Mangula, Dr. Slaa na Changamoto za Ufisadi Tanzania

Mangula, Dr. Slaa na Changamoto za Ufisadi Tanzania

DSN,

Namba 58 - hoja yako kuhusu ugumu wa bottom - up approach, hasa kuhusu jinsi gani kila mtu anachotafuta ni atoke ili asiwe kama wao tena, naikubali; ni moja ya vikwazo vikubwa sana, hasa kutokana na kukosekana kwa uzalendo, lakini muhimu zaidi, kutokana na uwepo wa a weak state ambayo sense of citizenship and civic duties ni kama haipo; Pia mchango wako juu ya suala hili unazidi kuthibitisha jinsi gani economy of affection ilivyokuwa na nguvu, hasa katika mjadala wako juu ya jinsi gani mtu akipata uongozi, ni muhimu kwa yeye kwenda kufanya ufisadi ili aje kununua tena nafasi ya uongozi kwa wale ambao hapo awali walikuwa ni wenzake (at the bottom), lakini sasa sio mwenzao tena;

Mfano wako juu ya Ullimboka - ni lazima watu wapoteze maisha, waumie, wafungwe, kwani kinachoendelea ni vita, sio mchezo wa kushindania kombe; bila watu kupoteza maisha, kufungwa n.k, hakuna la maana litakaloweza kutokea; umeona jinsi gani watu walivyo poteza maisha Libya, Tunisia, Algeria, Misri, na hata hivi sasa Syria; Kama kuna a political cause, watu kufa haitawazuia kujitafuta mabadiliko; Lakini hapa sina maana kwamba vita dhidi ya ufisadi ni lazima vifuate mkondo wa ghasia na mapinduzi, nia yangu ni kukueleza tu kwamba ikifikia hali hiyo, hayo ni maamuzi ya umma na kama wapo determined, watafanikiwa tu, bila ya kujalisha ni wangapi wamepoteza maisha; Vinginevyo, katika bandiko namba 59 nimeweka jedwali la kutusaidia tujadiliane iwapo tunahitaji a political party or a political movement kuondokana na mdudu ufisadi katika taifa letu;

Hoja yako kuhusu impact ya Jamiiforums katika jamii ya Tanzania - ni kweli, imetoa mchango mkubwa sana, lakini sidhani kama mtu ukiamua kuweka maslahi mbele na kujadili masuala badala ya watu utauawa, sana sana utatengwa, utatukanwa, utatishiwa maisha, na itaishia hapo; Lakini pia sishauri watu wajitokeze iwapo kazi yao ni kulipua tu mabomu na kuvua nguo viongozi, kwani hata kwa madogo haya ya kujadili CCM critically, kuna usumbufu wa hapa na pale unaojitokeza, na hata mimi nakumbana nao mara nyingi pamoja na vitisho vya hapa na pale, lakini kwa vile naamini zaidi katika taifa langu, na sivunji kanuni yoyote ya chama kama mwanachama au kutishia usalama wa nchi, sina haja ya kuogopa; Vinginevyo kwa kweli nasumbuliwa, na hata ikitokea siku nimepata matatizo, mjue nilitamka hilo;

Mwisho, kuhusu TAKUKURU mashuleni, kama ulinisoma vizuri, TAKUKURU haiwezi kufanya kazi ile kwa ufanisi bali NGO au taasisi yoyote yenye sura ya civil society; Kwa upande wa TAKUKURU, TISS, DPP, Polisi, sana sana ni kuboresha mfumo ili kuwepo na checks and balance ya kweli, sio ya ubabaishaji kama ilivyo hivi sasa;
 
Last edited by a moderator:
DSN,
Kuna hoja nyingi za kujibu, lakini kwa sasa naomba nijikite kwenye hoja kuu nne; Kwanza, ni kuhusu jitihada za Mwalimu kuunda taifa la Tanganyika/Tanzania, hasa kuweka misingi ambayo ililenga kutunusuru na matatizo tunayokabiliana nayo leo, hasa hili la Ufisadi; Kwa kweli Mwalimu alijitahidi lakini alishindwa kwani pamoja na uwepo wa Political Will, na pia kuonyesha kwa vitendo kabisa kwamba rushwa ni suala lisilo vumilika na kukubalika, hakuwa na timu nzuri ya kumsaidia kufanikisha vita hii; Wakati wa Mwalimu, rushwa ndani ya Serikali Kuu ilidhibitiwa kwa kiasi kikubwa, lakini tatizo lilikua kubwa sana kwenye Mashirika ya UMMA na Vyama Vya Ushirika; Huko Mwalimu palimshinda;

Ni kweli Mwalimu alizidiwa hapa!!!ila yasemekana alikuwa mkali sana lakini ndani ya ukali huo pia alikuwa na huruma sana pia.Kwa upeo wangu wa leo napojarinu kumuangalia yeye na kuimagine yeye ndani ya TAIFA hili kijana mdogo wa miaka 40 kuongoza nchi ya watu wenye kabila zaidi ya 120, na isiyo na wasomi,hakika nao ulikuwa mtihami kwa kweli.Ndio maana nikasema mchungambuzi utotoni ni tofauti na mtoto wa muuza duka.Mwalimu hakuwa mzamifu sana kwenye eneo la uchumi wa faida,bali alizama kwenye uchumi wa kuikimu jamii.Dunia imegeuka katika nyakati zake na kumucha kwenye njia panda ambazo nyakati hazikuweza kumpa nafasi kumaliza kile alichokiamini, hivyo kufungua na kutuacha na kile ambacho kwa maono yake vision,aliona tulistahiki kwenda huku.Nimatumaini yangu kuwa wewe na mimi tunakubaliana kuwa Nyerere hakupenda uchumi wa kujilimbilizia, hakuwa muumini wake hata kidogo,kuna seheu anasema haiwezekani kwa mtu mmoja kuwa na bidii zake binafsi kutafuata yeye binafsi na kupata utajiri huo basi binafsi anaamini kuwa utajiri huo utakuwa ni matokeo ya kunyonya nguvu ya wengine na yeye kuigeuza nguvu ya wengine kuwa yake binafsi.

Na pengie kuona huko kumlifanya kuona wale waliokuwa wanaharibu kupitia mashirka na kubatilishwa kwenda mengine walikuwa wanakosea kama binadamu na wakati mwingine akiamini kama labda hawakumwelewa pasipo kujua kuwa binadmu wengine wamezliwa ni materilaism by nature.

