Sio wanawake wote ni materialist au ni dependants golikipa.
Ambao ukiomba namba tu nywele zinafumka(anataka aende salon),gesi inaisha,kodi ya nyumba inaisha,mama anaugua,simu inaisha vocha,mavazi /viatu,mikoba yanaisha au anatakiwa sare za kuvaa kwenye matukio,nauli inaisha ,bando,n.k anakuletea bills nyingi uzilipie kana kwamba wewe ni sponsor kama wanavyosema enzi zetu zamani walikuwa wanaita buzi.kuchuna buzi.
Wengine wanaamini mwanamke anayekupenda hakuombi hela na wanaume wengine wanaaamini asipoombwa hela hapendwi na anakosa kumuamini au kujiamini.
POINT ninayoisema SIO WANAWAKE WOTE wapo kimaslahi,
Kuna superwoman ambao ni wife materials ,kwanza ni wapambanaji hawapendi kuwa tegemezi kwa kila kitu ,wana mawazo ya maendelea wana mchango katika familia na wanaupendo wa dhati.Pia ni wavumilivu waaminifu na wana hofu ya Mungu.
VIJANA AMBAO HAWAJAOA AU WALIOPATA CHANGAMOTO ZA MAHUSIANO.
Niwashauri wasife moyo wasikate tamaa wamuombe Mungu awape neema ,awapatie WENZA SAHIHI wakuendana nao.Mungu alipomuumba mwanadamu Adamu alimletea na mke Eva.Hata sasa ukimuomba Mungu atakupa mke au mume sahihi.
Vijana wa kiume na wakike nao wajitahidi kufanya kazi.Kazi ndio kipimo cha utu.Vijana wa kiume na wakike wasichukulie mahusiano kama ndio kazi au kitega uchumi,kuna vijana wa kiume wanajiuza wanaolelewa na mashangazi na vijana wakike wanajiuza kwa shugadadi au sponsor Vijana walioko masomoni ,wafuate kilichowapeleka shule wasijiingize katika tamaa mbaya za kujiuza na kuuza utubwak kwa tamaa ya pesa mafanikio ya haraka.
POLENI SANA WOTE MLIOPITIA CHANGAMOTO YA KUPATA WENZA WASIOSAHIHI.
Mungu awasaidie mpate wenza sahihi,msikate tamaa,msichukie mahisiano,msichukie ndoa ,Mungu awasaidie mpate wenza sahihi,ili muweze kufurahia maisha ya mahusiano.