Manyerere Jackton: Kila ukikutana na Mwalimu Nyerere unahisi nguvu fulani ya ajabu

Manyerere Jackton: Kila ukikutana na Mwalimu Nyerere unahisi nguvu fulani ya ajabu

Sawa .....

Hayati Nyerere alikuwa ni KIONGOZI BORA KABISA kupata kutokea duniani...hakuna mfano wake hata huko URUSI ,CUBA na CHINA.....

Aliwazuia UKOO wake KUTENGENEZA FURSA za kiuchumi kupitia jina lake....UKWAPUZI kupitia jina lake ...VYEO NA TEUZI kupitia jina lake .....kwani kipi KILIMZUIA ?!!!

Kwani alimuogopa nani ?!!!

TAIFA LINA DHIMA YA KUENDELEA KUUHUDUMIA UKOO WAKE....

NI WAJIBU WETU MKUBWA KWAO ....

#SIEMPRE EL COMANDANTE JK NYERERE🙏
#HASTA LA VICTORIA EL COMANDANTE JK NYERERE🙏
Aliwazuia kusoma wakabobea? Aliwazuia kulima kilimo Cha kisasa wakawa matajiri?
 
Nchi ilikuwa na nini haswa kabla ya hizo sera za ujamaa unazozichukia?!!!!

Kumbuka ni hizohizo sera za UJAMAA zilizoleta VIJIJI VYA UJAMAA.....

Ni hizohizo sera za ujamaa ziliondoa UKABILA MKUBWA....UBAGUZI MKUBWA....UCHIFU....na kuleta angalau mwingiliano uliopo.....

Azimio la Arusha lilishaachwa kutekelezwa.....hujalisoma azimio la Zanzibar ?!!!

#Siempre JMT 🙏
Ukabila uliondoka lakini njaa iliongezeka, bidhaa zilikuwa adimu. Sasa faida ya Ujamaa nini? Halafu biashara na makampuni yaliyotaifishwa na Nyerere baada ya Azimio la Arusha leo yako wapi?
 
Ukabila uliondoka lakini njaa iliongezeka, bidhaa zilikuwa adimu. Sasa faida ya Ujamaa nini? Halafu biashara na makampuni yaliyotaifishwa na Nyerere baada ya Azimio la Arusha leo yako wapi?
Kuondoka kwa ukabila si kipaumbele kikubwa sana na cha KWANZA kabisa ili mambo mengine mazuri YAFUATIE ?!!!!


#Siempre JMT🙏
 
Wademkaji wa kizazi hiki hamuwezi kukaribia hata robo ya personality ya Nyerere, kama viatu vya magu havikutoshi vya Nyerere utafanya nyumba ya kulala kabisa...

Kuhusu baba wa taifa JK Nyerere ni kweli kabisaaa .....
 
Mwalimu Nyerere anabaki kuwa ALAMA ya baraka tele kwa taifa letu adhimu.

Komredi Manyerere Jackton anasema kuwa kila ukikutana na kuongea na Mwalimu Nyerere ulikuwa unaihisi nguvu ya ajabu na ya kipekee ya Mtanzania huyo.....

Anasema kuwa pamoja na ucheshi na misimamo aliyokuwa nayo bado hakuna mtu atakayesema kuwa ALIMFAHAMU VYEMA labda mama Maria Nyerere😍

HASTA LA VICTORIA EL COMANDANTE MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE🙏

SIEMPRE JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TANZANIA KWANZA KABLA YA NAFSI ZETU💪😍👊

#Kazi Iendelee Kwa Kasi &Weledi Zaidi
mkuu heshima yako 🙏
 
Kuondoka kwa ukabila si kipaumbele kikubwa sana na cha KWANZA kabisa ili mambo mengine mazuri YAFUATIE ?!!!!


#Siempre JMT🙏
Kwa nini kuondoka kwa ukabila ni kipaumbele? Kwani tulikuwa na vita ya ukabila? Tulikuwa na umaskini na sera za Ujamaa zilizidisha huo umaskini.
 
Kwa nini kuondoka kwa ukabila ni kipaumbele? Kwani tulikuwa na vita ya ukabila? Tulikuwa na umaskini na sera za Ujamaa zilizidisha huo umaskini.
Taifa la kijamaa lililoundwa na kusimikwa lilikuta pande la ardhi liitwalo Tanganyika lisilo na umoja huu uliopo zaidi ya TAWALA ZA MAKABILA na kushirikiana kwa HAYA NA YALE ya uafrika na ubinaadamu tu........