Rumors moja inasema kuna waziri wake alifanya madudu akamuita ikulu, alipofika waziri yule,JK akaagiza alimwe pingu kisha apelekwe sero.Napata picha nikumuona waziri husika akilia mbele ya yule mzee!!kisha wasaidizi wake wakishrikiana na polisi kweli wanamlima pingu muhusika,kisha wanaanza safari kuelekea keko,wakishatoka tu getini anapiga simu aludishwe na kupewa onyo kali sana.Binafsi naona huruma yake hiyo ilichangia,nae kuwaona wasaidizi wake hao kama watoto wake,kana kwamba mtoto kajipaka kinyesi uwezi kumtupa.Udhaifu huo hasa kwa mtu ambae ndio kwanza ana wasomi wachache na baadhiyaondio hao wenye kutenda makosa hayo basi kila kitu shagala bala.Huruma ile unaweza kuiona kwenye moja ya hotuba yake kuwa kulikuwa na adhabu ya viboko na yeye anasema hakuwa anaipenda adhabu ile lakini ilikuwepo ili kuweka mambo sawa.

Kwa yeye kufanya makosa yale,nisingependa kusema alifanya makosa,ila niseme hakuwa na maalifahayo na kwa kuwa hatukuwa na wasomi.Lakin leo hii tunakili kitu!!!

Mwalimu alishindwa kuthibiti chini ya chama kimoja, na pia chini ya mfumo wa uchumi ambao njia zote kuu za uzalishaji na usambazaji zilikuwa chini ya serikali; Tofauti ya Mwalimu na viongozi waliomfuatia ni POLITICAL WILL, hasa kwa kuonyesha kwa vitendo kwamba rushwa haikubaliki na haivumiliki, na kulikuwa na sheria kadhaa za kukabiliana na tatizo hili; Lakini tukubaliane kwamba alichofanikiwa Mwalimu ilikuwa ni kudhibiti rushwa ya aina ya kwanza kama nilivyoijadili awali - yani ile itokanayo na rogue individuals/petty corruption; Lakini rushwa ya kimfumo, hii ilimshinda, ingawa awamu zilizofuatia hali ikawa mbaya zaidi, hasa kutokana na Uchumi kuvamiwa na mabepari katika mazingira ya a weak and fragile state (of Tanzania);
Naona sera ya aina yake ya ujamaa wa kiafrika nayo ilichangia kumuweka hapo!!!Alitegemea Nchi za soviet na china,na matokeo yake kifo cha soviet ulikuwa nao ni msiba mwingine kwake.Hivyo utashi wake ilikuwa ni kutengenea uchumi wa kuhudumia umma, wakai mataifa ya ulaya na amerika yalilenga kuunda uchumi wa faida, yakifuta utashi wa mwanadmu wa kuoenda kujilimbikizia

Katika mchango wako, moja ya mapendekezo uliyotoa ni pamoja na umuhimu wa Katiba Mpya; Kimsingi nakubaliana na wewe, lakini je, Katiba mpya itatusaidia to strengthen our weak ‘STATE' and its Civic institutions, ili iwe/ziwe over and above Community Institutions? Je unadhani ni kitu gani kitawafanya watanzania, hasa wa vijijini waache Loyalty to their communities and institutions, jambo ambalo wamekuwa wanalifanua tangia uhuru, na badala yake, wahamishie their loyalty to the State and its civic institutions? Kwani, kwa mtazamo wangu, hiki ni kikwazo, lakini pia ni njia mojawapo ya kufanikisha vita dhidi ya rushwa, iwapo utakuwa ulinisoma vizuri awali juu ya problematic state of Tanzania na madhara yake;

Katiba mpya itatupa ruksa ya kila raia kuwa na uwezo wa kuhoji kwa mujibu wa katiba.Uwezo wa kupewa taarifa na kushitaki taasisi, kiongozi, nk.Taasisi kama TISS, C.I.G,A.G na wengineo wanatakuwa nao na uwezo wa kushtaki na kusimamia taasisi jina ili kuweka uwiano.Watendaji wakuu wa taasisi hzio watakuwa tayari kuwajibishwa na bunge na watakuwa tayari kujibu tuhuma au kushauri bunge pale inapobidi.

Hoja yako ya pili inahusu tamaduni fulani fulani za makabila fulani fulani na jinsi gani zinachangia tatizo la ufisadi, na pia kuambukiza tamaduni nyingine; hii ni hoja nzito sana, na nategemea mjadala mzuri sana kutoka kwa wale watakaokusoma; Sina uhakika sana na maelezo yako kwamba mkoloni aligundua madhaifu haya katika makabila fulani fulani na kuyatumia kikamilifu kuimarisha ukoloni, lakini kimsingi naelewa hoja yako vizuri sana; Je una mifano ya makabila husika ambayo unaweza kutupatia, hasa yale unayodhania kwamba yamechangia sana kuenea kwa rushwa kutokana na jadi na mila zake/zao?

Mchambuzi ili ni sensitive ebu jaribu kufanya utafiti mdogo!!!
Ulishasikia masai,mnyaturu, mngoni, au mkurya asiye na msimamo? basi kama jamii kuna makabila yanajulikana kwa kuwa na tabia ya kupiga wake zao kama wakurya,nao wake ao uamini kupigwa ni dalili ya upendo.Kuna makabila ya kitanzania yana utamaduni ambao ulipelekea msemo wa kama mgeni njo mwenyeji apone!!Kuna makabila ya pwani hayana haya au aibu!!!

Hoja hii inaweza kutupatia mwanga kidogo kuhusu jinsi gani mradi wa national integration wa Mwalimu Nyerere ulipata changamoto kubwa; Vile vile ingawa tunajisifia tupo wamoja, lakini it is only to an extent; ningependa kuliacha hili kwanza hadi pale utakaponipatia majibu kwa maswali yangu hapo juu; Vinginevyo national integration ni kweli, ni suala la kikatiba, na lilifanikiwa kwa kiasi kikubwa chini ya katiba ya JMT (1977), lakini sustainability yake ilipata matatizo, hasa kutokana na Chama Cha Mapinduzi baadae kuja kuwa superior to Katiba ya JMT; Na ndio maana nchi imekuwa kwenye mgogoro mkubwa sana wa Kikatiba, kwanza kule Zanzibar kuanzia miaka ya mwanzo ya themanini, na hatimaye Bara kuanzia miaka ya mwanzo ya tisini; Ingawa mgogoro wa Katiba umehusishwa zaidi na the Union Question, mimi nadhani ni zaidi ya hapo, na ndio maana Mwalimu alikuwa mkali sana na kutuonya kwamba tukiruhusu Zanzibar kujitenga, basi nchi yote itasambaratika kwa mujibu wa makabila;
Kwa kujua mfumo wetu wa kiafrika, tuliitaji na tunaitaji mashrikiano,tuliunganishwa na mashirkino.na yeye kupitia lugh ya kiswahili dhahiri taifa lilipata ramani halisi kama ishara ya kuwa Taifa lilipita kweny daraja la lugha ya kiswahili kama nguzo kuu yenye kila ishara inyojitoshereza kuunda Taifa na muungano unaotegemea uvulivu toka makabila tofauti tofauti kwenye jamii.

