases maana yake lilikuwa na joto kali sana (core of the earth inafika 6600C) so lilihitaji kupoa kabla ya kuruhusu uhai kukaa juu yake..

Kwa Mungu siku moja ni sawa na miaka 1000 so uumbaji haukufanyika siku sita za kibinadamu? Ilikuwa siku sita za kimungu right? Turudi kwenye uumbaji siku ya pili aliuumba mwanga tukumbuke before that hakukuwa na uhai dunia ilikuwa tupu yenye giza na ukiwa, (swali jingine kipi kilitangulia kati ya Jua, mwezi na Dunia) neno ukiwa means no life right? ... then kijiografia tunaona mwanga ambao ndio Jua na mwezi.. uliumbwa baada ya dunia? Then tunaona kila element za jua 99% ndio zilizopo duniani... na jua lina control dunia right? Yaani dunia ina rotate jua na sio jua kuzunguka dunia pia mwezi unazunguka Dunia right?

Ok my point is tunahangaika na kumwelewa Mungu na Shetani wakati hizi contradiction za mwanzo tu hatujazielewa? Ubongo wetu ni mdogo sana kumwelewa Mungu UKISOMA Isaya 45:7 utaona maelezo ya Mungu kwamba huleta nuru na balaa zote... so shetani ananafasi ndogo sana ya kusababisha balaa kwetu... still yeye ni roho isiyo na mwili but binadamu anavyote na utashi juu. Kwenye maelezo haya ndio kina Kiranga huja na assumption theories za Anunaki's the godess... miungu nk.
 
Uumbaji una maeneo mbali mbali uumbaji (kwa mujibu wa bible) labda tuanze na stage ya kwanza ambayo baadae bado haitakuwa ya kwanza Mungu... (hakuna mahali iliposemwa Mungu aliumbaje roho (the holy trinity au malaika) Mungu aliumba mbingu na nchi stage 1.. ina maana gani mbingu ni universe na nchi ni Dunia hapo tunaona dunia ni sayari swali la kwanza sayari zipo ngapi? Au galaxy zipo ngapi? Ok tuassume sayari ni dunia tu... turudi kwenye structure of the earth ni dude linaundwa na nitrogen, herium and other gases maana ya lilikuwa na joto kali sana (core of the earth inafika 6600C) so lilihitaji kupoa kabla ya kuruhusu uhai kukaa juu yake..

Kwa Mungu siku moja ni sawa na miaka 1000 so uumbaji haukufanyika siku sita za kibinadamu? Ilikuwa siku sita za kimungu right? Turudi kwenye uumbaji siku ya pili aliuumba mwanga tukumbuke before that hakukuwa na uhai dunia ilikuwa tupu yenye giza na ukiwa, (swali jingine kipi kilitangulia kati ya Jua na Dunia) ukiwa means no life right? ... then kijiografia tunaona mwanga ambao ndio Jua... uliumbwa baada ya dunia? Then tunaona kila element za jua 99% ndio zilizopo duniani... na jua lina control dunia right? Yaani dunia ina rotate jua na sio jua kuzunguka dunia...

Ok my point is tunahangaika na kumwelewa Mungu na Shetani wakati hizi contradiction za mwanzo tu hatujazielewa? Ubongo wetu ni mdogo sana kumwelewa Mungu UKISOMA Isaya 45:7 utaona maelezo ya Mungu kwamba huleta nuru na balaa zote... so shetani ananafasi ndogo sana ya kusababisha balaa kwetu... still yeye ni roho isiyo na mwili but binadamu anavyote na utashi juu. Kwenye maelezo haya ndio kina Kiranga huja na assumption theories za Anunaki's the godess... miungu nk.
Ubongo wetu ni mdogo sana kumwelewa Mungu UKISOMA Isaya 45:7 utaona maelezo ya Mungu kwamba huleta nuru na balaa zote...[emoji848][emoji2827]
 
Ubongo wetu ni mdogo sana kumwelewa Mungu UKISOMA Isaya 45:7 utaona maelezo ya Mungu kwamba huleta nuru na balaa zote...[emoji848][emoji2827]

Labda nitoe tafsiri isiyo rasmi balaa ni majanga, laana, adhabu (misfortune, calamity, trouble, desaster eg) ila sio uovu ambao ni evil acts mfano sin, catastrophic, demonic nk. So balaa la Mungu ni kama adhabu endapo unakosa utii wa maelekezo yake, so the devil know the game rules and consequences when u mess up... ndio hapo ana take chance kuvuna wanaoendelea kumkaidi Mungu...

anyway Mungu is not an object kwamba utamshika ni kama shetani pia hana umbo moja ni super natural power ikiwa kwa Mungu ni positive ikija upande wa shetani ni negative na zote zinaweza kufanya kazi tukizuruhusu so the choice is ours.
 