Unadhani ilikuwa ni KAZI RAHISI kwa baba wa taifa kuuondoa UKABILA wa baadhi ya maeneo....hujui ama unajisahaulisha kuwa BAADHI YA MAENEO alipingwa vikali sana alipoleta wazo la kulifanya taifa moja ?!!!!

#Siempre JMT🙏
 
Taifa la kijamaa lililoundwa na kusimikwa lilikuta pande la ardhi liitwalo Tanganyika lisilo na umoja huu uliopo zaidi ya TAWALA ZA MAKABILA na kushirikiana kwa HAYA NA YALE ya uafrika na ubinaadamu tu........

Unadhani ilikuwa ni KAZI RAHISI kwa baba wa taifa kuuondoa UKABILA wa baadhi ya maeneo....hujui ama unajisahaulisha kuwa BAADHI YA MAENEO alipingwa vikali sana alipoleta wazo la kulifanya taifa moja ?!!!!

#Siempre JMT🙏
Ukabila hewa huo maana kulikuwa hakuna vita ya ukabila. Tatizo lilikuwa ni umaskini ambao Ujamaa wa Nyerere uliuzidisha.
 
Nyerere alikuwa na mapungufu mengi Sana
Kuendelea kuwaaminisha watu hakuwa na makosa ..alikuwa kama Mungu mtu ni kuendelea kuikosea nchi..

Kwa faida ya Taifa watu waanze kujadili makosa na mapungufu yake

Turekebishe alipokosea..

Leo tunajadili katiba mpya..hakuliona hili?
sidhani kama kuna wanaosema Nyerere hakuwa na Makosa. yeye mwenyewe aliwahi sema kuwa kuna makosa alifanya na kuwashauri watu wachukue mazuri yale ya kijinga wayaache. kipindi kile ameingia madarakani katiba haikuonekana kama ni issue kubwa kumbuka mahitaji yanakuwa na kubadilika kutokana na nyakati husika. so kama tuna chuki naye tuziweke pembeni bado nyerere alikuwa upekee ambao viongozi wa sasa hawajaweza ufikia. mpaka kuja kukubali kuwa sasa aaache mitazamo mipya kuendesha nchi ilikuwa ni akili au busara. si wenzake wengi tu walikuja ondolewa madarakani kwa mapinduzi,vita na kudhalilika?
 
sidhani kama kuna wanaosema Nyerere hakuwa na Makosa. yeye mwenyewe aliwahi sema kuwa kuna makosa alifanya na kuwashauri watu wachukue mazuri yale ya kijinga wayaache. kipindi kile ameingia madarakani katiba haikuonekana kama ni issue kubwa kumbuka mahitaji yanakuwa na kubadilika kutokana na nyakati husika. so kama tuna chuki naye tuziweke pembeni bado nyerere alikuwa upekee ambao viongozi wa sasa hawajaweza ufikia. mpaka kuja kukubali kuwa sasa aaache mitazamo mipya kuendesha nchi ilikuwa ni akili au busara. si wenzake wengi tu walikuja ondolewa madarakani kwa mapinduzi,vita na kudhalilika?
😍😍
 
Kwa nini kuondoka kwa ukabila ni kipaumbele? Kwani tulikuwa na vita ya ukabila? Tulikuwa na umaskini na sera za Ujamaa zilizidisha huo umaskini.
nyie watoto wa miaka ya 2000s hamjui mambo ya ukabila na athari zake katika nch. mmeshindwa hata kujifunza kwa kuangalia tu hapo jirani Kenya au Rwanda na burundi. hivi hii Elimu ya miaka hii inawaelimisha nini?
 
Hakuna aliyeaaminisha kuwa alikuwa Mungu, ila kati ya viongozi waliowahi kuongoza Tanzania hadi sasa hakuna wa viwango kama Nyerere
Kila awamu ina changamoto zake huwezi kufananisha. Yeye kwa kiwango kikubwa alikuwa anashughulika na ukombozi wa bara la afrika na akasahau vya nyumbani. Pia yeye ndiye aliyekuwa msingi wa nyumba hii iitwayo Tanzania, wengine wamekuja kujenga juu yake tu.
 
nyie watoto wa miaka ya 2000s hamjui mambo ya ukabila na athari zake katika nch. mmeshindwa hata kujifunza kwa kuangalia tu hapo jirani Kenya au Rwanda na burundi. hivi hii Elimu ya miaka hii inawaelimisha nini?
Mtu...
Katika nchi za Afrika ya Mashariki ukabila kutoka wakati wa ukoloni ulikuwa ni tatizo Kenya na Uganda.