Hoja yako ya tatu inahusu mfano ulioutoa kuhusu Mbunge mmoja Marehemu – jinsi gani mkewe alivyomuaribia safari yake ya siasa kutokana na Mke huyo kwenda kinyume na Kanuni za Economy of Affection; Mfano wako huu nadhani ni moja ya case studies juu ya jinsi gani mfumo huu wa uchumi ulivyokuwa na nguvu ndani ya jamii yetu; Lakini je, tutegemee katiba mpya pia kuondoa mfumo huu?

Yap kuanzishwa kwa taasisi za maadili ya kijamii na kitaasisi yani maadili ya sura ya Taifa kwa kuanzia mtu mmoja mmoja na mpaka Taifa.Kupitia taasisi zetu za kikatiba zenye nguvu zitasimamia maadili ya Taifa kwa kofia ya katiba.

Hoja yako ya mwisho kuijadili hapa ni juu ya umuhimu wa kuunda TANZANIA UFISADI RECONCILIATION COMMITTEE [TURC]; Hoja hii ni ya msingi sana, na nilizungumzia kitu kinachofanania na hiki wakati najibu hoja ya mwenzetu mwingine nguruvi3 kwenye bandiko namba 54 ambapo nilishauri uundwaji wa Anti Corruption Coalition in Tanzania; Ingawa hauja thibitisha, kama itakuwa nimekusoma vizuri, wewe (kama ilivyo mimi), ni muumini wa kambi inayoamini kwamba tatizo la rushwa linaweza kutatuliwa na wananchi wenyewe yani bottom – up, na sio na viongozi yani top – bottom/up; Je, nipo sawa katika hili?

Hapa mwisho mkuu nina imani kuwa ilo lawezekana kwa dhana kuwa wahusika wawe ni kizazic ha kuanzia miaka -40 kushuka chini.Lakini ukisema kundi la bottom-up lisimame pasipo kipimo cha umri hapo mzee itakuwa ngumu kama nilivyokwisha kueleza kupitia mchango number 52.Group la miaka 41+ kwa hakika walio wengi wamepumbazwa na mfumo na hivyo wao kuona kuwa ili tukwamuke hapo tulipo jibu ni apatikane na Rais au kiongozi mkali aina ya Sokoine, na Mrema, basi moja kwa moja tutatoka kifungoni.Nami pia naamini kupitia uwepo wa nafsi za kitaasisi zenye mamlaka ya kikatiba basi ni rahis sana bottom up kuelimishwa na kuambia kwamba kupitia katiba raia mmoja mmoja na pia raia kama kikundi wana uwezo wa kushtaki, serikali, Taasisi, ama kiongozi.
 
Lukolo,

Namba 60 - Unazidi kusisitiza kwamba initiation lazima itoke juu, na unajadili kwa mapana content ya bottom - up, na jinsi gani the approach cant work; naomba usome bandiko 59, hasa swali namba TISA, hii inaweza kutupatia a good guidance and a good analytical framework, juu ya subject husika;
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

cc: Lukolo

Nimekusoma namba 55, na ninazidi kukuelewa; Ningependa kukuuliza maswali yafuatayo:

1. Je, zaidi ya wananchi kuimbiwa majukwaani, wamewahi kushirikishwa katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi? When, Who, Where and How? Nini ilikuwa matokeo?

2. Kati ya wananchi na viongozi, nani ana wakati mgumu wa kupambana na rushwa? kwanini?

3. Kati ya wananchi na viongozi, nani amemwangusha mwenzake zaidi katika vita hivi? kwanini?

4. Je imani yako kwamba top - down approach can be more effective, ina uhusiano wowote na matarajio ya katiba mpya?

5. Je nikisema kwamba - Mwalimu kwa kutumia top - down approach alifanikiwa kudhibiti petty corruption lakini sio grand corruption, utakubaliana na hoja yangu? Na iwapo utakataa au kukubali, kilichomwangusha with grand corruption ilikuwa ni watu at the top au watu at the bottom?

6. Ni kweli Civil Society imejaribu sana lakini je, as an umbrella or as individual entities? Kuna any Community Based Organization au NGO ambayo its primary purpose is to fight corruption in Tanzania? Ni ipi au zipi? Kwa uelewa wangu, zina deal na loose issue ya good governance;

7. Kuhusu suala la Uswisi, EPA, Kagoda, Richmond...unaposema tumejaribu kuulizia na kushinikiza.., tumejaribu ni kina nani, individually au as a group?

8. Na mwisho, je, bottom - up approach lazima ihusishe ghasia?

Kama nakusoma vizuri, nahisi unahusisha bottom - up approach na mapinduzi; naomba unisahihishe iwapo sipo sahihi juu ya hili; Vinginevyo, bottom-up inaweza kuchukua sura ya political movement, na jedwali hapo chini linaweza kutusaidia kujadili jinsi gani suala la ufisadi tunaweza kulitatua nje ya vyama vya siasa; Source ya Jedwali hili ni Goran Hyden:

9. Je, vita dhidi ya ufisadi, in your view vifuate orientation gani, cause or issue?

Source: Goran Hyden
VARIABLE
MOVEMENT
PARTY
OrientationCauseIssues
Level of OperationRegimeGovernment
Main Arena of OperationSocietyParliament
Method of OperationMobilizationPersuasion
Member OrientationDiffuseSpecific
Claims to ResourcesNo Formal LimitsConstrained by Rule of Law

Mchambuzi ukiangalia parameters za swali la tisa unaweza kuona kuwa vita dhidi ya ufisadi hapa Tanzania ni ngumu kuliko tunavyodhani...kama kweli tunataka kuondoa ufisadi unaofanya nchi yetu iwe masikini tunatakiwa tupambane kutoka kila pembe. Hatuwezi kuchagua front moja na kuacha nyingine, la sivyo tuta-fail. Serikali imejaa ufusadi, maofisa wa serikali ni mafisadi, chama tawala ni fisadi, wanachama wake waandamizi ni mafisadi. Bunge lenyewe ukiangalia lina wabunge wengi tu na scandals nyingi tu za ufisadi. Hata ukiangalia sheria zetu, majaji wetu kote unaona ufisadi, hata taasisi ambazo zinatakiwa kuwa semi independent kama Takukuru au TISS wimbo ni ule ule.

So whether the arena is parliament or party conference, whether the target is MPs or party members......the approach should be holistic.

Lakini tuangalie mifano halisi. Kwenye mikutano miwili mikubwa ya CCM tumeona kuwa mafisadi wote wamedinda, hakuna aliyetoka tena wanatoa hata vitisho. Tukiangalia bunge letu ni weak kuliko CCM, kwa hiyo bunge haliweza kuwa battle ground. Judiciary ukiangalia ndio weakest of all pillars of our state. Kwa hiyo ukiangalia kwa lengo la kupata solution japo kutoka kwenye pillar moja ya state hakuna uwezekano hata kidogo. Structure yote ya nchi ina uozo mwingi sana.

