Utashindwa kujibu kwa kuwa kingereza chako ni hadi ule konyagi ndogo. Ila naunga mkono hoja wayafute waweke "LOWASA MABADILIKO, MADILIKO LOWASA"
Hivyo ni vibwagizo. Vibwagizo siyo kitu cha kudumu, ndiyo maana haviwekwi kwenye vitu vya kudumu.
Baadhi ya vibwagizo na tawala zake:
MWALIMU NYERERE
Uhuru na kazi - kililenga kuwahimiza watu wafanye kazi. Wasije wakafikiri kuwa huru maana yake ni kuwa na uhuru wa kutofanya kazi.
Siasa ni kilimo - kililenga watu wafahamu kuwa msingi wa siasa ni uchumi, na uchumi mkuu kwa nchi yetu ni kilimo.
MKAPA
Uwazi na ukweli = kililenga kuwahimiza viongozi kuwa wakweli kwa wananchi badala ya kuwalaghai.
JAKAYA
Maisha bora kwa wote - kililenga kuwapa hamasa watu kuwa kuna uwezekano wa wananchi wote kupata maisha bora
Ari mpya, kasi mpya = kililenga kuwahamasisha watu kuwa na mori na spidi mpya katika kuyatafuta maendeleo.
MAGUFULI
Hapa kazi tu - kililenga kuwaambia watu waache blabla, au kuwaeleza watu kuwa utawala wake hautakuwa wa blabla bali vitendo.
Hivi vyote ni vibwagizo ambavyo siyo sera wala siyo sheria. Ni vitu tu vinavyolenga kuamsha ari ya wananchi kwenye utawala fulani, siyo vitu vya kudumu, na wala havitakiwi kuwekwa kwenye vitu vya kudumu.
Lakini pia siamini kama Rais Magufuli aluwaamuru waandike mabebo hayo kwenye ndege au vivuko. Kwenye utawala ule, watu walikuwa wanashindana kusifu na kujipendekeza, hao ndio walioyafanya hayo.