Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,599
- 9,532
Umoja wa Mataifa (UN) umewapeleka likizo bila malipo wafanyakazi wake wawili ambao wanakabiliwa na kashfa ya kufanya vitendo vya ngono katika gari ya kazini nchini Israel.
Maafisa hao walipigwa picha ya video katika gari ambayo ilikuwa ina nembo ya UN- katika mji wa Tel Aviv katika mtaa wa ufukweni mwa bahari.
Katika video hiyo, mwanamke alikuwa amevalia gauni jekundu alionekana akiwa amemkalia mwanaume katika kiti cha nyuma cha gari.
UN imeanza kufanya uchunguzi wa video hiyo ya sekunde 18 ambayo imesambaa katika mitandao ya kijamii toka mwezi uliopita.
Stéphane Dujarric, msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, alikitaja kitendo hicho kinachoonekana katika kanda ya video kuwa kimemshtua na kimemchukiza.
Kufikia sasa UN imebaini kuwa wanaume hao ni waajiririwa katika taasisi yake ya Kusimamia Kusitishwa kwa Mapigano yaani Truce Supervision Organization (UNTSO).
Wawili hao wamesimamishwa kazi bila malipo yoyote mpaka uchunguzi kuhusu madai dhidi yao ukamilike.
Bwana Dujarric aliiambia BBC siku ya Alhamisi kuwa kusimamishwa kazi kwa muda kwa wafanyakazi hao ilikuwa ni hatua sahihi kutokana na ukubwa wa madai hayo ambayo ni kinyume cha utaratibu wa kazi katika kiwango cha kimataifa.
"UNTSO imeanza kampeni za kuwakumbusha wafanyakazi wake majukumu na wajibu wao kulingana na kanuni ambazo Umoja wa Mataifa umeziweka," bwana Dujarric alisema.
Maafisa hao walipigwa picha ya video katika gari ambayo ilikuwa ina nembo ya UN- katika mji wa Tel Aviv katika mtaa wa ufukweni mwa bahari.
Katika video hiyo, mwanamke alikuwa amevalia gauni jekundu alionekana akiwa amemkalia mwanaume katika kiti cha nyuma cha gari.
UN imeanza kufanya uchunguzi wa video hiyo ya sekunde 18 ambayo imesambaa katika mitandao ya kijamii toka mwezi uliopita.
Stéphane Dujarric, msemaji wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, alikitaja kitendo hicho kinachoonekana katika kanda ya video kuwa kimemshtua na kimemchukiza.
Kufikia sasa UN imebaini kuwa wanaume hao ni waajiririwa katika taasisi yake ya Kusimamia Kusitishwa kwa Mapigano yaani Truce Supervision Organization (UNTSO).
Wawili hao wamesimamishwa kazi bila malipo yoyote mpaka uchunguzi kuhusu madai dhidi yao ukamilike.
Bwana Dujarric aliiambia BBC siku ya Alhamisi kuwa kusimamishwa kazi kwa muda kwa wafanyakazi hao ilikuwa ni hatua sahihi kutokana na ukubwa wa madai hayo ambayo ni kinyume cha utaratibu wa kazi katika kiwango cha kimataifa.
"UNTSO imeanza kampeni za kuwakumbusha wafanyakazi wake majukumu na wajibu wao kulingana na kanuni ambazo Umoja wa Mataifa umeziweka," bwana Dujarric alisema.