Kwa hiyo hebu tuangalie kidogo Top down solution. Tuanze kuangalia ndani ya CCM kwa sasa, na chances that inashinda uchaguzi 2015. Ukiangalia ili upate labda mmoja msafi ndani ya CCM, achukue madaraka, kwanza asafishe ufisadi na pili ajenge system inayoweza kudeal na ufisadi, labda kunaweza kuwa na hope. Lakini bado swali linakuja, ni nani huyo msafi? kimsingi kati ya wale wanaotajwa tajwa hakuna hata mmoja anayeweza kusimama na kusema tupambane na ufisadi. CCM kwa sasa haina sera ya kupambana na ufisadi kama chama, inawezekana imeweka sera hiyo kwenye katiba na manifesto yake, lakini manifesto inayotekelezwa kihalisi ni ufisadi na kujitajirisha...hili linaonekana wazi sana na lina ushahidi, maana ukiangalia top cream ya CCM unaweza kuona ni jinsi gani walivyo matajiri (kitu walichokitaka baada ya kutangaza azimio la Zanzibar). Ukiangalia yanayosema Rushwa ni ahudi wa haki, binadamu wote ndugu zangu, haki, utu, heshima, hayo kimsingi kwa sasa hayapo tena. Yalizikwa kwenye kaburi moja na Nyerere. Kimsingi system ya sasa inawanufaisha waliokiteka chama, na hawako wiling kuruhusu ufisadi ufe. Si chama na si individuals ndani ya chama wanaweza kuondoa sera hiyo.

Top down inaweza kufanya kazi kama akiingia mtu wa oposition ambaye atakuwa na real power, na sio ceremonial figure.

Bottom up...inaweza kusaidia kuleta pressure lakini sina hakika kama kweli inaweza kusaidia kubadilisha system iliyowekwa na CCM. Itakuwa ni kuwandoa mafisadi na wezi, na kuwaweka watu safi ambao wataendelea kutumia system ile ile iliyowekwa na mafisadi, na baadaye watabadilika kuwa wachafu.



Lakini kuna sehemu moja umemnukuu mwalimu kuwa tatizo kubwa tanzania ni ujinga.......bado watu hawajui kuwa chanzo kikubwa cha matatizo yetu ni muundo wa CCM, ambao unaruhusu kustawi kwa rushwa. Kwa sasa unasikia kabisa kuwa fulani ni fisadi, ni mwizi, lakini anapigiwa kura na kuwa mbunge na rais anamteua kuwa waziri.

U
 
Mkuu Mchambuzi,
Nimekusoma katika bandiko# 59. Nitajitahidi kuzirejea hoja zako kwa vifungu.
 
Katika bandiko 59 Mchambuzi ameuliza maswali.
Awali, napenda kusema kuwa mfumo wa rushwa uliopo ni kama kaserikali kadogo.
Umeingia katika sehemu zote kuanzia vyombo vya serikali kama usalama na ulinzi(Polisi, jeshi, ofisi za DPP, DCI, PCCB na serikali yote ngazi zote). Sehemu zingine ni habari na waandishi kwa ujumla.

Mfumo huo umehakikisha asasi za kijamii zote zinakuwa katika wakati mgumu kama tulivyoshuhudia kwa HakiElimu n.k.
Ili kujihakikishia makazi na uhalifu salama, mfumo wa rushwa umejipenyeza katika vyama vya kisiasa kwa kujua maamuzi mengi na muhimu hufanywa huko.

Lakini pia sehemu kama Bunge nazo hazipo salama. Kuanzia uongozi wa Bunge na Wabunge wenyewe wengi wao ni ''wafanyakazi'' wa mfumo huu. Taasisi za kisheria kama mahakama sasa zinatumika kama vichaka vya kuchelewesha au kupindisha sheria kwasababu navyo pia vimeingilia kwa ukamilifu na mfumo wa rushwa ambao network yake ni kubwa sana.Kwa hapa tulipo grand corruption imefikia kiwngo cha Umafia wa kimataifa

Hii maana yake ni nini?
Swali(1) na (6) kwamba hakuna taasisi iwe ya kiraia au iwavyo inayoweza kufurukuta na kubaki salama.
Community based Org au NGO haziwezi ku-survive katika hostile environment kama hiyo kwasababu rushwa imeshika sehemu zote muhimu za jamii.

civic society, NGO n.k zimebaki kujibanza katika good governance ambayo ni kelele zisizo wasumbua wala rushwa.
Kwa mantiki hiyo hoja ya rushwa imebaki kama mtaji wa kisiasa.

Swali(2)na (3). Mwananchi amebaki kuwa muathirika wa mfumo huu kwasababu yeye yupo katika receiving end ya matokeo ya rushwa. Hawezi kujikomboa kwasabababu za kimfumo nilizozitaja hapo juu.

Wanaofaidika na mfumo huo ni viongozi kama tunavyoona mfanyakazi wa kawaida wa serikali akimiliki Bilions of Tshs Uswiss. Mikataba na yote yahusuyo rushwa huishia juu na mwananchi akibaki kulipa kodi kila uchao.

Swali(5) mazingira aliyokuwa nayo Nyerere yalikuwa magumu sana. Kwanza kujenga utaifa na pili kuhakikisha kuwa watu walioko katika euphoria itokanayo na uhuru hawa abuse system.

Rushwa ilikuwepo lakini ilidhibitiwa na pale ilipojitokeza hatua zilichukuliwa. \
Kwamba kulikuwa na mafanikio kiasi gani inabaki kuwa questionable lakini hatwezi kulinganisha na nyakati hizi.

Kitendo cha Mwl kujua Mr ABC anamiliki pesa kiasi fulani na kumkatalia uongozi ni dalili kuwa alikuwa well informed na alikerwa sana na hali ya mambo. Je, ndivyo tulivyo sasa hivi au tumebaki na ''huo ni upepo tu''!

Swali(7) ninaposema tumejaribu nina maanisha wananchi kwa ujumla wao.
Ni kweli kuwa inaonekana kama individual lakini utakumbuka sababu nilizozitaja hapo juu ya mfumo rushwa na nguvu iliyo nayo katika jamii.

Swali(8) Bottom-up si lazima ihusishe ghasia. Kwa hapa tulipofikia ghasia haziepukiki ni suala la muda tu.
Wanadamu wana kiwango cha uvumilivu. Inapofikia mahali PM anazomewa na Rais anarushiwa madongo, hiyo ni dalili kuwa bottom up inaanza kufanya kazi. Kwa bahati mbaya watawala wetu ambao si viongozi hawajasoma alama za nyakati. Hata kama kutakuwa na taratibu za kuongoza bottom up mwisho wa siku ni lazima machafuko yatatokea.

Muhimu hapa ni kuona kuwa wananchi wameachwa jangwani, hawana mtetezi popote pale. Si mhakamani, Bungeni, ndani ya vyama au serikali. Rushwa iliyoota mizizi na inayolindwa kama ya hapa nchini haina suluhu nyingine ili Ghasia (ukombozi) ndilo suluhisho lililobaki. Nachukia kuita ghasia kwasababu wanaoleta ghasia ni wala rushwa na mfumo wao.