Alienda/Alipelekwa wapi?
Mimi ni myahudi kiimani,, tunaamini mungu ndio huyohuyo shetani, hivyo hakutupwa kokote, ile aya inaongelea Nebukdinezar, siyo shetani.
Screenshot_20221130-234614.png
 
Kuna kitu nimejifunza hapa, nitachimba zaidi
Mimi nikitafakari MUNGU na Shetani napata picha kwamba,Shetani ni Roho tu kama Roho ya binadamu isipokuwa haiko ndani ya Mwili hivyo uwezo wa kujitutumua ni Mkubwa.

MUNGU ni Nguvu inayotawala na kuumba au kuzalisha Nguvu zingine chini yake.

MUNGU aliumba Dunia lakini akaweka Nguvu (positive and Negative) za kuitawala dunia au kuiendesha Dunia na nguvu hizo zinategemeana.

Kwa Mwanadamu Nguvu hizi akizitumia kwa msingi wa Sheria zilizowekwa (Biblia au Manual book) basi mwanadamu anaishi kwenye ulimwengu usio na madhara .Hii ni sawa na kupewa gari jipya au chombo kipya lakini lazima upewe Kitabu cha mwongozo ili usijikute umetumia kinyume na utaratibu na kusababisha madhara.Hivyo nguvu ya kudhurika kwa chombo au mtu ipo na itatokea na kuonekana ni Nguvu hasi pale utakapoenda kinyume na maelekezo vinginevyo inaendelea kuwepo bila madhara.

Shetani si Nguvu hasi wala Nguvu chanya bali ni roho inayofanya kazi ya kushawishi mwanadamu kwenda kinyume na utaratibu ili ile nguvu hasi ilete madhara.

Mfano Mzuri ni Nguvu ya Umeme.Umeme una Nguvu Chanya na hasi kwa mwanadamu.Ikiwa Umeme utatumika kwa mjibu wa maelekezo ya kisayansi hauleti madhara yoyote ila ukitumika kinyume ile Nguvu ya umeme inaweza kuleta madhara makubwa ikiwepo vifo.

Shetani yupo kushawishi mwanadamu kuitawala Dunia kinyume na kitabu cha mwongozo wa kuitawala Dunia na hivyo zile nguvu hasi zinaonekana.
Kama Miti mingi inavyovuta Mvua kwa mjibu wa Sayansi,ndivyo Matendo Maovu yanavyovuta nguvu hasi,kama Magonjwa,vita,njaa,dhiki,na mwisho ni kifo cha kiroho na Mwili. Na Shetani kwa jina rahisi anaweza akawa Roho ya Tamaa,Kiburi au choyo nk.
 
Mimi nikitafakari MUNGU na Shetani napata picha kwamba,Shetani ni Roho tu kama Roho ya binadamu isipokuwa haiko ndani ya Mwili hivyo uwezo wa kujitutumua ni Mkubwa.

MUNGU ni Nguvu inayotawala na kuumba au kuzalisha Nguvu zingine chini yake.

MUNGU aliumba Dunia lakini akaweka Nguvu (positive and Negative) za kuitawala dunia au kuiendesha Dunia na nguvu hizo zinategemeana.

Kwa Mwanadamu Nguvu hizi akizitumia kwa msingi wa Sheria zilizowekwa (Biblia au Manual book) basi mwanadamu anaishi kwenye ulimwengu usio na madhara .Hii ni sawa na kupewa gari jipya au chombo kipya lakini lazima upewe Kitabu cha mwongozo ili usijikute umetumia kinyume na utaratibu na kusababisha madhara.Hivyo nguvu ya kudhurika kwa chombo au mtu ipo na itatokea na kuonekana ni Nguvu hasi pale utakapoenda kinyume na maelekezo vinginevyo inaendelea kuwepo bila madhara.

Shetani si Nguvu hasi wala Nguvu chanya bali ni roho inayofanya kazi ya kushawishi mwanadamu kwenda kinyume na utaratibu ili ile nguvu hasi ilete madhara.

Mfano Mzuri ni Nguvu ya Umeme.Umeme una Nguvu Chanya na hasi kwa mwanadamu.Ikiwa Umeme utatumika kwa mjibu wa maelekezo ya kisayansi hauleti madhara yoyote ila ukitumika kinyume ile Nguvu ya umeme inaweza kuleta madhara makubwa ikiwepo vifo.