Kenya tatizo la ukabila liikuwa kati ya Wakikuyu na Wajaluo.
Tanganyika hapakuwa na tatizo la ukabila.

Hapakuwa na makabila ambayo walikuwa wanasigana.
Tatizo la Tanganyika toka ukoloni lilikuwa udini.

Kenya na Uganda hapakuwa na tatizo la udini kwa kuwa Ukristo ndiyo ulikuwa umetamalaki ka dini kuu.

Waislam walikuwa wachache Kenya na Uganda kiasi hawakuwa tishio.

Tanganyika ilikuwa na Waislam wengi wa kuonekana.
Natumia neno, ''tishio,'' kwa maana ya kuwa walikuwa na uwezo wa kuutikisa ukoloni.

Wajerumani walionja nguvu hii katika Vita Vya Maji Maji.

Waingereza waliishuhudia nguvu hii wakati wa siasa za utaifa baada ya Vita Vya Pili katika harakati za kupigania uhuru.

Ilikuwa tabu kuwatenganisha Waislam na joto lililokuwa linafukuta ndani ya TANU dhidi ya Waingereza.

Udini uliokuwapo Tanganyika wakati wa ukoloni ulikuwa kutoka kwa Waingereza na Wamishionari kutoka mataifa kadhaa ya Ulaya ambayo serikali iliwaachia kutawala elimu na wakaitoa elimu hii kwa kuwabagua Waislam.

Waingereza walipoja kuitawala Tanganyika baada ya kuondoka Wajerumani baada ya Vita Kuu Vya Kwanza, Wajeruamani walikuwa wameshafanya kazi ya kutosha ya kuiweka Tanganyika ndani ya mamlaka mbalimbali za Kikristo.

Tanganyika ilikuwa imegawanywa katika mamlaka mbalimbali za Kikristo kutoka nchi tofauti za Ulaya. Kanisa Katoliki ambalo ndilo lenye nguvu zaidi, lilikuwa tayari limeshajikita Tanganyika.

White Fathers walikuwa wapo Tabora, Karema, Kigoma, Mbeya, Mwanza na Bukoba; Holy Ghost Fathers walikuwa Morogoro na Kilimanjaro; Benedictine Fathers walikwepo Peramiho na Ndanda; Capuchin Fathers walikuwepo Dar es Salaam; Consolata Fathers walikuwepo Iringa na Meru; Passionist Fathers walikuwa Dodoma; Pallotine Fathers walikuwa Mbulu; Maryknoll Fathers walikuwapo Musoma; na Rosmillian Fathers walikuwa Iringa.

Hii ndiyo sababu harakati za kupambana zilipoanza Waislam walikuwa kitu kimoja jicho lao likimlenga adui ambae hawakuwa na shida kumtambua.

Waislam hawakupata hata siku moja kumwangalia Mwafrika Mkristo kama adui.

Hii ndiyo sababu Julius Nyerere aliweza kuchaguliwa kuongoza harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika na akawa kipenzi cha Waislam.

Udini na Ukabila haya yalikuja baada ya Tanganyika kuwa huru mwaka wa 1961.

Jambo la kusikitisha ni kuwa haya yalifanywa na Mwafrika mwenyewe baada ya kushika madaraka ambayo kabla ya uhuru yalishikwa na Mwingireza.

Maana ya ''udini,'' ikachukua maana nyingine.
Ikawa neno hili maana yake ni kuwa pale Muislam anapohoji, ''mbona nabaguliwa?''

Huyu ataitwa mdini.
Muislam hatakiwi kuuliza hilo.

Akiuliza ataambiwa analeta ''udini.''
Hapa ndipo tulipo miaka 61 baada ya uhuru.

Ndugu yangu Mtu...
Kabla hujatupia jicho Kenya na Burundi tupia kwanza jicho nchi yako na jifunze historia ya Tanganyika kwa ukweli wake.

