Maneno maarufu secondary za bweni

Maneno maarufu secondary za bweni

Tunaendelea
kunywa=kukarili
keki nyeupe=ugali
chai ya kininja=chaiîsiyo kuwa na sukar
vidonge va njaa=maharage
 
Kuendesha ndege = kuzunguka ukiomba msaada kwenye msosi ie sukari, majani ya chai, peanut butter etc

Lyamungo boys iyo wayback!!
 
Kubaki Lupango-kuwa darasa lenye hadhi ya chini kabisa kwa muda mrefu kwa kuwa alama zako za ufaulu hazikuruhusu kwenda madarasa yenye hadhi ya juu(mf. Form two c badala ya form two a au b)
 
Toboa ozone - kusoma hadi mornie.

Mr Jamaa - mzee wa puli

pola - uji

zambarao maharage mekundu.

Ossilation au kudonoa -kusinzia wakati unapiga msuli

horizontal - kulala kwa bed

msuli ndichi -kusomea porin
 
Wakuu,amani kwenu...
Ningependa tukumbushane maneno maarufu yaliyokuwa yanatumika shule za secondary hasa boarding.
Mi nakumbuka maneno kama:
1.Njuka,kitimoto,mkia,nyoya=form one
2.Kufufuka=kuamka usiku kusoma.
3.Kuwa Mongwe= Kuishiwa pesa.
Sifongo=Uji usiokuwa na sukari.
4.Kuchoma=Kuingia bwenini ukiwa umevaa viatu/kandambili
5.Top layer=watoto waliokuwa wanakuja kuchukua mabaki ya vyakula.
6.Nelkon,Abbot,Lambert,Lodgers,UP,BS,Mkate,Jacky Fernandes,Nalndel Kumar=miongoni mwa vitabu maarufu vya sayansi.
Mnaweza kuendeleza list...

Vp ndg ulipiga Tosa nn maana haya maneno nimeyatumia kpnd niko Tosa nakula ugali wa marata enzi za kwenda Ipamba na Karenga.
 
Back
Top Bottom