Shetani yupo kushawishi mwanadamu kuitawala Dunia kinyume na kitabu cha mwongozo wa kuitawala Dunia na hivyo zile nguvu hasi zinaonekana.
Kama Miti mingi inavyovuta Mvua kwa mjibu wa Sayansi,ndivyo Matendo Maovu yanavyovuta nguvu hasi,kama Magonjwa,vita,njaa,dhiki,na mwisho ni kifo cha kiroho na Mwili. Na Shetani kwa jina rahisi anaweza akawa Roho ya Tamaa,Kiburi au choyo nk.
MUNGU ni Nguvu inayotawala na kuumba au kuzalisha Nguvu zingine chini yake.[emoji1752][emoji817][emoji1533]
 
Kwa ninavyo waza mimi



-Adam ana hawa wange kua ni wachina wallah, wasinge kuala tunda, wangemla yule nyoka wange mla na mpaka leo shetani asinge kuwepo tena dunia


- wangekua ni wabongo/watu jamii ya africa, wange muula yule nyoka na tunda wangelila KIMASIHARA hivyo shetani angekufa huku na tunda tungelila tukajikalia zetu kimya kimasihara.


- shida walikua ni wazungu, wakala tunda na nyoka wakamuacha ndio haya waliyo tuletea vizaazzaa duniani pumbavu kabisa


- na ikitokea sasa hivi, mm nitamuua huyo nyoka, na matunda nitayazoa mengi ili na wengine wayale, sili peke yangu, na hawa na piga chini akatafute sokwe lingine aishi nalo
 
Ukisoma kwa umakini Mwanzo sura ya kwanza mstari wa kwanza utagudundua kuwa kulikuwa na maisha kabla ya uumbaji huu wa dunia ya sasa uliopo.

Na baadhi ya theolojia za Kikristo zinataja kuwa Mungu kabla ya kumuumba Adam na kizazi chake aliwahi kuumba kizazi kingine, ila kilijivuruga sana, hivyo akaamua kukifutilia mbali na hivyo kupelekea nchi kuwa giza na ukiwa na Roho Mtakatifu akapewa jukumu a kuishikilia dunia kwa muda mpaka pale Uumbaji mpya utakapofanyika.

Kwa muktadha wa theolojia hiyo ni kuwa mara baada ya Mungu kutaka kurudisha uumbaji upya kutokana na uumbaji wa kwanza kufutiliwa mbali, ilibidi kukaa kikao mbinguni kupitisha maazimio ya kumuumba mwanadamu wa sasa na kizazi chake, na hili lilileta mvutano sana.

Wengi wa malaika na viumbe vya mbinguni vilipinga wazo hili kwa hoja kuwa so long as Shetani bado yupo, haina maana ya kuleta upya kizizi kingine maana yatatokea yale yale ya kizazi cha kwanza.

Lakini theolojia hiyo haisemi kwa nini Mungu pamoja na hoja nzuri ya malaika zake aliamua kumuumba Adamu japo alijua kabisa kuwa angeyarudia makosa yale yale ya watangulizi wake.

Ikumbukwe pia kuwa Mungu amekuwa na kawaida ya kukaa vikao na malaika wake, kama inavyoonekana kwenye Biblia.

Mfano , wakati Mungu anataka kumuhukumu Mfalme katili sana wa Israel aliyejulikana kama Ahabu kilikaa kikao na majadiliano yakawepo ya jinsi ya kumdanganya Mfalme aende vitani ili auwawe ili neno la nabii Eliya litimie, habari hii inapatikana katika 1Wafalme 22:19-23.

Pia wakati Ayubu anaundiwa zengwe ili kujaribiwa kwa majipu yale kiliwahi kukaa kikao Mbinguni na inaonekana Shetani alipeleka hoja zake Mbinguni japo za uchongezi ili kumshitaki Ayubu ajaribiwe.

Pia kimewahi kukaa kikao kati ya Mungu na Wajumbe wake cha nani atumwe kuja duniani kuwaokoa wanadamu, wajumbe kwa kujua uzito wa kazi mbele yao walikaa kimya, ndipo Yesu akasema nitume mimi.

Pia kwenye kitabu cha Ufunuo 5:1 inaonekana kulikuwa kikao mbinguni kati ya Mungu na wajumbe wake cha kuangalia ni nani aliyekuwa na uwezo wa kufungua document moja iliyokuwa ina siri nzito sana, na wajumbe wote wakakosa qualifications , mpaka Yesu mwenyewe alipoamua kufungua document hiyo.