Swali(9), namshukuru sana Bongolander kwa kulijibu hili. Hakika rushwa tuliyo nayo haihitaji njia za kawaida. It needs variety approach including radical intervention.

Swali(4), nimewahi kuandika mara nyingi sana kuwa sina tumaini na katiba mpya.
Katiba hii inaratibiwa na kusimamiwa na mfumo wa rushwa ndio maana hawakukubali kukabidhi uandikaji kwa mamlaka za umma. Hayo ni maagizo ya mfumo rushwa na viongozi hawakuwa na ujanja.
Tunachotegemea ni kuandaa mazingira ya kuulinda mfumo.

Kwa mantiki hiyo top bottom approach haiwezi kuja na jambo tofauti na lililopo.
Nabaki kuamini kuwa tuna nafasi moja tu tuliyo nayo, clinically executed radical intervention. Yes, the consequences will be there but no freedom has ever come on silver plate, nadhani unakubaliana nami kwasababu umewahi andika kuwa katika jitihada lazima watu watapoteza maisha.

Hata hivyo bado naamini kuwa njia muhimu katika top bottom ni kuvunja uti wa mgongo, halafu tujenge kuanzia bottom up.

.
 
Katika bandiko 59 Mchambuzi ameuliza maswali.
Awali, napenda kusema kuwa mfumo wa rushwa uliopo ni kama kaserikali kadogo.
Umeingia katika sehemu zote kuanzia vyombo vya serikali kama usalama na ulinzi(Polisi, jeshi, ofisi za DPP, DCI, PCCB na serikali yote ngazi zote). Sehemu zingine ni habari na waandishi kwa ujumla.

Mfumo huo umehakikisha asasi za kijamii zote zinakuwa katika wakati mgumu kama tulivyoshuhudia kwa HakiElimu n.k.
Ili kujihakikishia makazi na uhalifu salama, mfumo wa rushwa umejipenyeza katika vyama vya kisiasa kwa kujua maamuzi mengi na muhimu hufanywa huko.

Lakini pia sehemu kama Bunge nazo hazipo salama. Kuanzia uongozi wa Bunge na Wabunge wenyewe wengi wao ni ''wafanyakazi'' wa mfumo huu. Taasisi za kisheria kama mahakama sasa zinatumika kama vichaka vya kuchelewesha au kupindisha sheria kwasababu navyo pia vimeingilia kwa ukamilifu na mfumo wa rushwa ambao network yake ni kubwa sana.Kwa hapa tulipo grand corruption imefikia kiwngo cha Umafia wa kimataifa

Hii maana yake ni nini?
Swali(1) na (6) kwamba hakuna taasisi iwe ya kiraia au iwavyo inayoweza kufurukuta na kubaki salama.
Community based Org au NGO haziwezi ku-survive katika hostile environment kama hiyo kwasababu rushwa imeshika sehemu zote muhimu za jamii.

civic society, NGO n.k zimebaki kujibanza katika good governance ambayo ni kelele zisizo wasumbua wala rushwa.
Kwa mantiki hiyo hoja ya rushwa imebaki kama mtaji wa kisiasa.

Swali(2)na (3). Mwananchi amebaki kuwa muathirika wa mfumo huu kwasababu yeye yupo katika receiving end ya matokeo ya rushwa. Hawezi kujikomboa kwasabababu za kimfumo nilizozitaja hapo juu.

Wanaofaidika na mfumo huo ni viongozi kama tunavyoona mfanyakazi wa kawaida wa serikali akimiliki Bilions of Tshs Uswiss. Mikataba na yote yahusuyo rushwa huishia juu na mwananchi akibaki kulipa kodi kila uchao.

Swali(5) mazingira aliyokuwa nayo Nyerere yalikuwa magumu sana. Kwanza kujenga utaifa na pili kuhakikisha kuwa watu walioko katika euphoria itokanayo na uhuru hawa abuse system.

Rushwa ilikuwepo lakini ilidhibitiwa na pale ilipojitokeza hatua zilichukuliwa. \
Kwamba kulikuwa na mafanikio kiasi gani inabaki kuwa questionable lakini hatwezi kulinganisha na nyakati hizi.

Kitendo cha Mwl kujua Mr ABC anamiliki pesa kiasi fulani na kumkatalia uongozi ni dalili kuwa alikuwa well informed na alikerwa sana na hali ya mambo. Je, ndivyo tulivyo sasa hivi au tumebaki na ''huo ni upepo tu''!

Swali(7) ninaposema tumejaribu nina maanisha wananchi kwa ujumla wao.
Ni kweli kuwa inaonekana kama individual lakini utakumbuka sababu nilizozitaja hapo juu ya mfumo rushwa na nguvu iliyo nayo katika jamii.

Swali(8) Bottom-up si lazima ihusishe ghasia. Kwa hapa tulipofikia ghasia haziepukiki ni suala la muda tu.
Wanadamu wana kiwango cha uvumilivu. Inapofikia mahali PM anazomewa na Rais anarushiwa madongo, hiyo ni dalili kuwa bottom up inaanza kufanya kazi. Kwa bahati mbaya watawala wetu ambao si viongozi hawajasoma alama za nyakati. Hata kama kutakuwa na taratibu za kuongoza bottom up mwisho wa siku ni lazima machafuko yatatokea.

Muhimu hapa ni kuona kuwa wananchi wameachwa jangwani, hawana mtetezi popote pale. Si mhakamani, Bungeni, ndani ya vyama au serikali. Rushwa iliyoota mizizi na inayolindwa kama ya hapa nchini haina suluhu nyingine ili Ghasia (ukombozi) ndilo suluhisho lililobaki. Nachukia kuita ghasia kwasababu wanaoleta ghasia ni wala rushwa na mfumo wao.

Swali(9), namshukuru sana Bongolander kwa kulijibu hili. Hakika rushwa tuliyo nayo haihitaji njia za kawaida. It needs variities of approach including radical intervention.

Swali(4), nimewahi kuandika mara nyingi sana kuwa sina tumaini na katiba mpya.
Katiba hii inaratibiwa na kusimamiwa na mfumo wa rushwa ndio maana hawakukubali kukabidhi uandikaji kwa mamlaka za umma. Hayo ni maagizo ya mfumo rushwa na viongozi hawakuwa na ujanja.
Tunachotegemea ni kuandaa mazingira ya kuulinda mfumo.

Kwa mantiki hiyo top bottom approach haiwezi kuja na jambo tofauti na lililopo.
Nabaki kuamini kuwa tuna nafasi moja tu tuliyo nayo, clinically executed radical intervention. Yes, the consequences will be there but no freedom has ever come on silver plate, nadhani unakubaliana nami kwasababu umewahi andika kuwa katika jitihada lazima watu watapoteza maisha.

