Manara:Siku ya Jumanne nitaongea mambo mazito,,Yanga hawatatumia mitandao ya kijamii

Manara:Siku ya Jumanne nitaongea mambo mazito,,Yanga hawatatumia mitandao ya kijamii

Manara ameshachanganyikiwa, ye anajua ni maneno gani atayaongea ili yanga tuumie hakuna, mimi kama fan wa yanga maneno ya Kuongea ili niumie moyo wangu na nisitumie mitandao ya kijamii labda yatoke kwa malaika sio kwa huyu mshamba wa kizaramo
 
Manara, kipofu kaona mwezi. Simba naifananisha na ukoo ambao umempoteza ndugu yao kwa muda mrefu, baada ya jitihada zote za kumtafuta kushindikana siku moja baada ya kuamua kukamilisha taratibu zote za kuhitimisha kuwepo kwake duniani ghafla akajitokeza tena akiwa na afya njema, ukoo mzima ukakesha kwa furaha, Hii ndiyo Simba na huyo ndiye Manara.
 
Aaache ujuha wake. Ana matatizo ya kichwa nini. Yeye na mtindio wake wa ubongo asituzingue. Yanga na Simba wametoka mbali utani wa jadi umeanza hata babaake hajazaliwa leo aisambaratishe Yanga kwa upuuzi waje. Acha hizo dogo.
Hahahaaa. Kazi ipo pale.
 
Jana akihojiwa na kituo cha Azam live kutoka Namfua stadium,msemaji wa simba Haji manara amesema,", Siku ya jumanne ataongea mambo mazito dhidi ya Yanga na kuanzia Siku hiyo wanayanga hawatatumia mitandao ya kijamii

Njooni tubashiri,ni mambo gani hayo ambayo Manara ataongea mpaka aivuruge Yanga
Au tambo za mpira wa miguu,watani wa jadi

Ni kweli jumanne Yanga watasambaratika?

Je, wengine wakiongea mambo mazito ya kwake itakuwaje??
 
Manara ameshachanganyikiwa, ye anajua ni maneno gani atayaongea ili yanga tuumie hakuna, mimi kama fan wa yanga maneno ya Kuongea ili niumie moyo wangu na nisitumie mitandao ya kijamii labda yatoke kwa malaika sio kwa huyu mshamba wa kizaramo
Hahahaaa. Tuko sawa Mkuu.

Mie pia haitakaa ikatokea cha zaidi tutakuja mkaanga nayo hayo maneno siku akiteleza.
 
Hajawazidi wanyamwezi
Ndio, kwa Nini wasiwe waswahili na treni iliyobeba kiswahili iliharibikia Tabora? Hebu niambie Nani anaongea kiswahili kizuri kama mnyamwezi? Nimekuelewa ila nadhani jibu hilo linakufaa [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Manara ana kaushamba fulani hivi ila yeye anajiona mjanja! Tangu waingie madarakani ndio wameshinda ligi kwa mara ya kwanza yani tangu mzee Jiwe akiwa waziri wa uvuvi mpaka sasa yupo magogoni! Simba acheni ulimbukeni bhana kuwa bingwa ni jambo la kawaida
 
Back
Top Bottom