Kimsingi suala la vikao mbinguni ni la kawaida sana, tatizo linakuwa ni moja tu kuwa wajumbe wa vikao huwa hawatajwi, anatajwa mwenyekiti wa kikikao pekee ambaye ni Mungu, na hii inatokana na mfumo wa utawala wa Kimbingu kuwa wa Kifalme.

Kawaida ya mfalme ni kubeba sifa zote hata kama watendaji wake ndio wamefanya maana mamlaka ya kiutendaji ya watendaji hao inatoka kwa Mfalme mwenyewe.

Kwa hiyo suala la uumbaji wa Adamu lilikuwa ni mwendelezo wa vikao hivyo hivyo, tatizo ni kuwa wajumbe wa vikao hawakutajwa, ila ukisoma Bibia kwa umakini utagundua kuwa waliokuwa wanazungumza katika kikao hicho walikuwa na cheo cha Uungu.

Kibiblia wenye cheo cha Uungu kwa mbinguni wako watatu, Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.
Kwa duniani cheo cha Uungu kipo kwa Shetani(Yesu alimuita Mungu wa dunia hii), Musa pia aliwahi kupewa cheo hicho, akawa kama Mungu kwa Farao na Haruni kuwa Nabii wake.

Kwa mantiki hiyo, kama kikao kile cha uumbaji kilikaa mbinguni bila shaka walikuwa watatu waliokaa ambao ni Mungu Baba, Yesu Kristo na Roho Mtakatifu.

Na hapo ndipo inapokuja kauli ya tumfanye mtu kwa sura yetu na mfano wetu.
Humu kuna heresy, wenye Roho wa Mungu watanielewa.
 
Kwa ninavyo waza mimi



-Adam ana hawa wange kua ni wachina wallah, wasinge kuala tunda, wangemla yule nyoka wange mla na mpaka leo shetani asinge kuwepo tena dunia


- wangekua ni wabongo/watu jamii ya africa, wange muula yule nyoka na tunda wangelila KIMASIHARA hivyo shetani angekufa huku na tunda tungelila tukajikalia zetu kimya kimasihara.


- shida walikua ni wazungu, wakala tunda na nyoka wakamuacha ndio haya waliyo tuletea vizaazzaa duniani pumbavu kabisa


- na ikitokea sasa hivi, mm nitamuua huyo nyoka, na matunda nitayazoa mengi ili na wengine wayale, sili peke yangu, na hawa na piga chini akatafute sokwe lingine aishi nalo
Nyoka amezua mjadala mkubwa sana.. Hasa uhalisia wake na kama alikuwa nyoka halisi ama alitumika kama lugha picha
20221201_143558.jpg
 
Mimi ni myahudi kiimani,, tunaamini mungu ndio huyohuyo shetani, hivyo hakutupwa kokote, ile aya inaongelea Nebukdinezar, siyo shetani.
View attachment 2432536
Ukisoma Ezekiel 28:13-15 ndo utajua shetani au ibilisi ilikuwaje akatupwa chini japo aliumbwa akiwa kerubi Malaika wa sifa, Pia katika Isaya 14:12-14 tunaona sababu zilizopelekea kerubi kutupwa chini sababu ya kutaka kuwa kama Muumba.
 
Ukisoma Ezekiel 28:13-15 ndo utajua shetani au ibilisi ilikuwaje akatupwa chini japo aliumbwa akiwa kerubi Malaika wa sifa, Pia katika Isaya 14:12-14 tunaona sababu za kerubi kutaka kuwa kama Muumba.
Ulikuwa Edeni, (A)
bustani ya Mungu;(B)
kila jiwe la thamani (C) lilikupamba:
kanelia, krisoliti na zumaridi;
topazi, shohamu na yaspi;
lapis lazuli, turquoise(D) na berili.[a]
Viwekeo vyako na viunga vyako vilitengenezwa kwa dhahabu;
siku ulipoumbwa yaliwekwa tayari.(E)
14 Ulitiwa mafuta (F) kama kerubi mlinzi, (G)
maana ndivyo nilivyokuagiza.
Ulikuwa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu;
ulitembea kati ya mawe ya moto.
15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako
tangu siku ulipoumbwa
mpaka uovu ulipoonekana ndani yako.
 