Hata hivyo bado naamini kuwa njia muhimu katika top bottom ni kuvunja uti wa mgongo, halafu tujenge kuanzia bottom up.

.


Mkuu inatia uchungu sana. Nakubaliana na wewe kuwa sasa hivi CCM inapalilia chuki na Serikali inaiunga mkono. Bob Marley alisema you can fool some people for some time, not all time....siku watu wakiamka na kusema tunataka nchi safi...hapo ndio vurugu zitatokea and that like you said, is not very far away.

Angalia jinsi wanavyoongelea mabilioni ya Uswisi, angalia jinsi wanavyozungumzia EPA wanajua tu kuwa wananchi wamelala, na hawatafanywa kitu. Lakini kuna siku wananchi wataamka.....dalili zimeanza kuonekana. Kupinga ufisadi kwa sasa kunaanza kuonekana kama ni crime, na wapinga ufisadi ndani ya CCM kwa sasa fate yao ni hatari. Kwa hiyo wakati mwingine collective efforts za kudeal na ufisadi ni njia nzuri zaidi.

Mchambuzi ameleta mjadala mzuri sana. Ingekuwa safi sana kama watu wa Takukuru wangekuja hapa nao watueleze yaliyo ndani ya Takukuru.
 
Nguruvi3,

Namba 66 una hoja za msingi, za kutusaidia kuzidi kuchimba suala hili kwa undani; Nianze na haya machache:

La Kwanza - Msomaji Raia – mmoja wa wachambuzi wazuri sana wa Gazeti la Raia Mwema katika toleo la jana amejadili vizuri sana suala hili chini ya kichwa kisemacho: Nani Adui wa CCM? Chadema au Ufisadi? Link ya makala hiyo ipo hapa:
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/364485-nani-adui-wa-ccm-chadema-au-ufisadi.html

Msomaji Raia anasema kwamba "mabadiliko ya kweli yatakuja pale tu CCM itakapoamua kuuchukia ufisadi (badala ya kuichukia Chadema) na kufanya Ufisadi Kuwa ni Adui Yake Namba MOJA (badala ya kufanya Chadema Adui yake namba moja)."

Naunga mkono hoja hii; Na pia nadhani inaweza kutusaidia kwa kiasi fulani kuelewa changamoto za kupambana na ufisadi katika muktadha wa Bottom – UP na Top – BOTTOM; Kwa mtazamo wako, tukianza na Chama Cha Mapinduzi kuonyesha mfano na mwongozo katika vita hivi, baina ya wapiga kura na wagombea, nani aanze kutekeleza kanuni ya CCM Kwamba:

"Rushwa ni Adui wa Haki, Sitatoa Wala Kupokea Rushwa"

Na je, ni upande upi unaweza zaidi ku - influence upande mwingine towards mabadiliko na kwanini?

La Pili – umezungumzia jinsi gani rushwa ilivyoota mizizi kwenye taasisi za serikali ambazo zina wajibu wa ku deliver katika law, order, and justice kama vile Polisi, PCCB, DPP, DCI na TAKUKURU; Hizi ni Civic Institutions zinazoendana na dhana na pia existence ya "A STATE" ya Tanzania; Iwapo utakubaliana na mimi, Civic institutions katika taifa letu licha ya kuwa weak, pia bado hazijaota mizizi katika jamii kwani kwa kiasi kikubwa, watanzania wanaishi as communities, sio a civil society (refer rural areas); Na Civil Society na Civic Institutions go Hand in Hand – kwa maana ya kwamba, effectiveness ya Civic Institutions zinapimwa katika muktadha wa Civil Society, not Communities; Katika nchi yetu, taasisi ulizotaja kwa kiasi kikubwa ni kama hazipo; Mwalimu hakugeuza communities into citizens, na badala yake, wale wale watawalwa, ndani ya mipaka ya mkoloni, wakaanza kuwa relocated katika vijiji na kuanza kuzalisha huku wakipewa huduma za kijamii; Hata baada ya Mwalimu, tumeendelea kupuuza hilo;

Kuna maswali mawili katika hili:

Kwanza: Je, iwapo ulifuatilia mjadala wangu kuhusu supremacy ya community institutions vis a vis Civic Institutions in Tanzania, We do have a VERY WEAK and FRAGILE and almost IRRELEVANT STATE with its institutions in the Hinterland; Je taasisi hizi zitafanikiwa vipi kutatua tatizo la rushwa in the context of the economy of affection and informal exchanges nilizojadili awali, zenye community/informal institutions ambazo wananchi walio wengi ndio loyal zaidi to them kuliko civic institutions? Incentives ya Wananchi kuhamishia loyalty kwa civic institutions ni zipi hasa, huduma za kijamii kama enzi za Ujamaa?

Pili: Je, katika mazingira ya Mwananchi na hizi civic institutions ulizojadili (PCCB, POLISI, TAKUKURU n.k), na pia MEDIA, nani aaanze kutekeleza kanuni ya CCM kwamba - "Rushwa ni Adui wa Haki, Sitatoa Wala Kupokea Rushwa", mwananchi au taasisi? Na kwa taasisi (watumishi), nini itakuwa ni incentives towards that end, Uzalendo? Kushiba elimu juu ya utawala wa haki na sheria? Any other?

Pia kuhusu Bunge – ambalo umelitaja pia – kimsingi, bunge linawajibika moja kwa moja kwa wananchi; Katika ya wananchi na wagombea ubunge, nani aanze kutekeleza kanuni ya CCM kwamba: "Rushwa ni Adui wa Haki, Sitatoa Wala Kupokea Rushwa"? Kwa incentives zipi? Unageuzaje utamaduni wa watanzania wa kutaka immediate rewards (before one gets into office), ubadilike kuwa ule wa kutajaria rewards once someone gets into office? Nchi za wenzetu wameweza hili;

Unaposema kwamba Mwananchi ni mwathirika wa rushwa kutokana na kuwa on the receiving hand, how about the other way round – yani, kiongozi ni mwathirika wa rushwa kutokana na kuwa on the giving end, under the principles of "Economy of Affection"? Nimewahi kugombea uongozi, nikaambiwa vipeperushi vyako havina mpinzani, upinzani wako ni kwenye vipeperushwa; Na kweli, wapiga kura wakatumai haki yao ya kikatiba kuchagua wengine wenye vipeperushwa vilivyokuwa na mvuto zaidi, licha ya mimi kutumia 90% ya muda wangu wa kampeni kutoa somo juu ya madhara ya rushwa katika chaguzi, kwa kutumia literature za Mwalimu, case studies n.k;