Ukienda Kilwa na Songea katika kumbukumbu za Vita Vya Maji Maji majina haya ndiyo utayokutananayo kuwa walinyongwa na Wajerumani kwa kunyanyua silaha dhidi yao:

1649677235213.png
1649677277620.png

Waingereza wao walipambana na hao unaowaona hapo chini:

1649677384547.png
 
Mwalimu Nyerere anabaki kuwa ALAMA ya baraka tele kwa taifa letu adhimu.

Komredi Manyerere Jackton anasema kuwa kila ukikutana na kuongea na Mwalimu Nyerere ulikuwa unaihisi nguvu ya ajabu na ya kipekee ya Mtanzania huyo.....

Anasema kuwa pamoja na ucheshi na misimamo aliyokuwa nayo bado hakuna mtu atakayesema kuwa ALIMFAHAMU VYEMA labda mama Maria Nyerere😍

HASTA LA VICTORIA EL COMANDANTE MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE🙏

SIEMPRE JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TANZANIA KWANZA KABLA YA NAFSI ZETU💪😍👊

#Kazi Iendelee Kwa Kasi &Weledi Zaidi
Jumbe...
Historia za viongozi wa Afrika zimegubikwa na kile Wazungu wanaita, mysticism, yaani kuwa na mambo ya kushangaza na kutofahamika na pengine kutisha kumfanya kiongozi atoke kwenye ubinadamu.

Ikiwa mitume wa Allah hawakupewa nguvu hizo Mwalimu Nyerere yeye atazitoa wapi?

Kuna mambo husoma na nikajizuia kueleza kile nikijuacho.

Lakini tatizo la kukaa kimya ni kuwabakisha watu katika ujinga.

Nataka nikuelezeni machache katika mengi niyajuayo ndani ya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Hii ni historia ya Mwalimu Nyerere.

Mwalimu Nyerere amepata kulia ndani ya mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU New Street pale Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU (1954 - 1958) alipomtuhumu kwa tuhuma mbaya kabisa ya upendeleo.

Nyerere siku ile alimwaga machozi na mkutano ukavunjika.

Yako mengine lakini hili linatosha kuwa jibu kwa Manyerere.

Hadi leo wanahistoria wa hapa nyumbani wanamuogopa Sheikh Takadir.

Hatajwi popote kama vile hakupata kuwapo.

Kama nisingemtaja Sheikh Suleiman Takadir katika kitabu cha Abdul Sykes asingejulikana na historia yake ingekufa yote.

1649686009829.png

Kushoto ni Sheikh Suleiman Takadir, John Rupia na Julius Nyerere​
 
Jumbe...
Historia za viongozi wa Afrika zimegubikwa na kile Wazungu wanaita, mysticism, yaani kuwa na mambo ya kushangaza na kutofahamika na pengine kutisha kumfanya kiongozi athletes kwenye ubinadamu.

Ikiwa mitume wa Allah hawakupewa nguvu hizo Mwalimu Nyerere yeye atazitoa wapi?

Kuna mambo husoma na nikajizuia kueleza kile nikijuacho.

Lakini tatizo la kukaa kimya ni kuwabakisha watu katika ujinga.

Nataka nikuelezeni machache katika mengi niyajuayo ndani ya historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Hii ni historia Mwalimu Nyerere.
Mwalimu Nyerere amepata kulia ndani ya mkutano wa Halmashauri Kuu ya TANU New Street pale Sheikh Suleiman Takadir Mwenyekiti wa Baraza la Wazee wa TANU (1954 - 1958) alipomtuhumu kwa tuhuma mbaya kabisa ya upendeleo.

Hadi leo wanahistoria wa hapa nyumbani wanamuogopa Sheikh Takadir.

Hatajwi popote kama vile hakupata kuwapo.

Nyerere siku ile alimwaga machozi na mkutano ukavunjika.

Yako mengine lakini hili linatosha kuwa jibu kwa Manyerere.
👍
 
nyie watoto wa miaka ya 2000s hamjui mambo ya ukabila na athari zake katika nch. mmeshindwa hata kujifunza kwa kuangalia tu hapo jirani Kenya au Rwanda na burundi. hivi hii Elimu ya miaka hii inawaelimisha nini?
Ujamaa wa Nyerere umefilisi nchi.
 
Back
Top Bottom