Nyoka amezua mjadala mkubwa sana.. Hasa uhalisia wake na kama alikuwa nyoka halisi ama alitumika kama lugha pichaView attachment 2432789
Nyoka kiuhalisia ni hila na sio kiumbe kama wengi wanavyodhani, maana kilele Cha nyoka ni hila, ndo maana tunasoma katika mathayo 12:34 "Enyi wazao wa nyoka, mwawezaje kunena mema, mkiwa wabaya? Maana, kinywa cha mtu huyanena yaujazayo moyo wake."

Na tunasoma Yohana akiwaambia mkutano katika Luka 3:7 "Basi, aliwaambia makutano ya wale waliomwendea ili awabatize, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?"

Pia Yohana mbatizaji akisema hayo katika mathayo 3:7 "Hata alipoona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake, aliwaambia, Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja?"

Iyo Luka 3:7 na mathayo 3:7 yohana anazungumzia kitu kilekile

So Nyoka anayezungumziwa katika kitabu sio kiumbe ni hila. Pia tujiulize kwann waitwe uzao wa nyoka nayo ni topic inayoanzia pale adam na Hawa walipodanganywa kula tunda maana yake hila ikaingia ndani yao na tangu hapo Kila aliyefuata alikuwa uzao wa nyoka.
 
Ulikuwa Edeni, (A)
bustani ya Mungu;(B)
kila jiwe la thamani (C) lilikupamba:
kanelia, krisoliti na zumaridi;
topazi, shohamu na yaspi;
lapis lazuli, turquoise(D) na berili.[a]
Viwekeo vyako na viunga vyako vilitengenezwa kwa dhahabu;
siku ulipoumbwa yaliwekwa tayari.(E)
14 Ulitiwa mafuta (F) kama kerubi mlinzi, (G)
maana ndivyo nilivyokuagiza.
Ulikuwa juu ya mlima mtakatifu wa Mungu;
ulitembea kati ya mawe ya moto.
15 Ulikuwa mkamilifu katika njia zako
tangu siku ulipoumbwa
mpaka uovu ulipoonekana ndani yako.
Katika hii Ezekiel 28:13-15 tunaona uumbaji wapili wa muumba akiwa amemuumba kerubi na kumweka katika bustani ya Adeni (sio Edeni) na kuweka madini ya Kila aina ili ampe sifa aliyemuumba lakin katika mstari wa 15 "Ulikuwa mkamilifu katika njia zako tangu siku ile ulipoumbwa, hata uovu ulipoonekana ndani yako."

Hila ikamwingia ndipo akatupwa chini ukisoma katika ufunuo 12:7-9
 
Ukisoma Ezekiel 28:13-15 ndo utajua shetani au ibilisi ilikuwaje akatupwa chini japo aliumbwa akiwa kerubi Malaika wa sifa, Pia katika Isaya 14:12-14 tunaona sababu za kerubi kutaka kuwa kama Muumba.
Ezekiel ni wa majuzi tu, ilukuaje waandishi wa mwanzo, kina moses wasiongelee hilo tukio?, Kuna misunderstanding kubwa sana ya maandiko, na watu huwa hawafanyi research, yaani wanaamini kiujumla,, ukweli ni kuwa, hakuna shetani,, tafuta maandiko ya kiyahudi usome kwa utulivu,, hizo habari sijui za kutupwa kwenye moto wa nini sijui,, hazipo ni story kama story tu, 🙆‍♀️
 
Ezekiel 28
1
The word of the LORD came to me:
2
"Son of man, say to the ruler of Tyre, `This is what the Sovereign LORD says: "`In the pride of your heart you say, "I am a god; I sit on the throne of a god in the heart of the seas." But you are a man and not a god, though you think you are as wise as a god.
3
Are you wiser than Daniel [1] ? Is no secret hidden from you?
4
By your wisdom and understanding you have gained wealth for yourself and amassed gold and silver in your treasuries.
5
By your great skill in trading you have increased your wealth, and because of your wealth your heart has grown proud.
6
"`Therefore this is what the Sovereign LORD says: "`Because you think you are wise, as wise as a god,
7
I am going to bring foreigners against you, the most ruthless of nations; they will draw their swords against your beauty and wisdom and pierce your shining splendor.
8
They will bring you down to the pit, and you will die a violent death in the heart of the seas.
9
Will you then say, "I am a god," in the presence of those who kill you? You will be but a man, not a god, in the hands of those who slay you.
10
You will die the death of the uncircumcised at the hands of foreigners. I have spoken, declares the Sovereign LORD.'"
11
The word of the LORD came to me:
12
"Son of man, take up a lament concerning the king of Tyre and say to him: `This is what the Sovereign LORD says: "`You were
 
Back
Top Bottom