Mwisho, Mwalimu hakuweza kuzuia ufisadi, aliweza kuzuia rogue individuals kutaka hongo kabla ya kutoa huduma za kijamii; Pia Mwalimu alitawala katika mazingira ambayo yalikwua controllable kwa maana ya kwamba the STATE was the only entity dominant in the Economy; Pamoja na hayo, bado ufisadi mkubwa sana ulikuwepo kwenye State Owned Enterprises na Vyama Vya Ushirika; Ufisadi ulichukua sura hizi mbili kwa 90%; Tofauti ya Mwalimu na waliomfuatia ni kwamba kwanza: Yeye he did not profit from politics, Kwahiyo hata uwepo wa rushwa haukumdhuru sana kwani whenever alipokemea, he had moral authority, na wananchi walifurahishwa na kitendo cha Kiongozi wa nchi kuonyesha kwa vitendo kwamba anaichukia rushwa, na kwamba serikali yake haivumilii rushwa;

Vile vile Mwalimu aliokolewa sana na the fact kwamba – serikali ilikuwa inatoa huduma za kijamii kwa wingi sana kupitia the developmental state model, huku itikadi inayohimiza usawa kimapato nayo ikizidi kuchochea; Vinginevyo Mwalimu hakuvishinda Vita dhidi ya Ufisadi, nguvu ya ufisadi iliendelea kuwepo na wahusika walikuwa ni wale wale – Wanasiasa wakishirikiana na Wafanya biashara wa ndani na nje waliopigana kufa na kupona to undermine Ujamaa ili Soko lifunguke wafanye makeke yao; Ndio maana Mwinyi alipoingia, Soko likavamiwa kwa vurugu kubwa; Mwalimu angeendelea na Urais ndani ya kipindi cha Mageuzi, hali isingekuwa mbaya kama ilivyokuwa wakati wa Mwinyi lakini Mwalimu asingeondoka na sifa alizoondoka nazo;
 
In the context of war against graft, let us ask ourselves for once. Why is CCM fighting so hard to win 2015 elections? What does it mean for the party to have Mangula as vice and Kinana as GS? Kutapatapa huku kuna maana CCM inajua kuwa ni irrelevant kwa Tanzania, na ni relevant kwa maslahi ya top cream ya Chama?

Kuna mtu yeyote anayeamini kuwa Kinana na Mangula wataifanya CCM irudi kwenye sura ya CCM before azimio la Zanzibar. Au kuondoa ufisadi na kuifanya CCM iwe safi. What can Kinana and Mangula do to, kwanza mafisadi na pili system ya ufisadi.

Inawezekana kuwa Mangula na Kinana wanafanya attempt ya kuifanya CCM ishinde, na baada ya ushindi itakuwa bizy as usual na ufisadi kwenda mbele? Tutegemee kuwa before 2015 viporo vya ufisadi na mafisadi vitashunghulikiwa ?

Wakuu naona giza tu, naona ni usanii na politiki zaidi.

Hata kama kutakuwa na Top down approach ya issue hii, inahitajika element ya mass movement. Juu kote ni kama kuna tope la ufisadi hakuna aliyesafi kusema atafanya kazi ya kudeal na tatizo.
 
Viongozi wa CCM kiwango chao pamoja na ubora wao hatima yake si ya kutumainisha kwa maana kwamba mabadiliko ya mara kwa mara nayo pia huadhiri stability ya chama. Kwa hoja hii kwa sasa hivi naweza kusema tathmini ya jumla ndani ya CCM is not stable kwani ndani ya miaka miwili tangu uchaguzi mkuu uliopita tumeshuhudia CCM ikifanya mabadiliko makubwa ya uongozi kitaifa kwa mara tatu huku mtendaji mkuu wa shughuli za chama (Katibu Mkuu) akibadilishwa katika vipindi vyote vitatu ndani ya miaka miwili. Hapa kuna kitu ambacho wao wenyewe wanakijua zaidi kinachoendelea ndani ya chama chao kuliko sisi tulio nje ya uringo.

Kutoka Kanali Yusufu Makamba, CCM ilikuja kumweka mzee Wilson Mukama aliyeonekana katuli kweli, mzee wa kiwango, mwenye busara na wa kukijenga chama na kuleta matumaini makubwa sana kwa CCM. Alianza na motomoto huku Katibu Mwenezi Nape wakiwa bega kwa bega kuwatia moto mafisadi, ni mmoja tu Rostam Aziz aliyeamua kwa hiari yake, wale waliotia ngumu blablaa zilikuwa ni nguvu ya soda na wakaja kupoa kutoka mhugo mchungu na kuwa kiazi kitamu. Wilson Mukama alionekana ni wa kiwango, hatimaye ameishia kuwa mkimya tofauti na alivyoanza, nini kilimfanya awe hivyo, labda hakukijua chama hicho kwa undani, kadiri alipokaa zaidi na kuijua ofisi akajikuta yuko peke yake na anafanya wasichokijua wala kutaka wenzake, kwamba siasa za majukwaani ni tofauti na utekelezaji, akabaki kunywea na kuacha liwalo na liwe.

Mkutano Mkuu uliopita huko Dodoma, yamekuja mabadiliko makubwa tena, huku Kikwete akimzawadia yule aliyekuwa meneja wake wa kampeni za uraisi, na baada ya mkutano wanaCCM wameonekana kufufua matumaini kwamba anaweza kurejesha hali ya kuaminika zaidi chama chao kwa wananchi. Kwangu mimi nikiangalia historia ya mabadiliko na hata kuwaingiza wale wa kiwango kama akina Wilson Mukama na kuishia kukata tamaa, haitakuwa ajabu hawa walioteuliwa juzi kuanzia Katibu Mkuu na Makamu Mwenyekiti wakaishia huko huko alikofikia Wilson Mukama.

Tatizo mabadiliko ni safu ya viongozi wengine wote walio chini ya Mwenyekiti, lakini mwenyekiti ni yule yule, na kama yaliyotokea kutotekelezeka pamoja na kufanya uamuzi katika vikao vyao, sitegemei jambo la pekee kwa safu hii mpya ya CCM. Kama safu zimebadilishwa mara kadhaa bila mafanikio ya pekee, basi tatizo ni viongozi waandamizi ila mkuu wa kaya ndiye mwenye matatizo.

Mleta mada ungejaribu kutenganisha hawa walili unaotaka kuwaunganisha katika ajenda sababu ni sawa na kuchanganya maji na mafuta. Kwa vyo vyote hata ukijitahidi kwa njia ye yote kitakachotokea ni mafuta kujitenga kwa kuelea juu ya maji.

 
Mkuu Mchambuzi,
Nitalirjea bandiko lako #68 kwa hoja zako nzuri sana.

Nimesoma mahali ambapo umeandika uwepo wa watch dog kama sehemu ya suluhu. Ninachoweza kusema hap ni kuwa tunazo tayari kama CAG, nadhani unaona matokeo ya kazi yake yanavyobezwa.

Tatizo linarudi pale pale kuwa taarifa ya CAG anaipokea Rais ambaye pia ana 'miliki' PCCB, Jeshi la Polisi, DPP, DCI na Usalama wa taifa (TISS). Vyombo vote hivyo haviwezi kutenda kinyume cha matakwa ya Rais.
Kwahiyo ubadhirifu wote unaofanyika ni ndani ya inner circle na mlinzi wao ni system nzima.

Kitendo cha Rais kuruhusu ripoti ya CAG kujadiliwa bungeni nacho ni kiiini macho. Tunakumbuka jinsi wala rushwa waliokamatwa na kufikishwa mbele ya rais walivyo achiwa kuendelea kula mafao.
Tunakumbuka jinsi maazimio ya bunge yalivyodharauliwa na Rais.

Rais ana nguvu za kufanya atakalo kwasababu yeye ndiye anaendesha system nzima na hivyo rushwa ambayo inaundwa na wanachama wa system haiwezi kukabiliwa ipasavyo.

Nchi za wenzetu Rais amewekewa mipaka ya kazi ili kuhakikisha kuwa hakuna abuse ya Ssytem ikiwa ni pamoja na kutumia vyombo visivyofungamana naye na vilivyohuru.

Haiwezekani PCCB itoe ripoti kwa rais na ikabaki kuwa na ufanisi. Nimepitia mashauriano katika kongamano na naweka link umsikie Jaji Manento na Ryoba wanavyoiongelea PCCB.
Jaji aicharukia Takukuru

Hoja yangu inabaki kuwa lazima kwanza kuwe na mechanism ya kuvunja system iliyopo halafu tujenge nyingine bottom up. Hata kama tutakuwa na watch dog 100, system itatumika kumiliki hizi watch dog.

Mfumo wa rushwa ni very complicated na intertwine kama anavyosema Bongolander. Mahali pa kuanzia ni kuvunja kwanza huo mfumo.
 
Mkuu Mchambuzi,
Nitalirjea bandiko lako #68 kwa hoja zako nzuri sana.

Nimesoma mahali ambapo umeandika uwepo wa watch dog kama sehemu ya suluhu. Ninachoweza kusema hap ni kuwa tunazo tayari kama CAG, nadhani unaona matokeo ya kazi yake yanavyobezwa.

Tatizo linarudi pale pale kuwa taarifa ya CAG anaipokea Rais ambaye pia ana 'miliki' PCCB, Jeshi la Polisi, DPP, DCI na Usalama wa taifa (TISS). Vyombo vote hivyo haviwezi kutenda kinyume cha matakwa ya Rais.
Kwahiyo ubadhirifu wote unaofanyika ni ndani ya inner circle na mlinzi wao ni system nzima.

Kitendo cha Rais kuruhusu ripoti ya CAG kujadiliwa bungeni nacho ni kiiini macho. Tunakumbuka jinsi wala rushwa waliokamatwa na kufikishwa mbele ya rais walivyo achiwa kuendelea kula mafao.
Tunakumbuka jinsi maazimio ya bunge yalivyodharauliwa na Rais.

Rais ana nguvu za kufanya atakalo kwasababu yeye ndiye anaendesha system nzima na hivyo rushwa ambayo inaundwa na wanachama wa system haiwezi kukabiliwa ipasavyo.

Nchi za wenzetu Rais amewekewa mipaka ya kazi ili kuhakikisha kuwa hakuna abuse ya Ssytem ikiwa ni pamoja na kutumia vyombo visivyofungamana naye na vilivyohuru.

Haiwezekani PCCB itoe ripoti kwa rais na ikabaki kuwa na ufanisi. Nimepitia mashauriano katika kongamano na naweka link umsikie Jaji Manento na Ryoba wanavyoiongelea PCCB.
Jaji aicharukia Takukuru

Hoja yangu inabaki kuwa lazima kwanza kuwe na mechanism ya kuvunja system iliyopo halafu tujenge nyingine bottom up. Hata kama tutakuwa na watch dog 100, system itatumika kumiliki hizi watch dog.

Mfumo wa rushwa ni very complicated na intertwine kama anavyosema Bongolander. Mahali pa kuanzia ni kuvunja kwanza huo mfumo.


Mkuu Nguruvi that is exactly the point. Unajua JKNyerere alikuwa honest kwa hiyo ilikuwa rahisi kumwamini na system kama hii. He was working for the people and for the country, not for himself. Labda ndio maana system haikulalamikiwa sana wakati wake.

Tatizo ni kuwa tuliweka system kwa assumption kuwa viongozi wote watafuata ahadi kumi za mwana TANU, lakini alipoingia Mwinyi chama kili abandon ahadi zote za mwana TANU, kwa hiyo tulipoua azimio la Arusha na kuleta la Zanzibar, we were supposed to come up with new rules, code of ethics and laws, but what we did was changing Azimio and hope that viongozi watakuwa safi waadilifu na wataheshimu nyadhifa zao.

Hata kama leo Slaa anaingia Magogoni akiamua kuwa fisadi atakuwa fisadi tu kutokana na system tuliyonayo.

Mchambuzi anazungumzia watch dogs, kimsingi tanzania kuna watch dogs wengi kisheria lakini wote ni toothless dogs or lap dogs.

Angalia tume ya maadili ilivyo kwa sasa, kama kweli ina relevance. Angalia Takukuru, inakamata wahasibu walioiba shilingi laki mbili, lakini walioiba trilioni mbili inawalinda. Angalia kama kweli Dr Hosea na Takukuru kama kweli wana maana yoyote kwa Tanzania, kama sio mzigo tu.

Umetaja vizuri kuwa viongozi wote wa watch dogs wanateuliwa kisiasa na Rais na wanatakiwa kuwa loyal kwa Rais. Kwa maana hiyo kama rais na wanaomhusu wakifanya uhalifu hakuna anayeweza kuchukua hatua zaidi ya kumwambia rais. Ukiangalia pia taasisi kama vile TISS, PCCB, POLICE, MILITARY na Viongozi wa taasisi hizo utaona kuwa they are loyal to the ruling party na si kwa Tanzania, viongozi wake wako loyal kwa anayewateua na sio kwa Tanzania. Hili ni tatizo kubwa, kuliko individuals.

Katiba yetu inamfanya Rais wetu awe mungu wa nchi, na si mtumishi wa wananchi, yeye ndio anatumikiwa. Na hakuna sheria zilizo wazi zinazomdhibiti Rais na matumizi ya madaraka.

can u imagine na sheria za sasa Mrema angekuwa rais, can you imagine for a second Magufuli awe rais katika katiba na sheria za sasa, can u imagine for a second Seif Sharif Hamad anakuwa rais na sheria na katiba ya sasa, angejideclare kuwa yeye ni sultani wa URT with absolute powers, na katiba inamruhusu. Ingekuwa hatari kuliko sasa.

Kwa hiyo kama kutakuwa na Top Down approach, kazi yake kubwa itakuwa ni kubadilisha system yote, huo utakuwa mwanzo mzuri. Rwanda style.
 
Back
Top Bottom